Wenje na Highness wabunge CHADEMA MWANZA, msiidhalilishe CHADEMA

Ndg. zangu
Hoja hii ni kweli ina mambo fulani ya kinafiki;
Matatizo ya mwanza ni ya kurithiwa kutoka enzi za zamani. Jiji hili liliplaniwa vibaya, halina miundo mbinu ya barabara, waloplan jiji hili hawakutegea kama litakuwa na kasi ya ukuaji namna hii. (Inasemekana ni jiji linalokua kwa kasi ya ajabu Afrika Mashariki). Alofanya survey ya jiji hili la mwanza alipal jiji lijengwe Nyamhongolo - hapa lilipo jiji ilikuwa ni sehemu tu ya Bandari. Kutokana na viongozi wa serikali yetu kutothamini mawazo ya wataalam; wakaruhusu ujenzi holela maeneo ya rufiji, uhuru, mabatini, igogo,, bugando n.k.

Wazo langu! Baadhi ya barabara ulozitaja ni matatizo ya Mkurugenzi wa jiji na watendaji wake. Ikumbukwe kuwa Mkurugenzi wa jiji ni Chaguo la Rais wa Magamba - kwa hali hiyo matatizo yote uloyataja hawezi kuyakwepa ila sisi wana CHADEMA tunajitahidi kumulika mapungufu katika jamii ili pale ambapo wenye nchi watakereka watajua la kufanya. CHADEMA wameshika makali ya jiji lakini mpini umeshikiliwa na MAGAMBA ndo maana tukifurukuta tu wanakimbilia kuwataarifu walala nje (Polisi) wenye siraha za kutisha raia.
TUWAPE MOYO WABUNGE WETU VIJANA WAFANYE KAZI KAMA TUTAKAVYOWASHAURI.

Nakusoma ndugu.
Ndo hapo sasa tunapohitaji wabunge/madiwani waje watueleze kuwa mambo hayafanikiwa kwa kuwa WILISONI KABWE Mkurugenzi wa jiji anakwamisha kila juhudi zetu. Na hapo watatoa suluhisho nini wana mwanza wafanye. Wewe unajua hayo, maorirty hawajui. Jukumu langu,, mie ninaye kipenda chama cha CDM kishike hatamu, ni kuwakumbusha wachaguliwa wetu wasiwatelekeze wapiga kura, kwani hawatakuwa wamejitofautisha na magamba
 
Mdogo wake masha huyu! hivi ule mpango wa vitambulisho vya raia aliondoka nao?

we ndo muhusika,, si waona unakumbuka na harakati zake? Ule mpango uko alive kwani kuna ajira zilitangazwa kwa ajili ya kufanya shughuli hiyo, lakini mpaka sasa naona wamekaa kimya. Ntamtafuta jamaa yangu aliyaaply nijue ziliishia wapi kwani mpaka sasa anaendelea na customer care voda
 
Inaonekana huyu jamaa katumwa; mi kila siku napita nikitokea Golden Rocky Pub kuongena na marafiki baada ya kazi then yeye anatuchemsha tu! NYAMBAFUUUUUUUUUUUUU - K.E.N.GE WA NADOADOA MTOA MADA!

unapita wapi, Kona ya bwiru hadi nyasaka? Pita leo uone mziki wake, usikimbilie kutukana tu
 
Nakubaliana na wewe, lakini na barabara mbovu lazima tuzungumzie. We unadhani machinga atatokaje maskani kwake iwapo gari zinaogopa kupia road ile? Ninacho washauri wabunge hawa, wasishushe Imani watu wa MWANZA waliyowapa. Siyo lazima sana kujenga kama uwezo hakuna, lakini ile kuonekana mitaani kwao, kuzungumza nao na kupanga mikakati ya pamoja watathaminiwa sana. Ndicho ninachokitaka kwa wabunge hawa hasa HIGHNESS ambaye yuko cul.

Wenje siyo tatizo sana kule kwake nyamagana

Ndg; kwa kweli huko kwa Hainess sijui mambo yake ni vipi. Lakini nakupa angalizo moja; mbunge anafanya kazi kwa kushirikiana na madiwani. Kuna uwezekano mkubwa kwenye matatizo madiwani wakawa ni wa CCM; wanafanya hivyo ili kuendeleza uongo kwamba mbunge hashirikiani naye katika kutatua kero.
Mfano hai ni huu; ukiwa Igoma barabara ya kuelekea Hill front Hotel ilikuwa ikipitika kwa shida; kipindi cha Diwani wa CCM mwenye kipara, alipoingia diwani wa CDM kijana mdogo tu akawa anafuatilia jiji namna ya kupatiwa BulDozer; kisingizio kilikuwa ni kwamba hakuna mafuta, kijana huyo alirudisha majibu kwa waliomchagua na kufanikisha kuchangisha hela ya mafuta – kazi ikafanyika. Tembelea huo ujionee ndg!
 
Uliyoyasema ni kweli, kwanza barabara zote hizo ulizozitaja ziko chini ya JIji (Sio Serikali kuu).
Mwenye Jukumu la kutengeneza hizo barabara ni Jiji. FYI, Jiji la Mwanza linaongozwa na CDM. Meya
anatoka CDM. Hivyo kushindwa kutengenezwa kwa barabara hizo it is down to CDM. Hili halina
mkono wa magamba.

Kama kweli CDM wanataka waonekane wako tofauti na Magamba na wako tayari kushika dola 2015
haya matatizo yaliyomo ndani ya uwezo wao LAZIMA wayatatue bila visingizio. Kama tatizo ni
MKURUNGEZI basi wamukatae apelekwe sehemu nyingine aletwe mwingine atayekwenda na
kasi ya CDM.

Afterall moja ya maazimio ya Wana-Mwanza ilikuwa kumfukuza Mkurungezo Willison Kabwe
mara CDM watakapotwaa uongozi wa JIji, kwani alionekana dhahiri kumbemba Lau Masha
hata pale ilipoonekana dhahiri ameshindwa uchaguzi.

Swali Je ni kwanini Wenje na Highness wame compromise na Willison Kabwe?! Wametusaliti wana MZA.
Uzuri ni kwamba Wana MZA huwa hatusahau kama hawajui wawaulize marehemu Bomani, Masha, Diallo
the list goes on, Mwanza tunafahamu kutumia kura zetu vizuri.

Bobuk hebu nenda kaiangalie akili yako kwenye kioo, inawezekana kabisa sio yenyewe. Huenda imehama unatumia ya ******
 
Nadhani Dr. Slaa na baadhi ya wakurugenzi ktk CDM mnasoma maoni ya wananchi hapa. Tafadhari waambie wabunge na madiwani wa CDM wachape kazi. Wananchi wanataka kuona tofauti kati ya CDM na CCM. Wananchi wa Sinza wanamsifia Diwani wao. Ni kijana mdogo,lakini ameanza kuonyesha tofauti kati yake na diwani wa CCM aliyepita. Tuchape kazi jamani.
 
Wana Jamvi habarini.

Jiji la Mwanza, ni jiji ambalo kwa sasa linaheshimika kwa harakati za kisiasa baada ya wabunge tena waliowahi kuwa mawaziri kubwagwa na vijana wado EZEKIEL WENJE-Nyamagana na HIGHNESS KIWIA-Ilemela. Wabunge hawa vijana, walichaguliwa kwa imani kubwa na Mwanza tuliamini wataonesha usimamizi wa rasilimali za umaa kwa manufaa ya umma.

Hali imekuwa tofauti kwa uchunguzi wangu, kwani wakati mvua zikinyesha, barabara za mitaani zile za vumbi zimekuwa kero hali inayopelekea watu kuhoji, HAWA NDO WABUNGE TULIOWACHAGUA?

Barabara ya kutoka kona ya BWIRU mpaka Nyasaka, madereva wa daladala wengi wanaikimbia kwa kuwa na mashimo. Magari yanaharibika kwa ubovu wa barabara hiyo. Na road hii ina wapiga kura, na tayari wameanza kulalama.

Barabara ya NUNDU-NYAKATO MECCO, nayo hali kadhalika. Hofu yangu ni kwamba, iwapo suluhisho halitatafutwa, basi wabunge hawa watakuwa wanawapa nafasi CCM kulitwaa tena JIJI la Mwanza.

Kulinusuru ni wao japo kuwa karibu na wananchi, kuwaelimisha kwa nini barabara hazitengenezwi na kama jamii ya eneo husika tufanyeje kuepuka hatari ya kukosa huduma ya usafiri inayotokana na uwepo wa barabara isiyopitika.

Kuendlea kujificha kwa wabunge hawa bila hata kutoa matamko kwa uzembe huu, inaonesha kwamba hawajali kwani kwa habari ya HIGHNESS alishahama na mtaa. Wakati akifanya kampeni alikuwa akilala nyumba moja iliyopo kwa Lema-Munazi, siku hizi hatumuoni pande hizo thus ametutelekeza na barabara yetu inayotutesa.

Watch out kijana, kwa ustawi wa chama.


Wewe kama kweli ni mwananchadema na unaishi mwanza ni wajibu wako kufika ofsini kwa wabunge hawa na kukaa nao kuwapa huu ujumbe. Ni ujumbe mzuri na ninauhakika wataupokea kwa mikono miwili. Mimi pia nilishawahi kuandika humu kuwa wabunge na madiwani wa chadema wasitegeme ccm na serikali yake itawapa nafasi ya wao kuonekana kwa wananchi wanaperform. Ni lazima watumie nguvu ya umma kuwalazimisha kutoa hela kwa ajili ya miradi muhimu ya maendeleo kama iko kwenye badget ya jiji/halmashauri.

Kazi ya mbunge si kutoa pesa mfukoni kwake ili kuleta maendeleo. kazi yake ni kufatilia na kusimamia utekelezaji wa yale yanayokubaliwa kwenye vikao vya halmashauri na bungeni. kama inathibitika kuwa watendaji wanafanya makusudi ya kuihujumu chadema, basi ni wajibu wa mbunge kuwaeleza wananchi hujuma hizo ili waweze kuwashughulikia watendaji hao. Mfano mzuri ni kijana Mnyika kwa swala la maji jimboni kwake aliamua kuandamana na wananchi wake mpaka ofsi za dawasco kujua ni kwanini maji hayatoki. Kwa kufanya hivyo mbunge hutapata lawama yoyote na utajenga uaminifu kwa wananchi wako. Hili lzaima lifanywe na wabunge wote wa chadema. Wabunge wa magamba ambao wanaogopa kutupwa nje 2015 wananfanya hivi majimboni kwao.
 
Ndg; kwa kweli huko kwa Hainess sijui mambo yake ni vipi. Lakini nakupa angalizo moja; mbunge anafanya kazi kwa kushirikiana na madiwani. Kuna uwezekano mkubwa kwenye matatizo madiwani wakawa ni wa CCM; wanafanya hivyo ili kuendeleza uongo kwamba mbunge hashirikiani naye katika kutatua kero.
Mfano hai ni huu; ukiwa Igoma barabara ya kuelekea Hill front Hotel ilikuwa ikipitika kwa shida; kipindi cha Diwani wa CCM mwenye kipara, alipoingia diwani wa CDM kijana mdogo tu akawa anafuatilia jiji namna ya kupatiwa BulDozer; kisingizio kilikuwa ni kwamba hakuna mafuta, kijana huyo alirudisha majibu kwa waliomchagua na kufanikisha kuchangisha hela ya mafuta – kazi ikafanyika. Tembelea huo ujionee ndg!

ndo hapo tunapowahitaji waje wawaeleze wananchi kuwa, maisha hayaendi kama tunavyotaka kwa kuwa kikakwazo ni fulani. akikaa kimya watu watajitafutia majibu ambayo ni ya kumshusha na kumpotezea imani kwa wananchi
 
Wewe kama kweli ni mwananchadema na unaishi mwanza ni wajibu wako kufika ofsini kwa wabunge hawa na kukaa nao kuwapa huu ujumbe. Ni ujumbe mzuri na ninauhakika wataupokea kwa mikono miwili. Mimi pia nilishawahi kuandika humu kuwa wabunge na madiwani wa chadema wasitegeme ccm na serikali yake itawapa nafasi ya wao kuonekana kwa wananchi wanaperform. Ni lazima watumie nguvu ya umma kuwalazimisha kutoa hela kwa ajili ya miradi muhimu ya maendeleo kama iko kwenye badget ya jiji/halmashauri.

Kazi ya mbunge si kutoa pesa mfukoni kwake ili kuleta maendeleo. kazi yake ni kufatilia na kusimamia utekelezaji wa yale yanayokubaliwa kwenye vikao vya halmashauri na bungeni. kama inathibitika kuwa watendaji wanafanya makusudi ya kuihujumu chadema, basi ni wajibu wa mbunge kuwaeleza wananchi hujuma hizo ili waweze kuwashughulikia watendaji hao. Mfano mzuri ni kijana Mnyika kwa swala la maji jimboni kwake aliamua kuandamana na wananchi wake mpaka ofsi za dawasco kujua ni kwanini maji hayatoki. Kwa kufanya hivyo mbunge hutapata lawama yoyote na utajenga uaminifu kwa wananchi wako. Hili lzaima lifanywe na wabunge wote wa chadema. Wabunge wa magamba ambao wanaogopa kutupwa nje 2015 wananfanya hivi majimboni kwao.

Nakushukuru mkuu kwa mawazo yako mazuri. Unajua unaweza kuwa eneo la tukio lakini ukashindwa kuwasilisha ujumbe. Lakini kupitia JF, mtu unakuwa huru hata kama ni baba yako utamkosoa, kama anajifanya ni kiziwi viongozi wake watamkosoa na kumrudisha kwenye msitari.

Ikumbukwe ni kupitia jarida hili, hata mpango wa kandoro wa kujiuzia V8 kwa tsh. 2,000,000 uliharibiwa. Ni matarajio yangu hata hili la KIWIA kuuchuna hataki kujichanganya na wananchi atarekebisha kwa manufaa yake lakini zaid kwa manufaa ya chama-CDM
 
Bobuk hebu nenda kaiangalie akili yako kwenye kioo, inawezekana kabisa sio yenyewe. Huenda imehama unatumia ya ******

NDYOKO ukitoa d, sijui inaitwaje.

Unajua kuna ushabiki halafu kuna upenzi. Ni maneno mawili yenye maana tofauti lakini na yenye wateja tofauti, ingawa kuna baadhi wanakuwa na yote. Mtu ubaweza kuwa mshabiki lakini si mpenzi, na unaweza kuwa mpenzi si mshabiki.

Mshabiki ni kama wewe ambaye pamoja na mtu kukupatia facts, unaendelea kumshabikia mtu wakati hayuko sahihi hata kidogo. huu ni ujinga halfu haujengi.

Menzi yuko tayari kuchangia kwa mstakabali wa maendeleo ya kitu anachokipenda. Iwe kimawazo(hali) au mali. Mpenzi wa kitu, anapopata taarifa ya kitu, haipuuizi, bali anaifanyia kazi ili kurekebisha udhaifu uliojitokeza.

Nakushauri uwe mpenzi wa CDM na siyo Mshabiki
 
Umesema vizuri sana.

maswali yangu.

1. Ameisimamia serikali?
2. Ameishauri serikali?

ukijibu haya ntakuheshimu na kukutambua unataka kujenga democrasia Tanzania na hasa kupitia CDM
je umekwenda kutazama kwenye muhtasari wa vikao vya RCC na vya KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI na BARAZA LA MADIWANI vya manispaa na kufuatilia michango yake ndani ya manispaa. pili fuatilia michango yake bungeni ya maswali ya msingi, ya nyongeza, na michango ya kimaandishi. nakupa home work ya kufuatilia. na kama kote amechangia ujue tatizo ni s/kali, na kama hakuchangia ndio uje kuandika hiyo thread yako hapa.
 
je umekwenda kutazama kwenye muhtasari wa vikao vya RCC na vya KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI na BARAZA LA MADIWANI vya manispaa na kufuatilia michango yake ndani ya manispaa. pili fuatilia michango yake bungeni ya maswali ya msingi, ya nyongeza, na michango ya kimaandishi. nakupa home work ya kufuatilia. na kama kote amechangia ujue tatizo ni s/kali, na kama hakuchangia ndio uje kuandika hiyo thread yako hapa.

unajua kuchangia mjengoni si ishu, ishu ni mrejesho huku kwa grassroot. ni wangapi wanafuatilia bunge? Wenje nilimkubali sana alipokuja na kutupa mrejesho wa vikao na akatoa modalities. Na kunapotokea matatizo ya kijamii, ni vizuri mbunge au watu waliokaribu naye wakajaribu kupata public opinion, kwa kufanya hivyo imani ya mtu kwa mbunge inakuwa kubwa na ya kuthaminiwa. Siyo kuongea bungeni, kule ni usanii mtupu, mtu anakujibu anavyojisikia na huwezi kumfanya lolote.

lakini unapokuja kwa wananchi, tayari unakuja kwenye utekelezaji wa kile kinachotakiwa kutekelezwa kwa wananchi
 
Fact kidogo, jockes kidogo m2 wangu

nimekusoma mkuu, nimefurahi kusikia na jitihada za dogo wa IGOMA, watu wana pesa mifukoni mwao, it depends on how you communicate with them. Ukiwasusa, na wao wanakususa.
 
Mbunge hakusanyi kodi yako bali huisimamia ili itumie vyema makusanyo yake kwa manufaa ya umma.Ikiwa serikali yako iloichagua inahangaika hata ulipaji wa mishahara ya watendaji wake imekuwa kwa zamu,itaikumbuka hata hizo barabara?Anyway naondoka mana hata mtoa hoja sijui ni darasa la ngapi,hoja zake ni kama la nne vile!!!reason before talk.
 
Mbunge hakusanyi kodi yako bali huisimamia ili itumie vyema makusanyo yake kwa manufaa ya umma.Ikiwa serikali yako iloichagua inahangaika hata ulipaji wa mishahara ya watendaji wake imekuwa kwa zamu,itaikumbuka hata hizo barabara?Anyway naondoka mana hata mtoa hoja sijui ni darasa la ngapi,hoja zake ni kama la nne vile!!!reason before talk.

inakuhusu sana hilo
 
unajua kuchangia mjengoni si ishu, ishu ni mrejesho huku kwa grassroot. ni wangapi wanafuatilia bunge? Wenje nilimkubali sana alipokuja na kutupa mrejesho wa vikao na akatoa modalities. Na kunapotokea matatizo ya kijamii, ni vizuri mbunge au watu waliokaribu naye wakajaribu kupata public opinion, kwa kufanya hivyo imani ya mtu kwa mbunge inakuwa kubwa na ya kuthaminiwa. Siyo kuongea bungeni, kule ni usanii mtupu, mtu anakujibu anavyojisikia na huwezi kumfanya lolote.

lakini unapokuja kwa wananchi, tayari unakuja kwenye utekelezaji wa kile kinachotakiwa kutekelezwa kwa wananchi
kule kweli bungeni wanajibu tu kama haufutilii na wao wanakausha ila kama ni mfuatiliaji wanatekeleza, mfano mnyika (kwy mkutano wake na wananchi alituambia) aliuliza swali kuhusu viwanja vya wazi vilivyotwaaliwa na ccm na watu wengine ktk jimbo lake, lakini bungeni alijibiwa kisiasa, mnyika hakuishia hapo alimuandikia barua tena waziri ya kumtaka utekelezaji wa swali lake, hivi ninavyozungumza nimepita sinza manispaa matangazo(mabango) ya viwanja vya wazi na kutaka waliojenga waondoe na vibaki wazi kwa shughuli za jamii. na ndivyo kwa wabunge wa mwanza wanawza wakawa wanafuatilia na akafika wakati s/kali ikaja kutengeneza hiyo barabara.
 
Back
Top Bottom