Wema ni keki isiyooza na itakupa faraja maishani mwako

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,597
215,268
Kabla ya Uhuru wakati Tanganyika ikiwa katika uangalizi wa Uingereza, kuna binti wa Kiingereza alikuja Tanganyika baada ya kumaliza mafunzo yake ya udaktari huko kwao.

Daktari Mkuu katika Hospitali ya kanisa alikopangiwa alikuwa raia wa Australia na yeye akawa Msaidizi wake. Siku moja akiwa kazini alimpokea mke wa mwalimu wa kijijini pale akiwa mjamzito. Mama yule alikumbwa na mauti wakati wa kujifungia lakini aliacha mtoto wa kiume

Habari za kifo cha mke wake zilimuumiza sana mMwalimu. Daktari Muingereza alimshauri amuachie mtoto yeye ashughulikie mazishi ya mke wake. Daktari alimuacha mtoto hospitali akiangaliwa na manesi. Baada ya mazishi Daktari alishajenga muungano na mtoto yule. Alimuomba mwalimu amlee mtoto yule aliyefiwa na mama.

Baada ya Uhuru, daktari alirudi kwao Uingereza. Alimuacha mtoto akiwa na miaka saba. Alimtafutia shule ya boda nzuri na kumpeleka. Alilipa ada ya mwaka na mahitaji mengine. Alipofika kwao, baada ya kupata ajira aliendelea kumtunza yule mtoto

Daktari alipoolewa na kupata watoto, aliwafahamisha watoto wake kuwa wana kaka mkubwa Tanzania. Watoto waliandikiana barua. Yule mtoto alifika mbali kielimu na kuwa mmoja wa viongozi wanaoaminika serikalini. Aliamua kulea watoto yatima kwani anafahamu kama asingepata msaada wa malezi asingefika hapo alipo.

Ndugu wanatembeleana na watoto wao wanajiona ni ndugu. Daktari alitengeneza keki isiyooza.
 
Umenikumbusha maneno ya keki isiyooza ilibandikwa nyumbani kwa mama mmoja jirani yetu maeneo ya Upanga alikiwa mwalimu wangu wa sekondari miaka ilee....

Pembeni yake alibandika sala ya kuombea chakula, "Ewe baba yetu, uje nyumbani kwetu, ubariki / uwe mkate wetu, ....... (mengine nimesahau)".

Na pembeni palikiwa na picha inayoonesha matukio ya kazi za kutwa nzima za mwanamke halafu chini yake kuna maneno, "halafu naambiwa sifanyi kazi".
 
Umenikumbusha maneno ya keki isiyooza ilibandikwa nyumbani kwa mama mmoja jirani yetu maeneo ya Upanga alikiwa mwalimu wangu wa sekondari miaka ilee....

Pembeni yake alibandika sala ya kuombea chakula, "Ewe baba yetu, uje nyumbani kwetu, ubariki / uwe mkate wetu, ....... (mengine nimesahau)".

Na pembeni palikiwa na picha inayoonesha matukio ya kazi za kutwa nzima za mwanamke halafu chini yake kuna maneno, "halafu naambiwa sifanyi kazi".
Kila unalolifanya hapa duniani litakuwa na matokeo. Kuna mke wa kibosile mmoja alitukana sana ukoo wa dereva wa mume wake baada ya mtoto wa dereva kumpa mimba binti yake. Aliwaambia masikini wakubwa nyinyi mtaweza kumtunza mtoto wangu?

Matokeo watoto wa yule mama wote hawana maisha mazuri kama yule mjukuu wake ambae ni mjukuu wa dereva pia. Alikuwa na akili darasani na ana maisha mazuri na sasa anamtunza bibi kiburi baada ya babu wote kufariki.
 
Ni kweli kabisa hiyo ni keki isiyooza
Mungu ambariki huyo mama mzungu 🙏🙏

Hakuna kitu nachopenda kumuona mtu anasaidiwa na kufanikiwa pale anaposaidiwa hata mimi niliponauwezo nipo tayari kumsaidia mtu
 
Kabla ya Uhuru wakati Tanganyika ikiwa katika uangalizi wa Uingereza, kuna binti wa Kiingereza alikuja Tanganyika baada ya kumaliza mafunzo yake ya udaktari huko kwao.

Daktari Mkuu katika Hospitali ya kanisa alikopangiwa alikuwa raia wa Australia na yeye akawa Msaidizi wake. Siku moja akiwa kazini alimpokea mke wa mwalimu wa kijijini pale akiwa mjamzito. Mama yule alikumbwa na mauti wakati wa kujifungia lakini aliacha mtoto wa kiume

Habari za kifo cha mke wake zilimuumiza sana mMwalimu. Daktari Muingereza alimshauri amuachie mtoto yeye ashughulikie mazishi ya mke wake. Daktari alimuacha mtoto hospitali akiangaliwa na manesi. Baada ya mazishi Daktari alishajenga muungano na mtoto yule. Alimuomba mwalimu amlee mtoto yule aliyefiwa na mama.

Baada ya Uhuru, daktari alirudi kwao Uingereza. Alimuacha mtoto akiwa na miaka saba. Alimtafutia shule ya boda nzuri na kumpeleka. Alilipa ada ya mwaka na mahitaji mengine. Alipofika kwao, baada ya kupata ajira aliendelea kumtunza yule mtoto

Daktari alipoolewa na kupata watoto, aliwafahamisha watoto wake kuwa wana kaka mkubwa Tanzania. Watoto waliandikiana barua. Yule mtoto alifika mbali kielimu na kuwa mmoja wa viongozi wanaoaminika serikalini. Aliamua kulea watoto yatima kwani anafahamu kama asingepata msaada wa malezi asingefika hapo alipo.

Ndugu wanatembeleana na watoto wao wanajiona ni ndugu. Daktari alitengeneza keki isiyooza.
Interesting indeed...!!!!!
 
Back
Top Bottom