Mtaka Haki
JF-Expert Member
- Oct 1, 2010
- 492
- 149
Ndani ya CCM wapo watu wengi tu wanaojua na kuona kuwa serikali yetu inaenda vibaya hasa kwenye suala zima la uwajibikaji au kuwajibishwa kwa watendaji wabovu, wezi, wala rushwa na wasiosimamia raslimali za nchi.
Wako wengi wanakubaliana na hali hiyo kwa kuwa maslahi yao binafsi hayawezi kutimizwa nje na CCM.
Wako wasiokubaliana na hali hiyo lakini pia malengo yao ya kisiasa hawaamini yanaweza kutimizwa nje na CCM, zikiwemo nafasi walizo nazo sasa.
UKWELI
Karibu kila mwenye ufahamu wa kawaida anaona na kushangaa jinsi ambavyo hata ahadi ndogo ya kawaida kwa mtawala yeyote ya kuwawajibisha wanaofanya maovu mbalimbali ndani ya serikali na ndani ya chama imekwama na haitekelezeki.
Wimbo wa gamba umekuwa aibu na hatimaye hakuna mwenye ujasiri wa kuuimba tena. Mama au baba anayeishia kumtishia mtoto "nitakuchapa" huku hatimizi, basi mtoto hujua kuwa sio kweli na huendelea na tabia au alifanyalo.
RADA, MEREMETA, KAGODA, KIWIRA, EPA, RICHMOND, BOT, TANESCO, NA MENGINE MENGI yamebakia kuwa kiini macho.
UMASKINI UMEONGEZEKA NA DENI LIMEKUWA KUBWA.
Maisha bora yamekuwa ni kwa kila fisadi, kila mwenye nafasi ya kutia sahihi mkataba uwao wowote na kila mwenye dhamana ya kuiwakilisha serikali katika jambo lihusulo fedha akiamua ana maisha bora na ana uhakika wa kuendelea.
VIJANA vijijini na mijini hawana ajira na hawashawishiki kwa lolote kuwa maisha yao yanaweza kuwa bora bila kubadilisha chochote. Kila mtu anajua kuwa " HUWEZI KUTARAJIA MATOKEO TOFAUTI KWA KUENDELEA KUFANYA ULIVYOKUWA UKIFANYA. People who keep on doing things the same way will always get the same results they have always got."
Ili kulinda heshima nawashauri wale wanaouchukia ufisadi kwa moyo wa kweli au wale wanaochukizwa na mwenendo mzima wa serikali basi wakati wa kuondoka ni sasa kwani ndio sauti pekee inayoeleweka katika jamii.
Ushujaa wa pekee ni wakati huu. Kubakia kwenye Chama tawala kunapaswa kuwa ni kwa wale ambao mwisho wa harakati zao za siasa yenye nia ya kuijenga nchi yao wanakomea 2014 .
Maamuzi yatakayofanywa huko mbele yatakuwa ya faida za kibinafsi zaidi kuliko ya nchi na wananchi.
Pamoja na kwamba Fred Mpendazoe sio mbunge lakini historia na future yake kisiasa ni bora mara nyingi kuliko hata mawaziri wqalioko serikalini kwa sasa. MASHUJAA WALISIMAMIA NA KUAMUA KUFUATANA NA IMANI YAO HATA KAMA WALISIMAMA WENYEWE. Kusimamia haki unaweza usiwe na mfuasi, lakini kama utadumu katika lililo haki wafuasi watakufuata na kukupongeza.
Nape kwa kuwa wewe ni Kijana nakushauri pima maji, chukua hatua Dunia itakuheshimu. Mke watoto wanaweza wasikubali, lakini historia itakuheshimu. Wewe ni kijana bado usiijibu hii kisiasa angalia moyo wako na kwa dhati ufanye maamuzi.
UCHAGUZI ARUMERU, SONGEA , MWANZA na kwingineko tuichukue kama ni sauti ya MUNGU.
Mh Lowasa anajulikana nguvu zake, Mkapa na wengineo wengi walioenda Arumeru Mashariki , sauti inasema nguvu yoyote huko mbele haitazidi nguvu ya uma na chuki ya maovu. Siku zote wanaochukia maovu watakuwa wengi.
Kilango na Sitta mlishiriki kampeni za madiwani. Mnakubalika na kupendwa lakini ujumbe unasema haiwezekani tena mkiwa ndani ya CCM.
Upepo unaonyesha wakati muafaka ni huu. Kwa kuwa maandishi haya ninaandika hapa basi nami historia itaamua kama nilikuwa sahihi au la. Mawaziri waadilifu ni wakati wa kuachia ngazi na kujiondoa hata kama mngeshindwa kwenye uchaguzi ukirudiwa lakini mtashinda moyoni kuwa mliamini na kuusimamia uadilifu. WAKO WAPI WAADILIFU WA LEO?
Wako wengi wanakubaliana na hali hiyo kwa kuwa maslahi yao binafsi hayawezi kutimizwa nje na CCM.
Wako wasiokubaliana na hali hiyo lakini pia malengo yao ya kisiasa hawaamini yanaweza kutimizwa nje na CCM, zikiwemo nafasi walizo nazo sasa.
UKWELI
Karibu kila mwenye ufahamu wa kawaida anaona na kushangaa jinsi ambavyo hata ahadi ndogo ya kawaida kwa mtawala yeyote ya kuwawajibisha wanaofanya maovu mbalimbali ndani ya serikali na ndani ya chama imekwama na haitekelezeki.
Wimbo wa gamba umekuwa aibu na hatimaye hakuna mwenye ujasiri wa kuuimba tena. Mama au baba anayeishia kumtishia mtoto "nitakuchapa" huku hatimizi, basi mtoto hujua kuwa sio kweli na huendelea na tabia au alifanyalo.
RADA, MEREMETA, KAGODA, KIWIRA, EPA, RICHMOND, BOT, TANESCO, NA MENGINE MENGI yamebakia kuwa kiini macho.
UMASKINI UMEONGEZEKA NA DENI LIMEKUWA KUBWA.
Maisha bora yamekuwa ni kwa kila fisadi, kila mwenye nafasi ya kutia sahihi mkataba uwao wowote na kila mwenye dhamana ya kuiwakilisha serikali katika jambo lihusulo fedha akiamua ana maisha bora na ana uhakika wa kuendelea.
VIJANA vijijini na mijini hawana ajira na hawashawishiki kwa lolote kuwa maisha yao yanaweza kuwa bora bila kubadilisha chochote. Kila mtu anajua kuwa " HUWEZI KUTARAJIA MATOKEO TOFAUTI KWA KUENDELEA KUFANYA ULIVYOKUWA UKIFANYA. People who keep on doing things the same way will always get the same results they have always got."
Ili kulinda heshima nawashauri wale wanaouchukia ufisadi kwa moyo wa kweli au wale wanaochukizwa na mwenendo mzima wa serikali basi wakati wa kuondoka ni sasa kwani ndio sauti pekee inayoeleweka katika jamii.
Ushujaa wa pekee ni wakati huu. Kubakia kwenye Chama tawala kunapaswa kuwa ni kwa wale ambao mwisho wa harakati zao za siasa yenye nia ya kuijenga nchi yao wanakomea 2014 .
Maamuzi yatakayofanywa huko mbele yatakuwa ya faida za kibinafsi zaidi kuliko ya nchi na wananchi.
Pamoja na kwamba Fred Mpendazoe sio mbunge lakini historia na future yake kisiasa ni bora mara nyingi kuliko hata mawaziri wqalioko serikalini kwa sasa. MASHUJAA WALISIMAMIA NA KUAMUA KUFUATANA NA IMANI YAO HATA KAMA WALISIMAMA WENYEWE. Kusimamia haki unaweza usiwe na mfuasi, lakini kama utadumu katika lililo haki wafuasi watakufuata na kukupongeza.
Nape kwa kuwa wewe ni Kijana nakushauri pima maji, chukua hatua Dunia itakuheshimu. Mke watoto wanaweza wasikubali, lakini historia itakuheshimu. Wewe ni kijana bado usiijibu hii kisiasa angalia moyo wako na kwa dhati ufanye maamuzi.
UCHAGUZI ARUMERU, SONGEA , MWANZA na kwingineko tuichukue kama ni sauti ya MUNGU.
Mh Lowasa anajulikana nguvu zake, Mkapa na wengineo wengi walioenda Arumeru Mashariki , sauti inasema nguvu yoyote huko mbele haitazidi nguvu ya uma na chuki ya maovu. Siku zote wanaochukia maovu watakuwa wengi.
Kilango na Sitta mlishiriki kampeni za madiwani. Mnakubalika na kupendwa lakini ujumbe unasema haiwezekani tena mkiwa ndani ya CCM.
Upepo unaonyesha wakati muafaka ni huu. Kwa kuwa maandishi haya ninaandika hapa basi nami historia itaamua kama nilikuwa sahihi au la. Mawaziri waadilifu ni wakati wa kuachia ngazi na kujiondoa hata kama mngeshindwa kwenye uchaguzi ukirudiwa lakini mtashinda moyoni kuwa mliamini na kuusimamia uadilifu. WAKO WAPI WAADILIFU WA LEO?