Wenye mamlaka ya kituo cha basi cha SIMU 2000, TANROADS na SUMATRA chagueni jibu lenu sahihi hapa

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,464
108,619
Leo nitawaomba tu mniache niteme " nyongo " kwani hasira niliyo nayo hata mkinipa " Kichuri " haitapungua.

Kuna Watu nadhani wamepewa dhamana ya kuwajibika ipasavyo kwa Wananchi lakini kwa hakika wanachokifanya au kutufanyia nadhani hata Shetani hawezi kutufanyia japo anatutawala " kimtindo ".
Haiwezekani kabisa barabara ambayo imeharibika vibaya sasa inakaribia hata mwaka lakini Wahusika wakuu wamenyamaza tu na wala hawachukui hatua yoyote ya basi hata tu kuirekebisha kidogo huku wakijipanga kwa matengenezo kamili.

KERO iliyopo sasa katika ile barabara ya kuelekea Kituo cha Mabasi kipya cha SIMU 2000 ama hakika haivumiliki. Magari ya Watu hasa " Madaladala " kila kukicha yanaharibika pale huku foleni zisizo na miguu wala kichwa zikitokea kila mara hadi kutusababishia sisi Watumiaji usumbufu mkubwa sana.

Hivi inachukua muda gani au gharama ipi kuamua tu kuitengeneza? Nimeyaweka hapo Makundi matatu Wenye Mamlaka na Kituo, Watu wa TANROADS na hawa wadau wengine wa SUMATRA kwakuwa Wao ndiyo walengwa wakuu katika hii KERO lakini cha kushangaza sana na kutia HASIRA hawa Watu kutwa tunakutana nao katika " Gambe " na " Gesti " kila mara tukistareheka na huku wengine wakinenepeana kama Matenki ya Maji kwa Pesa za Ushuru wa hawa hawa wenye magari ( Madaladala ) lakini hakuna hata mmoja wao mwenye uchungu na hawa Wanaoteseka na hiyo barabara ili kuwatengenezea miundo mbinu yao ili wafanye Kazi zao bila matatizo.

Jamani naomba kwanza niishie hapa nizitulize hizi hasira zangu kwani naona zinanizidi. Ila kwa mwenye " machungu " kama yangu haya juu ya Kituo cha Mabasi cha SIMU 2000 akaribie katika " kutiririka " kihasira hasira.
 
Leo nitawaomba tu mniache niteme " nyongo " kwani hasira niliyo nayo hata mkinipa " Kichuri " haitapungua.

Kuna Watu nadhani wamepewa dhamana ya kuwajibika ipasavyo kwa Wananchi lakini kwa hakika wanachokifanya au kutufanyia nadhani hata Shetani hawezi kutufanyia japo anatutawala " kimtindo ".
Haiwezekani kabisa barabara ambayo imeharibika vibaya sasa inakaribia hata mwaka lakini Wahusika wakuu wamenyamaza tu na wala hawachukui hatua yoyote ya basi hata tu kuirekebisha kidogo huku wakijipanga kwa matengenezo kamili.

KERO iliyopo sasa katika ile barabara ya kuelekea Kituo cha Mabasi kipya cha SIMU 2000 ama hakika haivumiliki. Magari ya Watu hasa " Madaladala " kila kukicha yanaharibika pale huku foleni zisizo na miguu wala kichwa zikitokea kila mara hadi kutusababishia sisi Watumiaji usumbufu mkubwa sana.

Hivi inachukua muda gani au gharama ipi kuamua tu kuitengeneza? Nimeyaweka hapo Makundi matatu Wenye Mamlaka na Kituo, Watu wa TANROADS na hawa wadau wengine wa SUMATRA kwakuwa Wao ndiyo walengwa wakuu katika hii KERO lakini cha kushangaza sana na kutia HASIRA hawa Watu kutwa tunakutana nao katika " Gambe " na " Gesti " kila mara tukistareheka na huku wengine wakinenepeana kama Matenki ya Maji kwa Pesa za Ushuru wa hawa hawa wenye magari ( Madaladala ) lakini hakuna hata mmoja wao mwenye uchungu na hawa Wanaoteseka na hiyo barabara ili kuwatengenezea miundo mbinu yao ili wafanye Kazi zao bila matatizo.

Jamani naomba kwanza niishie hapa nizitulize hizi hasira zangu kwani naona zinanizidi. Ila kwa mwenye " machungu " kama yangu haya juu ya Kituo cha Mabasi cha SIMU 2000 akaribie katika " kutiririka " kihasira hasira.
Leo nitawaomba tu mniache niteme " nyongo " kwani hasira niliyo nayo hata mkinipa " Kichuri " haitapungua.

Kuna Watu nadhani wamepewa dhamana ya kuwajibika ipasavyo kwa Wananchi lakini kwa hakika wanachokifanya au kutufanyia nadhani hata Shetani hawezi kutufanyia japo anatutawala " kimtindo ".
Haiwezekani kabisa barabara ambayo imeharibika vibaya sasa inakaribia hata mwaka lakini Wahusika wakuu wamenyamaza tu na wala hawachukui hatua yoyote ya basi hata tu kuirekebisha kidogo huku wakijipanga kwa matengenezo kamili.

KERO iliyopo sasa katika ile barabara ya kuelekea Kituo cha Mabasi kipya cha SIMU 2000 ama hakika haivumiliki. Magari ya Watu hasa " Madaladala " kila kukicha yanaharibika pale huku foleni zisizo na miguu wala kichwa zikitokea kila mara hadi kutusababishia sisi Watumiaji usumbufu mkubwa sana.

Hivi inachukua muda gani au gharama ipi kuamua tu kuitengeneza? Nimeyaweka hapo Makundi matatu Wenye Mamlaka na Kituo, Watu wa TANROADS na hawa wadau wengine wa SUMATRA kwakuwa Wao ndiyo walengwa wakuu katika hii KERO lakini cha kushangaza sana na kutia HASIRA hawa Watu kutwa tunakutana nao katika " Gambe " na " Gesti " kila mara tukistareheka na huku wengine wakinenepeana kama Matenki ya Maji kwa Pesa za Ushuru wa hawa hawa wenye magari ( Madaladala ) lakini hakuna hata mmoja wao mwenye uchungu na hawa Wanaoteseka na hiyo barabara ili kuwatengenezea miundo mbinu yao ili wafanye Kazi zao bila matatizo.

Jamani naomba kwanza niishie hapa nizitulize hizi hasira zangu kwani naona zinanizidi. Ila kwa mwenye " machungu " kama yangu haya juu ya Kituo cha Mabasi cha SIMU 2000 akaribie katika " kutiririka " kihasira hasira.
Wanataka hadi JPM aseme.
 
Ile barabara ilipaswa iwe ya lami.....hata ya makumbusho.......

Ni kweli kabisa na hata Mimi nashangaa sana. Kuna wakati huwa nakubaliana 100% na Donald Trump kuhusu sisi Waafrika. Sijui " tumerogwa " na nani hakyamungu. Hivi kwanini hatujui KUFIKIRI na KUWAJIBIKA tunavyostahili?
 
nasubiri tamko la mh. makonda kuhusu barabara hiyo....

hadi wenye daladala wagome... pengne ndio litafanyiwa kazi.
 
nasubiri tamko la mh. makonda kuhusu barabara hiyo....

hadi wenye daladala wagome... pengne ndio litafanyia kazi.

Na katika Management pamoja na Administration hakuna kitu au jambo baya kama Kiongozi kuanza kuwajibika au kukifanyia Kazi kitu fulani mara baada ya Watu " kugoma ". Hapa nikuulize swali Mkuu hivi hawa Viongozi wetu hasa wa hizi Taasisi au Idara fulani fulani huwa wanakuwa na background nzuri kweli ya kuwa Kiongozi au Wenzetu neno Uongozi / Ukubwa kwao ina maana tu ya kupiga " Selfies " za kufa Mtu na kuzituma WhatssApp, Facebook, Instagram na Twitter?
 
Mkuu pole kwa uchungu ulonao juu ya kero hiyo... Binafsi nyongo inakaribia kupasuka leo nimepita makumbusho barabara ni vumbi linatimka nyumba za watu waliopo pembezoni mwa barabara zimechakaa shauri ya vumbi....huwa najiuliza hivi vituo viwili cha Simu 2000 na Makumbusho vipo chini ya manispaa ama ni watu binafsi...manake haiwezekani wanakusanya ushuru mamilioni kwa siku then wanashindwa hata kutengeneza barabara ipitike vizuri.
 
Ni kweli kabisa na hata Mimi nashangaa sana. Kuna wakati huwa nakubaliana 100% na Donald Trump kuhusu sisi Waafrika. Sijui " tumerogwa " na nani hakyamungu. Hivi kwanini hatujui KUFIKIRI na KUWAJIBIKA tunavyostahili?
Kuna ujinga mwingine unafanyika wazi kabisa tunaona...........
 
Back
Top Bottom