kmp
Member
- Jun 18, 2009
- 39
- 0
Wednesday, 19 May 2010
SERIKALI imetoa waraka unaovielekeza vyuo vikuu vyote nchini, kuchelewa kuanza muhula wa masomo kwa mwezi mmoja, ili kupisha uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu.
Kwa mujibu wa waraka huo, badala ya kuanza Oktoba kama ilivyozoeleka, muhula kwa vyuo vikuu vyote katika mwaka huu, utaanza juma la kwanza la Novemba, baada ya kumalizika uchaguzi huo wa madiwani, wabunge na rais.
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Jumanne Maghembe, alisema vyuo hivyo vitafunguliwa kati ya Novemba 4 na 5.
Hata hivyo alisema hatua hiyo haitokani na uchaguzi na kwamba inatokana na mabadiliko yanayotarajiwa kufanywa na serikali katika utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu nchini.
"Fedha zinazohitajika kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi mwaka huu ni nyingi sana, zinafikia Sh250 bilioni ni pesa nyingi, kwa hiyo tunaandaa utaratibu mpya ambao tunatarajia utakuwa umekamilika ifikapo Novemba 3,"alisema Waziri.
Profesa Maghembe alisema hata mwaka wa masomo uliopita, vyuo vikuu vilifunguliwa Oktoba 25 na kwamba kuwa tarehe hiyo haipishani sana na ya kufunguliwa kwa vyuo hivgo katika mwaka huu.
"Tatizo kila kitu kinachofanywa sasa na serikali kinahusishwa na uchaguzi kwa sababu tu tunaelekea kwenye uchaguzi lakini hili la kufunguliwa kwa vyuo Novemba, halina uhusiano kabisa na uchaguzi,"alisisitiza Profesa Maghembe.
Waziri Maghembe alisema utaratibu wa mpya wa utoaji wa mikopo ambao hakuwa tayari kuuweka wazi, utasaidia kuharakisha ulipwaji wa mikopo hiyo ili wanafunzi watakaporejea vyuoni, wakute mikopo hiyo ikiwa tayari.
Kwa upande wake, Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu Nchini (TCU), Profesa Mayunga Nkunya, alithibitisha kupata taarifa kuhusu hatua hiyo.
Profesa Nkunya alisema, katika kipindi cha Oktoba, wanafunzi wengi watakuwa wakishughulia mikopo kutoka bodi ya mikopo na kwamba halitakuwa jambo zuri kazi hiyo isiingiliane na uchaguzi mkuu.
mwisho
Source: Vyuo vikuu sasa kufunguliwa Novemba
SERIKALI imetoa waraka unaovielekeza vyuo vikuu vyote nchini, kuchelewa kuanza muhula wa masomo kwa mwezi mmoja, ili kupisha uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu.
Kwa mujibu wa waraka huo, badala ya kuanza Oktoba kama ilivyozoeleka, muhula kwa vyuo vikuu vyote katika mwaka huu, utaanza juma la kwanza la Novemba, baada ya kumalizika uchaguzi huo wa madiwani, wabunge na rais.
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Jumanne Maghembe, alisema vyuo hivyo vitafunguliwa kati ya Novemba 4 na 5.
Hata hivyo alisema hatua hiyo haitokani na uchaguzi na kwamba inatokana na mabadiliko yanayotarajiwa kufanywa na serikali katika utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu nchini.
"Fedha zinazohitajika kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi mwaka huu ni nyingi sana, zinafikia Sh250 bilioni ni pesa nyingi, kwa hiyo tunaandaa utaratibu mpya ambao tunatarajia utakuwa umekamilika ifikapo Novemba 3,"alisema Waziri.
Profesa Maghembe alisema hata mwaka wa masomo uliopita, vyuo vikuu vilifunguliwa Oktoba 25 na kwamba kuwa tarehe hiyo haipishani sana na ya kufunguliwa kwa vyuo hivgo katika mwaka huu.
"Tatizo kila kitu kinachofanywa sasa na serikali kinahusishwa na uchaguzi kwa sababu tu tunaelekea kwenye uchaguzi lakini hili la kufunguliwa kwa vyuo Novemba, halina uhusiano kabisa na uchaguzi,"alisisitiza Profesa Maghembe.
Waziri Maghembe alisema utaratibu wa mpya wa utoaji wa mikopo ambao hakuwa tayari kuuweka wazi, utasaidia kuharakisha ulipwaji wa mikopo hiyo ili wanafunzi watakaporejea vyuoni, wakute mikopo hiyo ikiwa tayari.
Kwa upande wake, Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu Nchini (TCU), Profesa Mayunga Nkunya, alithibitisha kupata taarifa kuhusu hatua hiyo.
Profesa Nkunya alisema, katika kipindi cha Oktoba, wanafunzi wengi watakuwa wakishughulia mikopo kutoka bodi ya mikopo na kwamba halitakuwa jambo zuri kazi hiyo isiingiliane na uchaguzi mkuu.
mwisho
Source: Vyuo vikuu sasa kufunguliwa Novemba