Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,474
- 39,987
Nasikia kuna magenius wetu wengine wamekuja na suluhisho jipya la tatizo la nishati ya umeme nchini; kuruhusu makampuni binafsi kuzalisha umeme kwenye mkoa na kuuzia Tanesco. Kisingizio kikubwa kinachotolewa ni kuwa kitaifa suala la kampuni binafsi kuzalisha umeme limekuwa vurugu na gumu kutekelezeka kwa hiyo wameonelea ni bora kutoa tenda ya kuzalisha umeme kimkoa. Baadhi ya makampuni tayari inadokezwa yako mbioni kuanzisha kuzalisha umeme (kama kule Mwanza).
Baadhi ya majina yanayotajwa nyuma ya makampuni haya siyo mageni masikioni mwa Watanzania - mengine tulishayataja kuanzia kwenye Dowans na Meremeta. Sasa sijui wazo hili lina ukweli kiasi gani na litatekelezwa vipi bila kusababisha hasira kwa wananchi.
Nyinyi mnalionaje? Fikiria makampuni yatakayojitokeza kuzalisha umeme kuanzia Dar, hadi Kigoma!!
Baadhi ya majina yanayotajwa nyuma ya makampuni haya siyo mageni masikioni mwa Watanzania - mengine tulishayataja kuanzia kwenye Dowans na Meremeta. Sasa sijui wazo hili lina ukweli kiasi gani na litatekelezwa vipi bila kusababisha hasira kwa wananchi.
Nyinyi mnalionaje? Fikiria makampuni yatakayojitokeza kuzalisha umeme kuanzia Dar, hadi Kigoma!!