William J. Malecela
R I P
- Apr 27, 2006
- 26,588
- 10,374
- Hapa na wanafunzi wa shule ya msingi ya Nala, mkoani Dodoma ambayo nimekuwa nikiifadhili kwa muda mrefru sana sasa, ipo maili 12 kutoka Dodoma mjini ukiwa unelekea Singida.
Heheheheheeee...patamu hapa...heheheheheee....I got my popcorn ready....
Mmmhhhh!!! mkuu hii nini tena? Kazi ipo mwaka huu.
Nimecheka kweli leo. Itabidi watu tuanze kujitoa misituni.
Hii sinema ya leo kiboko yake, sijui kama kuna popcorns za kutosha!
Karibu sana mkuu tu tumshughulikie huyu nyani bila kumwangalia usoni.
Pundamilia,
Sijakataa uwazi (nimeusisitiza, rejea bandiko langu hapo juu) wala kutoheshimu matakwa ya mwanachama.
Nilitaka kujua zaidi ni kipi kinachosukumia personal contact ambacho forum hii haiwezi kukifanya? Nikatoa dukuduku kuhusu usalama.
Maswala yangu hayajajibiwa na wewe wala bwana Malecela mwenyewe.Maswali haya hayana lengo la kumvunjia mtu heshima, ila kama mtu ana heshima zake anaweza kuyajibu na kuhakikishia watu kwamba anazo heshima zake.Ni moja ya mambo tunayojivunia hapa JF, kwamba hakipiti kitu bila kuchambuliwa kwa kina.
Ningefurahi kama ningepata majibu.
huyu ni mwenyewe mazee,si mnaona mambo yake ya sifa sifa
mkuu utagombea jimbo gani mwakani??bwaa ha ha ha ha ahaa
Hayo y kugombea ubunge wenzio tulishayasikia tokea 2005 kule bcstimes.com....bila kusahau TV show
- Kulia nikiwa na Mwenyekiti wa UDP Ndugu Cheyo, na kushoto nipo na Naibu Spika wa bunge la Muungano wa Jamhuri yetu Mama Anna Makinda.
alisema atagombea wapi?
Hakusema wapi ila alisema anaenda kugombea...na aliaga kabisa!
Ndugu William Malecela,
Mgeni siku ya kwanza lakini mambo yako makubwa, you learn so fast. Nakukumbusha kwamba hapa JF tunajali sana maslahi ya Taifa kuliko maslahi ya mwanachama mmoja mmoja, kivyake vyake.
Picha yako, mawasiliano umeshaweka hapa. Mwenye shida ya kukujua zaidi na kuona sura yako, atawasiana na wewe. Mkuu unaweza bandika bandiko moja tu kueleza kwamba una picha aina mbali mbali na mwenye kuhitaji awasiliane na wewe kupitia njia za mawasiliano ulizo taja.
Ndugu, hao watoto wamekupa ridhaa ya kuweka picha zao humu, au umechukua advantage kwa vile wewe ni mfadhili wao? Usiwanyanyase ki hali tafadhali. Tenda wema nenda zako usingoje shukrani au recognistion.
Mkuu Uwiano,
Nadhani what we see here ni taste tofauti ya zile ambazo tulizoea kuzipata. Si kila kitu kinachotundikwa hapa JF kiwe na maslahi ya Taifa. Kuna mambo mengi na kadhaa yamo humu hayana maslahi yeyote kwa taifa. Let us get things in different ways and dimensions. Tunahitaji mawazo mbadala mitizamo totauti.
'Siku hazigandi' - Lady Jaydee
Kila member akija kwa staili hii itakuwaje? Kuna member karibu 9,000, wote wakiweka picha zao hapa tutatafutana na JF admin.
Tabia kama ya huyu bwana lazima ikemewe, asiendelee kuweka picha zenye maslahi yake binafsi hapa. JF ni kwa manufaa ya Taifa na sio sehemu ya mtu kujinadi au kujionyeshaonyesha!
You have gone too far. Kama tatizo lako ilikuwa ni hilo nadhani ulipaswa kufuata utaratibu tulioukubali hapa kwenye forum, yaani kurippti kwa wahusika. Lakini mimi nilidhani tunajadili hoja kwa kuzingatia uhalisia wake.
Samahani mkuu sikujua wapi ulipokuwa umelalia japokuwa sijaona tatizo na postings zake.
Kwa vile admin hajapata ripoti yeyote na wala hajasema lolote sioni sababu ya kukemea lolote. Wewe endelea na process ya kumripoti na mimi ninaendelea kujadili yale ninayoyaona yanafaa.