Wengi hawajaielewa kauli ya Dkt. Ally Bashiru kuhusu CCM kutumia faida ya kuwa na dola kuendelea kubaki madarakani

Nov 27, 2019
35
145
Nimeona tafsiri potofu/uelewa finyu kuhusu Kauli hiyo ya BASHIRU, Msingi wa kauli hiyo ni dhana ya kitaaluma ya INCUMBENCY ADVANTAGES inayotumika katika Political Science.

Chanzo cha tafsiri hio POTOFU inaweza kuwa uelewa hafifu wa dhana ya INCUMBENT ADVATANGE au inafanyika maksudi ili kupata manufaa ya kisiasa.

Nikiri wazi kwamba

1. Mimi ni mmoja wa Wanafunzi wa DKt BASHIRU ambapo nikiwa UDSM nasoma Shahada ya kwanza ya Sanaa katika Katika Siasa na usimamizi wa Umma alinifundisha Kozi inayohusu nadharia za masuala ya Uchaguzi.

2. BASHIRU amekuwa too academic kwa kutumia nadharia za kitaaluma jambo ambalo limechangia umma kwa sehemu kubwa kutoelewa ipasavyo ujumbe aliokusudia kuutoa

Katika taaluma ya Political Science, INCUMBENT is the current holder of an office or position usually in relation to election . Kwa tafsiri isiyo rasmi INCUMBENT ni anayeshikilia Ofisi au nafasi mara nyingi katika Uchaguzi.

INCUMBENCY ADVANTAGE
katika taaluma ya Sanaa ya Sayansi ya Siasa maana yake ni FAIDA au NAFUU inayopata Chama kilichopo Madarakani dhidi ya visivyo madarakani (Vyama Vya Upinzani).

NINI HASA BASHIRU ALIKUWA ANAMAANISHA?

Kwamba CCM kama vilivyo Vyama vingine kote Duniani vilivyopo Madarakani kina nufaika na faida ipasavyo na fursa ya kuwa Madarakani kwa kubuni na kusimamia miradi mbalimbali ya Maendeleo ikiwemo SGR, Kufufua Shirika la Ndege, Afya, Elimu n.k ambayo inajenga imani ya Wananchi kwa Chama hicho katika kukipigia kura kwenye Uchaguzi.

Hivyo basi ni SAHIHI kusema CCM haitumii vyombo vya DOLA PEKEE kuendelea kubaki Madarakani bali na taasisi zingine zote za Umma.

Pia itakuwa ni SAHIHI kwa Vyama visivyo Madarakani mfano Chadema, ACT Wazalendo vikishika Dola kuitumia Kushinda au kuendelea kubaki Madarakani ili mradi vinafanya hivyo kwa mujibu wa Kanuni, taratibu na Katiba.

Hata hivyo HASARA ambayo huikumba Chama kilichopo Madarakani ni kushindwa kufikia matarajio ya Wananchi au kutotekeleza ahadi ilizotoa kwa Wananchi ambapo kwa Vyama visivyo Madarakani inakuwa faida kwake.
 
binafsi ,nilivyomuelewa Bashiru aliposema "mwenye dola...." ni mwenye serikali na sio dola kwa maana ya mahakama au bunge. Bashiru ni msomi ambaye daima kauli zake zinahitaji uwezo mkubwa kuzielewa na kuzichambua.

Dola kwa Bashiru au Magufuli ni serikali ,Dola kwa Ndugai ni Bunge na dola kwa Prof. Juma ni mahakama hivyo tuwe waangalifu kujua dola inamaanisha nini kwa mtamkaji.

Bashiru yupo sahihi kabisa ,kwa kuwa kwake yeye dola ni serikali ambaye ni dola pekee inayochaguliwa na watu kupitia vyama basi ni njia sahihi ya kushinda kirahisi uchaguzi wowote kama unayo.

kwa kuwa serikali(dola) ni ya chama (CCM) basi Bashiru anawajibu wa kuitumia ili kukiwezesha chama kushinda.


kwa upande Wa pili, yanayofanywa na dola sifa zote zinaenda kwa chama chenye dola kwa muda huo na chama lazima kihakikishe dola inatumika na kusimamiwa kwa kiwango kinachotakiwa ili sifa ziwe za kutosha. hapo Bashiru akisema hivyo kuna tatizo?
 
We mwana usichoelewa nikuwa mwalimu wako keshabadilika ameacha taaluma kwa sasa anazingatia maslahi ya kikundi chao na propaganda zao.

Sikuhizi vyombo vya dola vinatumika waziwazi kukandamiza wapinzani kuwatisha, kuwashitaki bila msingi wowote, kuwaweka kizuizini, inadaiwa kuteka na kuwapiga "masasi"!!

Ma DC etc. wanalazimisha watumishi chini yao kuipenda ccm na kunavitisho ukishabikia upinzani utakosa haki kadhaa ikiwemo kuhamishiwa maeneo magumu kikazi.

Bunge kuwafukuza na kuwaadhibu vikali kuwanyima haki ya kusimamia walichotumwa na wananchi wenzao,
Kamati za chama zinatishia watumishi professional wa serikali na kuwaingilia kiutendaji unethically.

Ni upuuzi kujibu hoja hizi na nyingine kama hizi kwa kutumia ka-concept ka "incumbency advantages" na eti unajiita mwana zuoni huku unatetea pumba nyie ndo mnakujaga kuitwa prof. Lipumba
 
ALIKUWA ANAMAANISHA?

Kwamba CCM kama vilivyo Vyama vingine kote Duniani vilivyopo Madarakani kina nufaika na faida ipasavyo na fursa ya kuwa Madarakani kwa kubuni na kusimamia miradi mbalimbali ya Maendeleo ikiwemo SGR, Kufufua Shirika la Ndege, Afya, Elimu n.k ambayo inajenga imani ya Wananchi kwa Chama hicho katika kukipigia kura kwenye Uchaguzi.
Wote sio wajinga kama mlivyo wewe na Bashiru kuwa we can be deceived that much easily! An exact replica of Propesa njaa! An exact product of rubbish Propesa! PhD za kukopi kazi za watu na wapuzi wenzao UDSM kuzipitisha and hence products like you!

What he meant ni kutumia resources za serikali at his free disposal to get political benefits be it use of police to silence opponents (as it is done now) , funds, army, buildings, unequal political environment to their opponents, etc, etc, etc, etc
Words should be given their natural interpretation/meanings unless such interpretation/meaning leads to absurd.
Kwaheri ya kuonana.
 
Back
Top Bottom