Tulimumu
JF-Expert Member
- Mar 11, 2013
- 14,304
- 12,965
Wazo la RC wa Dar kuwasihi wenye nyumba kupunguza kodi hasa wakati huu wa janga la Korona siyo baya kutokana na hali mbaya ya uchumi kwa wengi kwa kuwa biashara nyingi zimesimama au kufa, ofisi na taasisi nyingi zinashindwa kulipa wafanyakazi wao. Kwa sasa wenye uhakika wa kipato ni watumishi wa serikali na mashirika yake tu lakini sekta binafsi ni shida shida tupu.
Mimi naona Makonda ameota ombi zuri lakini angeanza na kuisihi serkali ipunguze bei za mafuta, umeme, maji na kodi ili kuwapa nafuu watu wengi kwa wakati mmoja kuliko kuangalia kundi dogo sana la wapangaji. Serikali inapaswa ianze kuonesha mfano kwa kuona madhira yanayo wapata wananchi wake wengi kwa sasa. Hii hali ya sasa ni kama msiba ambao haujulikani tanga lake litavunjwa lini.
Cha mwisho na yeye Makonda ajitahidi kujikarantini kwa kuepuka kufanya mikusanyiko ya watu kwakuwa licha ya kuwa ni kinyume na maelekezo ya watalaamu lakini ni hatari zaidi kwake na anaowahutubia. Rais mwenyewe kaenda kujifungia Chato sasa na yeye atulie ndani na ikibidi atumie vyombo vya habari kama radio na TV atasikika tu sio lazima azunguke na Mike kama MC (Master of Confusion).
Mimi naona Makonda ameota ombi zuri lakini angeanza na kuisihi serkali ipunguze bei za mafuta, umeme, maji na kodi ili kuwapa nafuu watu wengi kwa wakati mmoja kuliko kuangalia kundi dogo sana la wapangaji. Serikali inapaswa ianze kuonesha mfano kwa kuona madhira yanayo wapata wananchi wake wengi kwa sasa. Hii hali ya sasa ni kama msiba ambao haujulikani tanga lake litavunjwa lini.
Cha mwisho na yeye Makonda ajitahidi kujikarantini kwa kuepuka kufanya mikusanyiko ya watu kwakuwa licha ya kuwa ni kinyume na maelekezo ya watalaamu lakini ni hatari zaidi kwake na anaowahutubia. Rais mwenyewe kaenda kujifungia Chato sasa na yeye atulie ndani na ikibidi atumie vyombo vya habari kama radio na TV atasikika tu sio lazima azunguke na Mike kama MC (Master of Confusion).