Wenye nia ya kumsaidia mtoto Charles Mbena wakumbuke bado ni mtoto anahitaji malezi ya wazazi wake

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,595
215,272
Nimeangalia video za mtoto Charles Mbena, Tumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kujalia maarifa ya ziada. Mtoto wa miaka sita kumudu hesabu za kutoa na kujumlisha kwa kiwango cha Charles ni kusema Jina na Mungu lihimidiee.

Kuna taasisi zilizojitokeza kumsaidia Charles, nimemuona mpaka RAS amefika shuleni kwa Charles. Katika misaada yote sijaona msaada unaojumlisha wazazi wa Charles. Charles ni mtoto wa miaka sita, anahitaji upendo na malezi ya wazazi wake waliomlea mpaka leo anaonekana alivyo.

Kumpeleka shule ya boda au kumtenga na wazazi wake ni kumnyima mapenzi ya wazazi anayostahili. Ikiwezekana, baba wa Charles arafutiwe ajira karibu na shule atakayosoma mtoto wake na jamii iendelee kuisaidia familia ili iweze kulea watoto wao akiwemo Charles.
 
Huyo mtoto Wana my overate sana, sijaona kipaji alichonacho wala u jiniaz alionao zaidi ya kukakariri

By the way mtoto wa miaka sita anakuaje chekechea, halafu hajui kuandika, hiyo ni kiki kama kiki nyingine tu.
Tuseme kama bahati yake tu. Vijana wanasema zali la mentali.

Najua kuna wakali zaidi yake tena wana umri mdogo zaidi yake lakini tufanye dogo ndio kabahatika. Tena ukimuangalia tu maisha yake inaonekana magumu, na ile shule dah.

Sema kurudi kwenye mada, naona pale msaada ungewagusa kuanzia wazazi, na walimu pamoja na wanafunzi wenzake. Yaani ata wangeboresha tu mazingira ya shule, na kuwaongezea vitabu/vifaa vya kusomea na kujifundishia.
 
Dogo anaakili yule nimemfuatilia wanavyo muhoji yupo smart sana, kuna swali aliulizwa unamjua Rais akamtaja vyema tu,akaulizwa ukimuona utamuambia nini akajibu nitamsalimia, akulizaa alafu utamwambia nini. Akajibu hana cha kumuambia, na ni kweli mfano wewe ungekutana na rais bu bah ungemwambia nini.

Hesabu anajua mwanzo nilidhani amekaririshwa kumbe hapana aliulizwa mahesBu mengi tu tofauti
 
Tuseme kama bahati yake tu. Vijana wanasema zali la mentali.

Najua kuna wakali zaidi yake tena wana umri mdogo zaidi yake lakini tufanye dogo ndio kabahatika. Tena ukimuangalia tu maisha yake inaonekana magumu, na ile shule dah.

Sema kurudi kwenye mada, naona pale msaada ungewagusa kuanzia wazazi, na walimu pamoja na wanafunzi wenzake. Yaani ata wangeboresha tu mazingira ya shule, na kuwaongezea vitabu/vifaa vya kusomea na kujifundishia.
Naweza kukunga mkono kwa ilo maana kuna katoto nako ni 6yers cha kike ila anaimba nyimbo zote za bongo fleva zinazotrend tena na mistari kwa usahihi kabisa muda wote utamkuta anaimba ,alafu muda mwingi utamkuta peke ake humkuti kucheza na wenzake ye ni kuimba tu na kusikiliza nyimbo
 
Huyo mtoto Wana my overate sana, sijaona kipaji alichonacho wala u jiniaz alionao zaidi ya kukakariri

By the way mtoto wa miaka sita anakuaje chekechea, halafu hajui kuandika, hiyo ni kiki kama kiki nyingine tu.
Unanikumbushia ule usemi wa madingi yetu,
Nilifeli kwa sababu ya umbali wa shule na kazi za nyumbani.. Au mie ningekuwa enzi hizi ningekuwa msomi zaidi ya mkuu wa chuo!
Dogo ana uwezo kiasi cha ziada
 
Naweza kukunga mkono kwa ilo maana kuna katoto nako ni 6yers cha kike ila anaimba nyimbo zote za bongo fleva zinazotrend tena na mistari kwa usahihi kabisa muda wote utamkuta anaimba ,alafu muda mwingi utamkuta peke ake humkuti kucheza na wenzake ye ni kuimba tu na kusikiliza nyimbo
Uyo ni zuchu wa kesho yeye atakuja kuimba asali
 
Huyo mtoto Wana my overate sana, sijaona kipaji alichonacho wala u jiniaz alionao zaidi ya kukakariri

By the way mtoto wa miaka sita anakuaje chekechea, halafu hajui kuandika, hiyo ni kiki kama kiki nyingine tu.
Sasa mkuu na wewe ume overlook,mtu unawezaje kukariri hesabu au umesikia alikuwa anaulizwa maswali ya kwenye table ya 1 mpaka 25.
 
Watanzania wengi ni mamburulula sana hushabikia shabikia tu mambo bila kuchimbua undani wake.
Ifahamike kwamba IQ hupimwa kwa vigezo na wataalamu mahususi.
Je tunafahamu mtoto wa miaka sita anatakiwa aweze nini?
Je tunafahamu kuwa mtoto wa miaka sita anatakiwa ashindwe nini?
Je tumewahi kujiuliza kuwa mambo wanayofundishwa darasa la kwanza na la pili yanaendana na umri unaokubalika kimataifa?
Je wataalamu wa kupima iq wamehusika katika kumpima huyo mtoto na kuthibitisha uwezo wake?
Ndugu wana JF kumpata exceptional child is not easy as we think,multiple activities must be involved like arithmatic activies,verbal activities,geometrical parten, shape arrangement nk.Mtoto amefanyiwa addition and substruction tu bado kuna kuzidisha,kugawanya,bado mpangilio, misamiati ,memory activities na mengine mengi tu.
Mtoto anauwezo mkubwa kulinganisha na wale aliokuwa anasoma na sio wale wa umri wake. Tanzania nzima au morogoro nzima. Geneus ni msamiati wa tofauti sana tusiuchukulie kiurahisi.
 
Naweza kukunga mkono kwa ilo maana kuna katoto nako ni 6yers cha kike ila anaimba nyimbo zote za bongo fleva zinazotrend tena na mistari kwa usahihi kabisa muda wote utamkuta anaimba ,alafu muda mwingi utamkuta peke ake humkuti kucheza na wenzake ye ni kuimba tu na kusikiliza nyimbo
Maajabu utakuta darasani hakaelewi chochote
 
Enzi zangu six years najua hadi kugawanya, sema utofauti wetu upande wangu my mum aliplay part kubwa sana. Nimejua kusoma na hesabu kabla sijaanza shule.

Sent from my Infinix X623 using JamiiForums mobile app
 
Ni kweli inabidi dogo asaidiwe sawa ila asitengwe sana na wazazi wake. Waisaidie familia nzima hiyo bond ya wazazi na huyo dogo ndiyo inayofanya anakua genius.

Ila Nimemtamania huyo mtoto! Maana nna mdogo wangu of the same age ila yeye achojua ni makelele na ugomvi na wenzake😀😀 darasani mmh
 
Dogo anaakili yule nimemfuatilia wanavyo muhoji yupo smart sana, kuna swali aliulizwa unamjua Rais akamtaja vyema tu,akaulizwa ukimuona utamuambia nini akajibu nitamsalimia, akulizaa alafu utamwambia nini. Akajibu hana cha kumuambia, na ni kweli mfano wewe ungekutana na rais bu bah ungemwambia nini.

Hesabu anajua mwanzo nilidhani amekaririshwa kumbe hapana aliulizwa mahesBu mengi tu tofauti
Yes Yuko vizuri
 
Back
Top Bottom