Wenye uchu walipotosha Azimio la Z'bar - Msuya

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797
[h=3][/h]

Heckton Chuwa na Flora Temba, Moshi

WAZIRI Mkuu mstaafu, Bw. Cleopa Msuya, amesema serikali haikulifuta Azimio la Arusha na kubadilishana na lile la Zanzibar, bali hayo ni mawazo ya wachache waliokuwa na
tamaa ya kunyakua mali ya umma.

Bw. Msuya alitoa kauli hiyo juzi wakati wa mahafali ya kumi ya Kidato cha Nne ya Shule ya Sekondari ya Mt. Maria Goreti ya mjini Moshi, mkoani Kilimanjarokwa mujibu wa Katiba ya Tanzania na kusisitiza kuwa, siasa ya Tanzania bado ni ya Ujamaa na Kujitegemea.

“Mimi nilikuwa kwenye kile kikao cha Zanzibar, tulichokubaliana kuwa kulingana na mabadiliko yaliyokuwepo wakati huo, mtu akiweza kujiingizia kipato kwa njia ya halali afanye hivyo ili mradi azingatie maadili mema na sio kuliua Azimio la Arusha”, alisema.

Alisema lengo lilikuwa ni kupotosha wale waliokuwa na tafsiri mbaya kuhusu Azimio la Arusha kwa kuwa ilifikia wakati mtu akifuga kuku ishirini, thelatini au hata mia moja ni sawa lakini akiwa na kuku zaidi ya mia mbili tena wa halali anaitwa kabaila jambo ambali alisema ilikuwa ni tafsri potofu ya Azimio la Arusha.

“Lakini wachache wenye uchu wa kunyakua mali ya umma wakaanza kufanya hivyo kwa kisingizio cha kikao kile cha Zanzibar huku wakitafsiri maazimio ya kikao kile visivyo ili kuhalalisha tamaa zao”, alisema.

Aliongeza: “Wananchi watashinda vita dhidi ya ufisadi kuwa bado wanalitaka Azimio la Arusha na ndio maana mnaona kwenye vyombo vya habari kila siku watu wakipambana na wavamizi wa ardhi na mali nyingine za umma”.

Kuhusu dhana kuwa Watanzania wanaogopa Shirikisho la Afrika Mashariki, Bw. Msuya alisema dhana hiyo si kweli na kwamba ukweli ni kwamba watanzania wanafuatilia suala hilo kwa umakini kutokana na hadhi na heshima ya Tanzania kimataifa.

“Sisi hatuogopi shirikisho bali tunachukua tahadhari na umakini mkubwa, lengo letu ni kuwa maamuzi yetu yasije kutuunganisha na matatizo ya wengine”, alisema.

Alisema kuwa kuna baadhi ya wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ambao bado hali zao kiusalama bado si nzuri na ndio sababu ya hadhari ya Tanzania na kwamba si vyema Tanzania ikaacha utaifa wake na kujiunga shirikisho bila ya kuwa na hadhari juu ya hali yake ya baadaye.

“Ushauri wangu ni kwamba tuimarishe eneo la biashara kwanza miongoni mwa mataifa yetu ya Afrika Mashariki na ndipo tufikirie ushirikiano wa kisiasa”, alisema.
 
Sehemu ya Hotuba ya Mwenyekitu wa CCM, Rais Alo Hassan Mwinyi wakati akizungumza na wazee wa Chama, Viongozi wa Taifa,
Mashirika ya UMMA na watu binafsi juu ya ufafanuzi wa maamuzi ya Halmashauri kuu ya Taifa katika kikao chake cha Zanzibar:
Diamond Jubilee Dar es Salaam, Tarehe 25/2/1991
Inasomeka hivi:

Mfano kuna mwananchi mmoja alikwenda kwenye kiwanda cha Umma kutaka huduma ya kusafishiwa ngozi zake. Alipofika hapo alikuta "pamelala paka" Yaani palikuwa kimya, hapakuwa na kazi yoyote inayofanyika. Kumbe kile kiwanda kilikuwa kimefungwa kwa kukosekana fedha za kukiendeshea ........... umeme ulikatwa na wafanyakazi walipewa likizo.

Meneja alimfahamisha huyo mteja kuwa kiwanda kimefungwa kwa sababu ya deni la maji na umeme pamoja na pesa za mishahara ya wafanyakazi. Huyo mteja alikubali kulipa arubuni (advance ) ya milioni saba ili kukikwamua kiwanda. Wiki ya pili yake kiwanda kilianza kufanya kazi zake za kuzalisha kama kawaida.

Kisa cha kiwanda hicho kusimama kazi ni kukosa fedha za kuendeshea. Kiswahili cha siku hizi huitwa ukwasi. Kwa hiyo kazi ilisimama.

Katika hali kama hii, tumeona ni vyema kuwaruhusu wananchi wote pamoja na wakulima, na wafanyakazi wa shirika lenyewe wakiwemo wanachama wa CCM kununua hisa chache kwa kila atakaetaka

Swali
Mfanyabiashara huyu wa Ngozi ni nani zaidi ya Rostamu???
 
Sehemu ya Hotuba ya Mwenyekitu wa CCM, Rais Alo Hassan Mwinyi wakati akizungumza na wazee wa Chama, Viongozi wa Taifa,
Mashirika ya UMMA na watu binafsi juu ya ufafanuzi wa maamuzi ya Halmashauri kuu ya Taifa katika kikao chake cha Zanzibar:
Diamond Jubilee Dar es Salaam, Tarehe 25/2/1991
Inasomeka hivi:

Mfano kuna mwananchi mmoja alikwenda kwenye kiwanda cha Umma kutaka huduma ya kusafishiwa ngozi zake. Alipofika hapo alikuta “pamelala paka” Yaani palikuwa kimya, hapakuwa na kazi yoyote inayofanyika. Kumbe kile kiwanda kilikuwa kimefungwa kwa kukosekana fedha za kukiendeshea ........... umeme ulikatwa na wafanyakazi walipewa likizo.

Meneja alimfahamisha huyo mteja kuwa kiwanda kimefungwa kwa sababu ya deni la maji na umeme pamoja na pesa za mishahara ya wafanyakazi. Huyo mteja alikubali kulipa arubuni (advance ) ya milioni saba ili kukikwamua kiwanda. Wiki ya pili yake kiwanda kilianza kufanya kazi zake za kuzalisha kama kawaida.

Kisa cha kiwanda hicho kusimama kazi ni kukosa fedha za kuendeshea. Kiswahili cha siku hizi huitwa ukwasi. Kwa hiyo kazi ilisimama.

Katika hali kama hii, tumeona ni vyema kuwaruhusu wananchi wote pamoja na wakulima, na wafanyakazi wa shirika lenyewe wakiwemo wanachama wa CCM kununua hisa chache kwa kila atakaetaka

Swali
Mfanyabiashara huyu wa Ngozi ni nani zaidi ya Rostamu???

Taifa kwanza wewe ni kichwa kwa kweli,si mwingine ndo huyo.Ufisadi haukuanza leo,haya mambo yalianzia kwa Mwinyi.
 
Sasa Huo Ukwasi Umetufikisha Wapi? Umezidisha Ulafi kwa Viongozi Wetu
 
Azimio la Arusha mwisho wake ulikuwa CHUMBE. Halikufika Zanzibar.

Hongera Karume 1
 
Mzee Msuya, wenye vipato halali siyo matajiri wa mali. Ukiwa tajiri hasa wa mali, ni hekaheka mtindo mmoja.
 
heckton chuwa na flora temba, moshi

waziri mkuu mstaafu, bw. Cleopa msuya, amesema serikali haikulifuta azimio la arusha na kubadilishana na lile la zanzibar, bali hayo ni mawazo ya wachache waliokuwa na
tamaa ya kunyakua mali ya umma.

Bw. Msuya alitoa kauli hiyo juzi wakati wa mahafali ya kumi ya kidato cha nne ya shule ya sekondari ya mt. Maria goreti ya mjini moshi, mkoani kilimanjarokwa mujibu wa katiba ya tanzania na kusisitiza kuwa, siasa ya tanzania bado ni ya ujamaa na kujitegemea.

“mimi nilikuwa kwenye kile kikao cha zanzibar, tulichokubaliana kuwa kulingana na mabadiliko yaliyokuwepo wakati huo, mtu akiweza kujiingizia kipato kwa njia ya halali afanye hivyo ili mradi azingatie maadili mema na sio kuliua azimio la arusha”, alisema.

Alisema lengo lilikuwa ni kupotosha wale waliokuwa na tafsiri mbaya kuhusu azimio la arusha kwa kuwa ilifikia wakati mtu akifuga kuku ishirini, thelatini au hata mia moja ni sawa lakini akiwa na kuku zaidi ya mia mbili tena wa halali anaitwa kabaila jambo ambali alisema ilikuwa ni tafsri potofu ya azimio la arusha.

“lakini wachache wenye uchu wa kunyakua mali ya umma wakaanza kufanya hivyo kwa kisingizio cha kikao kile cha zanzibar huku wakitafsiri maazimio ya kikao kile visivyo ili kuhalalisha tamaa zao”, alisema.

Aliongeza: “wananchi watashinda vita dhidi ya ufisadi kuwa bado wanalitaka azimio la arusha na ndio maana mnaona kwenye vyombo vya habari kila siku watu wakipambana na wavamizi wa ardhi na mali nyingine za umma”.

Kuhusu dhana kuwa watanzania wanaogopa shirikisho la afrika mashariki, bw. Msuya alisema dhana hiyo si kweli na kwamba ukweli ni kwamba watanzania wanafuatilia suala hilo kwa umakini kutokana na hadhi na heshima ya tanzania kimataifa.

“sisi hatuogopi shirikisho bali tunachukua tahadhari na umakini mkubwa, lengo letu ni kuwa maamuzi yetu yasije kutuunganisha na matatizo ya wengine”, alisema.

Alisema kuwa kuna baadhi ya wanachama wa jumuiya ya afrika mashariki ambao bado hali zao kiusalama bado si nzuri na ndio sababu ya hadhari ya tanzania na kwamba si vyema tanzania ikaacha utaifa wake na kujiunga shirikisho bila ya kuwa na hadhari juu ya hali yake ya baadaye.

“ushauri wangu ni kwamba tuimarishe eneo la biashara kwanza miongoni mwa mataifa yetu ya afrika mashariki na ndipo tufikirie ushirikiano wa kisiasa”, alisema.

kama kawaida ya viongozi hawa wakiwa hasa kwenye power hawasemi kitu leo upo nje and you are no more effective ndio unapiga kelele wakati ulikuwa waziri mkuu ungeweza kufanya mengi kubadilisha hali hiyo swali langu kwako wewe kama msuya ulichukua jitihada gani wakati ulipokuwa na uwezo wa kufanya hivyo kubadilisha hali hiyo ???
 
"Wananchi watashinda vita dhidi ya ufisadi kuwa bado wanalitaka Azimio la Arusha na ndio maana mnaona kwenye vyombo vya habari kila siku watu wakipambana na wavamizi wa ardhi na mali nyingine za umma".

It is long time now since such remarks could be heard from a former Nyerereian like Msuya. Many, including those who were long time Nyerere's political confidants like Kingunge, Mwinyi, Mkapa, to the incumbent Kikwete have since fallen off and have turned to be hegemonous bourgeoisie. The Arusha declaration, the declaration of humanity that CCM stalwarts celebrated its demise decades ago to pave way for their capitalistic ego is still spiritually alive in the hearts of many Tanzanians. The Tanzanian proletariat will eventually win the silent fight against the capitalists who have infected the york of the engine of our beloved humanistic declaration (CCM). The enemies of our beloved "Azimio" will perish and Tanzania will eventually regain its glorious past, this time not through the old, defunct and dilapidated CCM, but another movement that I believe will soon emerge to rekindle our lost hope.
 
Ndiyo maana tunafundishwa siku zote kuwa uongozi ni wito, na mtu hatafuti utajiri kwa kupitia uongozi, ingawa utajiri unaweza kumfuata mtu akiwa kiongozi kulingana na taratibu za nchi husikia, kama ilivyo kwa Malkia wa Uingereza

Tanzania iliyoundwa kuanzia awamu ya pili hadi leo ni ile ya viongozi kutafuta utajiri. Mzee Ruksa alitengeneza matajiri wengi sana waliokuwa watumishi ndani ya serikali yake, na hadi leo kuna viongozi wengi sana wanaojijengea utajiri kutokana na nafasi zao serikalini. Hiyo iliwezekana tu kutokana na Azimioa la Zanzibar. Inawezekana Mwinyi mwenyewe hakujua madhara ya tamko lake lile kwa vile hakuwa amelichambua kwa kina, na hiyo ndiyo inayomwekea doa kubwa sana katika rekodi yake ingawa sera yake ya ruksa imeendelea kuwa maarufu kwa upande mwingine na kusababisha taifa tulilo nalo leo lisiwe na order ya kibishara bali MONEY SPEAKS.
 
Narudia!.....mtu yoyote mwenye azimio la Zanzibar naomba anionyeshe au aniambie ni maktaba gani nitalipata hilo azimio,au website gani?...was it official?..how?
 
Narudia!.....mtu yoyote mwenye azimio la Zanzibar naomba anionyeshe au aniambie ni maktaba gani nitalipata hilo azimio,au website gani?...was it official?..how?

Kwa nini walichojadili Zanzibar walikifanya siri. Nani aliwakataza kukiandika kwa kukweka vitabuni tukisome.
 
Duh mkuu mbona unafanya uvivu kutafuta? haya Bofya
Mkuu mimi nakuheshimu sana, naomba tusileteane mambo ya kihuni. Lile si azimio, si official declaration of anything. Uliyonielekeza ni makala ya mtu wa kawaida tu kama mimi.
Kwa heshima na taadhima naomba nilione azimio la Zanzibar mnalolizungumzia!..liko wapi?
 
Mkuu mimi nakuheshimu sana, naomba tusileteane mambo ya kihuni. Lile si azimio, si official declaration of anything. Uliyonielekeza ni makala ya mtu wa kawaida tu kama mimi.
Kwa heshima na taadhima naomba nilione azimio la Zanzibar mnalolizungumzia!..liko wapi?


Hutaweza kulipata kwani limefanywa SIRI kama mkataba wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
 
Hutaweza kulipata kwani limefanywa SIRI kama mkataba wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Angalau articles of Union zipo wazi(but I really don't care about Zanzibar).Naomba hilo azimio linyeshwe au watu waache kulizungumzia....ni uwongo uliokithiri.
La Arusha lipo, la Zanzibar lipo wapi?
 
Mkuu mimi nakuheshimu sana, naomba tusileteane mambo ya kihuni. Lile si azimio, si official declaration of anything. Uliyonielekeza ni makala ya mtu wa kawaida tu kama mimi.
Kwa heshima na taadhima naomba nilione azimio la Zanzibar mnalolizungumzia!..liko wapi?
Mbona mkali hivyo! mkuu nimepitia haraka Google nikaona hiyo kama haikupeleki kwenye Azimio la Zanzibar basi haijawa tatizo naomba isome hotuba ya Mwinyi hapa au bado ni uhuni?..Bofya
 
Inasikitisha kuona wengi wenu muna ng'ang'ania siasa ya ujamaa wakati mwenyewe muasisi Julius K. Nyere alikiri kuwa amefeli baada ya jaribio la miaka 25 ya siasa hizo. Kwani kuna kosa gani Rostam kukiinua kiwanda ili walalahoi wapate ajira. ?. Acheni siasa za kumalizana. Rostam ni mwananchi kama wewe na mimi. Ana haki kuwa mmiliki kama yeyote yule. Alilokuwa amefanya kosa ni kutuzidi akili?. Mwacheni mfadhili mkuu aendelee na maisha yake.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom