Kama picha inavyojieleza yenyewe, hao jamaa wanawaingiza vifaranga wa samaki bwawani, ila naona nyaya kama za umeme zimetoka kwenye switch zikaingia bwawani na kuna kichwa kikubwa tu sijui nawaza ni kwa ajili ya nini. Anayejua matumizi yake tafadhali tusaidiane maarifa. kwa kuhisi tu nikafikiria ni heating system ili kuyapasha maji yapate joto ili vifaranga vizoee mazingira mapya bila mshtuko. sijui lakini sijawahi kuona hapa bongo