Wazo la kuwa na Mfuko wa wasiojiweza Tanzania

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,633
697,794
Kuna kitu kinaniumiza na kunishangaza sana mpaka leo... MAREHEMU KUDAIWA PESA YA MATIBABU!
Hili pengine liko hapa kwetu tuu tena kwenye hospital zetu za setikali ambako ndio wanyonge wengi hukimbilia Tuna viongozi wetu waliojivika wema sana lakini katu sijawahi kuona hili walau wakilinong'ona...NEVER!

Kama majirani ndugu na jamaa wanaweza kusamehe deni lolote walilokuwa wanamdai marehemu serikali yenye ukwasi inashindwa vipi kusamehe gharama za matibabu? Hii ni laana mjue

Kama hujawahi kukumbwa na hiki kitu ni ngumu kuelewa.. Lakini chukulia mfano mmemuuguza kwa hali ngumu sana ndugu yenu ambaye wakati mwingine ndio mtegemewa wa familia. Pengine alipata maradhi mbaya au ajali, mkamuuguza kwa muda mrefu lakini hatimaye akafariki dunia

Mkiwa mko kwenye uchungu mkubws wa kumpoteza mpendwa wenu ambaye sometimes anaacha yatima mjane au mgane.. Kuna dunia mpya ngumu inayoisubiri familia ya namna hiyo kuanzia chakula, mavazi, malazi elimu, afya nk.. Mnazuiwa na uongozi wa hospital husika kwamba hamuwezi kuuchukua mwili wa mpendwa wenu hadi mlipe gharama zake za matibabu! Hili jambo linaumiza sana

Unajiuliza hii ndio serikali yangu ndani ya nchi yangu huru inavyojali raia wake!? Tulimpoteza mjomba wetu mwaka 2007 tena kwa uzembe wa madaktari pale Muhimbili lakini tukanyimwa mwili hadi tulipe deni la matibabu yake kiasi cha million saba na ushee

Huwa nazikumbuka kwa uchungu mkubwa zile siku anko wetu akiwa kalala mochwari sisi tukihangaika kupata milion 7 tuukomboe mwili wa mpendwa wetu!

Tangu hapo nimeendelea kusoma visa vya kusonenesha mno vya ndugu kuzuiliwa kuchukua miili ya ndugu zao mpaka walipe gharama za matibabu ambazo ni mamilion ya shilingi...! Sijawahi kusikia serikali ikisema chochote
Msanii Profesa J yu mgonjwa.. Tunamtakia nafuu ya haraka.. Kwenye maradhi yake fanilia imejitokeza na kuomba msaada..na wamesaidika haraka sana.. Ikiwemo serikali...!

Hospital aliyolazwa Proffesa J kuna mamia ya wagonjwa wenye uhitaji sawa ama zaidi ya J lakini hawana pa kupazia sauti zao zikasikika nao wakasaidika kama J

Tukiamua kwa utayari wetu tunaweza kutenga siku moja kila mwezi tukafanya harambee kubwa na kile kinachopatikana kikaenda kuwasaidia wenye maradhi ya gharama kubwa na wasio na uwezo wa kumudu gharama zake! Harambee hiyo ikiambatana na kuikumbusha serikali walau kubeba gharama za wale wanaokufa huku wakidaiwa mamilion ya shilingi na hawana uwezo wa kupata hata robo yake

Harambee hiyo iende sambamba na kampeni ya bima kwa wote kwa gharama himilivu, Na haya yote yafanyike kwa upendo, kwa kujitoa kwa uaminifu mkuu, hofu ya kimungu na huruma ya kweli.. Kwa kufanya hivyo tunaweza hata kuepuka laana nyingi hasa hii ya kuzuia mwili kwa ajili ya madeni ya gharama za matibabu.

Screenshot_20220214-215253.jpg
 
Siku hizi mna zile saccos, vikoba nk, huko mnawezeshana, kusaidiana na kuchangisha.

Kuna wasio na vikundi hao utengwa na kuachwa na jamii, issue ya Upendo ni ngumu sana mshana, yaani ukizungumzia Upendo kwa wale wakristu unamgusa masiya, Yesu, Emmanuel, Mfalme wa Wafalme nk na kwa Uislam Upendo ndiyo dini yenyewe.

Mada yako nzuri ila kwa dunia ya Tanzania yetu ilipofikia kwa walio kwenye umoja wetu na wasiokuwepo madhira haya hayaepukiki.

Nimejifunza kwa kusoma tabia za Watanzania, yaani tuna roho mbaya na kutamani mwingine apate matatizo iwe msiba au janga hiyo ndiyo inapply sana.
 
Kinachotakiwa ni bima kwa wote,Mfuko wa wasiojoweza ndio nini?

Serikali tupeni bima na namna ya kufanya watu tumeshapendekeza frame work,sh.2000 kila miezi 6 kwa kila kichwa sawa na 4,000 kwa mwaka ,hapo tutapata til.2 ambazo zinatosha Sana kugharamia afya bure.
 
Kinachotakiwa ni bima kwa wote,Mfuko wa wasiojoweza ndio nini?

Serikali tupeni bima na namna ya kufanya watu tumeshapendekeza frame work,sh.2000 kila miezi 6 kwa kila kichwa sawa na 4,000 kwa mwaka ,hapo tutapata til.2 ambazo zinatosha Sana kugharamia afya bure.

Bila Bima tutajidanganya
Hakuna watu wasiokuwa na msaada kama sisi
 
Kinachotakiwa ni bima kwa wote,Mfuko wa wasiojoweza ndio nini?

Serikali tupeni bima na namna ya kufanya watu tumeshapendekeza frame work,sh.2000 kila miezi 6 kwa kila kichwa sawa na 4,000 kwa mwaka ,hapo tutapata til.2 ambazo zinatosha Sana kugharamia afya bure.
Kama umenisoma vema hiyo ni starting point ama kuokoa jahazi kwasasa huku wazo kuu la bima nafuu likichakatwa
 
Msije mkawa mnatengeneza mgogoro mwingine, Nani atakuwa accountable kuuchangia huo mfuko??
 
Kusaidiana ni msingi unaoanzia chini tangu mdogo ukiona wazazi wako wakisaidia wanaohitaji direct

Mzazi anapompa mtoto masikini shati au chakula mbele ya mwanae nae mwanae anajifunza kutoka kwa mzazi mwema na kukua hivyo

Huku niliko wazungu katika kila supermarkets wana sehemu karibu na mlango wa kutokea wameweka kwa ajili ya kuweka msaada wa chakula kwa wanaohitaji
Yaani umenunua mahitaji yako unaamua kuweka packet ya sukari au jam au pasta au chochote ni food bank wanapekewa wanaohitaji
Hapo mtoto anaona

Sisi hatuna utamaduni wa kusaidia

Huwa wanaweka children in need kwenye Tv wanajumuisha waigizaji wote na kuomba mchango huku wanachekesha.

Huwezi amini within an hour tu unaona watu wamesaidia mamilion

Sisi hata 500 kutoa mtu anaona atafilisika kumbe hajui ubahili mbaya
 
Kusaidiana ni msingi unaoanzia chini tangu mdogo ukiona wazazi wako wakisaidia wanaohitaji direct

Mzazi anapompa mtoto masikini shati au chakula mbele ya mwanae nae mwanae anajifunza kutoka kwa mzazi mwema na kukua hivyo

Huku niliko wazungu katika kila supermarkets wana sehemu karibu na mlango wa kutokea wameweka kwa ajili ya kuweka msaada wa chakula kwa wanaohitaji
Yaani umenunua mahitaji yako unaamua kuweka packet ya sukari au jam au pasta au chochote ni food bank wanapekewa wanaohitaji
Hapo mtoto anaona

Sisi hatuna utamaduni wa kusaidia

Huwa wanaweka children in need kwenye Tv wanajumuisha waigizaji wote na kuomba mchango huku wanachekesha.

Huwezi amini within an hour tu unaona watu wamesaidia mamilion

Sisi hata 500 kutoa mtu anaona atafilisika kumbe hajui ubahili mbaya
Nimeona kuna mataifa kadha yana utaratibu wa kufanya hivyo na wengjne kwenye migahawa hulipa zaidi ili bakshish iende kwa wasio na uwezo.. Conditioning ni jambo muhimu sana.. Hatujachelewa tunaweza kuanza sasa na matunda yakaonekana vizazi vijavyo
 
Nimeona kuna mataifa kadha yana utaratibu wa kufanya hivyo na wengjne kwenye migahawa hulipa zaidi ili bakshish iende kwa wasio na uwezo.. Conditioning ni jambo muhimu sana.. Hatujachelewa tunaweza kuanza sasa na matunda yakaonekana vizazi vijavyo

Kweli kabisa mkuu
Mimi nawajua wengi wanaosaidia hivyo kila wanapoona kuna sehemu Ina uhitaji

Na inahitaji waandishi wa habari na vituo vya tv kuwaelimisha watu na kukusanya michango na kusaidia watu

Unakuta huku kila sehemu ya biashara kuna makopo ya chenji inayobaki unatumbukiza humo na kila kopo limeandikwa unasaidia nini kama ni cancer research au vipofu au wagonjwa wa akili wote wanahitaji msaada

Sio eti kila kitu wanategemea serikali la hasha kwani serikali haiwezi kufanya kila kitu hata kama ni matajiri kama Ulaya au USA bali kuna wanaohitaji ambao serikali haiwafikii

Tunaweza sana ila inahitaji promo ya nguvu na kuhamasisha watu kusaidiana
 
Wabongo kodi na tozo ndogo ndogo atuzitaki na tukiwekewa tunalalamika sasa iyo mifuko ya kusaidia au kuudumia watu wasiojiweza mnataka pesa itoke wap kwa wafanyabiashara ambao ni 5% ya watanzania wote

Unapotoa wazo km ilo lako sawa ni zuri ila lazma utuambie na chanzo cha pesa cha kuweza kutimiza yote ayo

Suala la bima kwa waTz wote ilo lipo sku zote kuna mashilika kibao ya serikar yanatoa na kukata bima za bei juu na bima za bei nafuu au tunataka bima za bure bira kutoa kitu chochote
 
Back
Top Bottom