Wewe -Ungekuwa meneja mkuu wa Precision Air

shilanona

Member
Oct 31, 2010
55
22
Kwa mara ya kwanza katika maisha yangu ya miaka 55, Mungu amenijalia kupita kwenye usafiri wa hewani na fastJet kutoka DSM kwenda Mwanza kwa bei ya sawa na usafiri wa Mombasa raha kati ya Dar na Mwanza. Aliyeleta idea hii ili na sisi wenzangu mimi tunuse hewa tamu ya karibu na mbinguni apongezwe sana.
Mimi ningekuwa Meneja wa Precsion Air ningemshauri ajipange upya na aje na mkakati mbadala wa biashara ya usafirinwa ndege ambayo tayari ni tishio kwenye kampuni yake. kama hawa Fastjet wataendelea, basi NAOMBA usikubali Precision ife kwa sababu ya kukosa soko,. Anza kwa kupunguza matumizi yasiyo ya lazima kuanzia sasa, punguza wafanyakazi wako ambao wengi ni ndugu zenu, kata intertainment allowances, na ukiweza punguza hata mishahara ya wafanyakazi ukianzia ule wa kwako mwenyewe, halafu ongeza idadi ya flights kule ambapo hawa jamaa hawaendi na mwisho punguza nauli ili uanze kushindana na siyo kutanua.

Naipenda Precsion kwani nilikuwa naiona hewani kila siku lakini nadhani naipenda sana fastjet kwani nimeweza kwenda nayo hewani leo.
 
tuwe wazalendo toa ushauri kwa air Tanzania kwasababu ndo nchi yako regardless kama watakuwa wamekusikia or wakupuzie
 
Mkuu shilanona labda hujui system ilivyo,

Kuna mashirika ya ndege ya Umma na binafsi, ni ngumu sana kutoa ushauri wako(no offence) kwa shirika BINAFSI,
wewe uliipenda kwa "kuiangalia hewani" lakini kuna watu wanaipenda pia kwa kuwa na ubia nao, hisa n.k na wao wana wateja wao not only in economy class lakini hata BUSINESS class..ingawa ni kweli wateja watapungua(as hadi sasa Fastjet imejaa hadi February) lakini si kwamba watakosa wateja kabisa mkuu.

Ni vizuri, ushauri huo ungeenda kwa Air Tanzania(maana wanaanya kazi), na ni shirika la umma(Taifa).

Hopefully, ulisafiri vyema na fastjet mkuu.
 
Last edited by a moderator:
tuwe wazalendo toa ushauri kwa air Tanzania kwasababu ndo nchi yako regardless kama watakuwa wamekusikia or wakupuzie

Air Tnzania hata ukiwapa ushauri hautawafaa sababu wapo ki SIASA zaidi sio kibiashara wana ndege 2 wafanyakazi 225 majengo ya Ofice yakukodi 45 ghalama zote hizo zilipwe kwa Ndege 2 wanaishi kwa matumaini ya ahadi hewa toka Serkalini wakati hta selikali yenyewe inashidwa kujiendesha kwa mapato yake je kuna Wachumi hapo??wa biashara?? watoa maamuzi hawana mazi
 
mkuu wa wilaya ya Hai Bwana Makunga amelalamikia watu wanaoshuka kwenye ndege KIA kuulizia usafiri wa bodaboda
source uso wake wa kitabu
 
Fastjet inashindana na mabasi na si air Tz au precision air. Bigup fastjet!
 
mkuu wa wilaya ya Hai Bwana Makunga amelalamikia watu wanaoshuka kwenye ndege KIA kuulizia usafiri wa bodaboda
source uso wake wa kitabu

Huyu Makunga mwehu nini? Anataka ndege wapande matajiri tu wa kukodi tax?
 
Isije ikawa ni "kipya kinyemi, ingawa...." Mimi naamini ni muda tu utaamua kama ni "Fast Jetting" ama "Fast Betting"

"Usiache mbachao, kwa msala upitao"
 
Isije ikawa ni "kipya kinyemi, ingawa...." Mimi naamini ni muda tu utaamua kama ni "Fast Jetting" ama "Fast Betting"

"Usiache mbachao, kwa msala upitio"
Nauli ndogo za FastJet ni za muda tu. Ni MARKET ENTRY STRATEGY. Wanaweza kuondoka upesi sokoni kama walivyoingia kwa sababu nauli zao haziwezi kukidhi gharama kwa muda mrefu. Wataanza kupandisha bei taratibu baada ya muda. Kwenye miaka ya 1980 huko Uingereza alitokea jamaa mmoja anaitwa Sir Fredy Laker akaanzisha Laker Airlines kwa mtindo huo huo wa FastJet na kuchota abiria wa makampuni mengine ya ndege. Walichofanya washindani wake kama British Airways na wengine walishusha nauli chini ya zile za Laker katika route zote ambazo Laker ilikuwa ina-operate na abiria wao wakarudi. Haikuchukua muda Laker Airways ikafirisika na kujiondoa kwenye soko. Baada ya hapo nauli za kampuni zingine zikarudi kwenye viwango vya awali. Enjoy FastJet while it lasts.
 
mkuu wa wilaya ya Hai Bwana Makunga amelalamikia watu wanaoshuka kwenye ndege KIA kuulizia usafiri wa bodaboda
source uso wake wa kitabu
Du Makunga mbona yupo humu JF ajibu hizi hoja na kuanzia sasa aruhusu Bodaboda zote zisogee pale KIA kuliko kizizuia zisiingie km ni habari za kweli
 
Last edited by a moderator:
mkuu wa wilaya ya Hai Bwana Makunga amelalamikia watu wanaoshuka kwenye ndege KIA kuulizia usafiri wa bodaboda
source uso wake wa kitabu

Mbona unapotosha kwa makusudi nilichoongelea,haipendezi hata kidogo,labda kwa msaada kwa wale wasioona post yangu ni kwamba nilionyesha jinsi mageuzi yaliyotokea katika usafiri wa anga kiasi cha kwamba hata watu wa kawaida wanaweza kupanda ndege na walishuka wanauliza bodaboda kwa taarifa yako kuna rafiki yangu alishuka saa mbili na nusu wiki iliyopita na nikamtumia boda boda ama toyo hadi hai kwa kuwa nilikuwa mbali
 
Du Makunga mbona yupo humu JF ajibu hizi hoja na kuanzia sasa aruhusu Bodaboda zote zisogee pale KIA kuliko kizizuia zisiingie km ni habari za kweli

Sijuhi kwa sasa kama wanaweza ku make kwani jamaa wa ndege hiyo wameshaandaa mabasi kwa kila flight kwenda moshi na arusha kwa shilingi elfu kumi ni tofauti na dar ambako ukishuka katika ndege hakuna usafiri wa umma hivyo unalazimika kugongwa na taksi
 
Air Tnzania hata ukiwapa ushauri hautawafaa sababu wapo ki SIASA zaidi sio kibiashara wana ndege 2 wafanyakazi 225 majengo ya Ofice yakukodi 45 ghalama zote hizo zilipwe kwa Ndege 2 wanaishi kwa matumaini ya ahadi hewa toka Serkalini wakati hta selikali yenyewe inashidwa kujiendesha kwa mapato yake je kuna Wachumi hapo??wa biashara?? watoa maamuzi hawana mazi


Hao wame PARK wala hawajui kinachoendelea!
 
Sikutegemea kama Ningekuja kupokelewa K.I.A.,Maishani mwangu,Ahsente FastJet!!!!!.
 
me ningekuwa meneja ningejiunga na fastjet!mind,"if u can not fight ua enemy,join him"
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom