subadesubking
Senior Member
- Jan 17, 2015
- 195
- 324
😂😂😂😂😂😂final umerudi dawa yako mayai viza..Heheheeee
After being an addict for so long i died inside! Nje nilikiwa naishi sawa ila ndani nilikuwa nishakufa kitambooo sanaaa! Na jamiii ishanifanyia mazishi siku nyingi sanaaa! Manaka machoni pa jamii mimi ni tejaaa tu! There was no point of getting better because the society was gonna hold that one fact against me forver! Ndo maana moyoni nishajifia kitambooo! At this point katika maisha yangu nilikuwa siogopi kifo kabisaaa! Kabisaa kabisaa!
Hata huku ulaya na mama watoto we were betting our lives by swinging ghost! Conning the mater of them all! Seriously hata mimi sikuwa na uhakika mimba ni ya ghost au mwenzie! And yet sikustushwa hata chembe what ghost will do is cappable of doing!
Nikizungumza na mzazi mwenzangu namwambia bwana tungoje tuone mwisho wake! Hasira yake ikiwaka sanaa nitamwambia niue mimi apoze mori akuache wewe! Not that many people will miss me anyways! Maisha yangu nimechezea chezea mwenyewe! After all i am considering suicide only sijapata ujasiriwa kufanikisha! Mmmmmh! Na yeye bibie anasisitiza promise me Ghost akija kuniua huku you will pull yourself together na kumlea huyu mtoto! Promise me Hans! Na mdogo wake atakezaliwa utamlea cause you oweme that! I never gave upon you MF to the end so lazima uwalee wote! Hali kiukweli msomaji ilikuwa tete!
Ghost anatuma pesa ontime! Tutake nini kisije! Bibie ananiambia Hans anza kutubu ndigu yangu! Viama vyetu haviko mbali! Bibie woga akaamua aanze kumtafuta Sam! Just incase akituua wote abakie mtu kuwalea watoto! Hali ilikuwa tete!
Mi na mzazi mwenzangu mapenzi yashafarikigi siku nyingi mnoo! Na kama kitu kilichokufa chochote huwezi kukirudisha kwenye uhai! We just had this bond, ndugu si ndugu,marafiki si marafiki tupo tupo tu! Ila hisia za kimahaba baina yetu hakunaaa hakunaaaa!
Toka nije huku siku abuse kabisaaa! I am trying ndugu msomaji to quit! Sema sikuchukuliakama mile stone maana hata mwenyewe sijiamini kabisaa! Kesho tu nawezakutindinganya mambo! Nikawa nafanya zangu gym hapo nyumbani si nipo ideal! Body likaanza kukubali! Still the stigma na saikolojia zilikuwa in ashes! There was no point! And i was still suicidal!
Nikiwa nasafisha safisha nje ya hapo kwetu, nika mnotice dada mmoja mkaliiiiii hatariiii! Kila asubuhi namchungulia anavaa suit zake classic, anaendesha gari yake classic! Kazuriiiii!! Yani kazuriii! Na kako vizuriii! Kibongo bongo ningejitutumua ila kiulaya ulaya sio rahisi!
Nikamshirikisha mama mtoto my new crush! Kama mlitegemea atakuwa msaada ndo kwanza akazidi kunikausha uzazi wooote! Analalamika mwenzangu una ma crush ilihali mimi chakula hakishuki kwa utapeli tunaomfanyia yule kiumbe fedhuliiii na bandiduuu kuliko wote! Namwambia its just a crush dont be a party pooper! Mara akaniambia mwambie tu na usiache part ya wewe ni drug addict and see how it goes! Kauli hio ikanitoa upepo wote wa koro! There is no point ndugu msomaji!
Siku nikawa nafyekaaa! Akaja kuniuliza kama naweza kumfyekea na bei ikoje! Alikuwa high high kama anachelewa! Nikamwambia poa tutaongea bei! Nilifyekaaaajeeeee! Kama hakuna kesho! Mpaka pool nililiasafisha! Yaani ngaringari!
Akarudi akafurahi! Akaniambia aniajiri kwa kazi hio kwa mshahara wa kawaida! Nikakubali! Niji keep tu busy! Ghost alikiwa anatutunza tuna tunzika! Hatupungukiwi na chochote! Mwanangu kama hajaenda shule nae anakuja pale kucheza mi nafanya kazi za watu!
Siongei sana! Lugha yenyewe gongana! Shule sikusoma! Kichwani hamsini majulio! Mdada anaonekana hata mama mtoto hampati kwa vyeti! Siku akaniuliza umesomea nini? Anajifarangua i know europe can be hard unaweza kuwa umesoma na usipate kazi nimpe vyeti anisaidiekutafuta kazi! Mimi namuelewa ila kumjibu sasa kimbembe!
Nikamuita mwanangu aje awe translator! Namwambia haya Linda mwambie Aunty baba hajasoma sababu kichwani zero brain! Linda kunistiri baba ake nasema baba hajasoma sababu Afrika alizaliwa kijijini sana hamna shule! Damu nzito ndugu msomaji! Akauliza how do you live then? Doesyour mom work? Akadakia no she sleeps all day! Moms boyfriend is very rich! He sends lots of money from Africa! We dont need to work like you! Mmmmmh! Mwana sina hapaa! Akasema tu ooooh! So your mom and da are divorced? Dogo akapiga long time ago! Nikamsemesha kiswahii! Dogo acha shobooo! Mimi baba yako ujue!
Nikampanga kabisaa! Dogo mimi yule Aunty nimempenda, nataka awe mama yako sawa! Ili tuendele kwenda sawa issue zangu za madawa ziminyiemwanangu si unajua pops is trying his best! Akasema poa sitomwambia! Nikaendelea na usafi wa lile eneo kama miezi mi 2 hivi! Linda akaona kama sifanyi ma move yenye akili! Akaanza visa! Akamualika yule dada nyumbani! Anamuomba kabisaa mama ake! Dont be pain in the a.ss be nice! Mi mama mtoto namjuaaaa hawezagi unafiki! Na mimi sikuona ni akili nikasema anyways! Ngoja tuone!
Dinner haikwe da vibaya sanaa! Mama mtoto alijitahidi kusurvive na miguno ya hapa na pale! Huyu bibie anaitwa Serwaa ni mghana! Ni real estate agent! Alikuwa very nice! Na mwanagu alijitahii kunizibia gapes! Serwaa akamuuliza mama mtoto why did you 2 break up! Balaa ndo lilipoanzia! Akasema hakukuwa na sababu ya kuendelea! Nianzie wapi? Which part? Where i triedto mudder him? Or i served jail time for attempted mudder, orthe serial cheattings! Serwaa akamuwahi maybe you shouldnt start at al!
Kama kuniua ashanimalizaaaa! Alimuacha na maswali mengi sanaaa! Akaaga akaondoka zake! Ndugu msomaji kama unategemea tiffu lilifuatia wala hujakosea! Ila sio mimi wa sasa! Nikamuita tu kiutu uzima.
Nikamwambia kwanza naomba nikuombe msamaha kwa kukutoa kwa Sam! Perharphs nisingekutoa kuleusingepitia yote hayana niingekuharibia maisha! Naomba unisamehe kwa yote! Hakujibu kitu sasa sielewi alikubaliana au lipingana na hii hoja! Pili naomba nikuombe radhi tena kwa kuwa mzigo wa miba kwako! Kuwa dead beat dady, good for nothing! Mpaka unafanya mambo ya hatari kutuokoa mimi na mwanangu! Sina cha kukulipa! Akanyamaza!
Nikakandamiza lakini why dont you want me to go out with Serwa? Bado unanipenda? Hapana! Una hisia na mimi hapana? Hivo vyako visaaaa! Kweli nakwambia wewe mwanamke! Akasonyaaaaa!
Akasema mimi sina shida wewe kutoka na mwanamke yoyote ila sio Serwa! Akamaliza! Nikamuuliza wewe ulivotoka na Ghost nisingekuwa na shida ungetoka na mwanaume yoyote ila sioGhost! Lakini if he made youhappy iwas happy for you! Why cant you do the same!
Akasonyaa tenaaa! Hansa hunaa akili mbwa wewe! Kwa akili yako mimi kabisaa na majanga yangu nione wivu unatifua papa gani? Aaaah subutuuuuuu! Mimi nakuonea huruma! Serwaa sio size yako! Unakuwa mpanaaa kama kibao cha chapati ukiamua yako jpkama haya! Ukiyatindinganya utarudi kwenye addiction upyaaaa afu mimi ndo wa kuhangaika na wewe! Sitakiiiii! Hans niliokufanyia maishani mwako naweza kujivika cheoxha mama yako mzazi na nikiwa katika hii mamlaka nasema Serwa SIMTAKIIII! Tafuta msichana jinga jinga wa uwezo wako! Serwa anaweza kuwa hata CIA Ghost akakamatwa siwezi kiruhusu u risk maisha yetusababu ya Gapuchi! Na hio kazi ya usafi siitaki!
Kikao kikaishia hapo! Kesho nikampeleka mwangu shule na kuulizia kama kuna shuleya watu wazima! Nikaambiwa ipo night school! Nikajianikisha! Jioni namuaga mama mtoto naenda zangu shule! Mimi na shule tulivo vitu viwili tofauti sasa! Na mama mtoto anavonikatisha tamaa! Mwanangu ana ni support na Serwaa anani support! Japonimeacha kazi kwake bado tuna chat! Bahariabaharia tu!
Mambo aliokuwa anasema mama Linda yana mashiko! Kweli akijua mimi nabet drug addiction hawezi kunikubali! Sina kazi, sina mbele wala nyuma! Naelekea 40s! Pamoja na yote lazima nimle! Hata nikimkosa nimeonja!
Namtongoza kinge kidogo mwanangu n shule kikaanza kupanda! Ananiwekea uzibeeee! Namwambia toka nije huku ulaya sija do! Naumiaaa! Nionee huruma! Najua unanitaka! Protocal za nini maisha mafupi! Anazuga zuga! Jamaniiii! Sikati tamaaa!
Kumla pale kwake isingewezekana mwanagu mapepe sana!Atatuktisha! Nikalipia lodge mbali kidogo! Nikamwambia kama kubet tu ndouanaume njoo huku nikupige show! Nikajiwekeaakija poa, asipokuja poa!kama zali akaja! Nikamtafuna kisawasawa! Na hivi mwanaume suruali,msingi kiuno show moja ya kibabe! Heshima ikawepo!
Tofauti na nilivodhania atakuwa na tabia za kizungu kumbe walaaa! Mtotowa ki ghana ana maadili yote ya kiafrika! Kuniletea maji jikoni fresh! Nikasema wewe binti huna bahatiiii! Lazima nikutiemimba! Bongo sirudi ngoooo!
Mtotoana kazi nzuriana maweeee! Na mwanaume suruali napewama care! Nyumbani nikawa wa uhaba! Ma date kama yote! Mtoto kapagawa ananidolishia mpaka Accra huko kwa ndugu zake! Anawaambia Tanzania! Kanumbaa! Yes! Dimond platnumz! Yes!
Wasomaji wenyewe mnanijua kama mimi bahariaa! Nampanga mapemaaa kama umniridhia na hali yangu niko tayari kufunga ndoa na wewe! Anytime uko ready sema niko ready! Namvuruga kabisaaa! Mwanangu nae anatoa ushirikiano kwa mama wa kambo ulionyooka! Mama mtu dawa yake ndogo kuona Linda anafaidi pale kwa Serwa anapendwa na nini na yeye akajaaaa! Tukawa one big happy family! And i was trully happy after so long!
INAENDELEA KESHO SERIOUSLY
Nimerudi rasmiiii! Mida ya wanga kama kawaida!
Huko magharibi ya mbali mida ya wanga haijafika tu?Nimerudi rasmiiii! Mida ya wanga kama kawaida!
Asee pole , mi nikajua labda uwa unaandika at kwenye note pad kidogo kidogo then badae unkuja ku copy na ku oast. But mi ushaur wangu usiwe unatumia muda mwingi kutype just use five to eight min use iyo notepad yako ktk simu then save it badae uwe unadondosha ma vitu nasi uku maisha yatakua poa , jah bless kichwa na mikono yakoKichwani dear! Narumia nusu saa!
GOMA LILIIISHIA HAPA!Najua mshapata upande mmoja wa story yangu ya kufumaniwa! Nasisitiza msomaji huo ni upande mmoja tu! Na umeletwa kwa lengo la kunichafua na kuninyongonyeza! Na kunifanya nionekane sina thamani, wala sina maana yoyote!
Mwanzo kabisaa niliolewa out of fear na stigma huenda bikaishia peke yangu! Maana kasumba kasumba hizi! We kataa wanaume wa maana, wanapoteaga hawa! Utakosa hata wa kukupa mambo! We jitie mchagua sanaa! Mwisho utachagua koroma!
Hizi tantalila zikaniingia nikajikuta tu nipokwenye kona nalazika kufanya mamuzi magumu! Moyo haujaridhia ila jamii ndo imenoshika kidete! Maana ilifika stage mashosti wote wameolewa! Kila mtu anaenda kwake kupika! Yuko busy na mume wake! Nikasema hapa sina namna! Sina ujanja! Kuendana na kasi hiisina budi kuolewa! Liwalona liwe!
Kipindi hiko huyu mume wangu kubwa la maadui alikuwa malaya mbwa! Alikuwa na pesa kama yote! Na mimi i was doing more than okay! Nilikuwa nishakuwa head wa idara! Na napokea pesa nzuri! Nishajenga, nishanunua Prado! Kibongo bongo naweza sema nishamaliza kila kitu! Bado tu kuolewa na kuzaa!
Nilikuwa na challange moja! Kila mwanaume anaekuja anakuja kimaslahi! Siku mbili nyingi ashaanza umatonya! Na mimi jamani niwe muwazi kufuga mabwana sio zangu kabisaa kabisaa! Hata paka simfugi mie itakuwa bwana? Thubutuuuuuuu! Bwana akianza tu vizinga kanikosaaa!
Sasa huyu mwakitombile ndo ikawa na nafuu! Japo sasa file lake ndo chafu chafu halifai! Ila financially he was doing more than well! Ana kampuni zake mwenyewe! Na pesa anazo! Na familia yake pesa ipo! Hata akikupa ofa ya outing ni Dubenga, siku ingine Tokyo! Sio mambo ya kitoto!
Watu wananikumbusha mama chamba sanaaa! Chamba mpaka utoke na mavi! We mkaka mzuri, pesa anayo,unachotaka kitugani? Umalaya umalaya kitu gani baba ako mzazi mwenye malaya vile vile ukichunguzakama unabisha muulize mama yako mzazi! We pishana na fuko la pesa kwenye maandamano uone kama atakosa mke!
He was nice to me, and treating me nice! Nikakubali niolewe! Alivokuwa maloveee kipindi chote cha harusi ungemjua sasa? Mpaka kuchagua nguo huyu hapa! Sijui nini huyu hapa! Zikafanyika sherehekama zote! Nikajipa moyo sijafanya makosa!
Maisha yakawa ya kawaida mwanzo! Upendo upo upo kishkaji! Nikazaa watoto wa 3 still we were going strong! Baada ya hapo kurudi ndo saa 5! Ukimuuliza anakwambia nisinywe na washkaji! Kwanza nakuoa nakunywa! Itakuwa sasa! Usinipangie!
Inapita miezi mwanaume hakushikiiii! Hachokozi mechi! Mimi sinyoi na yeye hanyoi! Misitu ya Amazon na Congo! Ukiuliza sababu hamnaaa! Hamna ugomvi useme umuombe mtu msamaha hamnaaa! Imetokea tu!
Ukiulizakwawengine wanakwambia wembe ni ule ule! We mwezi tu hajakugusa mie nina miaka mi 3! Haki nakuapiaaa! Kaka angu yuleee! We mbona una nafuuu kubwa sanaaa! Ndo ndoa hio! Nawaulizasasa wenzangu mnajiburudishaje? Mzee ndo hanihitaji sasa genye zangu nafanya vipi! Naambiwa mtu mzima HAPANGWI! Jiongeze!
Watu hawakupi majibu ya moja kwa moja! Nikawaulizaau niombe talaka yangu? Wakasema alafu? Mitoto mi 3 utampelekea nani? Hio ramani ya kuzimu tumboni nani ataihitaji, na hizo nyama zilizolegea je? Papa hio imepitisha watoto wa 3, kama valuation of assets tunasema SCARP VALUE! We ndo basi ushafeliii! Na huo ndo ukweli! We bana hapo hapo! Acha kuwa postive! Think of your mother! She stayed with pops not because she loved him, she had no where to go na nyie! Overtime nafsi itakomaaa! Utazoea!
Nawaa!bia hapana aisee! Why do we have to end up like this? Mmmmmmh! Wanaguna! Wanakwambia huko nje kumebadilika! Sio kama ulivokuacha! Sahivi hata wewe ukimtaka kijana umlipe wewe! Umgharamie ndo aingize kojoleo lake akojoe! Ama sivo uibe mabwana za watu, na wakikumata wenywe topaz za uso tu kukuhusu! Bora uendelee kumbembeleza mumeo akufanye hivo hivo hata kwa kungangania!
Think on the bright side! Unajitamba mbele za watu una mume! Umepata wa kukustiri! Una familia! Watu wakiongea familia fyoko fyoko unayo pia! You basically have it all on the outside! Japo u ajua on the inside you have nothing! Who cares? Either way life facks us all!
Nawaambia huyu bwana hawezi kuwa ankaa miezi yote hii hana mwanamke uko nje! Lazima ana mwanamke nawaambia! Naambiwa unauliza majibu! Pigia jibu mstari funga kitabu! Ukisema ukichokonoe utayapata mazito kuliko unayotafuta! Unaweza kukuta mumeo hana wanawake hukonje ila ndo yeye mwenyewe anageuzwa mwanamke! Mwana kulitafuta mwana kulipata! Tuliza mishono mitatu hio lea watoto hao!
Nikaanza kuongea na mume wangu kidiplomasia? Nini tatizo? Nini kimebadilika? Mbona hakuwa hivo! Kama nimekukosea nisamehe! Anasema unapenda sanaa drama! Na mapenzi ya tamthilia! Sisiwazazi sahivi! Tushapita huko! Mara unapenda mapenzi ya kugeza sanaaa!
Nawauliza wenzangu nini kimebadilika! Wananiambia kilichobadilika ulikuwa kijana sasa ni mzee! Afu ubataka upewe wzifa wa vijana! Heheheeee! Kama mazuri vile! Nikambembeleza Mr! twende counseling! Marriage councelling! Akagoma kabisaa! Anasimamia ndoa haina tatizo tatiP ni mimi napenda drama!
Nimevumilia ndugu msomaji miaka kama mi 3! Wa 4 nikaja kufuma sms! Ana mwanamke afu kamjengea nyumba huko Kitunda kubwaa, nzuri hatariii! Nikamsaka huyo mwanamke mpaka nikamjua! Afu mtu mzima sasa! Ana watoto wa 4! Baba tofauti! Hana uzuri wowote ndugu msomaji! Anauza cafe ya chakula! Mama lishe apande juu kidogo!
Niliumiaaa sanaa moyo! Niliumia sanaaaa! Nikaanza kumchatisha kama mkaka nipo bank! Namba si ninayo! Akajaa haraka haraka! Akanielekeza mpaka hapo caffe! Nikaenda! Nikamuangaliaaa! Nikamtumi sms acha kutembea na waume za watu! Nitakitia ki cafe hiko kiberiti! Akajibu mumeo atanifungulia ingine kama alivonifungulia hii! Jeuriii ndugu msomaji! Navowaambia jeuri hamjamjua kabisaa!
Nikapata ujasiri wa kumuuliza kwani mume wangu unampa nini lakini? Akajibu hata nikikwambia jeuriya kumpa hiko nachompa unayo? Nikamuuliza nini unampa acha kuzunguka! Akajibu Matakoz! Mpe na wewe kama unaona rahisi atatulia kwenye ndoa kama maji ya mtungi heheheeeyaaaa!
Nikaona napoteza tu mda! Bwana nilimshika mashati si kidogo! Nikamwambia naondoka na wanangu! Akasema ukiondoka namuha!ishia humu ndani kama unataka kutukomoa bora tu ubakie! Nishakwambia nilipitiwa nitajirekebisha! Nikajipa matumaini anajitutumua tu ila atajirekebisha!
Kweli lileshangingi aliachana nalo! Manake likawalina ni text naona unaloga sanaa siku hizi kuniharibia! Sijui unalala na mganga! Heheheee! Nikajua ashaachika! Nikamjibu cha kuazima hakistiri wowoo! Asharudi nyumbani. Na matusi tukawa tunafanya kama kawaida! Upendo ukarejea!
Miezi mi 3 mingi! Ratiba zikarudia pale pale! Nikajaribu kujua anatembea na nani? Sikuwezakujua kabisaa! Nikakata tamaa! Nikawa nimejikalia nasononeka tu! Nikaja kupenyezewa anatembea na ndugu yake! Wa mbali ila udugi wa kuvuta manati upo! Nikamuuliza akaniambia wewe ni pumbavu kabisaa! Nikatembeee na ndugu yangu ili? Hata kama umaluuni ndo nimekosa kabisaaa kiasi hiko? Hataaaaa! Haiwezekani! Nikamuamini asilimia 100. Ikaja baadae kujulikana tena na mume wa huyu ndugu! Ilikuwa aibu ya kufungia mwaka ndugu msomaji! Alirudi nyumbani mikono nyuma!
Akaanza kutembea na binti wa 18 yrs! Msomaliiiii! Kadogo kakorofiiii Alshababu wa kike! Huyu ndo hajifichi kabisaa! Anawambia wanangu yeye anti! Mwambieni mama yenu anti anawasalimia! Kwanza sikutaka kufanya nae ligi sababu ni mdogo sanaa! Ningeweza kumzaa kama ningeamuaga kuzaa na miaka 16! Afu design nishachokaaa! Najua akitoka huyo ataokota mwingine! Nikakubali tu matokeo!
Akamtia mimba yule msomali akampangishia! Akawa ndo mke mdogo tena! Miminavumilia tu ndugu msoaji! Moyo ukawa u ejaa sumu! Sumu kaliii! Mpaka nikaanza kuumwa pressure! Watu waka ipeleka kwe ye maombi! Maombi yalinisaidia kusamehena kurejesha amani na pressure ikaisha kabisaa!
Nimezunguka makanisa mengi sanaa! Mpaka kufika kwa pastor! Pastor mara ya kwanza nawaona na mkewe kiukweli walinivutia! Anajua thamani ya mke! Anampa mkewe nafasi! Wanavosema apatae mke kapata kitu chema basi anavokienzi sasa! Mwanaume ndo yule!
Akaanza kunipa huduma! Wanangu wako boarding wote, Mr ndo vasco da gama! Nikamjaza mimi single mother! Huku na huku tukaanguka dhambini! Mkewe aliistukia! Na mimi sikuachia sababu na mimi nporwa mume natulia! Nabebewa mume natulia! Na safari hii mwenye mume atulize kitenesi!
Kama biliwaza danger ya fumanizi labda upande wa Mozah! Sio mume wangu! Maana ashanichoka na kunisusa kabisaakabisaa! Sikuwaza kwamba mimi kuchepuka kutamtoa roho kiasi kile! Sikuwahi kuwaza! After all the cheatings nilizomkamata sikutegemea angenivua nguo kiasi kile! Tuna watoto wakubwa! Uzuri wako nje! Na aliwahonga gazeti wamsanue pastor sanaa mimi wafunike funike! Hata sura yangu haikutoka! Wala kazini hawakijua! Still it was inhuman!
Yeye akanipa talaka akajua kanimaliza! Mimi nikaenda mahakamani kufungua kesi rasmi ya talaka na tugawane mali! Hapo kwenye kugawana mali palimvuruga sanaaa! Akakimbilia kwa paroko tusuluhishwe ndoa za kikristo hazina talaka! Paroko akaniandikia wito mara 3 wa kuitwa parokiani! Sikwenda! Akamtuma mwenyekiti wa jumuiya! Nikamwambia nimeokoka sahivi so automatically sio kondoo wake!
Mimi nimeweka wana sheria law firm! Na pendekezo langu nipewe 80% ya mali na custody ya watoto! Nika sight kuzaa nje kwamba kaoa mtu mwingine kiserikali ana ishi nae! Akaona kesi imemkalia vibaya! Akaja kidiplomasia! Anasisitiza watoto watoto! Akaomba msamaha hasira tu! Akaomba anipe mali kiduchu tuyamalize kishkaji! Nikamwambia tukutane mahakamani! Mchaga alidataaaa!
Mlokole kiukweli baada ya tukio alisikitisha sanaa! Mozah alimfukuza nyumbani! Kumbe nyumba wanayoishi ni ya Mozah! Nikampa pesa akapange hoteli ya gharama! Ananiambia siwezi kurudi madhabahuni naomba nitafutie
mtaji wa biashara yoyote!
Msomaji kama mjuavyo sifugi mabwanaa mimi!Kila sms akituma anaomba pesa! Kama mimi ndo nimemzaa vile! Alinichosha sio kidogo! Nifanyie hiki nifanyie kile! Like seriously! Utetezi wake siwezi kupanda madhabahuni! Nikamwambia inaweza kupanda vizuri sanaa! Akasema siwezi gazeti limesambaa nchi nzima!
Nikamwambia kwani mbona wenzio wanasimuliaga nilikuwa jambazi! Nilikuwa kibaka, nilikuwa jela ndo wokovu ukanijiaaa! Na waumini tunatoa Amen za kutoshaa tu! Sasa wewe utasema Nilikuwa Mzinzi, muasherati kasingiziwa! Nikafumaniwa na mke wa mtu, na kuandikwa gazetini! Tafuta gazeti la tarehe flani na mwaka flani utaniona front page! Lakini bwana kaniletea wokovuuuu! Haleluyaaaah! Sasa nahubiri neno! Mbona Amen zitakuwa za kutosha tu?
Anajitetea pale, shida yake asifanye kazi aishi kwa mgongo wangu! Aaaah subutuuuuuuu! Nikaona hatuelewani! Nika mblock! Akawa hana pa kunipataaa kabisaaa! Atanipatia wapi mie mtoto wa mjini? Kama Mozah ndo alikuwa anmfuga ni Mozah huko huko sio mie! Kabisaaa!
Woga tu ndugu msomaji ndo ulikuwa unanirejesha nyuma! Kesi yangu inanguruma! Nikaanza kutongoza vikaka vya bank! Hawa njaa kali! Nikampata mmoja! Kimuonekano ana njaaa na nilitegemea ana njaa! Lakini nimeanza kutoka nae hakuwahi kuniomba kitu! Labda mimi kwa nafsi yangu ndo nimpe!
Mwenyewe kwa kujisikia tu rohoni mwangu nikampatia MarkX, nikampangia na appartment niwe najiachia huko! Mtu wa bata sanaaa! Na mimi watoto wakubwa sina majukumu basi tunajiachia wote sanaa sanaaa! Burudaniii! Watu ofisni wanaongea, lazima waongeee si unajua jelousy, ila sisi hatuna habari!
Siku tunatoka kwenye bata akawa ana search station nikasikia kama sautinaijuaaa! Nikamwambia acha hapo hapo! Ilikuwa Wapo Radio! Nikasia " Mimi nilikuwa mzinzi tena muasherati kweli kweli, nishafumaniwa na mke wa mtu na picha kusambaa magazetini ila leo Nawtangazia wokovuuuu! Ameeeen! Ameeeen! Yesu huyuhuyu alieniokoa mimi mkaribishe kwenye maisha yako! Haleluyaaah! Ameeen! Za kutosha kabisaa!
ITAENDELEA!