Wekeza pesa kidogo kidogo upate gari ya ndoto yako

KIMOMWEMOTORS

JF-Expert Member
May 17, 2018
358
670
Habari ya Majukumu wana jukwaa?

Baada ya kupokea maoni kutoka kwa wadau wetu na wateja wetu mbali mbali, hatimae tumeamua kukubaliana na ombi la kuwekeza pesa kidogo kidogo kwa kati ya miezi 3- miezi 24 kwa anayehitaji kumiliki gari lakini hana pesa ya kulipia kwa pamoja.

Wajibu wa Mteja kwa huduma hii
1. Mteja anawajibika kusaini mkataba kwa ajili ya huduma hii
2. Mteja anatakiwa kua na shahidi ambae ni ndugu ambae tutatakiwa kumrejeshea kiasi kitakachokua kimewekwa iwapo mteja atafariki dunia kabla ya kukabidhiwa gari
3. Kutunza taarifa zake za kibenki kwa kipindi chote atakachokua akiwekeza

Wajibu wa Kampuni
1. Kuhifadhi pesa ya mteja mpaka itimie kama ilivyokusudiwa
2. Kumsaidia mteja kuchagua gari nzuri iliyo katika ubora na kumshauri kulingana na kipato chake
3. Kusaini mkataba wa makubaliano ya kupokea pesa za mteja kila mwezi mpaka zitakapotimia kwa dhumuni la kumuagizia gari

Faida za Huduma Hii kwa mteja

1. Itakulazimisha kutimiza ndoto yako ya kumiliki gari kwa kua utalazimika kupunguza matumizi mengine kwa mda ili utimize hili
2. Kujengewa nidhamu ya matumizi bora ya pesa yako na utaratibu wa kujiwekea vapaumbele
3. Hautahusika kuongeza pesa iwapo thamani ya dola itaongezeka


Usalama wa pesa yako
1. Kimomwe Motors ni Kampuni ya kitanzania iliyosajiliwa na inayofanya kazi kwa sheria za nchi yetu
2. Tunasaini mkataba wa kutunza pesa zako
3. Ndugu yako wa karibu atasaini mkataba kama mrithi wako na shahidi iwapo utafariki dunia kabla ya wakati sahihi
4. Hakutakua na gharama nyingine za ziada
5. Kimomwe Motors imedhamiria kua kampuni kubwa ya kwanza ya Kiafrika ya uagizaji wa magari kwa Africa Mashariki na kati ndani ya miaka michache ijayo hivyo usalama wa pesa ya mteja ni jambo la kwanza litakalotuwezesha kutimiza malengo hayo

N.B: KUHUSU KUSHUKA NA KUPANDA KWA DOLA
Iwapo dola itapanda au kushuka, mteja hatotakiwa kuongeza au kurejeshewa kiasi chochote kwa sababu tutatumia thamani ya dola wakati tunasaini mkataba

Kwa maelezo zaidi na ufafanuzi kuhudu huduma hii na nyinginezo waweza kutupigia sim namba 0746267740 au fika ofisini kwetu Magomeni Mapipa

KIMOMWE MOTORS: SAVE MONEY SAVE TIME
 

Attachments

  • 4.jpg
    4.jpg
    32.6 KB · Views: 71
  • 01w.jpg
    01w.jpg
    31.3 KB · Views: 67
  • 80.jpg
    80.jpg
    31 KB · Views: 62
  • 90.jpg
    90.jpg
    28.7 KB · Views: 63
  • 54563_4.jpg
    54563_4.jpg
    21.5 KB · Views: 63
  • 54831_3.jpg
    54831_3.jpg
    20.1 KB · Views: 69
  • 56061_3.jpg
    56061_3.jpg
    17.3 KB · Views: 70
  • 56458_3.jpg
    56458_3.jpg
    16.2 KB · Views: 64
  • 57102_4.jpg
    57102_4.jpg
    27.8 KB · Views: 57
  • 57232_3.jpg
    57232_3.jpg
    14.9 KB · Views: 61
  • 57267_3.jpg
    57267_3.jpg
    21.2 KB · Views: 60
  • 208745_image06.jpg
    208745_image06.jpg
    20.9 KB · Views: 66
  • 212694_image02.jpg
    212694_image02.jpg
    23.2 KB · Views: 58
  • 215168_image06.jpg
    215168_image06.jpg
    19.6 KB · Views: 60
Ingekua vizuri mngekua mnampa mtu gari kwa mkataba au mnaiagiza kabisa inabaki yard kwenu akifikisha nusu au robotatu ya pesa mnamkabidhi gari kwa makubaliano maalumu.
Iyo mnayofanya kwamba mpaka pesa ikamike ndio mnaagiza gari ?
 
BMW X3 Sh Ngapi pamoja na usajiri?
BMW X3 Sh Ngapi pamoja na usajiri?
BMW hii ya Silver ina Cc 3000 ni ya mwaka 2004 inafika kwa 20m, na BMW hiyo rangi ya Kijani ina Cc 2500 ya mwaka 2004 inafika kwa 21m

Vizuri ututembelee ofisini kwetu tupate kufaham hitaji lako kwa ukaribu zaidi au waweza kupiga sim namba 0746267740
12.JPG
13.jpg
13.jpg
 
I smell something fishy isije ikawa kama mambo ya deci ya kupanda na kuvuna..
Na pia kwanini huyo mteja asisaini mkataba akiwa na wakili wake..?
Shukrani kwa maoni na mawazo yako boss. Kwa upande wa kampuni yetu ni tofauti kabisa na deci. Sisi tunajiendesha kwa wateja wengi ambao hulipa cash na kuagiza gari zao, hii huduma ya wekeza tumeianzisha kwa ajili ya watanzania wenzetu wenye kiu ya kumiliki gari lakini ni ngumu kuichanga pesa mpaka itimie yeye kuagiza.

Kwa hiyo hatutaraji kushawishika kwa namna yoyote ile kuingia tamaa kwa pesa ya watakao wekeza huku tukiharibu biashara na kupoteza wateja wengi zaidi ambao hulipia cash.

Kuhusu mkataba tumesema atasaini ndugu kwa sababu ya kutaka jambo hili liwe la uwazi kwa wanafamilia ili ikitokea mlengwa amefariki na sisi tuna pesa yake iwe ni rahisi kuilejesha pesa hiyo kwa wanandugu, mwanasheria ni muhimu awepo na apitie mkataba na kujiridhisha na kumshauri mteja kuhusu ubora wa huduma hii kisheria, lakini pia kama unamwamini zaidi mwanasheria anaweza kusaini kama mrithi wako ikitokea umefariki
 
Taja specs zote iwe rahisi kupata bei
Details kwa hii ya kijani ni kama ifuatavyo


Chassis #WBAPA72070WB65672Version/Class2.5
Model Code GH-PA25
Find parts for this model code
Mileage 75,648 km
Engine Size2,490ccEngine Code256S
Drive4wheel driveSteeringRight
Transmiss.AutomaticExt. ColorBlack
Registration
Year/month
2004/12FuelPetrol
Manufacture
Year/month
N/A Seats5
Doors5


Details kwa hii Silver nikama ifuatavyo


Chassis #WBAPA92030WB34978Version/Class
Model Code GH-PA30
Find parts for this model code
Mileage 132,142 km
Engine Size2,970ccEngine Code306S
Drive - SteeringRight
Transmiss.AutomaticExt. ColorSilver
Registration
Year/month
2004/12FuelPetrol
Manufacture
Year/month
N/A Seats5
Doors5
 
Mikoani bado hatujawa na matawi ingawa mpaka kufikia mwenzi wa 10 tutafungua matawi Mwanza na Arusha. Iwapo uko mkoani na una ndugu au mwanafamilia ambae anaishi Dar es Salaam, vizuri umuombe afike kututembelea ofisini kwa ajili ya kujiridhisha mambo mbali mbali ndipo akushauri uendelee na huduma zetu au la
Ofisi si hoja (katika kujiridhisha). Tuliwahi tapeliwa na Kampuni wanaojidai ni International NGO na wakazuga na boss mzungu. Wakatukodisha Hiace na Rav 4 Kilitime siku tunagutuka tunaenda zilipokuwa Ofisi zao tunakutana na kufuli. Mayowe yake ilibid tutafutiwe Ambulance
 
Ingekua vizuri mngekua mnampa mtu gari kwa mkataba au mnaiagiza kabisa inabaki yard kwenu akifikisha nusu au robotatu ya pesa mnamkabidhi gari kwa makubaliano maalumu.
Iyo mnayofanya kwamba mpaka pesa ikamike ndio mnaagiza gari ?
Shukrani kwa mawazo yako mazuri boss. Kwa sasa kampuni yetu haijawa na mtaji mkubwa wa kukopesha ndio sababu tumeona bora tuanze na hatua hii ya wateja wenye uhitaji na utayari wawekeze kidogo kidogo.

Baada ya miezi kadhaa tutaweza kua kwenye nafasi ya kukopesha. Ingawa tunawashirikiana na microfinance mbili kwa ajili ya wateja waliopungukiwa kiasi cha fedha jama ulivyosema, changamoto ya microfinance hizo ni riba kubwa na mda wa marejesho ambapo inatakiwa isizidi miezi 6 na zaidi mkopaji awe ni mtumishi wa serikali
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom