Wazo Korofishi: Magufuli Amuondoe Makonda Aende akawe Mwinjilisti!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,460
39,928
1564871968809.png

PIchani RC Paul Makonda akizuzungumza na wafanyabiashara wa kazi mbalimbali za sanaa ikiwa sehemu ya maandalizi ya ujio wa Mkutano wa SADC. (Picha na habari zaidi kutoka kwa Issa Michuzi. )

Kuna mambo mengine ukiyaangalia yanakufanya ujisikie kufyatuka kidogo. Sina tatizo kwa Makonda kuvaa tshirt au mavazi yoyote yanayoonesha imani yake juu ya Yesu Kristu - Bwana na Mwokozi. Anaweza kuvaa mavazi hayo akiwa nyumbani kwake, akienda zake kanisani au kwenye huduma fulani au hata akiwa likizo.
Nina tatizo na yeye kuvaa vazi hili linaonesha maneno ya "Jesus is my Hope" - "Yesu Tumaini Langu" akiwa katika kitu kinachoonesha ni shughuli ya kikazi au ambapo anafanya kama Mkuu wa Mkoa wa Dar-es-Salaam. Kama Mkuu wa Mkoa wa Dar-es-Salaam siyo jukumu lake kuhubiri Injili au kutangaza imani yake akiwa kazini. Hili ni kweli kwani hata mfanyakazi mwingine wa umma hawezi kwenda kazini asubuhi amevaa tshirt yenye maneno ya kiimani kama hayo.
Huku ndio kunaitwa "kuchanganya dini na siasa" na kuifanya serikali ionekane kama ina "dini". Makonda siyo kiongozi wa kidini hivyo ni makosa ya wazi na yanaoonesha kutokukomaa kisiasa au kiuongozi.
Kama lengo lake ni kutangaza Injili na kushiriki katika huduma ya mavuno basi anaweza kumuomba Rais Magufuli ukipita ugeni wa SADC (au hata mapema) ajiuzulu nafasi yake ili aende kumtumikia Mungu kama Mwinjilisti! Lakini kama ataona vigumu kuomba hivyo basi Rais Magufuli amsaidie kumwarakisha aende kwenye huduma akatangaze habari za wokovu; na kwa jinsi anavyoonekana ana kipawa fulani hivi cha uhubiri. Rais Magufuli amshukuru kijana huyu kwa kazi aliyofanya Dar na ampe likizo hata ya mwaka mmoja (sabbatical) ili aende akahubiri. Akiona inafaa anaweza kumrudisha tena baadaye...

Hili ni wazo korofishi tu...
 
View attachment 1171789
PIchani RC Paul Makonda akizuzungumza na wafanyabiashara wa kazi mbalimbali za sanaa ikiwa sehemu ya maandalizi ya ujio wa Mkutano wa SADC. (Picha na habari zaidi kutoka kwa Issa Michuzi. )

Kuna mambo mengine ukiyaangalia yanakufanya ujisikie kufyatuka kidogo. Sina tatizo kwa Makonda kuvaa tshirt au mavazi yoyote yanayoonesha imani yake juu ya Yesu Kristu - Bwana na Mwokozi. Anaweza kuvaa mavazi hayo akiwa nyumbani kwake, akienda zake kanisani au kwenye huduma fulani au hata akiwa likizo.
Nina tatizo na yeye kuvaa vazi hili linaonesha maneno ya "Jesus is my Hope" - "Yesu Tumaini Langu" akiwa katika kitu kinachoonesha ni shughuli ya kikazi au ambapo anafanya kama Mkuu wa Mkoa wa Dar-es-Salaam. Kama Mkuu wa Mkoa wa Dar-es-Salaam siyo jukumu lake kuhubiri Injili au kutangaza imani yake akiwa kazini. Hili ni kweli kwani hata mfanyakazi mwingine wa umma hawezi kwenda kazini asubuhi amevaa tshirt yenye maneno ya kiimani kama hayo.
Huku ndio kunaitwa "kuchanganya dini na siasa" na kuifanya serikali ionekane kama ina "dini". Makonda siyo kiongozi wa kidini hivyo ni makosa ya wazi na yanaoonesha kutokukomaa kisiasa au kiuongozi.
Kama lengo lake ni kutangaza Injili na kushiriki katika huduma ya mavuno basi anaweza kumuomba Rais Magufuli ukipita ugeni wa SADC (au hata mapema) ajiuzulu nafasi yake ili aende kumtumikia Mungu kama Mwinjilisti! Lakini kama ataona vigumu kuomba hivyo basi Rais Magufuli amsaidie kumwarakisha aende kwenye huduma akatangaze habari za wokovu; na kwa jinsi anavyoonekana ana kipawa fulani hivi cha uhubiri. Rais Magufuli amshukuru kijana huyu kwa kazi aliyofanya Dar na ampe likizo hata ya mwaka mmoja (sabbatical) ili aende akahubiri. Akiona inafaa anaweza kumrudisha tena baadaye...

Hili ni wazo korofishi tu...
Mtoto wa rais hata ikulu anapiga chata...
 
H
View attachment 1171789
PIchani RC Paul Makonda akizuzungumza na wafanyabiashara wa kazi mbalimbali za sanaa ikiwa sehemu ya maandalizi ya ujio wa Mkutano wa SADC. (Picha na habari zaidi kutoka kwa Issa Michuzi. )

Kuna mambo mengine ukiyaangalia yanakufanya ujisikie kufyatuka kidogo. Sina tatizo kwa Makonda kuvaa tshirt au mavazi yoyote yanayoonesha imani yake juu ya Yesu Kristu - Bwana na Mwokozi. Anaweza kuvaa mavazi hayo akiwa nyumbani kwake, akienda zake kanisani au kwenye huduma fulani au hata akiwa likizo.
Nina tatizo na yeye kuvaa vazi hili linaonesha maneno ya "Jesus is my Hope" - "Yesu Tumaini Langu" akiwa katika kitu kinachoonesha ni shughuli ya kikazi au ambapo anafanya kama Mkuu wa Mkoa wa Dar-es-Salaam. Kama Mkuu wa Mkoa wa Dar-es-Salaam siyo jukumu lake kuhubiri Injili au kutangaza imani yake akiwa kazini. Hili ni kweli kwani hata mfanyakazi mwingine wa umma hawezi kwenda kazini asubuhi amevaa tshirt yenye maneno ya kiimani kama hayo.
Huku ndio kunaitwa "kuchanganya dini na siasa" na kuifanya serikali ionekane kama ina "dini". Makonda siyo kiongozi wa kidini hivyo ni makosa ya wazi na yanaoonesha kutokukomaa kisiasa au kiuongozi.
Kama lengo lake ni kutangaza Injili na kushiriki katika huduma ya mavuno basi anaweza kumuomba Rais Magufuli ukipita ugeni wa SADC (au hata mapema) ajiuzulu nafasi yake ili aende kumtumikia Mungu kama Mwinjilisti! Lakini kama ataona vigumu kuomba hivyo basi Rais Magufuli amsaidie kumwarakisha aende kwenye huduma akatangaze habari za wokovu; na kwa jinsi anavyoonekana ana kipawa fulani hivi cha uhubiri. Rais Magufuli amshukuru kijana huyu kwa kazi aliyofanya Dar na ampe likizo hata ya mwaka mmoja (sabbatical) ili aende akahubiri. Akiona inafaa anaweza kumrudisha tena baadaye...

Hili ni wazo korofishi tu...
Wewe ndie umechanganyikiwa
Mtu akivaa barakashia kuna tatizo gani?
Mzee mwinyi akiwa Rais alivaa barakashia mbona hukuhoji?

Wale wanaovaa Rozali muda wote mbona hujahoji?
Mama Samia, Makamu wa Rais masaa yote ushungi anavaa, Huoni anakwaza baadhi ya watu wanaoamini Katika uhuru na usawa, Ushungi ni iwe Jua kali au baridi
Mbona hujahoji ya Mama Samia kuvaa ushungi?

Kwa taarifa yako Makonda Yeye sio mkatoliki, Kwa Imani ya kikatoliki yakupasa kukiri Imani yako sehemu yeyote ile bila hofu na uoga

Makonda anakiri Imani yake kwa kuvaa T shirt na hii ni funzo kwa wakristo Wengine, Mkristu kubeba Bibilia sio dhambi au kuvaa alama ya msalaba wa Yesu msulubiwa sio dhambi

Mbona hujahoji January Makamba kuvaa kanzu wakati anamkabidhi ofisi Simbachawane?

Wewe ni nani hata uingilie watu kukiri imani zao mbele ya jamii?

Mkristu safi au Muislam safi haoni aibu kuvaa ushungi, kanzu, Rozali, barakashia au alama ya msalaba wa Yesu msulubiwa, wataendelea kukiri imani zao daima

Kiongozi wewe ni Gifted Fool,
Mbona hujahoji yale mapete wanayovaa wanasiasa mikononi, Jakaya aliyavaa sana akiwa Rais hata lowasa anayavaa sana na ni Waziri mkuu mstaafu, Je wote wanayapenda na kufurahia alama za mapete yakihusishwa na imani fulani
 
View attachment 1171789
PIchani RC Paul Makonda akizuzungumza na wafanyabiashara wa kazi mbalimbali za sanaa ikiwa sehemu ya maandalizi ya ujio wa Mkutano wa SADC. (Picha na habari zaidi kutoka kwa Issa Michuzi. )

Kuna mambo mengine ukiyaangalia yanakufanya ujisikie kufyatuka kidogo. Sina tatizo kwa Makonda kuvaa tshirt au mavazi yoyote yanayoonesha imani yake juu ya Yesu Kristu - Bwana na Mwokozi. Anaweza kuvaa mavazi hayo akiwa nyumbani kwake, akienda zake kanisani au kwenye huduma fulani au hata akiwa likizo.
Nina tatizo na yeye kuvaa vazi hili linaonesha maneno ya "Jesus is my Hope" - "Yesu Tumaini Langu" akiwa katika kitu kinachoonesha ni shughuli ya kikazi au ambapo anafanya kama Mkuu wa Mkoa wa Dar-es-Salaam. Kama Mkuu wa Mkoa wa Dar-es-Salaam siyo jukumu lake kuhubiri Injili au kutangaza imani yake akiwa kazini. Hili ni kweli kwani hata mfanyakazi mwingine wa umma hawezi kwenda kazini asubuhi amevaa tshirt yenye maneno ya kiimani kama hayo.
Huku ndio kunaitwa "kuchanganya dini na siasa" na kuifanya serikali ionekane kama ina "dini". Makonda siyo kiongozi wa kidini hivyo ni makosa ya wazi na yanaoonesha kutokukomaa kisiasa au kiuongozi.
Kama lengo lake ni kutangaza Injili na kushiriki katika huduma ya mavuno basi anaweza kumuomba Rais Magufuli ukipita ugeni wa SADC (au hata mapema) ajiuzulu nafasi yake ili aende kumtumikia Mungu kama Mwinjilisti! Lakini kama ataona vigumu kuomba hivyo basi Rais Magufuli amsaidie kumwarakisha aende kwenye huduma akatangaze habari za wokovu; na kwa jinsi anavyoonekana ana kipawa fulani hivi cha uhubiri. Rais Magufuli amshukuru kijana huyu kwa kazi aliyofanya Dar na ampe likizo hata ya mwaka mmoja (sabbatical) ili aende akahubiri. Akiona inafaa anaweza kumrudisha tena baadaye...

Hili ni wazo korofishi tu...

Unachosema ni sahihi na kibaya zaidi it seems anatumia dini kama siasa, yaani kuvuta hisia za watu na ndiyo maana kipindi kile akiharibu breki ya kwanza ni church na anamake sure camera zimemchukua akisali kwa hisia ili kuvuta public sympathy
 
Hii si mara ya kwanza kufanya kosa kama hili, hivi karibuni aliwaandalia waislamu futari pale Diamond Jubilee Hall, huku akijua asilimia kubwa waliopo pale ni waislamu akaomba aletewe T-shirt iliyoandikwa JESUS IS MY HOPE.

IMG-20190601-WA0000.jpeg
 
HWewe ndie umechanganyikiwa
Mtu akivaa barakashia kuna tatizo gani?
Mzee mwinyi akiwa Rais alivaa barakashia mbona hukuhoji?

Wale wanaovaa Rozali muda wote mbona hujahoji?
Mama Samia, Makamu wa Rais masaa yote ushungi anavaa, Huoni anakwaza baadhi ya watu wanaoamini Katika uhuru na usawa, Ushungi ni iwe Jua kali au baridi
Mbona hujahoji ya Mama Samia kuvaa ushungi?

Kwa taarifa yako Makonda Yeye sio mkatoliki, Kwa Imani ya kikatoliki yakupasa kukiri Imani yako sehemu yeyote ile bila hofu na uoga

Makonda anakiri Imani yake kwa kuvaa T shirt na hii ni funzo kwa wakristo Wengine, Mkristu kubeba Bibilia sio dhambi au kuvaa alama ya msalaba wa Yesu msulubiwa sio dhambi

Mbona hujahoji January Makamba kuvaa kanzu wakati anamkabidhi ofisi Simbachawane?

Wewe ni nani hata uingilie watu kukiri imani zao mbele ya jamii?

Mkristu safi au Muislam safi haoni aibu kuvaa ushungi, kanzu, Rozali, barakashia au alama ya msalaba wa Yesu msulubiwa, wataendelea kukiri imani zao daima

Kiongozi wewe ni Gifted Fool,
Mbona hujahoji yale mapete wanayovaa wanasiasa mikononi, Jakaya aliyavaa sana akiwa Rais hata lowasa anayavaa sana na ni Waziri mkuu mstaafu, Je wote wanayapenda na kufurahia alama za mapete yakihusishwa na imani fulani

Barakashia, kanzu ni ustaarabu wa middle east havihusiani na dini
Ndiyo maana hata Nyerere na Mrema walikuwa wakivaa hivyo vibaraghashia,
Tshirt pia siyo tatizo, ila maandishi hayo ukiwa ofisini haijakaa sawa kwa mtumishi wa wote
 
HWewe ndie umechanganyikiwa
Mtu akivaa barakashia kuna tatizo gani?
Mzee mwinyi akiwa Rais alivaa barakashia mbona hukuhoji?

Wale wanaovaa Rozali muda wote mbona hujahoji?
Mama Samia, Makamu wa Rais masaa yote ushungi anavaa, Huoni anakwaza baadhi ya watu wanaoamini Katika uhuru na usawa, Ushungi ni iwe Jua kali au baridi
Mbona hujahoji ya Mama Samia kuvaa ushungi?

Kwa taarifa yako Makonda Yeye sio mkatoliki, Kwa Imani ya kikatoliki yakupasa kukiri Imani yako sehemu yeyote ile bila hofu na uoga

Makonda anakiri Imani yake kwa kuvaa T shirt na hii ni funzo kwa wakristo Wengine, Mkristu kubeba Bibilia sio dhambi au kuvaa alama ya msalaba wa Yesu msulubiwa sio dhambi

Mbona hujahoji January Makamba kuvaa kanzu wakati anamkabidhi ofisi Simbachawane?

Wewe ni nani hata uingilie watu kukiri imani zao mbele ya jamii?

Mkristu safi au Muislam safi haoni aibu kuvaa ushungi, kanzu, Rozali, barakashia au alama ya msalaba wa Yesu msulubiwa, wataendelea kukiri imani zao daima

Kiongozi wewe ni Gifted Fool,
Mbona hujahoji yale mapete wanayovaa wanasiasa mikononi, Jakaya aliyavaa sana akiwa Rais hata lowasa anayavaa sana na ni Waziri mkuu mstaafu, Je wote wanayapenda na kufurahia alama za mapete yakihusishwa na imani fulani
Mmkjj kazungumzia maandishi siyo kibaragashia, kibaragashia hakina dini sawa na kanzu haina dini inaweza kuvaliwa hata na askofu, pete, ushungi ni vitu vya wote, ila ni ajabu kumkuta shehe kavaa kanzu au T-shirt imeandikwa Yesu ni Mwokozi Wangu.
 
Hiyo ndio imani yake kwa mimi sioni ajabu
Ukishakumbatiwa na kristo,lazima matendo,mavazi na maneno yawe kikristo
Ili mradi kuvaa fulana akiwa sokoni hakuharibu kazi zake,basi tuwe wavumilivu kwa imani za wenzetu
 
Team roho mbaya hamridhiki
Mtapata presha kisa Makonda
Mtataka kumkagua mpaka Rangi za chupi anazovaa, Jadilini ideas sio personal life ya mtu mtapata presha na kuacha familia nyuma zikitaabika
Barakashia, kanzu ni ustaarabu wa middle east havihusiani na dini
Ndiyo maana hata Nyerere na Mrema walikuwa wakivaa hivyo vibaraghashia,
Tshirt pia siyo tatizo, ila maandishi hayo ukiwa ofisini haijakaa sawa kwa mtumishi wa wote
 
Mlivyojaa Roho za chuki kwa Makonda, Hata kuandika mnashindwa
Mkuu wewe ukiona neno Makonda hata kusoma Maelezo husomi, Unaanza kuflow chorus ya Chuki na Roho mbaya

Vaa barakashia kanisani kama barakashia haina dini
Wewe huna lolote zaidi ya roho mbaya na chuki, mnajitakia magonjwa mengine wenyewe hasa presha
Mmkjj kazungumzia maandishi siyo kibaragashia, kibaragashia hakina dini sawa na kanzu haina dini inaweza kuvaliwa hata na askofu, pete, ushungi ni vitu vya wote, ila ni ajabu kumkuta shehe kavaa kanzu au T-shirt imeandikwa Yesu ni Mwokozi Wangu.
 
Sio kuvuta publicity
Hata wewe Ungekuwa mkuu wa mkoa waandishi wa habari watakufuata tu wakati wote

Mkuu wa mkoa ni mtu mkubwa kimamlaka anamuwakilisha mkuu wa nchi kwenye mkoa sio kitu rahisi

Kila binadamu ana mapungufu hata sisi tukikosea tunakimbilia huruma makanisani au misikitini sema huna cheo nani atakufuata na camera
Unachosema ni sahihi na kibaya zaidi it seems anatumia dini kama siasa, yaani kuvuta hisia za watu na ndiyo maana kipindi kile akiharibu breki ya kwanza ni church na anamake sure camera zimemchukua akisali kwa hisia ili kuvuta public sympathy
 
Mzee Mwanakijiji
Naomba nifanye kazi ya uwakili hasa katika mada ambazo baadhi hatuelewi mantiki yake
"GUSSIE, post: 32376010, member: 262438"]HWewe ndie umechanganyikiwa
Mtu akivaa barakashia kuna tatizo gani?Mzee mwinyi akiwa Rais alivaa barakashia mbona hukuhoji?
Mkuu Baraghashia ni kofia ambayo si vazi la dini.
Kule kwetu Bondei, Lushoto, Upareni, Makambako na Uchagani kofia ni vazi la kawaida hasa kwa wazee kutokana na hali ya hewa

Kofia zipo za aina nyingi, zipo ''pama, kapelo, baraghashia, tarabushi n.k.
Dhana kwamba baraghashia ni vazi la dini inashinikizwa na uelewa butu wa nini ni mavazi
Wale wanaovaa Rozali hujahoji?
Hizo Rozali na tasbihi zina mahali pake.

Inatia kinyaa kiongozi wa umma akiwa katika kazi za umma ambazo ni za wote akishika hizo rozali na tasbihi, achilia mbali mavazi yenye maneno
Mama Samia, Makamu wa Rais masaa yote ushungi anavaa, Huoni anakwaza baadhi ya watu wanaoamini Katika uhuru na usawa, Ushungi ni iwe Jua kali au baridi. Mbona hujahoji ya Mama Samia kuvaa ushungi?
Again, tunaurudi kule kule. Katika misiba hapa kwetu Tz wanawake wanavaa khanga na vitenge.Hilo halionyeshi imani, ni kitu cha utamaduni. Lakini basi huo ushungi hauna maneno!
Kwa taarifa Makonda sio mkatoliki, Kwa Imani ya kikatoliki yakupasa kukiri Imani yako sehemu yeyote ile bila hofu na uoga
NI kweli kwamba kila mtu anapaswa kuikiri imani bila woga au hofu, hata wasioamini wana nafasi yao.

Katiba ya nchi imeeleza hilo wazi.Ni ustaarabu kuelewa unafanya nini na kwa wakati gani.

Wakati mchungaji akisoma sala au Sheikh akiomba dua na wewe ukaingilia kati kutangaza imani yako hovyo hovyo kwasababu unatakiwa uikiri, huo ni ushenzi unaohanikizwa na ujuha wa imani . Kumbuka ushenzi si tusi ni kinyume cha ustaarabu
Makonda anakiri Imani yake kwa kuvaa T shirt na hii ni funzo kwa wakristo. Mkristu kubeba Bibilia sio dhambi au kuvaa alama ya msalaba wa Yesu msulubiwa sio dhambi
Tena hapa unamsaidia MM katika hoja yake.

Kama anaona analo jukumu la kukiri imani yake, basi afanye hivyo bila kutumia nafasi yake inayomtaka aongoze watu wote, wenye imani, wasio na imani , wachawi na vibaka.

Ndiyo maana MM kasema, hajafanya kosa kukiri imani ila apewe fursa ya kichungaji ili akaikiri bila kukirihi wengine kama mtumishi wa umma
Wewe ni nani hata uingilie watu kukiri imani zao mbele ya jamii?
MM anashauri huyu jamaa apewe fursa itakayomsaidia kukiri imani yake bila kutumia ofisi za umma

Kuvaa t-shirt yenye maneno yanayokera wengine akiwa mtumishi wa umaa kunazua ile hoja ya ''kuchanganya dini na siasa''. Pengine kuchanganya ''siasa na dini'' ni halali!!!
Mkristu safi au Muislam safi haoni aibu kuvaa ushungi, kanzu, Rozali, barakashia au alama ya msalaba wa Yesu msulubiwa, wataendelea kukiri imani zao daima
Hizi dini zinatutia upofu kwa baadhi ya nyakati.

Hivi nani anaweza kusimama na kusema ni Mkristo Safi au Muislam Safi?
Ni nani anatoa hizo hadhi!

Hakuna anayezuiliwa kuabudu, lakini hilo lifanyike kwa kuzingatia ustaarabu.
Tukianza kukiri imani hovyo tutakuwa na ''rule of the jungle''
Mbona hujahoji yale mapete wanayovaa wanasiasa mikononi, Jakaya aliyavaa sana akiwa Rais hata lowasa anayavaa sana na ni Waziri mkuu mstaafu, Je wote wanayapenda na kufurahia alama za mapete yakihusishwa na imani fulani
Hivi ukiwa si muumini wa dini huwezi kuvaa pete.

Mwanakijiji, kuna hoja nyingine hapa. Tatizo si la mavazi tu . Siku hizi kuna utamaduni unaoudhi sana. Wakati wa Nyerere na waliofuata salam kwa jamii ilikuwa ''Ndugu wananchi''

Zama hizi kila anayesimama kuzungumza ni '' asalama aleko, bwana yesu asifiwe''

Hivi wasioamini na wasio na dini wana nafasi gani katika jamii inayojinasibu serikali haina dini?

Asalaam alaikum ni ''amani iwe nanyi''. Hata hivyo inavyotumiwa ina viashiria vya udini

Kwanini basi watu wasitumie maneno ya ''amani iwe nanyi' ambayo ni common !!
 
Hiyo ndio imani yake kwa mimi sioni ajabu
Ukishakumbatiwa na kristo,lazima matendo,mavazi na maneno yawe kikristo
Ili mradi kuvaa fulana akiwa sokoni hakuharibu kazi zake,basi tuwe wavumilivu kwa imani za wenzetu

Utetezi wa kijinga sana, ukweli ni kuwa Makonda ni juha/limbukeni asiyejua avae vazi gani kwa hadhira iliyopo. Makonda huyo si alivaa jeans za vijana wa kileo iliyochanika magotini kwenye ibada ya mazishi ya Mengi? Sio mara moja au mbili amevaa t-shirt za kubana na kuacha misuli na kifua chake kuonyesha kilivyo tofauti kabisa na maadili ya kiongozi wa umma, tena huvaa hivyo anapokuwa kwenye shughuli za serikali.

Huyo dogo ni mshirikina sana, ila anavaa vazi hilo na kuigiza ni mcha Mungu ili kujikosha mbele ya umma kwamba ana hofu ya Mungu, jambo ambalo si kweli. Huyo dogo ni mmoja wa watu wanaoendesha siasa za kimafia ndani ya awamu hii. Hii tabia ya kuvaa mavazi yasiyo stahili kwenye hadhira mbali mbali wanayo hata wanaccm wenzake. Sio mara moja au mbili tunaona wanaccm wakivaa mavazi ya chama chao kwenye shughuli za kitaifa kama uzinduzi wa miradi, misiba, michezo nk. Yote haya ni kutokufahamu dressing code ya eneo husika ili kuonyesha misimamo, imani au itikadi zako kwenye hadhira isiyohitaji mavazi hayo.
 
Mzee Mwanakijiji
Naomba nifanye kazi ya uwakili hasa katika mada ambazo baadhi hatuelewi mantiki yake
Mkuu Baraghashia ni kofia ambayo si vazi la dini.
Kule kwetu Bondei, Lushoto, Upareni, Makambako na Uchagani kofia ni vazi la kawaida hasa kwa wazee kutokana na hali ya hewa
Kofia zipo za aina nyingi, zipo ''pama, kapelo, baraghashia, tarabushi n.k.
Dhana kwamba baraghashia ni vazi la dini inashinikizwa na uelewa butu wa nini ni mavazi
Hizo Rozali na tasbihi zina mahali pake. Inatia kinyaa kiongozi wa umma akiwa katika kazi za umma ambazo ni za wote akishika hizo rozali na tasbihi, achilia mbali mavazi yenye maneno Again, tunaurudi kule kule
Katika misiba hapa kwetu Tz wanawake wanavaa khanga na vitenge.
Hilo halionyeshi imani, ni kitu cha utamaduni. Lakini basi huo ushungi hauna maneno!
NI kweli kwamba kila mtu anapaswa kuikiri imani bila woga au hofu, hata wasioamini wana nafasi yao.

Katiba ya nchi imeeleza hilo wazi.Ni ustaarabu kuelewa unafanya nini na kwa wakati gani.
Wakati mchungaji akisoma sala au Sheikh akiomba dua na wewe ukaingilia kati kutangaza imani yako hovyo hovyo kwasababu unatakiwa uikiri, huo ni ushenzi unaohanikizwa na ujuha wa imani . Kumbuka ushenzi si tusi ni kinyume cha ustaarabu Tena hapa unamsaidia MM katika hoja yake.

Kama anaona analo jukumu la kukiri imani yake, basi afanye hivyo bila kutumia nafasi yake inayomtaka aongoze watu wote, wenye imani, wasio na imani , wachawi na vibaka.
Ndiyo maana MM kasema, hajafanya kosa kukiri imani ila apewe fursa ya kichungaji ili akaikiri bila kukirihi wengine kama mtumishi wa umma MM anashauri huyu jamaa apewe fursa itakayomsaidia kukiri imani yake bila kutumia ofisi za umma

Kuvaa t-shirt yenye maneno yanayokera wengine akiwa mtumishi wa umaa kunazua ile hoja ya ''kuchanganya dini na siasa''. Pengine kuchanganya ''siasa na dini'' ni halali!!!
Hizi dini zinatutia upofu kwa baadhi ya nyakati.

Hivi nani anaweza kusimama na kusema ni Mkristo Safi au Muislam Safi?
Ni nani anato hizo hadhi!

Hakuna anayezuiliwa kuabudu, lakini hilo lifanyike kwa kuzingatia ustaarabu.
Tukianza kukiri imani hovyo tutakuwa na ''rule of the jungle''Hivi ukiwa si muumini wa dini huwezi kubaa pete.

Mwanakijiji, kuna hoja nyingine hapa. Tatizo si la mavazi tu . Siku hizi kuna utamaduni unaoudhi sana. Wakati wa Nyerere na waliofuata salam kwa jamii ilikuwa ''Ndugu wananchi''
Siku hizi kila anayesimama kuzungumza ni '' asalama aleko, bwana yesu asifiwe''

Hivi wasioamini na wasio na dini wana nafasi gani katika jamii inayojinasibu serikali haina dini?

Asalaam alaikum ni amani iwe nanyi. Hata hivyo inavyotumiwa ina viashiria vya dini

Kwanini basi watu wasitumie maneno ya ''amani iwe nanyi' ambayo ni common !!
Maelezo marefu. Ila ngoja kwanza, hivi unaweza vaa baraghAshia kisa baridi? Unazungumzia Makambako ipi?

Jambo la hakika ni kua kuna maeneo kanzu na baraghashia siyo vazi la kidini ni la heshima, mfano Bukoba. Ila kuna mavazi yako Associated na dini, na yatachagizwa mno na jina Au asili ya mhusika.

Makamu wetu kwa namna anavyovaa tunAjua ni kutokana na asili yake na makuzi ya Kiislamu. Mwinyi akivaa baraghashia tutawaza hivyo piA.

Kama Makonda amEwahi kufanya maamuzi ya kiKazi na yakawa influenced na dIni basi hiyo likizo na imhusu. Na hii ndiyo maana halisi ya serikali kukosa dini, kwamba dini haitAathiri utendaji kazi wake.
 
Hii si mara ya kwanza kufanya kosa kama hili, hivi karibuni aliwaandalia waislamu futari pale Diamond Jubilee Hall, huku akijua asilimia kubwa waliopo pale ni waislamu akaomba aletewe T-shirt iliyoandikwa JESUS IS MY HOPE.

View attachment 1171793
Serkali inatakiwa kuwa na dress code kwa ajili ya wafanyakazi wake ili kuwatofautisha na watu was kijiweni. Mwezi uliopita tu Serkali imetoa orodha ya nguo ambazo hazitakiwi kuvaliwa ofisini au popote Serkalini.
 
Utetezi wa kijinga sana, ukweli ni kuwa Makonda ni juha/limbukeni asiyejua avae vazi gani kwa hadhira iliyopo. Makonda huyo si alivaa jeans za vijana wa kileo iliyochanika magotini kwenye ibada ya mazishi ya Mengi? Sio mara moja au mbili amevaa t-shirt za kubana na kuacha misuli na kifua chake kuonyesha kilivyo tofauti kabisa na maadili ya kiongozi wa umma, tena huvaa hivyo anapokuwa kwenye shughuli za serikali.

Huyo dogo ni mshirikina sana, ila anavaa vazi hilo na kuigiza ni mcha Mungu ili kujikosha mbele ya umma kwamba ana hofu ya Mungu, jambo ambalo si kweli. Huyo dogo ni mmoja wa watu wanaoendesha siasa za kimafia ndani ya awamu hii. Hii tabia ya kuvaa mavazi yasiyo stahili kwenye hadhira mbali mbali wanayo hata wanaccm wenzake. Sio mara moja au mbili tunaona wanaccm wakivaa mavazi ya chama chao kwenye shughuli za kitaifa kama uzinduzi wa miradi, misiba, michezo nk. Yote haya ni kutokufahamu dressing code ya eneo husika ili kuonyesha misimamo, imani au itikadi zako kwenye hadhira isiyohitaji mavazi hayo.
Naona unalia mpaka umetoa kamasi
Tujikite kwenye hii thread.Ulitaka makonda avae suti sokoni?
Umejuaje kama Makonda ni mshirikina kama wewe si mshirikana?
Acha kukariri maisha,kwani akivaa jeans iliopasuka magotini msibani kwa Mengi anavunja sheria gani?
Badala ya kujadili fursa za Sadc,mnajadili fulana ya yesu kuvaliwa
 
Team roho mbaya hamridhiki
Mtapata presha kisa Makonda
Mtataka kumkagua mpaka Rangi za chupi anazovaa, Jadilini ideas sio personal life ya mtu mtapata presha na kuacha familia nyuma zikitaabika

Wakati mwingine kama huna la kuchangia ni bora ukakaa kimya kuliko kutetea upuuzi. Nikupe mfano mrahisi, walimu wa shule hasa wanawake kwenye shule za serikali hawaruhusiwi kuvaa suruali hasa za jeans wakiwa kazini kwani hayo si maadili. Au pata picha unakutana na mwalimu wa umma anafundisha wanafunzi kavaa kaptula au t-shirt iliyokatwa mikono maarufu kama carwash au singland, na ili kunegosha hilo unaloiita ni personal life kalegeza suruali maarufu kama kata K.

Hakuna anayejadili maisha yake binafsi awapo nje ya kazi za serekali, huko hata akitaka atembee uchi nobody cares, bali dressing code uwapo kwenye hadhira ya umma ndio tunayozungumzia hapa.
 
Mlivyojaa Roho za chuki kwa Makonda, Hata kuandika mnashindwa
Mkuu wewe ukiona neno Makonda hata kusoma Maelezo husomi, Unaanza kuflow chorus ya Chuki na Roho mbaya

Vaa barakashia kanisani kama barakashia haina dini
Wewe huna lolote zaidi ya roho mbaya na chuki, mnajitakia magonjwa mengine wenyewe hasa presha
Mbona kama umepanic mkuu relax
 
39 Reactions
Reply
Back
Top Bottom