Wenzetu wanaenda mbele, sisi tunarudi nyuma

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,219
40,451
Mtu mnafiki, mwongo, na ambaye hana uhuru wa mawazo huwa hagundui kitu chochote, akijitahidi ataishia kuiga na kukariri.

Moja ya sababu, wanasaikolojia wanasema kwa nchi ya China kutokufanya ugunduzi, na kuwa nchi ya copy and paste, ni wananchi wake kuelelewa katika mazingira yasiyoheshimu uhuru wa mtu.

Tanzania kuna wakati ilikuwa inaunganisha malori aina ya Scania, sasa hivi tumeishia kuunganisha pikipiki za China.

Kuna wakati tulikuwa tunaunganisha matrekta bora kabisa ya valmet, sahizi hatuunganishi hata power tiller.

Tulikuwa tunatengeneza baiskeli aina ya swala, baiskeli nzuri kabisa,sahizi hatutengenezi hata sindano ya cherehani.

Kuna wakati tulikuwa tunatengeneza matairi bora kabisa yakijulikana General Tyre, sahizi tumebakia kuwa watumiaji wa matairi ya hovyo kabisa kwa ubora kutoka China.

Kuna wakati tulikuwa tunatengeneza mashuka bora kabisa toka kiwanda cha Mutex, siku hizi tumebakia kuwa watumiaji wa mashuka ya hovyo kabisa, yapo kama vikaratasi, kutoka China.

Kuna wakati tulikuwa tunatengeneza viatu bora vya ngozi toka kiwanda cha Moro Shoes, siku hizi tumebakia kuwa wanunuzi wa viatu duni kabisa toka China, ukijikwaa tu kimechanika au kuraruka.

Tulikuwa tunatengeneza ndoo za ubora wa hali ya juu, Amboni Plastics, siku hizi tumebakia na ndoo takataka ukibebea tu maji, mshikio unachomoka au ndoo yenyewe kupasuka.

Wakati ule ilikuwa kipimo cha umaskini kwa mama ni kuvaa kanga iliyotengenezwa China au India, huku mwenye uwezo akivaa kanga ya Urafiki, leo hata ukiwa na hela, kanga nzuri huipati popote, kila mahali ni takataka za kutoka China.

Zamani, katika Afrika Mashariki, Tanzania ndiyo nchi angalao ilikuwa inaonekana kuwa na demokrasia, leo ndiyo nchi ya mfano kwa utawala usiozingatia sheria, usioheshimu mgawanyo wa mihimili. Tena imekuwa ni nchi ya kidikteta ambayo hata kura ya mwananchi haina maana yoyote katika kuwapata viongozi.

Kenya tuliokuwa tunawaona hawajastaarabika kwa kuendekeza siasa za ukabila, sasa ni nchi ya mfano Afrika Mashariki kwa kuheshimu utawala wa sheria, demokrasia, haki za watu, uhuru wa maoni, na katika kuheshimu mfumo wa siasa za vyama vingi.

Wakati wenzetu, kuendelea inamaanisha kuboresha, sisi kuendelea inamaanisha kuendeleza uharibifu. Tumekuwa Taifa bandia, taifa linaloongozwa kwa hadaa na ulaghai. Majukwaani wanatamka vingine, matendo yanakuwa kinyume. Wateule wamebakia kuumsifia anayewateua kwa unafiki. Kila mahali watasimama na kumsifia aliyewateua ili awaone na kuwasikia, wakiachia mic, wanamsema vibaya. Unafiki mtupu.

Watawala, hata pale ambapo mambo yanaenda vibaya, watakuambia kuwa sasa ndiyo tunapaa, wakati hata vyandarua vya mbu tunapewa msaada. Zamani, Serikali ilikuwa na watu wanapita mitaani kufanya fumigation kuua mbu na mende, leo tunashindwa hata kununua chanjo kwaajili ya watoto wetu wanaozaliwa.

Ni nani atalirudisha Taifa kutoka kwenye unafiki kulipeleka katika uhalisia? Nani ataweza kusimama na kusema kuwa Taifa letu ni duni katika nyanja nyingi, tusimame, turudi na kuanza upya?

Siku zote hatua ya kwanza kuleta mabadiliko chanya ni kuutambua na kuukubali udhaifu wako.
 
Mkuu yote hayo uliyoyaandika ni kweli na humu tumo tulioshuhudia neema hizo wakati huo
Miaka hiyo kulikuwa na meter za maji kila nyumba yenye uwezo wa kulipia maji, tulikuwa na landlines manyumbani na unaongea na operator anakuunganisha au unasikia mlio unapokea unaambiwa ni simu ya fulani

Maisha yote hayo na makampuni yote kulikuwa na kitu kimoja in common
Kulikuwa wizi hakuna kama wa leo

Na rushwa ilikuwa sio kubwa sana au hakuna kabisa sehemu nyingi

Nakumbuka wazee walikuwa wanajua haki zao kuliko vijana wa leo ambao neno lao ni moja tu kuiba sana na kuomba rushwa

Viongozi wa juu wakiwa waadilifu naapa hata wa chini watanyooka

Ila tatizo viongozi wengi ni waizi na wanahalalisha wizi kwa kuwahamisha toka sehemu moja kwenda nyingine kufukia mashimo

Hatutafika popote kama juu kumeoza
 
Hata upinzani tulikuwa na akina Christopher Kasanga Tumbo aliyeambiwa na Nyerere " niko tayari kukuteua kwa Cheo chochote sema unapenda kuwa nani" Kasanga Tumbo akamjibu " Nataka hicho Cheo chako cha Rais wa JMT"

Lakini Wapinzani wa Leo ndio hao akina Mbowe,, Zitto, Dr Slaa na Halima Mdee na wenzake wanaorambishwa asali Bila aibu!
 
Wachache watakuelewa, nchi yetu imekua na matatizo mengi kuliko masuluhisho. Kigezo cha kupata teuzi sio uwezo wa utendaji na weledi bali uchawa.

Laana ya kupenda kusifiwa kwa viongozi wetu imewatafuna kama canser na hakuna dawa. Utawasikia bila aibu ati "Anaupigwa mwingi" stupid a*ss hipocrites.
 
Mkuu yote hayo uliyoyaandika ni kweli na humu tumo tulioshuhudia neema hizo wakati huo
Miaka hiyo kulikuwa na meter za maji kila nyumba yenye uwezo wa kulipia maji, tulikuwa na landlines manyumbani na unaongea na operator anakuunganisha au unasikia mlio unapokea unaambiwa ni simu ya fulani

Maisha yote hayo na makampuni yote kulikuwa na kitu kimoja in common
Kulikuwa wizi hakuna kama wa leo

Na rushwa ilikuwa sio kubwa sana au hakuna kabisa sehemu nyingi

Nakumbuka wazee walikuwa wanajua haki zao kuliko vijana wa leo ambao neno lao ni moja tu kuiba sana na kuomba rushwa

Viongozi wa juu wakiwa waadilifu naapa hata wa chini watanyooka

Ila tatizo viongozi wengi ni waizi na wanahalalisha wizi kwa kuwahamisha toka sehemu moja kwenda nyingine kufukia mashimo

Hatutafika popote kama juu kumeoza
Nakuhakikisha, hawa viongozi wa sasa, si mawaziri, si maRC, si maafisa wa Polisi au jeshi, si majaji, si wakuu wa TAKUKURU wala TISS, hakuna mmoja wa kukataa rushwa. Wenfine hawakatai wakipewa, wengine mpaka wanadai.

Jamaa zangu waliopo kwenye business nchini, sasa hivi wanasema ukitaka shughuli zako ziende, wekeza kwenye kutenga hela kwaajili ya wakubwa, na siyo kwenye kufuata sheria. Fuata sheria zote, lakini kama huwapi hela utakwama tu.

Na hiyo naamini ni kweli kabisa. Jamaa yangu mmoja alikuwa anataka kuunganishiwa umeme kwenye project yake. Wakamwambia eti hapo ni mbali, ni mradi. Wakapiga mahesabu yao wakasema utahitajika kulipa 28m ukienda kwa utaratibu wa kawaida. Akaenda akaongea na mkubwa, akaacha 2m tu kwake, umeme umeungwa kwa 1.6m.
 
Nachojua china ni watengenezaji bora wa bidhaa duniani.
China hutengeneza bidhaa kutokana na soko la bidhaa hizoo.
Kwenye hilo wengi hawaujui ukweli:

China kuna makampuni zaidi ya 3,000 ya nchi za Magharibi. Wanatengenezea bidhaa zao China halafu bidhaa hizo wanazipeleka kwenye mataifa yao, na nyingine huuzwa nchini China (elite group ya Wachina hawataki kununua/kutumia bidhaa zilizotengenezwa na makampuni ya Wachina kwa sababu wanajua huwa ni hafifu). Hizo zinakuwa na ubora wa hali ya juu kwa sababu makampuni mama ya Magharibi husimamia. Makampuni haya yapo China lakini siyo ya Wachina.

Halafu kuna makampuni ya Wachina, yanamilikiwa na Wachina wenyewe. Hawa wanaiga zile bidhaa zinazotengenezwa na makampuni ya Magharibi, na haya bidhaa zao hazigusi masoko ya nchi za Magjaribi, zinaletwa Afrika kwa watu wasio na viwango vya ubora.
 
Mkuu yote hayo uliyoyaandika ni kweli na humu tumo tulioshuhudia neema hizo wakati huo
Miaka hiyo kulikuwa na meter za maji kila nyumba yenye uwezo wa kulipia maji, tulikuwa na landlines manyumbani na unaongea na operator anakuunganisha au unasikia mlio unapokea unaambiwa ni simu ya fulani

Maisha yote hayo na makampuni yote kulikuwa na kitu kimoja in common
Kulikuwa wizi hakuna kama wa leo

Na rushwa ilikuwa sio kubwa sana au hakuna kabisa sehemu nyingi

Nakumbuka wazee walikuwa wanajua haki zao kuliko vijana wa leo ambao neno lao ni moja tu kuiba sana na kuomba rushwa

Viongozi wa juu wakiwa waadilifu naapa hata wa chini watanyooka

Ila tatizo viongozi wengi ni waizi na wanahalalisha wizi kwa kuwahamisha toka sehemu moja kwenda nyingine kufukia mashimo

Hatutafika popote kama juu kumeoza
Wakati ule nauli ilikuwa sh 5, yaani sawa na dola 1. Kwa hiyo nauli ya mabasi ya mzunguko mjini ilikuwa dola moja. Neno hilo dola ndiyo lilizaa jina daladala wakimaanisha kila unakoenda unalipa dola moja. Watu walikuwa wakilipa na kuona ni hela ya kawaida. Leo waambie abiria kuwa nauli ya daladala ni sh 2,350; watatweza kutoa, au itakuwa ni malalamiko kila mahali?
 
Nakuhakikisha, hawa viongozi wa sasa, si mawaziri, si maRC, si maafisa wa Polisi au jeshi, si majaji, si wakuu wa TAKUKURU wala TISS, hakuna mmoja wa kukataa rushwa. Wenfine hawakatai wakipewa, wengine mpaka wanadai.

Jamaa zangu waliopo kwenye business nchini, sasa hivi wanasema ukitaka shughuli zako ziende, wekeza kwenye kutenga hela kwaajili ya wakubwa, na siyo kwenye kufuata sheria. Fuata sheria zote, lakini kama huwapi hela utakwama tu.

Na hiyo naamini ni kweli kabisa. Jamaa yangu mmoja alikuwa anataka kuunganishiwa umeme kwenye project yake. Wakamwambia eti hapo ni mbali, ni mradi. Wakapiga mahesabu yao wakasema utahitajika kulipa 28m ukienda kwa utaratibu wa kawaida. Akaenda akaongea na mkubwa, akaacha 2m tu kwake, umeme umeungwa kwa 1.6m.
Kwa sasa hivi hatutapiga hatua hata moja tena kwa jinsi watu walivyo waroho

Unakuta kila mmoja anataka kazi ili aibe
Sasa riziki unayopewa halafu unaomba rushwa halafu hela unalisha familia kwa hela za dhulma unategemea nini

Hizi hela zina laana na wanaokula ni mlolongo wa laana tu kwani ni nuksi
Cha ajabu kutwa PM anaita waandishi wa Habari na kuwakosoa wabadhirifu ila mwisho wa siku huoni la maana analofanya

Watu hawafungwi kwa sababu wote ni waizi
Mwizi hamfungi mwizi
 
Ila waafrika tunapokuwa tunajaribu kuelezea kwanini tupo nyuma kimaendeleo huwa kila mtu anaongea lake mbali kabisa na mwenzie tunachanganya mambo ambayo hayahusiani na kuwa kwetu nyuma kimaendeleo.
 
Mtu mnafiki, mwongo, na ambaye hana uhuru wa mawazo huwa hagundui kitu chochote, akijitahidi ataishia kuiga na kukariri.

Moja ya sababu, wanasaikolojia wanasema kwa nchi ya China kutokufanya ugunduzi, na kuwa nchi ya copy and paste, ni wananchi wake kuelelewa katika mazingira yasiyoheshimu uhuru wa mtu.

Tanzania kuna wakati ilikuwa inaunganisha malori aina ya Scania, sasa hivi tumeishia kuunganisha pikipiki za China.

Kuna wakati tulikuwa tunaunganisha matrekta bora kabisa ya valmet, sahizi hatuunganishi hata power tiller.

Tulikuwa tunatengeneza baiskeli aina ya swala, baiskeli nzuri kabisa,sahizi hatutengenezi hata sindano ya cherehani.

Kuna wakati tulikuwa tunatengeneza matairi bora kabisa yakijulikana General Tyre, sahizi tumebakia kuwa watumiaji wa matairi ya hovyo kabisa kwa ubora kutoka China.

Kuna wakati tulikuwa tunatengeneza mashuka bora kabisa toka kiwanda cha Mutex, siku hizi tumebakia kuwa watumiaji wa mashuka ya hovyo kabisa, yapo kama vikaratasi, kutoka China.

Kuna wakati tulikuwa tunatengeneza viatu bora vya ngozi toka kiwanda cha Moro Shoes, siku hizi tumebakia kuwa wanunuzi wa viatu duni kabisa toka China, ukijikwaa tu kimechanika au kuraruka.

Tulikuwa tunatengeneza ndoo za ubora wa hali ya juu, Amboni Plastics, siku hizi tumebakia na ndoo takataka ukibebea tu maji, mshikio unachomoka au ndoo yenyewe kupasuka.

Wakati ule ilikuwa kipimo cha umaskini kwa mama ni kuvaa kanga iliyotengenezwa China au India, huku mwenye uwezo akivaa kanga ya Urafiki, leo hata ukiwa na hela, kanga nzuri huipati popote, kila mahali ni takataka za kutoka China.

Zamani, katika Afrika Mashariki, Tanzania ndiyo nchi angalao ilikuwa inaonekana kuwa na demokrasia, leo ndiyo nchi ya mfano kwa utawala usiozingatia sheria, usioheshimu mgawanyo wa mihimili. Tena imekuwa ni nchi ya kidikteta ambayo hata kura ya mwananchi haina maana yoyote katika kuwapata viongozi.

Kenya tuliokuwa tunawaona hawajastaarabika kwa kuendekeza siasa za ukabila, sasa ni nchi ya mfano Afrika Mashariki kwa kuheshimu utawala wa sheria, demokrasia, haki za watu, uhuru wa maoni, na katika kuheshimu mfumo wa siasa za vyama vingi.

Wakati wenzetu, kuendelea inamaanisha kuboresha, sisi kuendelea inamaanisha kuendeleza uharibifu. Tumekuwa Taifa bandia, taifa linaloongozwa kwa hadaa na ulaghai. Majukwaani wanatamka vingine, matendo yanakuwa kinyume. Wateule wamebakia kuumsifia anayewateua kwa unafiki. Kila mahali watasimama na kumsifia aliyewateua ili awaone na kuwasikia, wakiachia mic, wanamsema vibaya. Unafiki mtupu.

Watawala, hata pale ambapo mambo yanaenda vibaya, watakuambia kuwa sasa ndiyo tunapaa, wakati hata vyandarua vya mbu tunapewa msaada. Zamani, Serikali ilikuwa na watu wanapita mitaani kufanya fumigation kuua mbu na mende, leo tunashindwa hata kununua chanjo kwaajili ya watoto wetu wanaozaliwa.

Ni nani atalirudisha Taifa kutoka kwenye unafiki kulipeleka katika uhalisia? Nani ataweza kusimama na kusema kuwa Taifa letu ni duni katika nyanja nyingi, tusimame, turudi na kuanza upya?

Siku zote hatua ya kwanza kuleta mabadiliko chanya ni kuutambua na kuukubali udhaifu wako.
Endelea kushangilia mama anaupiga mwingi kama kawaida yako
 
57 Reactions
Reply
Back
Top Bottom