Wazoefu wa biashara ya boda boda na bajaji, njoo mtujuze changamoto mnazokumbana nazo

Biashara ya boda boda ni nzuri Sana, ila inachangamoto zake km zilivyo biashara zingine tu. Chamoto kubwa kabisa ni uaminifu kwa hao vijana wanao tufanyia kazi. Ili kukabiliana na changamoto hizo yafuatayo uyazingatie.

1. Anza pikipiki mpya but zile za Bei nafuu
2. Fanya utafiti wa tabia za hao vijana unaotaka kuwapatia.
3. Zingatia umri wa hao vijana above 18 age na ikwezekana awe ameoa.
3. Malipo yawe kwa kila wiki
4. Fanya kwa mkataba(miezi 11)
5. Kila siku akuletee 10000 chukua malipo kwa wiki
6. Funga GPS kwenye hizo boda hiyo itakurahisishia kuzifuatilia popote utakapokuwepo.
7. Hakikisha pikipiki umeikatia vibali vyote mhimu km vile bima, Sumatra n.k
8. Hakikisha kijana unaemkabidhi hicho chombo lazima awe na leseni ya drive. pia km anafamilia yake karibu ni vyema kuishirikisha familia yake na ikiwezekana wamzamini.

Nafikiri kwa kuanzia hayo yanatosha mengine, utapa izoefu huko mbele ya Safari
Hii comment ndio imemaliza maelekezo yote.
Hata Mimi mwaka huu mkataba wangu wa kazi uliisha nikanunua pikipiki 2 mwezi wa kwanza nikawapa vijana wastaarabu ninaowafaham nashukur mungu hawanisumbui kabisa.
Na hizo pikipiki ndio zinanisaidia kunipa hela za kulisha familia.
Ingekuwa Nina pesa nyingi ningenunua hata 10 niwe na uhakika wa hela za kuendesha familia halaf baada ya hapo ndio ningewaza biashara nyingine.
Uzur wa hii biashara naipenda kwa sababu hainiharibii muda wangu na pia hakuna haja ya kumlipa mshahara dereva bali anajilipa mwenyewe.
 
Hii comment ndio imemaliza maelekezo yote.
Hata Mimi mwaka huu mkataba wangu wa kazi uliisha nikanunua pikipiki 2 mwezi wa kwanza nikawapa vijana wastaarabu ninaowafaham nashukur mungu hawanisumbui kabisa.
Na hizo pikipiki ndio zinanisaidia kunipa hela za kulisha familia.
Ingekuwa Nina pesa nyingi ningenunua hata 10 niwe na uhakika wa hela za kuendesha familia halaf baada ya hapo ndio ningewaza biashara nyingine.
Uzur wa hii biashara naipenda kwa sababu hainiharibii muda wangu na pia hakuna haja ya kumlipa mshahara dereva bali anajilipa mwenyewe.
Hapo kwenye kuweka GPS , ni Best idea
 
Kasumba ya bajaji au pikipiki kwa mkataba imeharibu kabisa upatikanaji wa faida kwa mmiliki.
Unanunua pikipiki 2,200,000/ halafu unatoa kwa mkataba wa miezi 10 unapata 3,000,000/ Faida 800,000/ Bado insurance n.k. Heri utafute biashara itakayokupa laki 1 kea mwezi.
Umenena vyema kabisa. Laki 8 faida kutoka 2.2mil ni kama 3% tu kwa mwezi. Heri hata ukaange mihogo stand aisee.
 
Kasumba ya bajaji au pikipiki kwa mkataba imeharibu kabisa upatikanaji wa faida kwa mmiliki.
Unanunua pikipiki 2,200,000/ halafu unatoa kwa mkataba wa miezi 10 unapata 3,000,000/ Faida 800,000/ Bado insurance n.k. Heri utafute biashara itakayokupa laki 1 kea mwezi.
Lakini kumbuka hiyo staili ya mkataba sio lazima.
Ni wamiliki wa pikipiki ndio walibuni hvyo baada ya kuona madereva ni wasumbufu kuleta hesabu.
Kwa hyo ukiona staili ya mkataba huipendi unaweza kutumia ile staili nyingine ya bila mkataba ambayo unapokea 7000 kwa siku bila kikomo yaani pikipiki inabaki kuwa yako miaka yote.
 
Lengo la biashara ya bodaboda libaki tu kuwa ni kuwainua vijana wanaoendesha sio faida kwa BOSS, kwa style ya mkataba unapata kama 1M faida kwa mwaka (say 10k kila siku) baada ya hapo boda sio yako tena.... bila mkataba utapokea kama elfu 7 kila siku bila kikomo ila service ni juu yako na utajuta kwa maana dereva ni kama atataka kukukomoa.
 
Hiyo biashara pasua kichwa, sikushauri mkuu m10 yako fikiria jambo jingine.

Nikitulia nitakupa changamoto zake kwa uzoefu wangu mimi.
 
Kama huendeshi wewe bora hizo hela uzitunze

Msimtishe Bhana kwani Boda boda zote , unazoziona mitaani kila mtu dereva ndo mmiliki wa chombo? Kila biashara unayoina mtaani jua ina faida ndiyo maana unaendelea kuiona
 
Hiyo biashara pasua kichwa, sikushauri mkuu m10 yako fikiria jambo jingine.

Nikitulia nitakupa changamoto zake kwa uzoefu wangu mimi.
Kiukweli Bodaboda sio biashara ya kudumu na kuitegemea kwa miaka yote bali unaweza kuifanya Kama daraja wakati unafikiria vitu vingine vya kufanya.
Kwa mfano biashara ya bodaboda huwa naipenda inapotokea nimepata hela za ghafla na sijajipanga kibiashara akilini mwangu huwa nawahi kununua bodaboda ili nipate pesa za kujikimu na kuulinda mtaji wangu.
Kwa mfano Kama nimepata milioni 10 Sasa hivi nitanunua bodaboda 2 fasta kwa mil 4 ili nipate hela za kula na milioni 6 zinatulia benki wakati huo natafuta biashara nyingine ya kufanya.
 
Msimtishe Bhana kwani Boda boda zote , unazoziona mitaani kila mtu dereva ndo mmiliki wa chombo? Kila biashara unayoina mtaani jua ina faida ndiyo maana unaendelea kuiona
Jambo si kutishana ila tunaelezea uhalisia wake.. Biashara hii inalipa endapo ukipata kijana mzuri na mwenye kujali chombo
Mimi mwenyewe niliingiza 7m ila kilichotokea sina hamu
 
Nunua bodaboda 6,toa kwa mkataba,itakuwa rahisi kuzidabo kufikia 12,then uweke bajaji.
Changamoto ipo kupata dereva mwaminifu.
 
Mkuu hiyo biashara pasua kichwa inabd uwe mkorofi haswaa..km una plot kajenge msururi ht nyumba vitatu upokee kodi. Otherwise piga uber mwenyewe kama una muda
 
Ukiataka kufanya jambo lolote usiwasikilize waliofeli watakukatisha tama, jifunze kwa waliofaulu. period
Biashara yoyote inahitaji research. Kama utashindwa kufanya research kwa walioshindwa na kufaulu lazima hiyo biashara itakushinda. Siku zote binadamu hutamani na kupenda kusikia mazuri kwenye masikio yake.
Hauna tofauti na wale wenye biashara za makaratasi yaani anaangalia faida tu huku amesahau kuwa biashara yoyote ina changamoto zake.
 
Biashara yoyote inahitaji research. Kama utashindwa kufanya research kwa walioshindwa na kufaulu lazima hiyo biashara itakushinda. Siku zote binadamu hutamani na kupenda kusikia mazuri kwenye masikio yake.
Hauna tofauti na wale wenye biashara za makaratasi yaani anaangalia faida tu huku amesahau kuwa biashara yoyote ina changamoto zake.
Ukitaka kujua utamu wa Ngoma ingia ucheze. Research ni muhimu sanaa lakini usifanye research kwa walioshindwa. Mfano mdogo tuu ukiwa chuo field si unaenda sehemu ambayo ni productive ili ufanye kwa vitendo ujifunze, How can you go and learn to unproductive entity. Point yangu ni kwamba tafuta mtu anae run biashara then ndo atakupa the best experience then utajua faida na changamoto.
 
Salamu wana Jukwaa....

Nimepata wazo la kuanzisha biashara ya Boda boda na Bajaji kuanzia mwezii wa 11 jijini Dar es salaam, naanza biashara hii baada ya kujibana kwa kipindi cha miaka 3 sasa.


Nimewekeza kiasi cha Milioni 10, nitaanza kwa Bajaji 1 na Boda boda 1. Nipata wazo hili huku nikiamini suala la usafiri kwa jiji la Dar es salaam bado ni Changamoto kwa ujumla.


Nimeshaanza mchakato wa kutafuta vijana wawili kutoka mtaa ninao toka, Changamoto nilizonazo kwa sasa ambazo ningependa mawazo wakuu na utatuzi ni:


1. Kwa wale wazoefu ni changamoto/ hasara gani mnakumbana nazo?

2. Mfano wa mkataba kuweza kuwapatia wafanyakazi kabla ya kuanza kazi.

3. Makusanyo ya hela yafaa kwa muda gani hasa (wiki au siku)?

4. Mbinu za kumbana dereva aweze kuleta hela kwa wakati unaotakiwa.

5. Pikipiki (boda boda) & Bajaji za kampuni gani ndo bora zaidi?
Wasikukatishe tamaa kila biashara ina changamoto zake huwezi kuishi bila changamoto mm mwenyewe nilianza ivo ivo sasa ivi naona kawaida tu ww kama unayo 10 ingiza kwenye biashara unaweza kushangaa imekubali


Asanteni Wakuu...
 
Back
Top Bottom