Wazo: Serikali ianzishe kura ya maoni wananchi wafichue Ofisi, Idara, Vitengo na Taasisi za Serikali zilizokithiri kwa urasimu nchini

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
46,887
143,983
Moja ya vitu vinavyokera sana nchi hii ni urasimu ulioko katika maofisi, idara, vitengo na taasisi mbalimbali za serikali.,urasimu unaopaswa kuwekewa mkakati maalumu kudhibiti.

Urasimu huu sio kero tu watanzania, bali hata kwa wageni wakiwemo wawekezaji wanaotafuta vibali au huduma nyingine serikalini na hivyo kuchangia kufukuza wawekezaji.

Unakwenda katika wizara au taasisi fulani ya serikali kutafuta kibali, leseni , n.k au hata kugongewa muhuri lakini utasumbuliwa mpaka unaweza kujuta kuzaliwa nchi hii.

Yote hii ni kwasababu katika baadhi ya idara na taasisi za serikali, kumejaa miungu watu waliolewa madaraka na bahati mbaya hakuna utaratibu uliowekwa kudhibiti urasimu serikalini na ndio maana wanatesa na kusumbua watu.

Urasimu mwingine unachangiwa na taratibu na sheria mbovu zinazopelekea mchakato mirefu kabla ya mtu kupata kile anachohitaji na wakati mwingine taratibu ndefu ndio huchangia rushwa pale mtu anapochoka na kuuamua kutafuta shortcut.

Binafsi nafikiri wakati umefika wananchi wapige kura ya maoni ya wazi au vinginevyo kufichua idara na taasisi za serikali zilizokithiri kwa urasimu hapa nchini na matokeo yawekwe wazi kwa umma

Idara na taasisi zitazoonekana kupigiwa jura nyingi, zichunguzwe na hatua stahiki zichukuliwe.

Sometimes kuna urasimu hata wa kupitisha mambo ya kiserikali pale taasisi au idara fulani inapotakwa kutoa kibali kwa taasisi nyingine au kupitisha maombi ya idara au taasisi nyingine ndani ya serikali.

Urasimu na rushwa ni vitu viwili tofauti vinavyofaa kushughulikiwa kila kimoja kwa uzito wake ingawa vinaonekana kwenda pamoja.

Nakerwa sana na urasimu uliopo katika nchi yetu kuliko hata rushwa.
 
Yaani mkuu unataka Nyani amsnitch sokwe?

Btw, huwezi kutenganisha urasimu na rushwa. Kimoja ni njia ya kumtengeneza mwenzie, na mwenzake ni matokea ya njia iliyotengenezwa na huyo mmoja.
 
Yaani mkuu unataka Nyani amsnitch sokwe?

Btw, huwezi kutenganisha urasimu na rushwa. Kimoja ni njia ya kumtengeneza mwenzie, na mwenzake ni matokea ya njia iliyotengenezwa na huyo mmoja.
Ni rahisi kudhibiti urasimu kuliko rushwa na ukidhibiti urasimu utakuwa umedhibiti na rushwa.

Kwa mfano, kuchukua hatua kwa Maafisa au watumishi wa serikali wasiojfanyia kazi maombi yanayoletwa katika ofisi zao ndani ya muda fulani(kuweka time limit kwa kila ofisa kufanyia kazi document anazopewa na kulalamika kutoa maelezo muda huo unapopita).

Ni rahisi kuweka mikakati ya kudhibiti ucheleweshaji kuliko kudhibiti rushwa inayofanyika kwa siri(rushwa haionekani bali urasimu kila mtu anauona hata kama mtu ni kipofu)


Ni bahati mbaya tumeshindwa kuwaza kwa mapana kujua sometimes hivi ni vitu viwili tofauti ingawa vinaenda pamoja.

Tunatumia nguvu nyingi kudhibiti rushwa halafu urasimu tumeuacha wakati kuna mazingira ya urasimu yanayozaa rushwa ingawa sometimes pia rushwa ndio chanzo cha urasimu.

Tunachosau ni kuwa sio kila rushwa ndio inatengeneza urasimu bali sometimes urasimu unatokana na watu kuwa wavivu, kutokaa ofisini, n.k ndio kunapelekea watu watoe rushwa ili mambo yao yaende hata kama muhusika amechelewesha jambo kwa uvivu au uzembe bila kuwa na nia ya kutaka rushwa.

Kinachotokea ni mtu anaehitaji kuhudumiwa kutafsiri ucheleweshaji huo unatokana na muhusika kutaka rushwa kumbe sometimes ni matokeo ya uvivu, uzembe, kutokaa ofisini na mambo mengine ya aina hiyo na hivyo atatoa rushwa ili jambo lake lifanyiwe kazi haraka(hapa urasimu ndio unakuwa ni chanzo cha rushwa).

Vile vile panapokuwa na taratibu ndefu za kufuata kabla ya kukamilisha mchakato wa kupata huduma au kibali, n.k, michakato hii mirefu teyari inatengeneza urasimu hivyo sometimes watu huona ni bora watoe rushwa taratibu zisifuate ili jambo lake likamilike haraka( hapa napo urasimu ndio unakuwa ni chanzo cha rushwa.
 
Tuna kazi! Unaweza kuta taratibu za kupata huduma au kibali ni fupi ila mtoa huduma anarefusha process ili apate chochote..
 
dhalimu kaondoka haya mambo sio ya kuomba yanatakiwa yawepo by default.
 
Moja ya vitu vinavyokera sana nchi hii ni urasimu ulioko katika maofisi, idara, vitengo na taasisi mbalimbali za serikali.,urasimu unaopaswa kuwekewa mkakati maalumu kudhibiti.

Urasimu huu sio kero tu watanzania, bali hata kwa wageni wakiwemo wawekezaji wanaotafuta vibali au huduma nyingine serikalini na hivyo kuchangia kufukuza wawekezaji.

Unakwenda katika wizara au taasisi fulani ya serikali kutafuta kibali, leseni , n.k au hata kugongewa muhuri lakini utasumbuliwa mpaka unaweza kujuta kuzaliwa nchi hii.

Yote hii ni kwasababu katika baadhi ya idara na taasisi za serikali, kumejaa miungu watu waliolewa madaraka na bahati mbaya hakuna utaratibu uliowekwa kudhibiti urasimu serikalini na ndio maana wanatesa na kusumbua watu.

Urasimu mwingine unachangiwa na taratibu na sheria mbovu zinazopelekea mchakato mirefu kabla ya mtu kupata kile anachohitaji na wakati mwingine taratibu ndefu ndio huchangia rushwa pale mtu anapochoka na kuuamua kutafuta shortcut.

Binafsi nafikiri wakati umefika wananchi wapige kura ya maoni ya wazi au vinginevyo kufichua idara na taasisi za serikali zilizokithiri kwa urasimu hapa nchini na matokeo yawekwe wazi kwa umma

Idara na taasisi zitazoonekana kupigiwa jura nyingi, zichunguzwe na hatua stahiki zichukuliwe.

Sometimes kuna urasimu hata wa kupitisha mambo ya kiserikali pale taasisi au idara fulani inapotakwa kutoa kibali kwa taasisi nyingine au kupitisha maombi ya idara au taasisi nyingine ndani ya serikali.

Urasimu na rushwa ni vitu viwili tofauti vinavyofaa kushughulikiwa kila kimoja kwa uzito wake ingawa vinaonekana kwenda pamoja.

Nakerwa sana na urasimu uliopo katika nchi yetu kuliko hata rushwa.
Urasimu ni moja ya sifa ya serikali zote duniani. Tunatofautiana viwango tu!
 
Moja ya vitu vinavyokera sana nchi hii ni urasimu ulioko katika maofisi, idara, vitengo na taasisi mbalimbali za serikali.,urasimu unaopaswa kuwekewa mkakati maalumu kudhibiti.

Urasimu huu sio kero tu watanzania, bali hata kwa wageni wakiwemo wawekezaji wanaotafuta vibali au huduma nyingine serikalini na hivyo kuchangia kufukuza wawekezaji.

Unakwenda katika wizara au taasisi fulani ya serikali kutafuta kibali, leseni , n.k au hata kugongewa muhuri lakini utasumbuliwa mpaka unaweza kujuta kuzaliwa nchi hii.

Yote hii ni kwasababu katika baadhi ya idara na taasisi za serikali, kumejaa miungu watu waliolewa madaraka na bahati mbaya hakuna utaratibu uliowekwa kudhibiti urasimu serikalini na ndio maana wanatesa na kusumbua watu.

Urasimu mwingine unachangiwa na taratibu na sheria mbovu zinazopelekea mchakato mirefu kabla ya mtu kupata kile anachohitaji na wakati mwingine taratibu ndefu ndio huchangia rushwa pale mtu anapochoka na kuuamua kutafuta shortcut.

Binafsi nafikiri wakati umefika wananchi wapige kura ya maoni ya wazi au vinginevyo kufichua idara na taasisi za serikali zilizokithiri kwa urasimu hapa nchini na matokeo yawekwe wazi kwa umma

Idara na taasisi zitazoonekana kupigiwa jura nyingi, zichunguzwe na hatua stahiki zichukuliwe.

Sometimes kuna urasimu hata wa kupitisha mambo ya kiserikali pale taasisi au idara fulani inapotakwa kutoa kibali kwa taasisi nyingine au kupitisha maombi ya idara au taasisi nyingine ndani ya serikali.

Urasimu na rushwa ni vitu viwili tofauti vinavyofaa kushughulikiwa kila kimoja kwa uzito wake ingawa vinaonekana kwenda pamoja.

Nakerwa sana na urasimu uliopo katika nchi yetu kuliko hata rushwa.
Kuna Whistleblower Protection Act kamanda. Itumie vizuri. By the way Dj utamu wa asali umemuelemea😁😁😁
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom