Werema: Nilichoongea ni maoni yangu si msimamo wa serikali

Hatutaki Mwanasheria Mkuu wa Serikali MBUMBUMBU kama Werema.

Poti Mzima unakuwa MBUMBUMBU !

Shame on U Werema !
 
Afadhali ya mkapa huwa haongei ovyo, ili ukimuuliza juu ya ufisadi wakati wa utawala wake, Unyamaza tu,. Ukiuliza Kiwira, Yeye Mhuu, RADA- Mhuuu, Ndege Mbovu ya Rais Mhuu, Meremeta Mhuu. mwisho anaibuka na neno moja tu , kuwa yeye ni Kilimanjaro sie Kokoto, lakini Werema kupayuka kutamweka Pabaya, Ukiuliza EPA atakwambia kamuulize rais, Dowansi, Siwajui lakini sijui ni RA ambaye alipewa Nguvu za kisheria kutoka kwa Mkono sio serikali kuishitaki Tanesco ya TZ, Zanzibar haimo maana kwao umeme bei chee
 
Kwani aliulizwa kama Werema au AG? mbona kabla hujapewa wadhifa huo hakuna alokuwa akikufata kutaka maoni yako? ndio aina ya viongozi wetu wepesi kuruka kimanga hata kwa kauli zao na labda na majina yao waweza yakana siku moja nyie subirini tu.
 
Ndo maana Africa hatuendelei. Mtu tunayetarajia atusaidie na awe msitari wa mbele katika kuandaa katiba mpya, anaanza kusema haoni sababu ya kuibadili katiba iliyopo. Bado hata bosi wake anaposema kuna umuhimu wa kutoa katiba mpya, yeye anasema haoni sababu ya kujiuzulu. Hii ni akili au ni matope?

Wapo watu wengi kweli wanafaongoza wenzao kufanya kazi ambazo hata wenyewe hawazijui. Ninakumbuka siku moja tukiwa chuoni tukamwita dean wetu wa faculty. Tukamweleza kuwa hatufanyi practical na madarasani hamna viti. Alitujibu kuwa tujifunze kuzoea matatizo kwani hata yeye ni mwenyekiti wa bodi ya shule moja ya kata na wanafunzi wa hiyo shule wanakalia ndoo. Tulimzomea kweli huyo mama lakini hata hivyo tulimaliza chuo bila kufanya practical.

Kwa mfano huo Huyu Dean Werema na Kombani, wanajua kuwa watanzania waendelee na matatizo yaliyopo maadam wao wanapata Mshahara. Wakiulizwa tufanye mabadiliko gani watakuambia tulinganishe katiba yetu na ya DRC, Lyibia, Uganda tuone na wao wanafanyaje. Ukiwaambia kwa nini tusiandike ya kwetu wenyewe au tuchukuae ya kenya au ya Amerca watakuambia Kenya na Amerca ziko juu kiuchumi au hali ya hewa ya kule haifanani na ya hapa.

Umefikia wakati wa watanzania haswa Watanganyika kuanza kumkataa kila mtu aliyekabidhiwa madaraka akiwa bado mvivu wa kufikiri.

Hii imenikuna sana....
Africa ndio viongozi wetu hao...akili ni mbayuwayu...hata wakiongezewa zinazidi kupungua...

Unakumbuka pale Werema aliposema kuwa mtu anayehoji yeye kusema Katiba Mpya hapana ila viraka vinaruhusiwa, alitamka kuwa anayebisha au kuhoji kuhusu kauli yake hiyo hana fikra au hafikirii kwa umakini....! Na sasa anakuja na kusema yeye ni kama mwanafunzi aliyefeli darasani, je atafukuzwa? ukiunganisha haya utaelewa kuwa hatuna mtendaji hapo! Na inatia wasiwasi kutambua kuwa reasoning, judgment na logic alizokuwa anafanya huyu jamaa kama kweli alikuwa jaji, kama zilikuwa na uhakika au ukweli hata wa 30%..!

Mie kwa mtizamo wangu, ningechukua maamuzi yake aliyoyafanya wakati akiwa jaji, ningeya-classify kama null and void! Yamekosa hadhi na credibility kwani ni mtu aliyeonyesha kufeli kifikra. Halafu anasema hatojiuzulu? Hivi hawa watu wanatumikia taifa gani, na wanatumikia wananchi gani? au wakeshakula mshahara huenda kukoroma kusubiri kesho ije, aendelee kutavanga na mawazo mgando kuyumbisha uhai wa taifa??

Sembuse anapewa nafasi makini kama hii ya kumshauri rais kuhusu masuala yote ya kitaifa kuhusu sheria? Huu ni mzaha kwa dira ya taifa letu. This is really a dark continent with dark-hearted rullers.......(tunayaona haya pia ya Gbagbo...upofu na aibu)!
 
Werema umedhihirisha jinsi gani ulivyo kilaza, Mwanasheria huwa haongei bila utafiti wa kutosha unaropoka halafu unaanza ku -justify. Nonsense sijawahi kuuamini uwezo wako, sitakuamini asilan, we endelea na ufisadi ila fani ya sheria ishakushinda...
 
jamani m.sugu yuko wapi aje aseme MNAMKOSOA KWA AJILI YA DINI YAKE! Haya sasa unayesemaga eti wakristo hata wakifandya madudu hawakosolewi, 2nakosoa MTANZANIA KILAZA na sio MKRISTO KILAZA, nyambaf
 
Yeye kama amegundua kuwa alikosea ajuzulu tu mbona bado nafasi anayo? Jaji mzima ovyo!
 
Kwa mtizamo wangu huyu mwanasaria mkuu wa serikali ni kiazi kama aliyemteua.wakati wa kupitisha mswada wa gharama za uchaguzi alikua anahangaika sana kufafanua vufungu,kiingereza kwanza kinamsumbua sana
 
Serikali ya Dr.Kikwete ni kama kundi la kambale kwenye bwawa la tope. Wote wana sharubu, babu,bibi,baba,mama,watoto na wajukuu.... Hakuna chain of command. kila mtu anafyatuka kivyake.Mtoto wa mkulima kasema hivi, kesho Kombani naye anakuja na lake,Werema naye anatoa lake,Kesho tutamsikia Makamba naye akija na lake wakibanwa wanasema ni maoni yao tu.Si wakatoe maoni yao kwa wake zao nyumbani...
 
MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Frederick Werema ametetea kauli yake ya hivi karibuni iliyotaka Katiba iliyopo ifanyiwe marekebisho badala ya kuandikwa upya na kusema, yalikuwa ni maoni yake binafsi na si msimamo wa serikali.

Katika mazungumzo yake na gazeti hili Werema alisema, “sikuzungumza kwa kificho na kila mtu alinisikia nikitoa maoni yangu, sielewi ni kwa nini jambo hili linakuzwa, sasa hao wanaotaka nijiuzulu nao wajiulize, ina maana mwanafunzi akiwa wa mwisho kwenye mtihani darasani watamwambia ajiuzulu kusoma?

Kaogopa kibarua kuota majani hivi hivi, anatafuta sababu ya kuficha dharau zake wa watanzania.

Kiongozi lazima ujue nini unaongea, AU na JK akirudi kesho aseme yale yalikuwa maoni yake si msimamo wa serikali? Taifa linapelekwa wapi?

AG ni cheo kikubwa sana, sikutegemea kuona mzaha katika mambo ya msingi.

Je ile ya Dowans nayo ni maoni yake au msimamo wa Serikali?
 
unajua tatizo la vongozi wetu ni "bendera fata upepo"..,wanateuliwa kwa fadhila na utashi wa goigoi.,sishangai wakiwa na tabia za kindumilakuwili na wakiwa hawana maamuzi katika mambo yao.,wengi wao ni "figurehead"

nasikia huyo AG almanusura aanguke aliposikia katewa cheo icho..

mungu atunusuru na na hawa akina yuda iskarioti.!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Luteni said:
"sasa hao wanaotaka nijiuzulu nao wajiulize, ina maana mwanafunzi akiwa wa mwisho kwenye mtihani darasani watamwambia ajiuzulu kusoma?"
Ivi hawa waandishi wa habari wa kibongo wakoje? Yani AG anajifananisha na mwanafunzi afu haulizwi maswali?! Kujiuzulu kwa mwanafunzi aliekua wa mwisho ktk mtihani ni kuachishwa shule au kurudia darasa. Sasa taaata mura werema asubiri aidha kurudia darasa au kuachishwa masomo sasa.
 
hujui wajibu wako.........? kimtokacho mtu mdomoni ndicho kilicho moyoni. HUTUFAIIIIIIIIIIIII
 
MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Frederick Werema ametetea kauli yake ya hivi karibuni iliyotaka Katiba iliyopo ifanyiwe marekebisho badala ya kuandikwa upya na kusema, yalikuwa ni maoni yake binafsi na si msimamo wa serikali.

Katika mazungumzo yake na gazeti hili Werema alisema, “sikuzungumza kwa kificho na kila mtu alinisikia nikitoa maoni yangu, sielewi ni kwa nini jambo hili linakuzwa, sasa hao wanaotaka nijiuzulu nao wajiulize, ina maana mwanafunzi akiwa wa mwisho kwenye mtihani darasani watamwambia ajiuzulu kusoma?


Tulitakiwa tumkumbushe Mheshimiwa wetu yale aliyoyasema kwa gazeti la Mwananchi na akawa quoted “Mimi kama Mwanasheria Mkuu wa Serikali nimeisoma hukumu hiyo kwa makini na nimeridhika nayo kuwa iko sawa,” alisema Jaji Werema. Au labda mwandishi alimsikia vibaya?
 
Back
Top Bottom