Wenje asakwa kwa uchochezi....adaiwa kutimkia Dar!

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,427
911,172
Gazeti La CCM Uhuru la leo linatuhabarisha ya kuwa Wenje ametimkia Dar akikimbia mkono mrefu wa dola ambayo inamsaka kwa kuhamasisha machinga kufanya vurugu endapo Chadema haitanyakua nafasi ya umeya wa jiji la Mwanza......

Wenje asakwa kwa uchochezi

Thursday, 09 December 2010 14:23 newsroom




* Adaiwa kutimkia Dar
NA PETER KATULANDA, MWANZA
POLISI mkoani hapa inamsaka Mbunge wa Jimbo la Nyamagana kupitia CHADEMA, Ezekia Wenje kwa tuhuma za uchochezi.
Aidha, limemuonya mbunge huyo pamoja na wafuasi wa chama hicho kwamba wasithubutu kuvunja au kuchoma mali za halmashauri ya Jiji la Mwanza na mali za wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM). Akitoa onyo hilo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Simon Sirro aliwataka wafuasi wa chama hicho pia kutothubutu kuvamia kituo kikuu cha polisi kwa lengo la kukomboa pikipiki zilizokamatwa kwa mujibu wa sheria, vinginevyo watakiona cha moto. Wenje katika mkutano wake alioufanya katika viwanja vya Sahara mjini hapa Desemba 6, mwaka huu, alihamasisha wanachama wa chama hicho kuharibu mali za jiji na za wanaCCM.

ìPolisi tuko imara, ole wao watakaothubutu kufanya hayo watakiona cha moto maana tulikuwa tunapima kujua tunashughulika na watu wa aina gani, lakini sasa tumegundua ni wahuni na vibaka,î alisema Sirro. Alisema: ìIkifikia kiongozi kama Mbunge unasema maneno kama hayo ina maana haujui utawala wa kisheria, lakini pia kutojua kwako hakutafanya tusikuchukulie hatua za kisheria, hivyo tumefungua jalada la uchunguzi, tunamtafuta tumhoji.î Alisema baada ya Wenje kupata taarifa kuwa anasakwa, inadaiwa amekimbilia mjini Dar es Salaam, na kwamba atakapopatikana atahojiwa kuhusiana na kauli hizo.
Kamanda Sirro alifafanua kwamba alipata taarifa kuwa Wenje katika mkutano huo alikuwa akihamasisha wananchi, wakiwemo wafuasi wake kwamba Desemba 17, mwaka huu waende katika ofisi za halmashauri hiyo kusubiri matokeo ya Meya wa Jiji la Mwanza na iwapo hatatoka katika chama chake, wachome viwanda na hoteli za matajiri zinazomilikuwa na wana CCM.
Katika uchaguzi mkuu uliopita Oktoba 31, mwaka huu, jijini Mwanza, CCM ilipata viti tisa vya madiwani, CHADEMA 11 na CUF kimoja ilichoambulia Novemba 28, mwaka huu, wakati wa kukamilisha uchaguzi wa madiwani kwenye kata za Mirongo na Mkuyuni.
Aidha, katika jimbo la Nyamagana pekee, CCM ilipata viti sita, CHADEMA vitano na CUF kimoja, wakati Ilemela, CCM ilipata viti vitatu na CHADEMA sita.
Alidai pia kwamba Wenje alikaririwa akisema pikipiki za baadhi ya watu zinazoshikiliwa kwa makosa mbalimbali katika hicho, watazitoa kwa nguvu ya umma.
Sirro alisema juzi saa 12.40 jioni wafuasi wa CHADEMA walifunga barabara za Makongoro na Nyerere wakati wakiandamana kutoka eneo la Magomeni Kirumba kwenye mkutano wa wabunge Wenje na Hines Kiwia wa jimbo la Ilemela hadi maeneo ya kati kati mji na kusababisha usumbufu.
 
Gazeti La CCM Uhuru la leo linatuhabarisha ya kuwa Wenje ametimkia Dar akikimbia mkono mrefu wa dola ambayo inamsaka kwa kuhamasisha machinga kufanya vurugu endapo Chadema haitanyakua nafasi ya umeya wa jiji la Mwanza......


This is where I tend to say no! Give the source plse.
 
Gazeti la Uhuru! hivi halijajifia tuu? maana haliuziki kwa vile linaandika sana unazi/uongo uliopitiliza unaowauzi hata wana CCM. Au linapata ruzuku ya serikali?
 
Wewe unayepata muda wa kusoma gazeti la UHURU inabidi tukupime kwanza akili. Tangu lini gazeti la uhuru likaandika mazuri ya CHADEMA !! Walishindwa hata kuipa uzito habari ya jk kususiwa bungeni. Siku zote gazeti la uhuru linaandika habari za kuiponda chadema au zile zinazoeelezea kile wanachokiita "mpasuko". ndani ya chadema.. Mimi nikisikia habari imeandikwa na uhuru, RAI mtanzania na habari leo ,I dont BOTHER..
 
Gazeti La CCM Uhuru la leo linatuhabarisha ya kuwa Wenje ametimkia Dar akikimbia mkono mrefu wa dola ambayo inamsaka kwa kuhamasisha machinga kufanya vurugu endapo Chadema haitanyakua nafasi ya umeya wa jiji la Mwanza......
Hivi u analyst wako ni wa kukopi na kubadilisha heading za magazeti tu huna kazi zingine mara Wenje mchochezi mara Shibuda matatani, na mara nyingi huwa unatafuta habari za uchochezi za CDM ndizo unazikopi. Stop distorting informations.
 
Gazeti La CCM Uhuru la leo linatuhabarisha ya kuwa Wenje ametimkia Dar akikimbia mkono mrefu wa dola ambayo inamsaka kwa kuhamasisha machinga kufanya vurugu endapo Chadema haitanyakua nafasi ya umeya wa jiji la Mwanza......


Bado kidogo utaenda kutafuta habari chooni!!
 
Wewe unayepata muda wa kusoma gazeti la UHURU inabidi tukupime kwanza akili. Tangu lini gazeti la uhuru likaandika mazuri ya CHADEMA !! Walishindwa hata kuipa uzito habari ya jk kususiwa bungeni. Siku zote gazeti la uhuru linaandika habari za kuiponda chadema au zile zinazoeelezea kile wanachokiita "mpasuko". ndani ya chadema.. Mimi nikisikia habari imeandikwa na uhuru, RAI mtanzania na habari leo ,I dont BOTHER..
 
Gazeti La CCM Uhuru la leo linatuhabarisha ya kuwa Wenje ametimkia Dar akikimbia mkono mrefu wa dola ambayo inamsaka kwa kuhamasisha machinga kufanya vurugu endapo Chadema haitanyakua nafasi ya umeya wa jiji la Mwanza......


Sources zangu zinasema kuna mkutano wa wabunge wa CHADEMA Dar, ulianza jana na unaendelea leo, yawezekana amekuja kuhudhuria mkutano, au kweli kakimbia.
 
Kwahiyo, Dar na Mwanza polisi wao ni tofauti? Bahati yako umeanza na Gazeti la CCM Uhuru....
 
Chadema viti 11, ccm 9 na cuf 1. Hakuna kuchakachua hapo, ni wazi CDM itachuka umeya, labda kama baadhi ya madiwani wa CDM watahongwa!
 
Ushauri/ombi kwa kakangu Rutashubanyumba, kama unaweza jaribu tu kuwapotezea kabisa uhuru, habari leo na daily news kwenye mpango wako kamambe wa kutuhabarisha... wanatuharibia siku tu
 
Gazeti La CCM Uhuru la leo linatuhabarisha ya kuwa Wenje ametimkia Dar akikimbia mkono mrefu wa dola ambayo inamsaka kwa kuhamasisha machinga kufanya vurugu endapo Chadema haitanyakua nafasi ya umeya wa jiji la Mwanza......

Wenje asakwa kwa uchochezi

Thursday, 09 December 2010 14:23 newsroom




* Adaiwa kutimkia Dar
NA PETER KATULANDA, MWANZA
POLISI mkoani hapa inamsaka Mbunge wa Jimbo la Nyamagana kupitia CHADEMA, Ezekia Wenje kwa tuhuma za uchochezi.
Aidha, limemuonya mbunge huyo pamoja na wafuasi wa chama hicho kwamba wasithubutu kuvunja au kuchoma mali za halmashauri ya Jiji la Mwanza na mali za wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM). Akitoa onyo hilo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Simon Sirro aliwataka wafuasi wa chama hicho pia kutothubutu kuvamia kituo kikuu cha polisi kwa lengo la kukomboa pikipiki zilizokamatwa kwa mujibu wa sheria, vinginevyo watakiona cha moto. Wenje katika mkutano wake alioufanya katika viwanja vya Sahara mjini hapa Desemba 6, mwaka huu, alihamasisha wanachama wa chama hicho kuharibu mali za jiji na za wanaCCM.

ìPolisi tuko imara, ole wao watakaothubutu kufanya hayo watakiona cha moto maana tulikuwa tunapima kujua tunashughulika na watu wa aina gani, lakini sasa tumegundua ni wahuni na vibaka,î alisema Sirro. Alisema: ìIkifikia kiongozi kama Mbunge unasema maneno kama hayo ina maana haujui utawala wa kisheria, lakini pia kutojua kwako hakutafanya tusikuchukulie hatua za kisheria, hivyo tumefungua jalada la uchunguzi, tunamtafuta tumhoji.î Alisema baada ya Wenje kupata taarifa kuwa anasakwa, inadaiwa amekimbilia mjini Dar es Salaam, na kwamba atakapopatikana atahojiwa kuhusiana na kauli hizo.
Kamanda Sirro alifafanua kwamba alipata taarifa kuwa Wenje katika mkutano huo alikuwa akihamasisha wananchi, wakiwemo wafuasi wake kwamba Desemba 17, mwaka huu waende katika ofisi za halmashauri hiyo kusubiri matokeo ya Meya wa Jiji la Mwanza na iwapo hatatoka katika chama chake, wachome viwanda na hoteli za matajiri zinazomilikuwa na wana CCM.
Katika uchaguzi mkuu uliopita Oktoba 31, mwaka huu, jijini Mwanza, CCM ilipata viti tisa vya madiwani, CHADEMA 11 na CUF kimoja ilichoambulia Novemba 28, mwaka huu, wakati wa kukamilisha uchaguzi wa madiwani kwenye kata za Mirongo na Mkuyuni.
Aidha, katika jimbo la Nyamagana pekee, CCM ilipata viti sita, CHADEMA vitano na CUF kimoja, wakati Ilemela, CCM ilipata viti vitatu na CHADEMA sita.
Alidai pia kwamba Wenje alikaririwa akisema pikipiki za baadhi ya watu zinazoshikiliwa kwa makosa mbalimbali katika hicho, watazitoa kwa nguvu ya umma.
Sirro alisema juzi saa 12.40 jioni wafuasi wa CHADEMA walifunga barabara za Makongoro na Nyerere wakati wakiandamana kutoka eneo la Magomeni Kirumba kwenye mkutano wa wabunge Wenje na Hines Kiwia wa jimbo la Ilemela hadi maeneo ya kati kati mji na kusababisha usumbufu.

kama wana akili timamu wamfuate bagamoyo kwenye retreat.
 
Mwacheni Rutashubanyuma awe anatuhabarisha maana vinginevyo tunaweza tusijue wapinga maendeleo wana mpango gani maana wengine huwa hutuyasomi haya magazeti
 
Gazeti La CCM Uhuru la leo linatuhabarisha ya kuwa Wenje ametimkia Dar akikimbia mkono mrefu wa dola ambayo inamsaka kwa kuhamasisha machinga kufanya vurugu endapo Chadema haitanyakua nafasi ya umeya wa jiji la Mwanza...

Haifai kutumia gazeti la Uhuru kama chanzo cha habari. Hakuna mtu yeyote sasa hivi, hata wana CCM wanaolitumia gazeti hilo kama chanzo cha habari. Leo nilikuwa naongea na Kiongozi mmoja wa CCM kuhusiana na wahisani kutoa tamko kuhusu msaada wao kwa Tanzania. Akaniambia kuwa, 'nimesoma kwenye gazeti la uhuru wameandika maneno fulani kuhusiana na wahisani lakini siwezi kusema chochote maana huwezi kuamini habari yoyote kwenye gazeti hili mpaka uone hiyo habari imeandikwa na magazeti mengine kama Mwananchi'. Kwa ushauri tusipoteze kuongelea habari zinazoandikwa na magazeti kama Uhuru ambayo waandishi wao hawaelewi hata maana ya 'HABARI'.
 
Wewe unayepata muda wa kusoma gazeti la UHURU inabidi tukupime kwanza akili. Tangu lini gazeti la uhuru likaandika mazuri ya CHADEMA !! Walishindwa hata kuipa uzito habari ya jk kususiwa bungeni. Siku zote gazeti la uhuru linaandika habari za kuiponda chadema au zile zinazoeelezea kile wanachokiita "mpasuko". ndani ya chadema.. Mimi nikisikia habari imeandikwa na uhuru, RAI mtanzania na habari leo ,I dont BOTHER..


Mkuu hapo kidsogo umepotoka. Ni muhimu kujua maadui zako wanakuchukuliaje ili ujihami. Usiposoma hayo magazeti hutajua wanakuchukuliaje na wao wanajivunia nini. Heko Ruta kwa kupata huo moyo wa kuyasoma maana yanakera ila ni muhimu kuyasoma ili kujua jinsi ya kupambana na CCM
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom