Wazo Mbadala: Mkataba wa kuajiriwa uwe mwisho miaka 10 ili kukabiliana na changamoto ya ukosefu wa Ajira.

FAJES

JF-Expert Member
Oct 29, 2017
714
627
Amani kwenu Wadau,

Kama tuonavyo kuwa idadi ya Wahitimu wa Vyuo katika fani mbalimbali ni kubwa kuliko uwezo wa Upatikanaji wa Ajira hasa Serikalini.

Na ni dhahiri kuwa, si rahisi kwa vijana wahitimu kuwa na mitaji ya kujiajiri. Hivyo basi, Serikali inaonaje kama ikifupisha umri wa mtu kustaafu kazi kutoka miaka 55-60 na kuweka utaratibu wa mtu kusitisha mkataba wake wa kazi anapofikisha miaka kumi kazini.

Faida za kufanya hivyo ni kama ifuatavyo:

1) Vijana wengi wanaomaliza vyuo mbalimbali na kutegemea ajira na wao watapata haki ya kufanya kazi kwa wingi wao maana fursa za ajira zitakuwa nyingi.

2) Waajiriwa wengi watapambana usiku na mchana kufanya kazi kwa bidii ili kuwekeza zaidi maana watakuwa na fursa ya kufanya kazi muda mfupi wa miaka 10 kuliko ilivyo sasa kuwa mtu akishapata kazi anabweteka kwakujua ana ajira ya kudumu hadi uzeeni.

3) Usemi wa asiye na ajira ajiajiri utafanikiwa kivitendo maana hawa watakaomaliza mkataba wao wa miaka 10 watakuwa na mtaji ambao watautumia kujiajiri.

Karibu kwa mawazo mbadala wakuu.!
Yangu ni hayo...
 
Bado changamoto zitakuwepo tu hapo uenda umewaza vyema, lakini mfano MTU anayehitimu Leo ukimwambia asubirie ndani ya miaka kumi ili kusubiri MTU ambaye mkataba wake utaisha ndani ya maiaka kumi siamini kama bado Huyo anayesubiria atakuwa kwenye mstari Wa kuhitaji hiyo ajira.
 
Niliwahi suggest katika majadiliano ya kawaida na wenzangu kuwa umri wa ku retire uwe maximum 45 ili kutengeneza ajira.

Maana yangu kubwa ilikuwa waliopo kwa muda wa miaka 20 wamejitosheleza kwenye capital na possibility ya kujishughulisha na mambo mengine ni kubwa kulinganisha na ambao wapo mtaani.

Ilileta tabu kweli office, kwa kweli ni namna bora ya kushare national cake. Binafsi nakuunga mkono.

Ita encourage wawekezaji na wajisiriamali wakubwa kwa wadogo.

Dah nilishambuliwa sana, sometimes wanakumbushia kama utani.
 
Tatizo la ukosefu wa ajira rasmi Tanzania linachangiwa zaidi na mabwanyeye au watendaji dhaifu ambao kazi zao ni kukaa maofisini wakipitisha sera na sheria ambazo hazina tija wala msaada kwa raia na badala yake sheria hizi zimekuwa kandamizi na za kurudisha nyuma maendeleo......


Mifano ni mingi, nenda katika maofisi ya serikali na work plan nzuri ambayo inaweza ajiri watu na kutengeneza ajira, kuna utaowakuta watakuzima aidha kwa kukwambia uwatoe kitu kidogo au watakukata kwa kuhofia kuonekana hawajui kitu......
 
Tumeona umetoa FAIDA za uamuzi huo pekee hujaongelea upande wa ATHARI HASI za mpango huo.

Kimsingi uamuzi huo utakuwa na athari pamoja na zingine:-

1). Mabadiliko makubwa ya sheria e.g sheria za kazi, utumishi pamoja na sera zake e.g PSSSF, ELRA, PSA n.k

2). Kutokuwa na watumishi wenye ujuzi na uzoefu kazini e.g Majaji, Madaktari, mathalani tutakuwa na majaji wenye uzoefi miaka 2 kazini tofauti na sasa kuwa jaji lazma uwe na miaka 10 na zaidi.

3). Kuongezeka kwa magonjwa ya akili na msongo wa mawazo (depression and strokes) baada ya mtumishi kuachishwa kazi pale tu miaka 10 inapotimia angali ndo anaoa, anasomesha watoto, anajenga n.k

4). Kushamili/Kukithiri kwa rusha kwan kila mtumishi atakuwa anapambana/anawahi muda wake mfupi kabla haujaisha. (Km ambavyo sasa inawanakabiri wenyeviti wa mabaraza ya Ardhi na nyumba wilaya (DLHT), Wahadhiri wa vyuo vikuu n.k ambao huajiliwa kwa mkataba wa miaka mitatu mitatu.

NINI CHA KUFANYA/KIFANYIKE
Sio kama ambavyo wewe umependekeza bali ni:-
(a) Kubadili mitaala mashuleni, vyuo n.k ili kuendana na elimu ya kujiajiri. Hii ni pamoja na kusisitiza KILA KATA KUWA NA CHUO CHA UFUNDI STADI kilichoboreshwa. E.g ususi, ufugaji nyuki, ushonaji, uhunzi, ujenzi, usindikaji n.k

(b) Serikali kuunda chombo/taasisi/mamlaka ya kukopesha wahitimu wa vyuo mitaji ya kujiajili isiyokuwa na RIBA na ya muda mrefu ili wahitimu kutumia elimu yao baada ya wao kuandika ANDIKO MRADI (Business Plan) na kupeleka wny chombo hicho. Kama HESLB inavyofanya. Yaan kiwepo chombo ambacho kama HESLB inavyokopesha wanafunzi basi chenyewe kikopeshe WAHITIMU ili waendeshe miradi yao bila riba.

MFANO: watu/mtu amehitimu utabibu/maabara na hana ajira na yupo mtaani wakati kuna maeneo km nyanda za juu kusini, kati, na kanda ya ziwa mgonjwa huhitaji kusafiri zaidi ya Km 20 kwa pikipiki (almost 10,000 to and 10,000 fro) kupata huduma tu ya kupima kiwango cha PROTEIN, HB, na BP pindi AKIWA MJAMZITO ili dokta aone kama hana KIFAFA CHA MIMBA.

Wakati huo kuanzisha kituo cha upimaji magonjwa (Maabara) kidogo hata kwa shilingi 10Milioni inatosha, tatzo ni 10m anatoa wapi huyu graduate, so taasisi hiyo inampa bila riba mfn kwa miezi 84 na mwaka wa kuanza biashara asilipe chochote. Ila apeleke BUSINESS STATEMENT kila mwezi kwa chombo hicho.
 
Tumeona umetoa FAIDA za uamuzi huo pekee hujaongelea upande wa ATHARI HASI za mpango huo.

Kimsingi uamuzi huo utakuwa na athari pamoja na zingine:-

1). Mabadiliko makubwa ya sheria e.g sheria za kazi, utumishi pamoja na sera zake e.g PSSSF, ELRA, PSA n.k

2). Kutokuwa na watumishi wenye ujuzi na uzoefu kazini e.g Majaji, Madaktari, mathalani tutakuwa na majaji wenye uzoefi miaka 2 kazini tofauti na sasa kuwa jaji lazma uwe na miaka 10 na zaidi.

3). Kuongezeka kwa magonjwa ya akili na msongo wa mawazo (depression and strokes) baada ya mtumishi kuachishwa kazi pale tu miaka 10 inapotimia angali ndo anaoa, anasomesha watoto, anajenga n.k

4). Kushamili/Kukithiri kwa rusha kwan kila mtumishi atakuwa anapambana/anawahi muda wake mfupi kabla haujaisha. (Km ambavyo sasa inawanakabiri wenyeviti wa mabaraza ya Ardhi na nyumba wilaya (DLHT), Wahadhiri wa vyuo vikuu n.k ambao huajiliwa kwa mkataba wa miaka mitatu mitatu.

NINI CHA KUFANYA/KIFANYIKE
Sio kama ambavyo wewe umependekeza bali ni:-
(a) Kubadili mitaala mashuleni, vyuo n.k ili kuendana na elimu ya kujiajiri. Hii ni pamoja na kusisitiza KILA KATA KUWA NA CHUO CHA UFUNDI STADI kilichoboreshwa. E.g ususi, ufugaji nyuki, ushonaji, uhunzi, ujenzi, usindikaji n.k

(b) Serikali kuunda chombo/taasisi/mamlaka ya kukopesha wahitimu wa vyuo mitaji ya kujiajili isiyokuwa na RIBA na ya muda mrefu ili wahitimu kutumia elimu yao baada ya wao kuandika ANDIKO MRADI (Business Plan) na kupeleka wny chombo hicho. Kama HESLB inavyofanya. Yaan kiwepo chombo ambacho kama HESLB inavyokopesha wanafunzi basi chenyewe kikopeshe WAHITIMU ili waendeshe miradi yao bila riba.

MFANO: watu/mtu amehitimu utabibu/maabara na hana ajira na yupo mtaani wakati kuna maeneo km nyanda za juu kusini, kati, na kanda ya ziwa mgonjwa huhitaji kusafiri zaidi ya Km 20 kwa pikipiki (almost 10,000 to and 10,000 fro) kupata huduma tu ya kupima kiwango cha PROTEIN, HB, na BP pindi AKIWA MJAMZITO ili dokta aone kama hana KIFAFA CHA MIMBA.

Wakati huo kuanzisha kituo cha upimaji magonjwa (Maabara) kidogo hata kwa shilingi 10Milioni inatosha, tatzo ni 10m anatoa wapi huyu graduate, so taasisi hiyo inampa bila riba mfn kwa miezi 84 na mwaka wa kuanza biashara asilipe chochote. Ila apeleke BUSINESS STATEMENT kila mwezi kwa chombo hicho.
Mkuu, safi sana. Umetoa maoni kinzani kwa ufasaha na ustadi wa hali ya juu. Hata hivyo, baadae kidogo nitaleta majibu au maoni kinzani tena kuhusu hoja zako ulizotoa hapo juu..
 
Amani kwenu Wadau,

Kama tuonavyo kuwa idadi ya Wahitimu wa Vyuo katika fani mbalimbali ni kubwa kuliko uwezo wa Upatikanaji wa Ajira hasa Serikalini.

Na ni dhahiri kuwa, si rahisi kwa vijana wahitimu kuwa na mitaji ya kujiajiri. Hivyo basi, Serikali inaonaje kama ikifupisha umri wa mtu kustaafu kazi kutoka miaka 55-60 na kuweka utaratibu wa mtu kusitisha mkataba wake wa kazi anapofikisha miaka kumi kazini.

Faida za kufanya hivyo ni kama ifuatavyo:

1) Vijana wengi wanaomaliza vyuo mbalimbali na kutegemea ajira na wao watapata haki ya kufanya kazi kwa wingi wao maana fursa za ajira zitakuwa nyingi.

2) Waajiriwa wengi watapambana usiku na mchana kufanya kazi kwa bidii ili kuwekeza zaidi maana watakuwa na fursa ya kufanya kazi muda mfupi wa miaka 10 kuliko ilivyo sasa kuwa mtu akishapata kazi anabweteka kwakujua ana ajira ya kudumu hadi uzeeni.

3) Usemi wa asiye na ajira ajiajiri utafanikiwa kivitendo maana hawa watakaomaliza mkataba wao wa miaka 10 watakuwa na mtaji ambao watautumia kujiajiri.

Karibu kwa mawazo mbadala wakuu.!
Yangu ni hayo...
Aliyewaambia serikalini ni pakuja kupatia uzoefu nani? Miaka ya zamani ulikuwa haujariwi serikalini kama huna uzoefu japo wa miaka 2, kama unataka kuishi kwa stress anzia kazi serikali utazeeka huna kitu kichwani, Maana serikalini hautendi ila unasimamia sasa utasimamia kwa kutumia madesa uliyosoma Chuo? Na kumbuka mambo mengi unayosoma huko ukija kazini utakutana na miongozo, taratibu, sera mwishowe utachoka
 
Hili wazo lilikuwepo toka zamani ila naona wengi wanalichukulia juu juu tu,angalieni na urahisi wa mapuppet kuingia kwenye mifumo yetu kirahisi zaidi.
 
Kwa taarifa yako tu, Serikali inafikiria kuongeza umri wa kustaafu, na tayari wameshafanya kwa wahadhiri, madaktari na majaji. Sasa hivi ukistaafu kwa hiari kwa miaka 55 unakatwa baadhi ya fedha. Yaani kifupi hawafurahii watu kustaafu mapema wana discourage watu kustaafu mapema.

Sera ya menejimenti ya Utumishi wa umma inasema kustaafu kwa hiari ni miaka 50 kwa lazima ni 55. Lakini sheria za hifadhi ya jamii zimekwenda tofauti na Sera hiyo ya kitaifa.

Unajua kwanini? Mifuko ya hifadhi ya jamii haina uwezo uwezo wa kuhudumia wastaafu wengi, na jinsi maendeleo yanavyoongezeka umri wa kuishi unaongezeka hivyo mzigo wa kulipa pension unakuwa mkubwa sana kwao. Kwahiyo mifuko inaweza kufa mapema. Pili jumlisha na kukopwa, Serikali chungu chake kikuu cha pili baada hazina ni mifuko ya hifadhi ya jamii sasa waruhusu hiyo sheria itaenda kuponea wapi?
 
Amani kwenu Wadau,

Kama tuonavyo kuwa idadi ya Wahitimu wa Vyuo katika fani mbalimbali ni kubwa kuliko uwezo wa Upatikanaji wa Ajira hasa Serikalini.

Na ni dhahiri kuwa, si rahisi kwa vijana wahitimu kuwa na mitaji ya kujiajiri. Hivyo basi, Serikali inaonaje kama ikifupisha umri wa mtu kustaafu kazi kutoka miaka 55-60 na kuweka utaratibu wa mtu kusitisha mkataba wake wa kazi anapofikisha miaka kumi kazini.

Faida za kufanya hivyo ni kama ifuatavyo:

1) Vijana wengi wanaomaliza vyuo mbalimbali na kutegemea ajira na wao watapata haki ya kufanya kazi kwa wingi wao maana fursa za ajira zitakuwa nyingi.

2) Waajiriwa wengi watapambana usiku na mchana kufanya kazi kwa bidii ili kuwekeza zaidi maana watakuwa na fursa ya kufanya kazi muda mfupi wa miaka 10 kuliko ilivyo sasa kuwa mtu akishapata kazi anabweteka kwakujua ana ajira ya kudumu hadi uzeeni.

3) Usemi wa asiye na ajira ajiajiri utafanikiwa kivitendo maana hawa watakaomaliza mkataba wao wa miaka 10 watakuwa na mtaji ambao watautumia kujiajiri.

Karibu kwa mawazo mbadala wakuu.!
Yangu ni hayo...
Hizo level bado sana kijana
 
Sio ufumbuzi,ufumbuzi ni kufumua mfumo wa elimu,tutumie wa China wao unawajenga watu kwenye uzalishaji yaani kila MTU anaweza jitegemea asubiri ajira
 
Kwa serikali na private ? Maana private sidhani, itakua gharama sana kwao kuachisha mtu mwenye experience ya miaka 10 na kuajiri waliotoka fresh na mafao uwalipe
Pow hata serikalini itakua gharama kubwa mno

Tatizo linalosababisha ukosefu wa ajira nchi nyingi za Afrika ni udhaifu wa sekta binafsi
Kama kulipa mafao ya Mtumishi anayestaafu ni haki yake kisheria kwanini asilipwe.?

Umejaribu kuzungumzia kuhusu suala la Experience kazini, Je ni nafasi zipi katika ajira zinahitaji mtu kuwa na experience kubwa.? Nijuavyo mimi ni kuwa, senior positions ndizo zinahitaji mtu kuwa na experience. Sasa ukiangalia katika mfumo wa ajira, Seniors positions ni chache ukilinganisha na Junior positions. Na hawa wahitimu wengi wa vyuo kwa kiasi kikubwa wapo kwenye category ya Junior positions kuliko senior positions.
 
Unapelekaje mpango kazi wako ofisi ya serikali??
Au sijakuelewa vzr


Tatizo la ukosefu wa ajira rasmi Tanzania linachangiwa zaidi na mabwanyeye au watendaji dhaifu ambao kazi zao ni kukaa maofisini wakipitisha sera na sheria ambazo hazina tija wala msaada kwa raia na badala yake sheria hizi zimekuwa kandamizi na za kurudisha nyuma maendeleo......


Mifano ni mingi, nenda katika maofisi ya serikali na work plan nzuri ambayo inaweza ajiri watu na kutengeneza ajira, kuna utaowakuta watakuzima aidha kwa kukwambia uwatoe kitu kidogo au watakukata kwa kuhofia kuonekana hawajui kitu......
 
Unapelekaje mpango kazi wako ofisi ya serikali??
Au sijakuelewa vzr
Ndio....mwisho wa siku serikalini huwa wanatarajia ubunifu wa miradi ya maendeleo kutoka kwa watu binafsi na raia ili waweze kufanya maendeleo na kuleta mabadiliko.....
 
Back
Top Bottom