Wenger MUST GO!

Gang Chomba

JF-Expert Member
Feb 29, 2008
20,301
4,681
maandiko matakatifu yanasema ukweli hukuweka huru na mimi leo hii nimeamua kuongea ukweli ambao nahisi utaniweka huru.
ukweli huu uko wazi kwa baadhi ya watu wanaoifuatilia na kuitakia mema arsenal.
natanguliza maneno haya kwa baadhi ya watu kwa ajili ya kujihami "naomba nisionekane adui kwa kusema ukweli".
ni wazi kocha wa arsenal mfaransa mchumi arsene wenger ameshindwa kutupatia mafanikio tunayoyahitaji katika klabu yetu.
sera zake na mbinu zake zimeonekana kushindwa kumudu ushindani wa kubeba vikombe nchini uingereza na hata barani ulaya.
sera yake ya kuamini sana vijana na ubahiri uliokomaa na kuota mizizi pia vimechangia kuzorota kwa arsenal kwa siku za karibuni.


SERA YA MIAKA 30...
sera hii amekuwa akiitumia kwa miaka ya hivi karibuni kwa kuwauza wachezaji wenye umri wa miaka 30 na zaidi au kuwa anawapa mkataba wa msimu mmoja kitu ambacho kinachukiwa na wachezaji wa kulipwa barani ulaya.
sera hii pia imepelekea kuondoka kwa wachezaji wengi ambao kwa namna moja au nyingine wangeweza kutumia uzoefu wao kuhakikisha mafanikio yanapatikana klabuni.


SERA YA KUKUZA VIPAJI...
moja kati ya sera anayojivunia mfaransa huyu ni kukuza vipaji vya wachezaji.
lakini hii haileti maana kwa sababu wachezaji anaowakuza mwisho wa yote huwa hawatumii na huwauza kwa timu nyingine.
tumeona mifano mingi kama fabrice muamba, sebastian larson, jermain penant, mathew upson, jermain aliadiere, david bentley na wengine wengi wakiunguruma na kung'ra katika klabu zao.


CAPTAIN...
katika vitu vilivyoniuma msimu huu ni kumnyang'anya wadhifa wa captain mpiganaji Gilberto Silva ambaye kwa kweli hujituma kwa moyo wake wote awapo uwanjani ili kuhakikisha arsenal wanapata ushindi.
girberto alipokwa wadhifa huo pasipo kupewa hata taarifa na kupoteza namba yake uwanjani, namba ambayo ilikabidhiwa kwa mfaransa mwenzie wenger bwana mathew flamini ambaye siwezi kumuelezea kwa jinsi alivyotutenda na kuhamia AC milan.
lakini baadae wenger alipohojiwa alisema kuwa ameamua kumpa gallas wadhifa huo kwa sababu gallas yupo nyuma hivyo anaiona timu nzima na hivyo ataweza kutoa maelekezo kwa wachezaji woote.
lakini waandishi wakamuhoji je kwa nini hukumpa lehman ambaye ndio mtu wa mwisho na anaiona timu nzima pamoja na huyo gallas? kisha wakamtwanga na swali jingine je mbona ulishawahi kumteua thiery henry ambaye ni mshambuliaji kuwa captain je hapo ilikuwaje?
mzee wenger alikosa jibu.
gilberto aliingia kwenye kumbukumbu ya vitabu vya arsenal siku alipoifungia gunners goli la pekee katika mechi yake ya kwanza kuichezea arsenal, pale alipofunga goli dhidi ya liverpool katika mchezo wa ngao ya hisani akiingia mwanzo wa kipindi cha pili kuchukua nafasi ya mbrazil mwenzie Edu aliyetoka kutokana na majeraha ya paja. hivyo ni wazi kuwa wenger hakumtendea haki gilberto kwa maamuzi hayo ya kumnyang'anya wadhifa wa captain.


KUIAMINI TIMU MOJA...
wenger amejenga timu ambayo nikilala nikiamka najua ni wachezaji gani watakaoanza katika mechi, pia wenger ameshindwa kufanya mzunguko ambao matokeo yake sasa yamekuja kuonekana kuwa kuna baadhi ya wachezaji wamebweteka wakijua kuwa wana namba za kudumu na hakuna swala la kugombea namba wala kuwa na ushindani.


ARSENAL WANASHINDWA KUMALIZIA LIGI WAKIWA KILELENI...
kwa mara nyingine tena arsenal tunashindwa kumalizia ligi tulioianza vizuri na matokeo yake tunakuja kuiachia nafasi ya kwanza tulioishikilia kwa muda mrefu na kumaliza ligi tukiwa katika nafasi ya tatu.
hii inatokana na ubishi wa mzee wenger kwani wachunguzi wa maswala ya soka walimwambia anunue wachezaji katika kipindi cha dirisha dogo la usajili la january, lakini mzee huyu alijibu siwezi kununua mchezaji kwani Robin Van Persie akipona atakuja kutuongezea nguvu hivyo itakuwa ni kama mchezaji mpya kwetu, lakini haikuwa hivyo kwani baada ya usajili kufungwa Eduardo aliumia vibaya mguu na kutakiwa kukaa nje kwa kipindi kirefu sana hivyo Van Persie alilazimishwa kucheza ili kuja kuziba pengo la Eduardo.


UCANT TAKE PREMIERSHIP WITH TEENAGER...
maneno haya alianza kuambiwa na sir bobby robinson, pia maneno haya aliyarudia captain wa heshima wa arsenal Tony Adams na hivi majuzi maneno haya kaambiwa tena na Jose' Mourinho wakiwa na maana kuwa huwezi kuchukua ligi kuu ya uingereza ukiwa na wachezaji vijana.
na hapa ndo ninawakumbuka kina Fleddie Ljungberg, Robert Pires, Sol Campbell, Patrick Vieira, Edu, Thiery Henry, Lauren na wengine wengi ambao wangeweza kutumia uzoefu wao kuhakikisha arsenal tunapata mafanikio, leo hii watoto wameshindwa kumalizia mkia kwa kukosa uzoefu.


ADEBAYOL...
kama utazungumzia uozo wa arsenal basi huwezi kuacha kumtaja jamaa huyu.
yeye msimu huu ndie amekuwa kielelezo cha uozo wa klabu kwa kukosa nafasi nyingi za kufunga, kupoteza mipira mingi uwanjani, kushindwa kujipanga katika mitego ya offside awapo uwanjani, kutoitumikia timu kwa juhudi zake binafsi, na pia ameshindwa kuyamudu majukumu aliyopewa na kuaminiwa na arsenal.
ni kweli adebayol ametufungia magoli mengi msimu huu lakini ni wazi kuwa magoli hayo ni magoli ya utamaduni wa arsenal kwani ni magoli ambayo yeye binafsi anatakiwa kumalizia kwa kufunga kitu ambacho kama angekuwa makini na jukumu hilo alilopewa basi angekuwa na magoli mengi zaidi ya haya ya sasa.
ni wazi kuwa adebayol si mshambuliaji wa hadhi ya klabu kama arsenal, na hapa ndipo tunakuwa na wasiwasi na uwezo wa arsenal.


USHINDANI WA VILABU VIKUBWA BARANI ULAYA...
wachunguzi wa maswala ya soka walihoji kwa nini wenger huwa hajitosi kwenye vinyang'anyiro vya kugombea kununua wachezaji wenye majina na uwezo mkubwa? ukizingatia kuwa soka la ulaya kwa sasa limekumbwa na ushindani mkubwa kutokana na timu nyingi kumilikiwa na matajiri ambao wanatumia hela kununua wachezaji ili wapate mafanikio, je wenger na watoto wake wataweza kumudu ushindani huu? au ndo tutakuwa tunawaachia usukani wenzetu zikiwa zimesalia mechi saba ligi kuisha?


hivyo mifumo na imani zilizopitwa na wakati za wenger ndizo zilizotufanya kukosa raha msimu huu na kusemwa vibaya kila tutakapopita, ni wazi kuwa kwa mifumo hiyo ya wenger haiwezi kutusaidia kupata kikombe chochote kwa sasa, hivyo wakati umefika kwa mfaransa huyu kuachia timu na kutafuta changamoto kwingine...
 
Name Arsène Wenger
Position Manager
Born October 22nd, 1949
Strasbourg, France
Previous clubs as player Mutzig
Mulhouse
Strasbourg
Joined Arsenal 28 September 1996
First match as manager Blackburn Rovers (a)
Premier League
October 12, 1996
Won 2-0
Clubs as manager/coach Strasbourg (youth)
Cannes (assistant)
Nancy
AS Monaco
Grampus Eight Nagoya
Honours (Monaco): French League championship 1988
French Cup winners 1991
French 'Manager of the Year' 1988
Honours (Grampus Eight): Japan's 'Manager of the Year' 1995
Emperor's Cup winner 1996
Japanese Super Cup winner 1996
Honours (Arsenal): League championship 1998, 2002, 2004
F.A. Cup winners 1998, 2002, 2003, 2005
Voted 'Manager of the Year' 1998, 2002, 2004


na hiyo ndo CV yake huyo bwana
 
Kwa wadau wa Arsenal huyu kocha anaonekana ana mifumo mingi na anataka apate uprofesor wa soccer kwa design mifumo na kuifanyia kazi..na ilete mafanikio..ndio maana wakati mwingine huwa inashindwa na anaonekana yeye amechemka........pia suala la kuwachezesha watu hao hao hao...mwaka mzimaaa ...sidhani...kama analiona hilo maana anchoamini yeye ndicho hichoooooo
 
Nakuunga mkono GANG CHOMBA ingawa mimi si mnazi wa arsenal lakini ni mfuatiliaji mzuri wa soka la uingereze. Kifupi ni kwamba strategies za wenger ni nzuri ingawa zinahitaji muda sana kuwa implemented na hatimaYe kutoa matunda yanayotarajiwa. Ukiangalia ushindani wa soka ya uingereza na ulaya kwa ujumla ni dhahiri unahitaji kuwa na mchanganyiko wa wachezaji wazoefu na vijana ili kuweza kutoa ushindani.

" To win english premier league or european championship you need to have combination of both experienced and young players". STAN COLEMORE former WESTHAM UNITED player...alitoa maoni haya siku ya mechi kati ya Liverpool na Manchester City katika dimba la Anfiled tarehe03.05.2008.

Kwa kweli hiki kilishaonekana na wafuatiliaji wengi wa soka. Sasa sielewi kama wenzetu huko uhuru wa kocha kufanya decisionS bila kuingiliwa ndio unaompa huyu mzee kufanya haya yote au vipi but kwa kweli Arsenal wametumia nguvu na juhudi kubwa tangu mwanzoni mwa ligi na hatimaye kuongoza kwa takriban miezi 8 mfululizo....lakini ndio hivyo ngoma ya watoto huwa haikeshi hata siku moja..But ni juu ya management ya Arsenal kuliona hilo na kutafuta ufumbuzi otherwise mtakula kwa macho siku zote.Poleni sana
 
Mkubwa mi mshabiki wa MANU but kwa maendeleo ya ARSENAL nafikiri umefika wa kati WENGER anatakiwa kuondoka kutokana na maamuzi anayoyafanya na hataki kubadilika

1.HATAKI KUNUNUA WACHEZAJI WAZURI
Namshangaa kwani sasa ARSENAL ni kabu ya 3 kwa utajiri duniani so pesa si tatizo yeye anastick na sera yake ya wachezaji vijana
DAVID VILLA amesema anapenda kuchezea ARSENAL,C Ronaldo Arsenal ndio ilikuwa timu ya England ya kwanza kumuona but Mzee akagoma kutoa hela hadi leo anajuta

2.ANAPENDA WACHEZAJI AMBAO HAWA STAHILI KUCHEZA ARSENAL
Arsenal ya sasa ni timu kubwa wana uwanja mkubwa ukiacha MANU
Nafikiri EBOUE,SENDEROUS,GALLAS,BERTNDER,DENILSON hawastahili kucheza ARSENAL ya sasa
Hivi ni kwanini aliwauza PIRES,CYGAN,DIARRA,PENANT,BENTLEY,ALIEDERE,MUAMBA,LARSSON
Nafikiri ni kosa kubwa kumuuza mchezaji chini ya maiaka 23 waache wacheze kwa mkopo then baadae wakikomaa warudishe kwenye timu kama hawafai ndio uwauze
Wachezaji anaowapenda WENGER ni kutoka FRANCE ambao ni wachache wanaoweza kumudu PREMIER league

3.KWA NINI ALIMPA GALLAS UKAPTENI
Kwa maoni yangu nafikiri GILBETO alitakiwa kuchukua UKAPTENI au KOLO TOURE na sio GALLAS

Asipoangalia hata FABREGAS,HLEB,CLICHY nao wataondoka hivi karibuni
 
...pia suala la kuwachezesha watu hao hao hao...mwaka mzimaaa ...sidhani...kama analiona hilo maana anchoamini yeye ndicho hichoooooo

labda ni kweli unachosema lakini ukiangalia hapa kwenye list hii, kuna variation nyingine unadhani ingefaa? kumbuka majeruhi nao walikuwemo!

1 Jens Lehmann
2 Abou Diaby
3 Bacary Sagna
4 Cesc Fabregas
5 Kolo Toure
6 Philippe Senderos
7 Tomas Rosicky
9 Eduardo
10 William Gallas
11 Robin Van Persie
13 Alexander Hleb
15 Denilson M
16 Mathieu Flamini
17 Alexandre Song
19 Gilberto M
20 Johan Djourou
21 Lukasz Fabianski
22 Gael Clichy
24 Manuel Almunia
25 Emmanuel Adebayor
26 Nicklas Bendtner
27 Emmanuel Eboue
30 Armand Traore
31 Justin Hoyte
32 Theo Walcott
Kerrea Gilbert
Mark Randall
Nacer Barazite
Kieran Gibbs
Henri Lansbury
Fran Merida

SERA YA MIAKA 30...
...sera hii pia imepelekea kuondoka kwa wachezaji wengi ambao kwa namna moja au nyingine wangeweza kutumia uzoefu wao kuhakikisha mafanikio yanapatikana klabuni.

...sidhani kama kuna over 30 aliyeondoka ambaye kwa namna moja au nyingine angeisaidia timu labda Robert Pires pekee! Freddie Ljumberg performance yake tangu ajiunge na West Ham itakupa jibu. Wengineo nani? Lauren? au Sol Campbell? angalau Sol unaweza sema ana feature kwenye 1st eleven ya Portsmouth, lakini Lauren ni majeruhi wa kudumu.

SERA YA KUKUZA VIPAJI...
moja kati ya sera anayojivunia mfaransa huyu ni kukuza vipaji vya wachezaji.
lakini hii haileti maana kwa sababu wachezaji anaowakuza mwisho wa yote huwa hawatumii na huwauza kwa timu nyingine.
tumeona mifano mingi kama fabrice muamba, sebastian larson, jermain penant, mathew upson, jermain aliadiere, david bentley na wengine wengi wakiunguruma na kung'ra katika klabu zao.

naamini nidhamu na competition ya 1st team selection pia iliwashinda baadhi ya hawa wachezaji walouzwa. Kwa mfano; Silvinho alikuwa 1st choice FB left wa arsenal wakati Ashley Cole akisugua Benchi, alipoondoka Clichy naye alistahmili seasons zote wakati Cole anang'ara, sasa ndio 1st Choice ingawa Armand Traore naye ukiangalia uchezaji wake unajua kweli kijana anastahmili kukaa benchi, Its all about competition na ku fight kuwa 1st selected! au?... vile vile, Kumbuka Bendtner ndiye alikuwa best scorer wa Birmingham alipokuwa on loan!!!

CAPTAIN...
katika vitu vilivyoniuma msimu huu ni kumnyang'anya wadhifa wa captain mpiganaji Gilberto Silva ambaye kwa kweli hujituma kwa moyo wake wote awapo uwanjani ili kuhakikisha arsenal wanapata ushindi.
girberto alipokwa wadhifa huo pasipo kupewa hata taarifa na kupoteza namba yake uwanjani, namba ambayo ilikabidhiwa kwa mfaransa mwenzie wenger bwana mathew flamini ambaye siwezi kumuelezea kwa jinsi alivyotutenda na kuhamia AC milan.
lakini baadae wenger alipohojiwa alisema kuwa ameamua kumpa gallas wadhifa huo kwa sababu gallas yupo nyuma hivyo anaiona timu nzima na hivyo ataweza kutoa maelekezo kwa wachezaji woote.
lakini waandishi wakamuhoji je kwa nini hukumpa lehman ambaye ndio mtu wa mwisho na anaiona timu nzima pamoja na huyo gallas? kisha wakamtwanga na swali jingine je mbona ulishawahi kumteua thiery henry ambaye ni mshambuliaji kuwa captain je hapo ilikuwaje?

nadhani alijibu; "[The captain] will be William Gallas," he said. "There will also be two vice-captains, Kolo Toure and Gilberto.

"I feel centre back is always the best position to lead on the pitch and it is Gallas who has more experience at the back. But Gilberto has always been a great captain and Kolo Toure has a stature too.

"Aswell I made a decision that I want all those experienced players, along with Jens Lehmann, to be involved off the pitch. Players like Jens and Gilberto can play the role of a club captain. They can have a very strong impact mentally on the team. I want them to take on that responsibility."

FLAMINI amecheza mechi zaidi ya 30 katika msimu huu, position ambayo aliimudu vizuri sana tu kucheza na FABREGAS kwenye midfield kuliko GILBERTO. Huoni hapo Captain angekuwa benchi mechi 30 na ushee?

KUIAMINI TIMU MOJA...
wenger amejenga timu ambayo nikilala nikiamka najua ni wachezaji gani watakaoanza katika mechi, pia wenger ameshindwa kufanya mzunguko ambao matokeo yake sasa yamekuja kuonekana kuwa kuna baadhi ya wachezaji wamebweteka wakijua kuwa wana namba za kudumu na hakuna swala la kugombea namba wala kuwa na ushindani.

Labda ni kweli usemayo, lakini vipi substitutes za Arsenal? zilikuwa zinazaa matunda yeyote? Theo WALCOTT bado sana, labda msimu ujao, Eboue na mapungufu yake lakini angalau katusaidia kuliko na one-two zake kuliko mtu kama ROSICKY ambaye hatujamwona tena!!!... nakukumbusha tena majeruhi wa muda mrefu; Denilson, Van persie, Eduardo, Rosicky, etc... na halafu angalia tena 2007-2008 choice of players.
nakubaliana nawe, ilitakiwa tupate striker angalau mmoja wa ziada. Lassana DIARRA was a waste of time and money. Mchezaji mzuri lakini ana too much ego!

UCANT TAKE PREMIERSHIP WITH TEENAGER......
ninawakumbuka kina Fleddie Ljungberg, Robert Pires, Sol Campbell, Patrick Vieira, Edu, Thiery Henry, Lauren na wengine wengi ambao wangeweza kutumia uzoefu wao kuhakikisha arsenal tunapata mafanikio, leo hii watoto wameshindwa kumalizia mkia kwa kukosa uzoefu.

...lakini 'vijana' hao hao waliifikisha arsenal kwenye champsleague final two years ago, na msimu huu wanamaliza league wakiwa wamepoteza mechi tatu tu kati ya 37 walizokwisha cheza kwenye premiership!... nadhani hayo ni mafanikio.

ADEBAYOR
kama utazungumzia uozo wa arsenal basi huwezi kuacha kumtaja jamaa huyu.
...adebayol si mshambuliaji wa hadhi ya klabu kama arsenal, na hapa ndipo tunakuwa na wasiwasi na uwezo wa arsenal.

Premiership Top Goalscorer 2007/08

Ronaldo Man Utd 30
Adebayor Arsenal 24
Torres Liverpool 23

Arsenal's top scorers in the Premier League Season Player Goals In League

Stats pia zinaonyesha kwa wastani wa mechi 24 za Premiership, Adebayor anashika nafasi ya tatu nyuma ya Thierry Henry na Ian Wright!...

1993/94 Ian Wright magoli35 mechi 23
2001/02 Thierry Henry magoli 32 katika mechi 24
2002/03 Thierry Henry magoli32 katika mechi 24
2007/08 Emmanuel Adebayor magoli 30 katika mechi 24

no wonder baada ya mechi na Derby Arsene Wenger alisema "I didn't think Adebayor would reach 30 goals this season," said Arsène Wenger after the game. "I thought he would get 15.

hivyo mifumo na imani zilizopitwa na wakati za wenger ndizo zilizotufanya kukosa raha msimu huu na kusemwa vibaya kila tutakapopita, ni wazi kuwa kwa mifumo hiyo ya wenger haiwezi kutusaidia kupata kikombe chochote kwa sasa, hivyo wakati umefika kwa mfaransa huyu kuachia timu na kutafuta changamoto kwingine...

Hapana, maturity comes with age, hivi unadhani msimu ujao utakuwa hivi hivi? No way!...hebu tuangalie baada ya yule 'mchumi' ELDEMAN kuondoka zile £70m zinaweza tosha kununua wachezaji wengine kuongezea nguvu. So far sijaona ubaya wa timu 'yetu'.
 
labda ni kweli unachosema lakini ukiangalia hapa kwenye list hii, kuna variation nyingine unadhani ingefaa? kumbuka majeruhi nao walikuwemo!

1 Jens Lehmann
2 Abou Diaby
3 Bacary Sagna
4 Cesc Fabregas
5 Kolo Toure
6 Philippe Senderos
7 Tomas Rosicky
9 Eduardo
10 William Gallas
11 Robin Van Persie
13 Alexander Hleb
15 Denilson M
16 Mathieu Flamini
17 Alexandre Song
19 Gilberto M
20 Johan Djourou
21 Lukasz Fabianski
22 Gael Clichy
24 Manuel Almunia
25 Emmanuel Adebayor
26 Nicklas Bendtner
27 Emmanuel Eboue
30 Armand Traore
31 Justin Hoyte
32 Theo Walcott
Kerrea Gilbert
Mark Randall
Nacer Barazite
Kieran Gibbs
Henri Lansbury
Fran Merida



...sidhani kama kuna over 30 aliyeondoka ambaye kwa namna moja au nyingine angeisaidia timu labda Robert Pires pekee! Freddie Ljumberg performance yake tangu ajiunge na West Ham itakupa jibu. Wengineo nani? Lauren? au Sol Campbell? angalau Sol unaweza sema ana feature kwenye 1st eleven ya Portsmouth, lakini Lauren ni majeruhi wa kudumu.



naamini nidhamu na competition ya 1st team selection pia iliwashinda baadhi ya hawa wachezaji walouzwa. Kwa mfano; Silvinho alikuwa 1st choice FB left wa arsenal wakati Ashley Cole akisugua Benchi, alipoondoka Clichy naye alistahmili seasons zote wakati Cole anang'ara, sasa ndio 1st Choice ingawa Armand Traore naye ukiangalia uchezaji wake unajua kweli kijana anastahmili kukaa benchi, Its all about competition na ku fight kuwa 1st selected! au?... vile vile, Kumbuka Bendtner ndiye alikuwa best scorer wa Birmingham alipokuwa on loan!!!



nadhani alijibu; “[The captain] will be William Gallas,” he said. “There will also be two vice-captains, Kolo Toure and Gilberto.

“I feel centre back is always the best position to lead on the pitch and it is Gallas who has more experience at the back. But Gilberto has always been a great captain and Kolo Toure has a stature too.

“Aswell I made a decision that I want all those experienced players, along with Jens Lehmann, to be involved off the pitch. Players like Jens and Gilberto can play the role of a club captain. They can have a very strong impact mentally on the team. I want them to take on that responsibility

FLAMINI amecheza mechi zaidi ya 30 katika msimu huu, position ambayo aliimudu vizuri sana tu kucheza na FABREGAS kwenye midfield kuliko GILBERTO. Huoni hapo Captain angekuwa benchi mechi 30 na ushee?



Labda ni kweli usemayo, lakini vipi substitutes za Arsenal? zilikuwa zinazaa matunda yeyote? Theo WALCOTT bado sana, labda msimu ujao, Eboue na mapungufu yake lakini angalau katusaidia kuliko na one-two zake kuliko mtu kama ROSICKY ambaye hatujamwona tena!!!... nakukumbusha tena majeruhi wa muda mrefu; Denilson, Van persie, Eduardo, Rosicky, etc... na halafu angalia tena 2007-2008 choice of players.
nakubaliana nawe, ilitakiwa tupate striker angalau mmoja wa ziada. Lassana DIARRA was a waste of time and money. Mchezaji mzuri lakini ana too much ego!



...lakini 'vijana' hao hao waliifikisha arsenal kwenye champsleague final two years ago, na msimu huu wanamaliza league wakiwa wamepoteza mechi tatu tu kati ya 37 walizokwisha cheza kwenye premiership!... nadhani hayo ni mafanikio.



Premiership Top Goalscorer 2007/08

Ronaldo Man Utd 30
Adebayor Arsenal 24
Torres Liverpool 23

Arsenal's top scorers in the Premier League Season Player Goals In League

Stats pia zinaonyesha kwa wastani wa mechi 24 za Premiership, Adebayor anashika nafasi ya tatu nyuma ya Thierry Henry na Ian Wright!...

1993/94 Ian Wright magoli35 mechi 23
2001/02 Thierry Henry magoli 32 katika mechi 24
2002/03 Thierry Henry magoli32 katika mechi 24
2007/08 Emmanuel Adebayor magoli 30 katika mechi 24

no wonder baada ya mechi na Derby Arsene Wenger alisema "I didn’t think Adebayor would reach 30 goals this season," said Arsène Wenger after the game. "I thought he would get 15.



Hapana, maturity comes with age, hivi unadhani msimu ujao utakuwa hivi hivi? No way!...hebu tuangalie baada ya yule 'mchumi' ELDEMAN kuondoka zile £70m zinaweza tosha kununua wachezaji wengine kuongezea nguvu. So far sijaona ubaya wa timu 'yetu'.

mchongoma
ahsante sana kwa uchambuzi wako ndugu yangu, hebu tuanze na shavu la kushoto, mi nadhani ilikuwa inawezekana kabisa siku nyingine kumtupa upande ule flamini ili nae clichy apate kupumzika au hata kupata changamoto...

tuje shavu la kulia,
pia nako alikuwa na uwezo wa kumpanga Eboue na kumpumzisha Sagna au hata siku nyingine kumuanzisha alhaj kolo toure.

pale kati mi nahisi ulikuwa ni wakati muafaka kwa sanderous kuzidi kujiongezea experience zaidi kwani kuna mechi nyingine alikuwa anatakiwa acheze na kolo toure au siku nyingine acheze na gallas, na ni wazi kuwa sanderous alitusuta pale kolo toure alipokwenda ghana katika african cup of nations, sanderous alicheza vizuri sana na kuudhihirishia ulimwengu wa gunners kuwa na yeye pia anaweza.

twende kwenye dimba, mi mpaka kesho napingana na matendo ya wenger aliyomfanyia gilberto.
ni dhahiri kuwa kama flamini kuna siku angekuwa anapangwa namba 3 basi kulikuwa na nafasi ya gilberto au denilson kuanza katikati.
na ukumbuke kuwa msimu uliyopita flamini alishaambiwa atafute timu kwa sababu hana jipya na yeye akatuambia yupo tayari kubaki arsenal ilimradi acheze namba yoyote na msimu huu alipopewa namba na kucheza mechi nyingi alifanya vizuri, kitu ambacho hata mchezaji wa bongo anaweza kutuonyesha. na ukumbuke msimu tunaingia final ya champions league flamini alicheza mechi zote namba tatu kasoro ya final ndo alicheza ashley cole.

twende wingi yaa kulia...
hapakuwa na sababu ya kumpandisha juu eboue kwani alikuwa ameshalimudu vizuri shavu la kulia na ukumbuke katika final ya chamions league yeye ndiye aliyepata credits 9 kati ya wachezaji wote wa arsenal so ilidhihirisha wazi kuwa alicheza vizuri namba hiyo. mi nilivyoona angeendelea kumuacha hleb kule kule na angeanza kumuaminisha walcott kama alivyofanya kwa flamini mi nadhani wangeweza kutubeba tu.

dimba la juu...
maestro fabregas kafanya kazi kubwa sana msimu huu na siwezi kumsahau maishani mwangu kwa kile alichokifanya sansiro mpaka akaitwa sanhero.
lakini kuna mechi ambazo zilikuwa zimeshaonyesha mwelekeo wa ushindi hivyo hapakuwa na sababu ya cesc kumaliza mechi na kuingia mtu kama diaby au denilson au hata mechi nyingine alitakiwa apumzishwe kabisa na asihusishwe katika mapambano.

tisa na kumi...
hapa ndipo mahali palipotuliza msimu huu, kwani kama kwenye dirisha dogo la usajiri la january angenunua strikers wa ukweli basi wangeweza kuja kumalizia ligi na kutufanya saa hizi tuwe tunakunywa mvinyo huku tukitamba kama kawaida yetu na kutembea vifua wazi kwa furaha. lakini wenger yeye still aliamini kuwa adebayol anaweza kumalizia kazi, so mwisho wa siku akaanza kumlazimisha van persie kucheza ile hali hakuwa fit 100%.
na hata kwa hii

Ian Wright magoli35 mechi 23
Thierry Henry magoli 32 katika mechi 24
Thierry Henry magoli32 katika mechi 24
Emmanuel Adebayor magoli 30 katika mechi 24


narudia kukwambia kuwa magoli aliyokuwa anafunga adebayol ni magoli ya utamaduni wa arsenal ambayo mpaka leo anelka, wiltord, kanu na henry wanashindwa kuyafunga huko waliko kwani waliuacha utamaduni wa mabao yale pale pale arsenal, na hizo hat trick adebayol anazifunga na marehemu derby kwa nini na chelsea, man, wigan, aston villa, middlesbrough na birmingham hakufanya kitendo hicho?

winga wa kushoto...
rosicky kaifanya kazi yake vizuri sana na tena alipambana vilivyo na ukumbuke tom alikuwa anaunguruma kila eneo uwanjani ili kuhakikisha tunacheka mwisho wa mechi na ukumbuke majeruhi kwenye mpira yapo so usimkatae kisa majeruhi, lakini pamoja na hayo alikuwa anatakiwa kupumzishwa na wakati mwingine diaby au hleb wangeweza anza upande ule.

huo ndio mzunguko niliouzungumzia ndugu yangu.

GILBERTO...
nakubaliana na wewe kuwa flamini alicheza vizuri msimu huu, lakini ukumbuke gilberto amecheza vizuri zaidi kwa kipindi chote alichotutumikia. aliweza kucheza vizuri katika nafasi hiyo ya kiungo pamoja na cesc na kutufikisha final ya champion league ambayo hakuna kiungo yeyote kuanzia david o'lery, david platt na hata viera walimudu kufanya, na utaamini maneno yangu kuwa kwa uwezo wake huyu gilberto kocha wa brazil dunga amempa unahodha wa taifa, hivyo kwa uwezo wake hakukuwa na sababu ya kumdhalilisha vile.
pia kwa kipindi ambacho gilberto amekuwa captain unaweza kufananisha uongozaji wake wa timu na jinsi anavyotuongoza gallas?

tuje kwenye swala la over 30...
naweza kusema pires, campbell, ljungberg, vieira na TH14 hawa jamaa kuwepo kwao kungeweza kutusaidia kwa namna moja au nyingine kupata mafanikio, naweza kukukumbusha tu sio lazma wote waanze bali hata kuingia kwao kungeweza kutusaidia sana kwani wana uzoefu, mbinu, na wanaelewa mifumo ya uchezaji ya arsenal.
mfano mzuri wa kukupa ni kutoka kwa denis bergkamp, huyu jamaa hakuwa anaanza mechi zote, lakini mara nyingi alizokuwa anaingizwa alikuwa anakwenda kuweka mambo sawa na kutusaidia kupata ushindi.
jiulize kwa nini wenzetu bado wanawazee wao na ndio hao wamewapeleka final kwa nini sisi tunawauza?
utu uzima dawa na pia wanasema simba hazeheki meno....ni hayo tu kwa sasa
 
Naweza kusema huyu Mzee aangalie mi nadhani ARSENAL ndio mahali pa kuchukulia wachezaji.FABREGAS,HLEB,CLICHY,SAGNA nao wataondoka tu

Adebayor pamoja na kufunga magoli 30 but nafikiri alitakiwa kufunga magoli zaidi ya 90 kwa nafasi alizopata

Nadhani tangu wameondika kina TONY ADAMS,LEE DIXON,DAVID SEAMAN,MARIN KEOWN,BERGKAMP sijui kama ARSENAL watapata LEGEND wengine.Nafikiri VIEIRA,HENRY,COLE,CAMPBELL wangeweza kuwa ma-LEGEND but WENGER ameshindwa kuwazuia

Kuhusu wachezaji over 30 mi nafikiri wana umuhimu mkubwa sana kwenye timu ,wanawasaidia hawa chipukizi
ManU-Van de sar,Giggs,Scholes
Pompey-David James
Liverpool-Caragher,Hypia
Chelsea-Ballack,Makelele

Wataalamu wa soka wanasema WENGER ndio wa kulaumiwa na sio FLAMINI
Ashley Cole alivyohama walimwita CASHLEY COLE
na FLAMINI sasa anaitwa FLAMONEY
Hakuna mchezaji ambae hapendi kuchezea klabu kubwa
 
Wakuu,

Jumanne Wenger alijaribu kujieleza sana mbele ya "shareholders" wote pale Emirates.

Lakini amelaumu suala la kuwa na wachezaji wengi majeruhi na wengine waliokuwa wamemaliza "mafuta" mwilini kabisa kama Fabregas.

Wachezaji ambao Wenger anawatumia bado ni wadogo, ukiondoa Gilberto, Alex Hleb na Gallas. Lakini unaweza pia kusema kwamba hii timu imejitahidi sana mwaka huu na wengi tuna matumaini kuwa msimu ujao Arsenal itakuwa na wachezaji waliopevuka vizuri kiasi cha kuweza kutulia na kujua wapo uwanjani na wanahitaji kufunga magoli na kuyalinda.

Lakini huo ndio mpira na kama ingekuwa Arsenal imeshikilia magoli iliokuwa ikiongoza dhidi ya Liverpool, Man Utd na Chelsea pengine kusingekuwa na masimulizi yote haya. Suala ni kwamba hii timu ilikuwa na wachezaji wengi chipukizi na waliokuwa hawana uzoefu wa kutisha kuhimili mikikimikiki ya ligi hii ngumu ya UK.

Suala lingine ni kuhusu mishahara, ambapo Wenger ameweka mfumo wa kutolipa kiholela fwedha kwa wachezaji hasa wale wadogo kama Flamini ambae akiwekewa mezani paundi 55,000 na yeye akaziona ni ndogo.

AC Milan wao wakamuahidi kumpa paundi 60,000 baada ya makato ya kodi. Ila kwa hali jinsi ilivo kwa sasa itabidi Wenger atumie fwedha hasa ili kumfurahisha Cesc Fabregas ambae anatamani awe na kikombe chochote na aone maendeleo yoyote ambayo ni kununua wachezaji wenye majina hapo msimu wa usajili utapowadia.

Kwa hio kuna ile tabia ya wachezaji wale wenye umri mdogo kuwa rahisi kurubuniwa kwa fwedha nyingi ambapo wanaweza kutumia sababu kama za Arsenal kutoweza kuibua kikombe chochote kukimbilia timu zingine.

Kutokana na matatizo ya msimu uliopita kuna dalili kwamba Wenger amejiandaa kufanza manunuzi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kumnunua Obafemi Martins kutoka Newcastle ambao wameweka bei ya paundi 15milioni. Oba, kama anavojulikana atamsaidia sana Adebayo kumalizia mipira wavuni kwa uhakika zaidi.

Jean ll Makoun wa Lille ya Ufaransa anaweza kununuliwa kuzipa pengo la Flamini endapo Gilberto nae alaonesha kulegalega. Na m-Croatia Niko Kranjcar wa Portsmouth anaweza kununuliwa ili kuziba pengo la Alex Hleb endapo Alex ataamua kwenda Inter Milan kama inavosemekana.

Kwa hio Arsene Wenger amesikiliza mawazo ya watu na atafanza mabadiliko makubwa kabla ya msimu ujao.
 
mawazo yangu;
- Arsenal au Wenger ni bahili. Lakini inaonekana hakuna pesa ya sio tu kununua, bali kulipa pesa kubwa.

- Arsenal kuna mipangilio ya mishahara. Wakati mwingine mchezaji kama kafika miaka 30, anategemea career kuisha muda wowote, je utakubali ulipwe 40K kwa wiki na contract ya mwaka mmoja (huna guarantee ya kuongezewa baada ya mwaka mmoja), au uende sehemu nyingine unapewa guarantee ya miaka 3 kwa labda 60K-70K kwa wiki. Logic ya hao wachezaji wazee kubaki sikubaliani nayo. Mimi naona Arsenal wameumia tu kwenye defence (Tony adams and Co.) na mfungaji kama Ian Wright.

- Gilberto hata mimi namheshimu kichizi. Jamaa alikuwa na stats za ajabu kila akicheza misimu iliyopita. Ila alichelewa kuripoti kambini. Flamini akapewa nafasi na akafanya kweli. Gilberto labda alijua namba ni yake. Give credit where credit is due. Flamini na Fabregas combo yao ilikuwa nzuri sana. Kumbuka combo ya Gilberto na Viera ilikuwa solid, ila Gilberto na Fabregas haikukubali kama ya Fabregas na Flamini. Halafu Flamini ilikuwa msimu wake wa mwisho, kwahiyo aliifanyia namba usongo akijua akifanya vizuri timu zitakuja kumtafuta.

-Arsenal wanahitaji pyua finisher, Inzaghi staili au V. Nisterlooy. Wengi watasema hawaendani na staili ya Arsenal. Ukweli ni kwamba, Arsenal wanatengeneza nafasi nyingi mno kiasi kwamba wana uwezo wa kufunga magoli mengi mno sana sana katika vi mechi vya kijinga kama Birmingham. Tatizo wachezaji kama hawa ni aidha wa kubahatisha wakiwa un-established (kama Eduardo), au hawezi kuwalipa. Kama Manu wanalipa striker 120K kwa wiki, kwanini aende Arsenal kwa 40K? Halafu mchezaji huyo huyo hata kama analipwa kama Arsenal, je kama Manu, Liverpool, Madrid au Barca wanamfuata, kwanini aende Arsenal?? Club zenye historia zinavutia wachezaji (Chelsea hawana historia hao hawahesabiki).

-Hii system ya vijana, yes, atawa-groom, kama hushindi chochote within 2-3yrs wanaondoka, maana wanakuwa wamejitengenezea jina na watalipwa zaidi. Its money talks!! Hili ni tatizo linaikabili Ajax. Hamna system inawachezaji wazuri kama Ajax, lakini kwa Holland, PSV wanawapiga bao maana jamaa wanapesa zaidi. Ajax mchezaji akitengeneza jina, anaondoka...angalia kijana aliye Madrid anayezungusha midfield. Angalia kijana aliye liverpool. Angalia aliye Hamburg. Kuna mwingine anafunga magoli, huyo hawacheleweshi...Manu wanausongo naye. Man its money talks, bullshit walks. ARSENAL NEED A BILLIONAIRE who can compliment their smart Accounting.
 
Naweza kusema huyu Mzee aangalie mi nadhani ARSENAL ndio mahali pa kuchukulia wachezaji.FABREGAS,HLEB,CLICHY,SAGNA nao wataondoka tu

Adebayor pamoja na kufunga magoli 30 but nafikiri alitakiwa kufunga magoli zaidi ya 90 kwa nafasi alizopata

Nadhani tangu wameondika kina TONY ADAMS,LEE DIXON,DAVID SEAMAN,MARIN KEOWN,BERGKAMP sijui kama ARSENAL watapata LEGEND wengine.Nafikiri VIEIRA,HENRY,COLE,CAMPBELL wangeweza kuwa ma-LEGEND but WENGER ameshindwa kuwazuia

Kuhusu wachezaji over 30 mi nafikiri wana umuhimu mkubwa sana kwenye timu ,wanawasaidia hawa chipukizi
ManU-Van de sar,Giggs,Scholes
Pompey-David James
Liverpool-Caragher,Hypia
Chelsea-Ballack,Makelele

Wataalamu wa soka wanasema WENGER ndio wa kulaumiwa na sio FLAMINI
Ashley Cole alivyohama walimwita CASHLEY COLE
na FLAMINI sasa anaitwa FLAMONEY
Hakuna mchezaji ambae hapendi kuchezea klabu kubwa

naungana na wewe coz hakuna timu isiyo na legend, milan mpaka leo kuna kina maldini, serdolf, ambrosini, cafu, dida, inzaghi na wengine.
juventus utakutana na kina del piero, bilinderi, nedved, trezeguet na wengine wengi tu.
inter ndo kuna kina javier zanetti, cordoba, materazzi, vieira, figo na wengine wengi.
madrid utawakuta kina guti, raul, casillas.

ukija arsenal wao wanawauza sasa je hiyo ni akili kweli jamani?
 
mawazo yangu;
- Arsenal au Wenger ni bahili. Lakini inaonekana hakuna pesa ya sio tu kununua, bali kulipa pesa kubwa.

- Arsenal kuna mipangilio ya mishahara. Wakati mwingine mchezaji kama kafika miaka 30, anategemea career kuisha muda wowote, je utakubali ulipwe 40K kwa wiki na contract ya mwaka mmoja (huna guarantee ya kuongezewa baada ya mwaka mmoja), au uende sehemu nyingine unapewa guarantee ya miaka 3 kwa labda 60K-70K kwa wiki. Logic ya hao wachezaji wazee kubaki sikubaliani nayo. Mimi naona Arsenal wameumia tu kwenye defence (Tony adams and Co.) na mfungaji kama Ian Wright.

- Gilberto hata mimi namheshimu kichizi. Jamaa alikuwa na stats za ajabu kila akicheza misimu iliyopita. Ila alichelewa kuripoti kambini. Flamini akapewa nafasi na akafanya kweli. Gilberto labda alijua namba ni yake. Give credit where credit is due. Flamini na Fabregas combo yao ilikuwa nzuri sana. Kumbuka combo ya Gilberto na Viera ilikuwa solid, ila Gilberto na Fabregas haikukubali kama ya Fabregas na Flamini. Halafu Flamini ilikuwa msimu wake wa mwisho, kwahiyo aliifanyia namba usongo akijua akifanya vizuri timu zitakuja kumtafuta.

-Arsenal wanahitaji pyua finisher, Inzaghi staili au V. Nisterlooy. Wengi watasema hawaendani na staili ya Arsenal. Ukweli ni kwamba, Arsenal wanatengeneza nafasi nyingi mno kiasi kwamba wana uwezo wa kufunga magoli mengi mno sana sana katika vi mechi vya kijinga kama Birmingham. Tatizo wachezaji kama hawa ni aidha wa kubahatisha wakiwa un-established (kama Eduardo), au hawezi kuwalipa. Kama Manu wanalipa striker 120K kwa wiki, kwanini aende Arsenal kwa 40K? Halafu mchezaji huyo huyo hata kama analipwa kama Arsenal, je kama Manu, Liverpool, Madrid au Barca wanamfuata, kwanini aende Arsenal?? Club zenye historia zinavutia wachezaji (Chelsea hawana historia hao hawahesabiki).

-Hii system ya vijana, yes, atawa-groom, kama hushindi chochote within 2-3yrs wanaondoka, maana wanakuwa wamejitengenezea jina na watalipwa zaidi. Its money talks!! Hili ni tatizo linaikabili Ajax. Hamna system inawachezaji wazuri kama Ajax, lakini kwa Holland, PSV wanawapiga bao maana jamaa wanapesa zaidi. Ajax mchezaji akitengeneza jina, anaondoka...angalia kijana aliye Madrid anayezungusha midfield. Angalia kijana aliye liverpool. Angalia aliye Hamburg. Kuna mwingine anafunga magoli, huyo hawacheleweshi...Manu wanausongo naye. Man its money talks, bullshit walks. ARSENAL NEED A BILLIONAIRE who can compliment their smart Accounting.

kumbuka gilberto aliunguruma mpaka final ya champions league yeye pamoja na cesc so mpaka hapo utakubaliana na mimi kuwa jamaa na fabregas wanaelewana zaidi.

na kuhusu pure finisher kwani club haina pesa za kuwanunua?
mbona hata teves alisema yeye anaweza kuziba pengo la TH14 kwa nini wenger hakumnunua?

mi naungana na wewe kuwa ni bora sasa arsenal inunuliwe ili aje billionaire atakayenunua players wa ukweli na tupate vikombe
 
mi naungana na wewe kuwa ni bora sasa arsenal inunuliwe ili aje billionaire atakayenunua players wa ukweli na tupate vikombe

Mkuu katika timu ambazo utakuja kushangaa hazinunuliwi ni pamoja na Arsenal.

Usiione Arsenal vile ilivyo ina mizizi ya ajabu juu ya kitu kinaitwa "Heritage" (kumbukumbu).

Hata hivo Asenal wana deni la paundi 305milioni ambalo ni la ujenzi wa Emirates na watu 60,000 wanaoingia Emirates wanaleta paundi milioni 3 kwa kila mechi na kwa kuwa deni hilo linalipwa taratibu sasa hivi Wenger ana kiasi kama paundi 25 milioni, zikiwemo zile ambazo angetumia kuwashawishi Flamini na Alex Hleb katika suala la mishahara ili wabaki Arsenal ingawa ameshindwa kwa Flamini.

Kwa hio katika kuimarisha safu ya ulinzi na kiungo anaweza akatumia hio pesa kununua wachezaji watatu au wanne.

Lakini katika suala la Arsenal kununuliwa kwa sasa watu wamesahau.
 
Mkuu katika timu ambazo utakuja kushangaa hazinunuliwi ni pamoja na Arsenal.

Usiione Arsenal vile ilivyo ina mizizi ya ajabu juu ya kitu kinaitwa "Heritage" (kumbukumbu).

Hata hivo Asenal wana deni la paundi 305milioni ambalo ni la ujenzi wa Emirates na watu 60,000 wanaoingia Emirates wanaleta paundi milioni 3 kwa kila mechi na kwa kuwa deni hilo linalipwa taratibu sasa hivi Wenger ana kiasi kama paundi 25 milioni, zikiwemo zile ambazo angetumia kuwashawishi Flamini na Alex Hleb katika suala la mishahara ili wabaki Arsenal ingawa ameshindwa kwa Flamini.

Kwa hio katika kuimarisha safu ya ulinzi na kiungo anaweza akatumia hio pesa kununua wachezaji watatu au wanne.

Lakini katika suala la Arsenal kununuliwa kwa sasa watu wamesahau.

richard mbona kiungo na beki havina tatizo?
tatizo lipo pale kwa adebayol, yaani piga ua tunatakiwa na strikers mwizi wa kuweza kupokea pasi za mwisho na kufunga, so katika beki na kiungo mi sioni tatizo
 
richard mbona kiungo na beki havina tatizo?
tatizo lipo pale kwa adebayol, yaani piga ua tunatakiwa na strikers mwizi wa kuweza kupokea pasi za mwisho na kufunga, so katika beki na kiungo mi sioni tatizo

Twaib,

Je ni "strikers" gani unafikiri ni wataifaa Arsenal?
 
Twaib,

Je ni "strikers" gani unafikiri ni wataifaa Arsenal?

dimitray berbatov wa spurs, ukatae ukubali thiery henry wa barca, david villa wa valencia, benzema wa lyon, david suazo inter, david trezeguet, eto'o barca nna wengine wengi ambao watakuja kumfanya adebayol achangamke awapo uwanjani au aondoke.
 
kumbuka gilberto aliunguruma mpaka final ya champions league yeye pamoja na cesc so mpaka hapo utakubaliana na mimi kuwa jamaa na fabregas wanaelewana zaidi.

na kuhusu pure finisher kwani club haina pesa za kuwanunua?
mbona hata teves alisema yeye anaweza kuziba pengo la TH14 kwa nini wenger hakumnunua?

mi naungana na wewe kuwa ni bora sasa arsenal inunuliwe ili aje billionaire atakayenunua players wa ukweli na tupate vikombe

Tatizo sio kununua, tatizo ni wakati wa kuwalipa. Kuridhisha wachezaji wengi ni ishu. Huwezi ukaleta mchezaji anayeweza ku-command 120K halafu wachezaji wengine wanalipwa 40K kwa wiki. utagawanya timu. we fikiria sijui Fabregas yuko 75K, sawa wachezaji wanakubali, lakini Fabregas ana uwezo wa kuvuta si chini ya 100K sehemu nyingine. Kuvutia mchezaji mwenye potential sio vigumu, wengi wao ni vijana, wako tayari kulipwa hela mshenzi. Akitengeneza jina, hashindi makombe, kwanini asiende sehemu nyingine atalipwa zaidi, atacheza timu iliyo tayari kuvutia established players...na nafasi ya kushinda kombe ipo kubwa zaidi?

Kitu kingine, naona Wenger anaogopa kununua established players...labda hawezi ku-handle egos. Anaweza kucontrol chipukizi.labda!

Mkuu katika timu ambazo utakuja kushangaa hazinunuliwi ni pamoja na Arsenal.

Usiione Arsenal vile ilivyo ina mizizi ya ajabu juu ya kitu kinaitwa "Heritage" (kumbukumbu).

Hata hivo Asenal wana deni la paundi 305milioni ambalo ni la ujenzi wa Emirates na watu 60,000 wanaoingia Emirates wanaleta paundi milioni 3 kwa kila mechi na kwa kuwa deni hilo linalipwa taratibu sasa hivi Wenger ana kiasi kama paundi 25 milioni, zikiwemo zile ambazo angetumia kuwashawishi Flamini na Alex Hleb katika suala la mishahara ili wabaki Arsenal ingawa ameshindwa kwa Flamini.

Kwa hiyo katika kuimarisha safu ya ulinzi na kiungo anaweza akatumia hio pesa kununua wachezaji watatu au wanne.

Lakini katika suala la Arsenal kununuliwa kwa sasa watu wamesahau.

Arsenal itauzwa. Thats the only way forward.

dimitray berbatov wa spurs, ukatae ukubali thiery henry wa barca, david villa wa valencia, benzema wa lyon, david suazo inter, david trezeguet, eto'o barca nna wengine wengi ambao watakuja kumfanya adebayol achangamke awapo uwanjani au aondoke.

Thierry Henry hafai tena. Ukiangalia Adebayor anaipa balance nzuri zaidi Arsenal. TH too much one show.
Wengine naweza kubaliana nao. Berbatov sidhani.......
 
dimitray berbatov wa spurs, ukatae ukubali thiery henry wa barca, david villa wa valencia, benzema wa lyon, david suazo inter, david trezeguet, eto'o barca nna wengine wengi ambao watakuja kumfanya adebayol achangamke awapo uwanjani au aondoke.


Wachezaji hao wote wanafaa na wengine wanapenda kuchezea ARSENAL but WENGER hawezi kuwanunua sababu ni bei kali
VILLA-Madrid,Barca & Chelsea wanamtaka na PESA wanayo

BENZEMA-BARCA,MILAN,MANU wote wanamtaka na LYON hawauzi wachezaji bei ndogo angalia DIARA,ESSIEN,ABIDAL,MALOUDA,TIAGO

TREZEGUET-LEGEND wa JUVE na pacha wa DELPIERO nafikiri atastafia JUVE

BERBATOV-Spurs wanaweza kumuuza lakini sio ARSENAL hadi leo wanajuta kumuuza CAMPBELL then jamaa ni BEI GHALI

ETOO -Barca wanaweza kumuuza lakini tatizo bei ila huyu angeifaa sana ARSENAL

HENRY -Jinsi alivyoondoka itakuwa aibu akirudi
SUAZO-England kutamshinda

NAFIKIRI HAWA WANAIFAA GUNNERS WENGER INABIDI ATOBOE MFUKO
1.HUNTELAAR
2.KRANKJAR
3.MARTINS-huyu kashazoea ligi ya England
4.DEAN ASHTON
 
belo hao kina krnkjar na dean ashton mi sidhani kama wana hadhi ya kuchezea arsenal, ujue unapoizungumzia arsenal ujue ni moja kati ya timu kubwa ulaya so hatutakiwi kununua wachezaji wa kuja kuwajaribu ndugu yangu, na ukumbuke nxt season tupo champions league so ni wazi kuwa hatuhitaji mtu asiyekuwa na uzoefu na mashindano yale.
kuhusu martini ni mzuri ila alidanganya umri alipokuwa inter na ndio kitu kilichomfanya akimbie serie A, so tunaweza kumsajili kumbe ana miaka 37 so tutakuwa tumechemsha, na kama ulikuwa hujagundua wachezaji wa kiafrika wanaridhika mapema ndo maana mara nyingi hawafikagi 35 na kuendelea wanakosa timu badala yake wanakimbilia qatar kula hela ya bure.
kuhusu huntelaar ukweli ni kuwa sijawahi kumuona akicheza mpira so siwezi kumtathmini.
 
belo hao kina krnkjar na dean ashton mi sidhani kama wana hadhi ya kuchezea arsenal, ujue unapoizungumzia arsenal ujue ni moja kati ya timu kubwa ulaya so hatutakiwi kununua wachezaji wa kuja kuwajaribu ndugu yangu, na ukumbuke nxt season tupo champions league so ni wazi kuwa hatuhitaji mtu asiyekuwa na uzoefu na mashindano yale.
kuhusu martini ni mzuri ila alidanganya umri alipokuwa inter na ndio kitu kilichomfanya akimbie serie A, so tunaweza kumsajili kumbe ana miaka 37 so tutakuwa tumechemsha, na kama ulikuwa hujagundua wachezaji wa kiafrika wanaridhika mapema ndo maana mara nyingi hawafikagi 35 na kuendelea wanakosa timu badala yake wanakimbilia qatar kula hela ya bure.
kuhusu huntelaar ukweli ni kuwa sijawahi kumuona akicheza mpira so siwezi kumtathmini.

Ndio ni timu kubwa but wachezaji hao waliopo mbona wengi hawastahili.SENDEROUS,EBOUE,BERTNDER,GALLAS,DENILSON,DIABY hawafai kucheza ARSENAL
Wanaostahili ni CLICHY,SAGNA,TOURE,CESC,ROSISKY,RVP,HELB& WALCOTT

Mchezaji hata kama ana miaka 40 but kama anafunga magoli/anacheza vizuri kwa nini asinunuliwa
Angalia INZAGHI,TONI,ZIDANE,MAKELELE,LARSON mbona wamecheza hadi uzeeni
Wenye uzoefu wapo but WENGER NI BAHILI HAWEZI KUWANUNUA
 
Back
Top Bottom