Wenye umri mkubwa kama Mimi chukua ushauri huu

Matanga

JF-Expert Member
Nov 13, 2019
2,281
3,973
KUSTAAFU

1
. Siku moja utastaafu.
Hautakua ukienda kazini, hautakua na madaraka tena, hautakua na nguvu ya ushawishi, mzunguko wako wa pesa utapungua kabisa!
Chunguza/fuatilia tarehe yako ya kustaafu kwenye risiti yako ya malipo ya mshahara.

2. Tumia vizuri siku zako za likizo ya Mwaka.
Chochote utakachokifanya Likizo ndio utakachokifanya ukistaafu. Kama unatumia likizo kulala au kuangalia Luninga ndicho utakachokifanya ukistaafu. Tumia wakati wako wa ziada kujifunza kitu, kitakuja kuwa na manufaa ukistaafu.

3. Wekeza kwa ajili ya kustaafu kwako.
Watoto wako sio uwekezaji kwa ajili ya kustaafu kwako. Usiwategemee watoto, ndugu au marafiki kama benki yako. Utapoteza heshima na utu wako.

4. Tafuta shughuli unayoipenda/unayoifurahia wakati bado upo kazini ikuongozee katika kustaafu kwako mfano kufuga kuku au miliki duka pata ujuzi unaojiuza (sio vyeti visivyo na matumizi)

5. Utastaafia wapi?.
Jijengee nyumba. Usistaafu ukiwa bado unapanga nyumba.
Usigome kutoka kwenye nyumba ya serikali.

6. Ni nani watakua wategemezi wako?
⁸Wakati unastaafu watoto wako wanatakiwa wawe wamevuka miaka 18 na wanajitegemea wenyewe.

7. Usistaafu na ukaendelea kukaa katika jiji kubwa
Labda endapo unajimudu kweli kweli, kama utakuwa na vyanzo vya fedha hafifu na itakuwia vigumu. Ikiwezekana hamia mahali penye gharama ndogo za maisha ili pensheni yako ikusogeze mbali kidogo.

8. Miliki mali inayoweza kukodishika au inayoweza kubadilika na kuwa Fedha taslimu
Miliki hisa zinazokunufaisha

Panda Miti ya biashara mfano mirunda, mitiki, n.k. au fuga, lima mboga mboga ukiweza. Shughuli hizi zitakuingizia mapato pamoja na kukufanya uwe mwenye afya njema.

9. Ishi maisha ya kawaida (maisha yasio na makuu Kama hujajenga nyumba kijijini kwenu, usitumie pesa ya kustaafu kujenga, si busara kufanya hivyo labda kama utageuza kijiji makazi yako ya kudumu.

Tambua kwamba Wastaafu wengi wanakufa mapema kwasababu zifuatazo:-

1.Hawajajiandaa kiakili kustaafu.
2.Kukosa vipato.
3.Msongo wa mawazo.
4.Wanapatwa na shinikizo la juu la damu/kisukari kutokana na wasiwasi, uoga, n.k

MEZA YAKO PALE KAZINI SIO YA KUDUMU, JIPANGE KWA AJILI YA KUSTAAFU.
 
tatizo kwenye ajira wapo wazee wengi ambao wamefiikisha umri wa kustaafu lkn kwa sababu ya kutokuwa na vyeti vya kuzaliwa wakasogeza miaka mbele hivyo kuziba nafasi za vijana kuajiriwa.

ktk kipindi cha awamu ya 5 chini ya Hayati JPM alikusudia kuchunguza watumishi walio foji umri wa kustaafu.

Hata JPM alishangaa sana kuona kuna baadhi ya watumishi amekuwa akiwasikia tangu anasoma hadi alipo kuwa Rais bado walikuwa wanaendelea na ajira!

wazee wanaifia makazini kwa sababu ya miili na akili kuchoka!

wanaziba nafasi za vijana.

asilimia kubwa ya watumishi tayari wamepitiliza umri wa kustaafu na bado wapo makazini, jambo hili lili sababishwa na kutokuzingatia vyeti vya kuzaliwa wakati wa kuajiriwa miaka ya nyuma.

Vyeti vya kuzaliwa vilianza kuzingatiwa kwenye ajira miaka ya 2005s, kabla ya hapo watumishi walikuwa wanataja mwaka anao jisikia au kukisia tu, jambo hili limepelekea kuwa na mlundikano wa wastaafu wengi wakiwa bado makazini.

Mhe. Jenista mhagama na timu yake wanapaswa wafanye utafiti ktk jambo hili.
 
Nimestaafu 2018 two years before due date.

Namshukuru Mungu maana muda wangu wa kuamka ni ule ule nikiwa Mtumishi wa umma, muda wa kulala nimesogeza sana nalala kuanzia saa tano usiku.

Naamka saa 11 alfajiri, nafanya mazoezi, nafanya cleaning ya house ambayo nayo niliijenga ndogo ndogo ili nimudu kuisafisha, I clean myself.

Saa moja asubuhi nafungua ujasiriamali wangu, saa nne nakunywa chai na kwenda ku do clean outside na kuangalia maua, that time naachia kijana duka, najua ataiba kidogo but it doesn't matter.

Nakuwa bize so bize sina muda wa kupoteza even a second.

Natamani wastaafu wajitahidi kuwa bize, wasijipe muda wa kulala mchana.

Just do something uza hata barafu hata bisi will keep you alive.

......... Mamndenyi unaongea mno..... stop
 
Kustaafu ni mindset ya mtu; na kujiandaa na mabadiliko ya shughuli na nyakati ni mipango ya mtu mwenyewe pia.

Wengi tunaposema kustaafu ni kwa kuwazia mkataba wa ajira peke yake huku tukiacha kuuwazia umri na uwezo wa mtu kufanya vitu

Ndio maana Kuna watu wamestaafu kazi ya kuajiriwa at 40s wengine at 60s lakini wote wanafanya vitu vinavyofanana sasa

Mimi binafsi kila siku namwomba Mungu anipe uwezo wa kuendelea kufanya mambo mapya yanayoendana na nyakati za uhai wangu. Sababu naamini nitastaafu nikifa
 
KUSTAAFU

1
. Siku moja utastaafu.
Hautakua ukienda kazini, hautakua na madaraka tena, hautakua na nguvu ya ushawishi, mzunguko wako wa pesa utapungua kabisa!
Chunguza/fuatilia tarehe yako ya kustaafu kwenye risiti yako ya malipo ya mshahara.

2. Tumia vizuri siku zako za likizo ya Mwaka.
Chochote utakachokifanya Likizo ndio utakachokifanya ukistaafu.Kama unatumia likizo kulala au kuagalia Luninga ndicho utakachokifanya ukistaafu.Tumia wakati wako wa ziada kujifunza kitu, kitakuja kuwa na manufaa ukistaafu.

3. Wekeza kwa ajili ya kustaafu kwako.
Watoto wako sio uwekezaji kwa ajili ya kustaafu kwako. Usiwategemee watoto, ndugu, au marafiki kama benki yako. Utapoteza heshima na utu wako.

4.Tafuta shughuli unayoipenda/unayoifurahia wakati bado upo kazini ikuongozee katika kustaafu kwako mfano kufuga kuku au miliki duka pata ujuzi unaojiuza (sio vyeti visivyo na matumizi)

5.Utastaafia wapi?.
Jijengee nyumba. Usistaafu ukiwa bado unapanga nyumba.
Usigome kutoka kwenye nyumba ya serikali.

6.Ni nani watakua wategemezi wako?
⁸Wakati unastaafu watoto wako wanatakiwa wawe wamevuka miaka 18 na wanajitegemea wenyewe.

7.Usistaafu na ukaendelea kukaa katika jiji kubwa
labda endapo unajimudu kweli kweli, kama Utakua na vyanzo vya fedha hafifu na itakuwia vigumu. Ikiwezekana hamia mahali penye gharama ndogo za maisha ili pensheni yako ikusogeze mbali kidogo.

8.Miliki mali inayoweza kukodishika au inayoweza kubadilika na kuwa Fedha taslimu
Miliki hisa zinazokunufaisha,
Panda Miti ya biashara mfano mirunda, mitiki, n.k. au fuga, lima mboga mboga ukiweza. Shughuli hizi zitakuingizia mapato pamoja nakukufanya uwe mwenye afya njema.

9.Ishi maisha ya kawaida (maisha yasio na makuu Kama hujajenga nyumba kijijini kwenu, usitumie pesa ya kustaafu kujenga, si busara kufanya hivyo labda kama utageuza kijiji makazi yako ya kudumu.

Tambua kwamba Wastaafu wengi wanakufa mapema kwasababu zifuatazo:-

1.Hawajajiandaa kiakili kustaafu.
2.Kukosa vipato.
3.Msongo wa mawazo.
4.Wanapatwa na shinikizo la juu la damu/kisukari kutokana na wasiwasi, uoga, n.k

MEZA YAKO PALE KAZINI SIO YA KUDUMU, JIPANGE KWA AJILI YA KUSTAAFU.
huwa sipendi kupasua kichwa changu kuwazia maisha yangu ya mbeleni.

naishi kwa nyakati zilizopo. kuzeeka ni majaliwa. unaweza usifike umri wa uzee.

wakati unapanga hayo yote, Kifo naye anapanga kukuchukua miezi michache ijayo.


giphy.gif
 
Nimestaafu 2018 two years before due date.

Namshukuru Mungu maana muda wangu wa kuamka ni ule ule nikiwa Mtumishi wa umma, muda wa kulala nimesogeza sana nalala kuanzia saa tano usiku.

Naamka saa 11 alfajiri, nafanya mazoezi, nafanya cleaning ya house ambayo nayo niliijenga ndogo ndogo ili nimudu kuisafisha, I clean myself.

Saa moja asubuhi nafungua ujasiriamali wangu, saa nne nakunywa chai na kwenda ku do clean outside na kuangalia maua, that time naachia kijana duka, najua ataiba kidogo but it doesn't matter.

Nakuwa bize so bize sina muda wa kupoteza even a second.

Natamani wastaafu wajitahidi kuwa bize, wasijipe muda wa kulala mchana.

Just do something uza hata barafu hata bisi will keep you alive.

......... Mamndenyi unaongea mno..... stop
Hongera mamndenyi! Kustaafu kunawafanya walio wengi kupata depression na hatimae kufa.

Nimependa dondoo namba tatu.
 
Nimestaafu 2018 two years before due date.

Namshukuru Mungu maana muda wangu wa kuamka ni ule ule nikiwa Mtumishi wa umma, muda wa kulala nimesogeza sana nalala kuanzia saa tano usiku.

Naamka saa 11 alfajiri, nafanya mazoezi, nafanya cleaning ya house ambayo nayo niliijenga ndogo ndogo ili nimudu kuisafisha, I clean myself.

Saa moja asubuhi nafungua ujasiriamali wangu, saa nne nakunywa chai na kwenda ku do clean outside na kuangalia maua, that time naachia kijana duka, najua ataiba kidogo but it doesn't matter.

Nakuwa bize so bize sina muda wa kupoteza even a second.

Natamani wastaafu wajitahidi kuwa bize, wasijipe muda wa kulala mchana.

Just do something uza hata barafu hata bisi will keep you alive.

......... Mamndenyi unaongea mno..... stop
Vp haujawa mchawi bado......
au kwenye hili huna comment
 
Kustaafu ni mindset ya mtu; na kujiandaa na mabadiliko ya shughuli na nyakati ni mipango ya mtu mwenyewe pia.

Wengi tunaposema kustaafu ni kwa kuwazia mkataba wa ajira peke yake huku tukiacha kuuwazia umri na uwezo wa mtu kufanya vitu

Ndio maana Kuna watu wamestaafu kazi ya kuajiriwa at 40s wengine at 60s lakini wote wanafanya vitu vinavyofanana sasa

Mimi binafsi kila siku namwomba Mungu anipe uwezo wa kuendelea kufanya mambo mapya yanayoendana na nyakati za uhai wangu. Sababu naamini nitastaafu nikifa
Uko sahii
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom