Wenye diploma GPA chini ya 3.0 hawaruhusiwi tena kusoma degree kama zamani

Hata kama kuna muujiza wa kuongeza majengo na lab facility, lakini issue kubwa itakuwa staffing levels (walimu, technicians na field offier) na juu ya hilo weka usafiri wa kupeleka vijana field. Nisicho elewa onezeko kubwa hili linaongozwa na sera gani? Ukizalisha wote hawa unawapeleka wapi.

Siri ya Mwal. Nyerere University of Agriculture and Technology nafikiri anayo Ndalichako na bosi wake wengine tunashangaa tu yanayo endelea-utakuaje na chu karibia miaka 4 hakuna udahili on the ground. Chuo kile kiki kick-off kitaimsha SUA kwa kiasi fulani, lakini pia kitafika na kusaidia kilimo sehemu SUA haiwezi kufika. Kwa nchi ya kilimo SUA pekeyake haitoshi tunahitaji uwekezaji mkubwa zaidi.

Tuombeane uzima ili tuyashuhudie mengi
 
Hio ya GPA kuanzia ya 3 ni kuanzia mwaka jana imekua applied. Kuhusu afanyeje ajaribu kuulizia CHUO KIKUU HURIA CHA TANZANIA nasikia wana Foundation Program ya mwaka mmoja kisha ataendelea na digrii.
 
Kuna kitu kinaitwa RPL, kinaratibiwa na TCU wao wenyewe, unafanyiwa mafunzo fulani na chuo husika yanayohusu kozi unayotaka kusoma kwa muda, kisha TCU wanakupa mtihani kupitia kile chuo, ukifaulu huo mtihani kwa viwango walivyoviweka basi unadahiliwa kuisoma hiyo kozi. Hebu jaribu kufuatilia kwenye website ya TCU kuhusu hiyo RPL utapata mwanga zaidi. (Maelezo yangu yanaweza yasiwe sahihi kwa 100% ila amini niko "relevant" katika hili).
Imesimamishwa kwa muda.
 
Mwambie akasome FOUNDATION COURSE(OPEN UNIVERTY) Mwaka mmoja wa pili anasoma degree chuo chochote kile kupitia hiko cheti....

Nb,,,,,Hyo program imefunguliwa na uache ubishi.
Na uzi wake upo hapa hapa jf juzi tu uliwekwa
 
Veta sijui kwanini watu wanaidharau.


Veta ni taasisi pekee ambayo asilimia 90 ya wahitimu wamejiajiri au kuajiriwa (Huu ni utafiti wangu binafsi)
Kaka utafungwa! COSTECH hawana masihara
 
Swali dogo nje ya mada, mkuu unalizungumziaje ongezeko la udahili kwa chuo kikuu cha Sokoine hasa kwa kozi Veterinary Medicine, kwa mujibu wa admission guidebook ya TCU inaonyesha kwamba mwaka huu watadahili wanafunzi 350, vipi kuna miundombinu kweli toshelezi ?

Najua kwa namna moja au nyingine wewe ni mdau
Acha uongo admission capacity ya vet sio hiyo
 
Foundation course ya OUT ni kwa ajili ya kusoma degree pale pale OUT!
Wenyewe WANADAI ukifaulu vyuo vingine unakuwa na vigezo. Hii sijajua in practice mambo yakoje au yatakuaje kwani huku kwetu twaweza kusema megine na kutenda vingine kabisa.
 
Acha uongo admission capacity ya vet sio hiyo

Kwanza asante kwa tuhuma, pili naomba ufanye mambo yafuatayo kama hautojali.

1. Tembelea www.tcu.go.tz kuna kitu utakikuta kinaitwa ''Admission guidebook for form six applicants 2018/2019" (ni nyaraka yenye kurasa 177).

2. Tafuta chuo cha sokoine (SUA), kisha nenda kozi namba 21 (Bachelor of Veterinary Medicine), angalia sehemu ya admission capacity, (kuna idadi utaikuta hapo).

3. Karibu sana kuniomba radhi kwa kuniita muongo.

I will be waiting.
 
Acha uongo admission capacity ya vet sio hiyo

Kabla ya kumtuhumu mtu ni vizuri ujiridhishe na kile usemacho. Admission Guide book inaonyesha hizo takwimu alizotoa ndio walewale kuwa ni sawa. Na takwimu hizo hutokea vyuoni sasa labda utuambia SUA au TCU wamekosea, lakini si mchangiaji.
 
Watu wengi huamini wanaosona veta ni wale waliofeli. Lakini ukweli ni kwamba ni taasisi ambayo ni muhimu kwa mustakabali wa taifa. Kiwanda kimoja kinaweza kuwa na electrical engineer mmoja lakini FTC zaidi ya mmoja.
ftc ni ya veta au technical coleje enz hizo?
 
Vipi kwa wale wa diploma Ambao hizo GPA Ni Below 3. Then wakasoma nche Kama Kampala university. So mwisho Wa siku watakubaliwa kutambulika wakileta hizo Bachelor zao? Msaada please
 
Nawashauri waende veta wajipatie ujuzi wowote itawasaidia mbeleni
Mm ni Bachelor degree holder. Ila nimeajiriwa kwa chet cha VETA nakula maisha Vibàya mnoooooo hadi degree yangu nilio isotea siikumbuki tena. I recommend this
 

Similar Discussions

3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom