Byendangwero
JF-Expert Member
- Oct 24, 2010
- 871
- 56
Siku iliyofuatia mkutano wa hadhara wa waziri mkuu hapa Bukoba mjini, nyumba nyingi maalum hapa mjini, ziliwekwa alama ya "X" kuashiria ya kwamba nyumba hizo zitavunjwa kwakuwa ziko kwenye hifadhi ya barabara. Kutokana na watu kulipigia kelele suala hilo, waziri mkuu alipohutubia mkutano wa hadhara nyumbani kwa waziri wa barabara na ujenzi Pombe Magufuli huko Chato, aliagiza husitishwaji wa zoezi hilo nchi nzima. Hata hivyo watu wengi waliokuwepo wakati wa majumuhisho ya ziara yake mkoani Kagera wamejenga hisia kwamba kauli ya kusitisha zoezi la bomoabomoa aliyoitoa huko Chato ilikuwa ni ya kisiasa, lakina bomoa bomoa hiyo bado iko pale pale.