Hute
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,537
- 6,458
kuna jamaa kanipigia simu leo hii kutoka Biharamuro huko kagera, anasema kuna wafanyakazi wanne wa immigration hapo mjini kwao, wamekamatwa kufunguliwa kesi mahakamani kwa kosa la kuwapatia vibali feki wawekezaji wa kizungu mgodi wa Tulawaka wa Barick, vibali ambavyo selikali ingepata milion zaidi ya hamsini, lakini watu hawa waliziweka pesa hizo mifukoni mwao na kutoa vibali visivyo tambulika na uhamiaji. issue hiyo nasikia ilikuwa kubwa sana kwasababu hapo mjini hao jamaa walikuwa maarufu sana, hasa kwa kuchukua mademu na kutembelea magari mazuri. kama kuna waandishi wa habari kutoka huko, tunaomba updates na kesi imeendeleaje. idara ya uhamiaji imeoza. wazungu hao wamekaa hapa kwa muda, walikuwa wakiingia na kutoka kupitia boda zetu bila shaka, vipi hawakukamatika hadi leo hii? au kuna mtandao wa ufisadi uhamiaji?