Wekeza pesa kidogo kidogo upate gari ya ndoto yako

Hawa waagiza magari wengi wao wezi na sababu kuu ni ujinga wa Watanzania.
Mtu anatumia smartphone ila anashindwa tafuta gari mtandaoni.

Hawa jamaa kama Crown ya 2004 GRS180 kuagiza hadi mkononi ni 10.5mil ila wao wanakuuzia kwa 14.5mil.

Wameongeza zaidi ya 4mil.

IST pia hivyo hivyo ukiiagiza inafika kwa 10mil na point wao wanaongeza 1 mil hadi 2.

Zaidi watakachofanya ni kuchezea speed o meter
BONGO BAHATI MBAYA
.
.
.
mkuu acha kuharibu biashara ya wenzio mana mpaka kufika hapa walipo ni nguvu kubwa wanaitumia

Sent from my SM-J320H using JamiiForums mobile app
 
Hawa waagiza magari wengi wao wezi na sababu kuu ni ujinga wa Watanzania.
Mtu anatumia smartphone ila anashindwa tafuta gari mtandaoni.

Hawa jamaa kama Crown ya 2004 GRS180 kuagiza hadi mkononi ni 10.5mil ila wao wanakuuzia kwa 14.5mil.

Wameongeza zaidi ya 4mil.

IST pia hivyo hivyo ukiiagiza inafika kwa 10mil na point wao wanaongeza 1 mil hadi 2.

Zaidi watakachofanya ni kuchezea speed o meter
Shukrani kwa maelezo na mawazo yako boss. Ila sijakupata vizuri hapo unamaanisha wezi ni wenye showrooms au sisi waagizaji?

Kama unatusema sisi waagizaji nataka kukupatia ushahidi wa Royal Saloon inafika kwa kiasi gani na Athlete inafika kwa kiasi gani na Ist pia. Halafu nawe utaweka ushahidi wa aliyewahi kuibiwa na hizi kampuni za uagizaji magari za kitanzania lengo likiwa ni kuhakikisha kila kitu kinakua sawa na watu hawaendelei kuibiwa.

Sisi kama waagizaji hatupangi bei na wala mteja hatolipa tunachosema sisi, bei inapangwa japan, sisi tunasaidia calculations, ushauri, tunabeba dhamana ua pesa ya mteja mpaka tunakabidhi gari.

Bei ya jumla tunayokua tunaisema ni baada ya kukaa na mteja uso kwa uso kwenye computer bila usiri wowote atashuhudia bei ya Japan, atashuhudia ushuru wa TRA na ataelekezwa gharama za bandari kwa vielelezo hivyo atakapata Jumla ya gharama zote.

Hapa chini nimekupatia screenshot ya ushuru wa Crown Royal Saloon na Athlete pamoja na bei zake za kununulia Japan.
Mda mwingine tunalazimika kuomba discount kwa niaba ya mteja ili hii bei iweze kupoa kidogo. Mfano hapo chini ukijumuisha CIF ambayo ni dola 2577 sawa na Tsh 5,965,755, jumlisha 6,529,123 ya ushuru, Jumlisha 1,000,000 ya whalphage, port charge, clearing, plate number, na transfer fee Jumla ni 13,494,000....tukiomba discount gari hii mteja ana uwezo wa kuipata kwa mpaka 12m, wewe ndugu yetu Crown Royal Saloon unaipataje kwa 10m???


Screenshot_20190814-121345.png
Screenshot_20190814-121356.png
Screenshot_20190814-121103.png
 
BONGO BAHATI MBAYA
.
.
.
mkuu acha kuharibu biashara ya wenzio mana mpaka kufika hapa walipo ni nguvu kubwa wanaitumia

Sent from my SM-J320H using JamiiForums mobile app
Shukrani kwa kuliona hioo boss. Tumchukulie kama mtu anayezungumza jambo asilolijua hivyo anatakiwa kupewa maelezo yatakayomsaidia kujua zaidi.

Hujawahi kusikia vijana mtaani wanabishana kuhusu gari flani kwamba ni ya bei mbaya sana lakini kati yao hakuna hata mmoja ambae ameshawahi kumiliki gari yoyote.

Nimempatia maelezo ya na ushahidi wa hizi bei ili aweze kujiridhisha kuhusu mawazo yake
 
CLS 250 paka hapa ni kiasigani?
Wamaanisha C Class series 250, au S Class series 250? Kama hapo unamaanisha S CLASS 250 HIZO ZIPO ZA SERIES 220 AMBAZO NI ZA MWAKA 2015, lakini za C Class utapata bila shaka hizo za 250 series. Kwanza nifahamishe vizuri hapo unalenga C class au S class?

C Class series 250 zinafika kwa 22m mpaka 23m
 
Habari ya Majukumu wana jukwaa?

Baada ya kupokea maoni kutoka kwa wadau wetu na wateja wetu mbali mbali, hatimae tumeamua kukubaliana na ombi la kuwekeza pesa kidogo kidogo kwa kati ya miezi 3- miezi 24 kwa anayehitaji kumiliki gari lakini hana pesa ya kulipia kwa pamoja.

Wajibu wa Mteja kwa huduma hii
1. Mteja anawajibika kusaini mkataba kwa ajili ya huduma hii
2. Mteja anatakiwa kua na shahidi ambae ni ndugu ambae tutatakiwa kumrejeshea kiasi kitakachokua kimewekwa iwapo mteja atafariki dunia kabla ya kukabidhiwa gari
3. Kutunza taarifa zake za kibenki kwa kipindi chote atakachokua akiwekeza

Wajibu wa Kampuni
1. Kuhifadhi pesa ya mteja mpaka itimie kama ilivyokusudiwa
2. Kumsaidia mteja kuchagua gari nzuri iliyo katika ubora na kumshauri kulingana na kipato chake
3. Kusaini mkataba wa makubaliano ya kupokea pesa za mteja kila mwezi mpaka zitakapotimia kwa dhumuni la kumuagizia gari

Faida za Huduma Hii kwa mteja

1. Itakulazimisha kutimiza ndoto yako ya kumiliki gari kwa kua utalazimika kupunguza matumizi mengine kwa mda ili utimize hili
2. Kujengewa nidhamu ya matumizi bora ya pesa yako na utaratibu wa kujiwekea vapaumbele
3. Hautahusika kuongeza pesa iwapo thamani ya dola itaongezeka


Usalama wa pesa yako
1. Kimomwe Motors ni Kampuni ya kitanzania iliyosajiliwa na inayofanya kazi kwa sheria za nchi yetu
2. Tunasaini mkataba wa kutunza pesa zako
3. Ndugu yako wa karibu atasaini mkataba kama mrithi wako na shahidi iwapo utafariki dunia kabla ya wakati sahihi
4. Hakutakua na gharama nyingine za ziada
5. Kimomwe Motors imedhamiria kua kampuni kubwa ya kwanza ya Kiafrika ya uagizaji wa magari kwa Africa Mashariki na kati ndani ya miaka michache ijayo hivyo usalama wa pesa ya mteja ni jambo la kwanza litakalotuwezesha kutimiza malengo hayo

N.B: KUHUSU KUSHUKA NA KUPANDA KWA DOLA
Iwapo dola itapanda au kushuka, mteja hatotakiwa kuongeza au kurejeshewa kiasi chochote kwa sababu tutatumia thamani ya dola wakati tunasaini mkataba

Kwa maelezo zaidi na ufafanuzi kuhudu huduma hii na nyinginezo waweza kutupigia sim namba 0746267740 au fika ofisini kwetu Magomeni Mapipa

KIMOMWE MOTORS: SAVE MONEY SAVE TIME
Safi, idea nzuri nikipata muda nitawatembelea kwenye office yenu ili kujua zaidi
 
Wamaanisha C Class series 250, au S Class series 250? Kama hapo unamaanisha S CLASS 250 HIZO ZIPO ZA SERIES 220 AMBAZO NI ZA MWAKA 2015, lakini za C Class utapata bila shaka hizo za 250 series. Kwanza nifahamishe vizuri hapo unalenga C class au S class?

C Class series 250 zinafika kwa 22m mpaka 23m
Cls mercedes sio C series
 
Umeambiwa tukitunza kwenye bank yetu ndyo tukaagiza izo pesa zitaoza?
Hazitaoza boss, kupanga ni kuchagua, kwa upande wako ni vizuri utunze mwenyewe ila kuna mwenzio anaona ili kujiepusha na matumizi ya dharula zisizoisha katika maisha ni bora awekeze moja kwa moja kwenye kampuni kama hii ya kwetu ili imtie msukumo wa kutimiza lengo lake.
 
Mkuu naomba unipe bei ya cash ya hiyo Hilux Surf nyeusi. Naomba details zake, stock mliyonayo na bei zake. Ninatanguliza shukrani.
 
Vp kuhusu Toyota Raum ya 2011 na kuendelea mpaka naipata mkononi kwa Tsh ngapi? Je ofisi zenu zinafanya kazi mpk jumapili?
 
Hawa waagiza magari wengi wao wezi na sababu kuu ni ujinga wa Watanzania.
Mtu anatumia smartphone ila anashindwa tafuta gari mtandaoni.

Hawa jamaa kama Crown ya 2004 GRS180 kuagiza hadi mkononi ni 10.5mil ila wao wanakuuzia kwa 14.5mil.

Wameongeza zaidi ya 4mil.

IST pia hivyo hivyo ukiiagiza inafika kwa 10mil na point wao wanaongeza 1 mil hadi 2.

Zaidi watakachofanya ni kuchezea speed o meter
Acha uchawi wewe kwa wanaume wenzio ..
 
Wewe unafanyaje mpaka bei inakua ndogo kuliko nikiagiza Mimi?
Mimi kwa sababu ni kampuni na nashirikia na kampuni za Japan zipatazo 12 nakua kwenye nafasi nzuri ya kupewa punguzo la bei boss.

Tupigie 0746267740 au fika ofisini kwetu magomeni mapipa kwa msaada zaidi. Iwapo uko nje ya Dar es Salaam, unaweza kumuomba ndugu au jamaa aliye hapa afike ofisini kwetu kwa niaba yako
 
Back
Top Bottom