Dr. Chapa Kiuno
JF-Expert Member
- Sep 11, 2009
- 443
- 18
</SPAN>
Tovuti ya Beautifulpeople.com inayosajili watu wenye mvuto pekee
Tovuti kwaajili ya kutafuta wachumba ambayo huwatenga watu wenye sura mbaya zisizo na mvuto imezidi kukua na wanachama wake wamezidi kuongezeka.
Pamoja na kupigiwa kelele kwa kutengeneza matabaka ya watu, website kwaajili ya kutafuta wachumba ambayo huwatenga watu wote wenye sura mbaya ambazo hazina mvuto, imezidi kukua na kufungua matawi zaidi ya tovuti hiyo kwenye nchi mbali mbali duniani.
Beautifulpeople.com inasisitiza kuwa mtu anayetaka kuwa mwanachama wa tovuti hiyo lazima atume picha yake kwanza ili wanachama waliopo waijadili kama ana sura yenye mvuto aruhusiwe kuwa mwanachama.
Kutokana na njia hiyo inayotumika kupata wanachama, ni mtu mmoja tu kati ya watano wanaotamani kujiunga na tovuti hiyo ndiye hufanikiwa kukubaliwa kujiunga na kundi la watu wenye mvuto duniani la tovuti hiyo.
Tovuti hiyo ilianzishwa miaka michache iliyopita nchini Denmark na baadae ilifungua matawi yake nchini Uingereza, Japan na Marekani na sasa imeamua kuruhusu wanachama toka nchi zote duniani.
"Kama utaenda baa na kuamua kumtongoza mtu lazima utamchagua yule aliyekuvutia, huwezi kwenda kwa mtu mwenye sura mbaya asiye na mvuto", alisema Greg Hodge mwenye umri wa miaka 34 ambaye ni mkurugenzi mtendaji wa tovuti hiyo.
"Watu wamechoka kupoteza muda na pesa kukutana na watu ambao hawana mvuto wowote wa kimapenzi", alisema Greg.
Hadi sasa tovuti hiyo ina jumla ya wanachama 180,000 ambao wanakubalika na tovuti hiyo kama watu wenye mvuto.
Tovuti ya Beautifulpeople.com inayosajili watu wenye mvuto pekee
Tovuti kwaajili ya kutafuta wachumba ambayo huwatenga watu wenye sura mbaya zisizo na mvuto imezidi kukua na wanachama wake wamezidi kuongezeka.
Pamoja na kupigiwa kelele kwa kutengeneza matabaka ya watu, website kwaajili ya kutafuta wachumba ambayo huwatenga watu wote wenye sura mbaya ambazo hazina mvuto, imezidi kukua na kufungua matawi zaidi ya tovuti hiyo kwenye nchi mbali mbali duniani.
Beautifulpeople.com inasisitiza kuwa mtu anayetaka kuwa mwanachama wa tovuti hiyo lazima atume picha yake kwanza ili wanachama waliopo waijadili kama ana sura yenye mvuto aruhusiwe kuwa mwanachama.
Kutokana na njia hiyo inayotumika kupata wanachama, ni mtu mmoja tu kati ya watano wanaotamani kujiunga na tovuti hiyo ndiye hufanikiwa kukubaliwa kujiunga na kundi la watu wenye mvuto duniani la tovuti hiyo.
Tovuti hiyo ilianzishwa miaka michache iliyopita nchini Denmark na baadae ilifungua matawi yake nchini Uingereza, Japan na Marekani na sasa imeamua kuruhusu wanachama toka nchi zote duniani.
"Kama utaenda baa na kuamua kumtongoza mtu lazima utamchagua yule aliyekuvutia, huwezi kwenda kwa mtu mwenye sura mbaya asiye na mvuto", alisema Greg Hodge mwenye umri wa miaka 34 ambaye ni mkurugenzi mtendaji wa tovuti hiyo.
"Watu wamechoka kupoteza muda na pesa kukutana na watu ambao hawana mvuto wowote wa kimapenzi", alisema Greg.
Hadi sasa tovuti hiyo ina jumla ya wanachama 180,000 ambao wanakubalika na tovuti hiyo kama watu wenye mvuto.