Wewe ni Mtoto wa kwanza au wa Mwisho?

October

JF-Expert Member
Oct 5, 2009
2,145
92
Kuna jambo moja ambalo watu wengi hulichukulia mzaha, masihara au utani wakati wa kutafuta mwenzi wa maisha (mke au mume) nalo ni suala la mtoto wa kwanza kuzaliwa na mtoto wa mwisho kuzaliwa.

Swali la kujiuliza je, kuna matokeo yoyote au athari zozote kuoa au kuolewa na mtoto wa mwisho au kwanza kuzaliwa katika familia yao ?

Jibu la kweli ni NDIYO KUBWA,
Kuna athari kubwa kama ni kweli unayeoana naye ni mtu wa kwanza au wa mwisho kuzaliwa ingawa kuna exceptions.

Kama una mchumba ambaye kwao ni mtoto wa mwisho kuzaliwa jambo la msingi ambalo naweza kukushauri ni wewe kuwa tayari for adventures, na kama ni mtoto wa kwanza kuzaliwa basi jiandae kuwa audited kila kitu au kukaliwa au kuongozwa bila kujali ni mwanaume au mwanamke period.
Mtoto wa kwanza kuzaliwa kawaida hujikuta ni kiongozi mahali popote na hupenda kuongoza, kupenda kuhakikisha kila kitu kinaenda vizuri na kama kilivyopangwa maana ndivyo alikuwa anaagizwa na wazazi kwake kuhakikisha wadogo zake wanatii kile ameagizwa;

"Hakikisha wadogo zako wamekula, wametandika kitanda, waosha vyombo, wamefagia uwanja, wamelala mapema nk".

Mtoto wa mwisho kuzaliwa hujikuta ni mtoto hata akiwa mtu mzima kwa kuwa kwao bado ni mtoto na huwa hana shida na kitu chochote kwani kwake kila kitu ni rahisi na anapenda raha, sherehe na life is easy.
Kila kitu nyumbani kilikuwa ni kwa ajili yake kwa kuwa yeye ndiye mtoto hata baada ya kuwa mtu mzima bado anajiona ni mtoto Ndiyo maana huchelewa hata kuongea, kufanyia vitu mwenyewe kama vile kujua muda wa kula, sehemu ya kuweka nguo, kutandika kitanda, kuoga nk, yeye hujiona ni special kid, ni mtoto wa baba na mama na amekua wakati wazazi wamezoea maisha.
Kwa ujumla tabia za watoto wa kwanza kuzaliwa huwa ni kukaliwa wenzao (controlling, bossy, leading, perfectionist, auditors, no fun, firm and rigid) wengi ni viongozi na watoto wa mwisho kuzaliwa hujiona ni special kid, hujiona mtoto miaka yote, watu wa sherehe, don't care, easy wengi ni comedians.

Je, inakuwaje wakioana mtoto wa kwanza na mtoto wa mwisho kuzaliwa?
Kama mmoja ni wa kwanza kuzaliwa na mwingine ni wa mwisho kuzaliwa (au mmoja ana tabia ya mtoto wa kwanza kuzaliwa na mwingine tabia ya mtoto wa mwisho kuzaliwa basi ndoa itakuwa nzuri kwani tabia zitawafanya wa-balance.

Uzembe wa mtoto wa mwisho utakomeshwa na mtoto wa kwanza kuzaliwa ambaye hupenda kuongoza na kuhakikisha kila kitu kinakuwa sawa haijalishi ni mke au mume.
Hujasikia mwanamke analalamika kwamba mume wake hakustahili kuoa au kuishi na mke, maana yake ni mtoto wa mwisho na haijalishi amesoma au hajasoma watoto wa mwisho tabia hufanana.
Je, inakuwaje wakioana wote ni watoto wa mwisho au wote watoto wa kwanza kuzaliwa?
Ukweli ni kwamba match ya ndoa ya aina hii huwa inakera sana kwani kama wote ni watoto wa kwanza kuzaliwa kila mmoja atapenda kuwa kiongozi na sidhani kama hiyo meli haitazama. Na wakikutana wote watoto wa mwisho basi ni balaa kwani ndoa itakuwa haina kiongozi na itakuwa ni adventures.

Watoto wengi wa kwanza Ndiyo marais, wachungaji na viongozi mbalimbali na watoto wengi wa mwisho ni ma-MC na comedians.

Watoto wa kwanza kuzaliwa likija suala la sex wanachagua sana na kuwa na utaratibu ambao huchosha (routine sex), pia hufanya sex kama wakaguzi kama vile lazima kuoga kabla ya sex, taa zizimwe, kusiwe na mtu hajalala usingizi within 100m, piga mswaki, usiku tu tena baada ya saa tatu na si baada ya saa nne nk, ni usumbufu.

Bila watoto wa mwisho sherehe huwa hazinogi ingawa wao tatizo lao si kawaida yao kuwahi na kufika on time kwenye sherehe, ingawa watoto wa kwanza kwao ratiba ni muhimu.
Likija suala la siasa first born wengi ni wagombea na wanapenda kuwa viongozi wakati last born ni viongozi wa kuwasemea au kushabikia first born.

Watoto wengi wa kwanza kuzaliwa ni selfish, wachoyo, hawatoi vitu kirahisi bila maelezo ya kutosha, wakati wale wa mwisho ni easy, ni rahisi, hugawa ovyo si wachoyo ni watu wa to have fun.
Kumbuka kama unaoana na mtoto wa mwisho kuzaliwa hakikisha huweki matarajio makubwa sana kwani kwake ndoa ni jambo la kawaida tu naamini wale ambao tayari mpo kwenye ndoa mnafahamu hili kwani mmmeshakutana na maajabu ya kutosha.

Pia mimi ni mmoja ya watoto wa katikati (middle) hivyo sisi ni waasi (rebels) hatutaki tabia zenu ninyi watoto wa mwisho (don't care) na ninyi watoto wa kwanza kuzaliwa (controlling) Ndiyo maana tunajua kuboko cha mtoto wa mwisho kuzaliwa ni mtoto wa kwanza kuzaliwa ingawa mkioana na sisi watoto wa mwisho hatuna shida ndoa inaenda tu maana tunawajua sana.

Anyway ninyi watoto wa kwanza kuzaliwa ni muhimu sana kwetu maana bila ninyi ndoa zingekuwa za kizembe sana, na ninyi watoto wa mwisho ni muhimu sana maana bila nyingi ndoa haziwi na sherehe wala "to have fun", ila mmezidi yaani hata kumaliza kupaka nyumba rangi unalilia sherehe?
 
Mtoto wa mwisho kwa baba au kwa mama? Kuna wengine tunmezaliwa kwenye ndoa za 'mitala'?
 
umeongea jambo la msingi! Kuna rafiki yangu akitaka kumuajiri mtu yeyote huwa anapenda kuuliza kujua mwombaji ni mtoto wa ngapi katika family. Kuna correlation kati ya attitude na hicho ulichokizungumzia¬!
 
Mtoto wa kwanza na mtoto wa kwanza wakioana inakuwaje....kwa mfano wewe ni kwanza kwenu na yeye ni wa kwanza kwao??Same kwa wa mwisho....
 
it can be true , lakini upbringings r different, m sure there are many factors to determine a person rather than being a first or last born, ..... niimekubali hyo anyway,
 
Mtoto wa kwanza na mtoto wa kwanza wakioana inakuwaje....kwa mfano wewe ni kwanza kwenu na yeye ni wa kwanza kwao??Same kwa wa mwisho....

Mimi na mke wangu wote ni watoto wa kwanza. Ngoja nijaribu kutafakari nadharia hii ilivyotuinfluence.
 
Kuna jambo moja ambalo watu wengi hulichukulia mzaha, masihara au utani wakati wa kutafuta mwenzi wa maisha (mke au mume) nalo ni suala la mtoto wa kwanza kuzaliwa na mtoto wa mwisho kuzaliwa.

Swali la kujiuliza je, kuna matokeo yoyote au athari zozote kuoa au kuolewa na mtoto wa mwisho au kwanza kuzaliwa katika familia yao ?

Jibu la kweli ni NDIYO KUBWA,
Kuna athari kubwa kama ni kweli unayeoana naye ni mtu wa kwanza au wa mwisho kuzaliwa ingawa kuna exceptions.

Kama una mchumba ambaye kwao ni mtoto wa mwisho kuzaliwa jambo la msingi ambalo naweza kukushauri ni wewe kuwa tayari for adventures, na kama ni mtoto wa kwanza kuzaliwa basi jiandae kuwa audited kila kitu au kukaliwa au kuongozwa bila kujali ni mwanaume au mwanamke period.
Mtoto wa kwanza kuzaliwa kawaida hujikuta ni kiongozi mahali popote na hupenda kuongoza, kupenda kuhakikisha kila kitu kinaenda vizuri na kama kilivyopangwa maana ndivyo alikuwa anaagizwa na wazazi kwake kuhakikisha wadogo zake wanatii kile ameagizwa;

"Hakikisha wadogo zako wamekula, wametandika kitanda, waosha vyombo, wamefagia uwanja, wamelala mapema nk".

Mtoto wa mwisho kuzaliwa hujikuta ni mtoto hata akiwa mtu mzima kwa kuwa kwao bado ni mtoto na huwa hana shida na kitu chochote kwani kwake kila kitu ni rahisi na anapenda raha, sherehe na life is easy.
Kila kitu nyumbani kilikuwa ni kwa ajili yake kwa kuwa yeye ndiye mtoto hata baada ya kuwa mtu mzima bado anajiona ni mtoto Ndiyo maana huchelewa hata kuongea, kufanyia vitu mwenyewe kama vile kujua muda wa kula, sehemu ya kuweka nguo, kutandika kitanda, kuoga nk, yeye hujiona ni special kid, ni mtoto wa baba na mama na amekua wakati wazazi wamezoea maisha.
Kwa ujumla tabia za watoto wa kwanza kuzaliwa huwa ni kukaliwa wenzao (controlling, bossy, leading, perfectionist, auditors, no fun, firm and rigid) wengi ni viongozi na watoto wa mwisho kuzaliwa hujiona ni special kid, hujiona mtoto miaka yote, watu wa sherehe, don't care, easy wengi ni comedians.

Je, inakuwaje wakioana mtoto wa kwanza na mtoto wa mwisho kuzaliwa?
Kama mmoja ni wa kwanza kuzaliwa na mwingine ni wa mwisho kuzaliwa (au mmoja ana tabia ya mtoto wa kwanza kuzaliwa na mwingine tabia ya mtoto wa mwisho kuzaliwa basi ndoa itakuwa nzuri kwani tabia zitawafanya wa-balance.

Uzembe wa mtoto wa mwisho utakomeshwa na mtoto wa kwanza kuzaliwa ambaye hupenda kuongoza na kuhakikisha kila kitu kinakuwa sawa haijalishi ni mke au mume.
Hujasikia mwanamke analalamika kwamba mume wake hakustahili kuoa au kuishi na mke, maana yake ni mtoto wa mwisho na haijalishi amesoma au hajasoma watoto wa mwisho tabia hufanana.

Je, inakuwaje wakioana wote ni watoto wa mwisho au wote watoto wa kwanza kuzaliwa?
Ukweli ni kwamba match ya ndoa ya aina hii huwa inakera sana kwani kama wote ni watoto wa kwanza kuzaliwa kila mmoja atapenda kuwa kiongozi na sidhani kama hiyo meli haitazama. Na wakikutana wote watoto wa mwisho basi ni balaa kwani ndoa itakuwa haina kiongozi na itakuwa ni adventures.

Watoto wengi wa kwanza Ndiyo marais, wachungaji na viongozi mbalimbali na watoto wengi wa mwisho ni ma-MC na comedians.

Watoto wa kwanza kuzaliwa likija suala la sex wanachagua sana na kuwa na utaratibu ambao huchosha (routine sex), pia hufanya sex kama wakaguzi kama vile lazima kuoga kabla ya sex, taa zizimwe, kusiwe na mtu hajalala usingizi within 100m, piga mswaki, usiku tu tena baada ya saa tatu na si baada ya saa nne nk, ni usumbufu.

Bila watoto wa mwisho sherehe huwa hazinogi ingawa wao tatizo lao si kawaida yao kuwahi na kufika on time kwenye sherehe, ingawa watoto wa kwanza kwao ratiba ni muhimu.
Likija suala la siasa first born wengi ni wagombea na wanapenda kuwa viongozi wakati last born ni viongozi wa kuwasemea au kushabikia first born.

Watoto wengi wa kwanza kuzaliwa ni selfish, wachoyo, hawatoi vitu kirahisi bila maelezo ya kutosha, wakati wale wa mwisho ni easy, ni rahisi, hugawa ovyo si wachoyo ni watu wa to have fun.
Kumbuka kama unaoana na mtoto wa mwisho kuzaliwa hakikisha huweki matarajio makubwa sana kwani kwake ndoa ni jambo la kawaida tu naamini wale ambao tayari mpo kwenye ndoa mnafahamu hili kwani mmmeshakutana na maajabu ya kutosha.

Pia mimi ni mmoja ya watoto wa katikati (middle) hivyo sisi ni waasi (rebels) hatutaki tabia zenu ninyi watoto wa mwisho (don't care) na ninyi watoto wa kwanza kuzaliwa (controlling) Ndiyo maana tunajua kuboko cha mtoto wa mwisho kuzaliwa ni mtoto wa kwanza kuzaliwa ingawa mkioana na sisi watoto wa mwisho hatuna shida ndoa inaenda tu maana tunawajua sana.

Anyway ninyi watoto wa kwanza kuzaliwa ni muhimu sana kwetu maana bila ninyi ndoa zingekuwa za kizembe sana, na ninyi watoto wa mwisho ni muhimu sana maana bila nyingi ndoa haziwi na sherehe wala "to have fun", ila mmezidi yaani hata kumaliza kupaka nyumba rangi unalilia sherehe?


Ni nzuri but hapo nilipoweka rangi sio kuwa inategemea? Najaribu kufikiria kama mtoto wa kwanza kuzaliwa ni mwanamke na ameoana na mwanaume ambaye ni wa mwisho kuzaliwa..............wanaweza wasibalance kama mwanaume atakuwa na ile machoism kuwa yeye ndo kichwa cha familia.....si ataona mkewe kama anataka kumtawala??

Hii analysis yako imenifanya nijiulize mahusiano yanakuwaje kama wataoana mtoto wa kwanza (mwenye siblings) na mtoto wa pekee katika familia kwa maana ya kuwa (mwanaume pekee kwenye familia ya watoto wengi wa kike skadekezwa kiasi cha kuwa na tabia za mtoto wa mwisho je haiweziathiri ndoa hiyo bwana analizer??
 
nimefatilia hii makala yako,sio siri imetulia na si ajabu ikachukua 96%:smile-big:
 
vipi kuhusu mtoto ambaye yy ni wa kwanza na wa mwisho?
 
Duh, ukweli mtupu. Mimi ni firstborn kuna baadhi ya tabia hapo ninazo.
 
Kuna jambo moja ambalo watu wengi hulichukulia mzaha, masihara au utani wakati wa kutafuta mwenzi wa maisha (mke au mume) nalo ni suala la mtoto wa kwanza kuzaliwa na mtoto wa mwisho kuzaliwa.

Swali la kujiuliza je, kuna matokeo yoyote au athari zozote kuoa au kuolewa na mtoto wa mwisho au kwanza kuzaliwa katika familia yao ?

Jibu la kweli ni NDIYO KUBWA,
Kuna athari kubwa kama ni kweli unayeoana naye ni mtu wa kwanza au wa mwisho kuzaliwa ingawa kuna exceptions.
Noted
 
Yaweza kuwa na ukweli kiasi chake...Mi ni first born kwetu na mke wangu ni first born kwao lakini dah! mshikaji mpaka anatia huruma maana anapenda ku-audit mpaka nina kufuri ngapi zikiongezeka bila kuambiwa anakuwa mkali sana..:smile-big:
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom