Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Mojawapo ya mijadala mikubwa si kwa Tanzania tu bali hata nchi nyingine ni suala hili la chanjo dhidi ya ugonjwa wa COVID-19. Nchi mbalimbali zimejaribu na zile tajiri zimefanikiwa kwa haraka kujitengenezea chanjo zao na kujinufaisha wao wenyewe kwanza kabla ya wengine. Cuba ni miongoni mwa nchi zinazojitegemea kwa kiasi kikubwa sana linapokuja suala la afya na utaalamu wa tiba.
Kujitegemea huku kumeifanya Cuba kuwa miongoni mwa taifa yaliyofanikiwa sana linapokuja suala la tiba na afya. Kwenye suala la corona Cuba iliamua kutumia uwezo wake wa ndani wa kupambana na gonjwa hili na hili limekuwa kweli pia katika chanjo.
Nimefuatilia toka mwanzo walipoanza kutanganza kuwa wanatengeneza chanjo yao wenyewe Soberana 2. Serikali yao imetangaza jana kuwa tayari chanzo yao inaenda kufanyiwa majaribio ili kupima usalama wake na uwezo wake (safety and efficacy) katika kupambana na virusi vya corona. Wamesema wanaenda kujaribu kati ya watu wenye umri wa miaka 2-18. Ikumbukwe hii chanjo ni kwa ajili ya vijana na watoto. Kwa watu wazima Cuba inatumia chanjo iitwayo Abdala ambayo inaonesha mafanikio ya karibu asilimia 92 (inakaribiana na zile za Pfizer, Moderna na Astrazeneca na hata Sputnik ya Warusi.
Kutokana na ushirikiano wetu na udugu wa kihistoria kati ya Tanzania na Cuba; serikali ione jinsi gani inaweza kuzungumza na Cuba kuruhusu majaribio ya chanjo yao na endapo inafanya kazi ipasavyo kutumia njia hiyo badala ya kutumia njia ya COVAX na mitego mingine ambayo inaacha maswali kama ni suala la afya au ni mtaji fulani.
Kama tuna lengo la kuwalinda Watanzania tuone namna ya rahisi na salama zaidi kwa kushirikiana na Cuba. Na nina uhakika Cuba hawatochukua muda mrefu kushirikiana naasi hata kuzalisha chanjo hiyo hapa hapa nyumbani na kuwa namna ya kusaidia chanjo kwa bara letu badala ya kuwasubiri wakubwa watuamulie.
Ni wazo tu. Hakuna kujitegemea kwa maana zaidi kama kule kwa mawazo. Vinginevyo, wakubwa hawa watatubana na hatutajua nini... si tuna msemo "rafiki wakati wa shida..." Ninajua kuna masuala ya vikwazo vya kiuchumi ambavyo vimewekwa na wakubwa uhusiana na Cuba... tuna uthubutu wa kushirikiana nao licha ya vikwazo?
Habari zaidi:
Cuba says Abdala vaccine 92.28% effective against coronavirus
Cuba said on Monday its three-shot Abdala vaccine against the coronavirus had proved 92.28% effective in last-stage clinical trials.
www.reuters.com
Cuba's vaccine rivals BioNTech-Pfizer, Moderna – DW – 06/27/2021
Cuba's health authorities said this week the domestically produced Abdala vaccine has proven to be 92% effective against the coronavirus in clinical trials. DW takes a closer look.
www.dw.com