Wazo: Biashara ya usimamizi wa magari ( daladala, bajaj, bodaboda )

snochet

JF-Expert Member
Mar 31, 2011
1,407
1,110
Kikwazo kikubwa kinachoathiri biashara ya Daladala leo ni njia na usimamizi wa haya magari. Hii inajumuisha wasimamizi yaani TRA & trafiki, Bima etc.

Biashara ya Daladala imekuwa moja ya uwekezaji hatari zaidi hadi sasa kutokana na wamiliki kushindwa kushika mambo yote,tena ukizingatia wengi wamechukua mikopo na wana shughuli zingine mbali na usimamizi wa daladala.

Nimeona biashara hii kwenye nchi jirani ambapo wanaziita SACCO sijui uhusiano wake na Saccos lakini huwa wanasimamia magari ya watu..Kampuni hii inahusika na usimamizi kamili wa magari na kusimamia ufuatiliaji na tarehe na mileage ya service ya kawaida(oil, mafuta, tairi etc).

Kwa mtu mwenye muda,uwezo anaweza kubeba wazo hili na kulifanyia kazi.

Mtu huyu atakuwa na authority ya kuajiri madereva/deywaka, kupokea hesabu ya siku,pamoja na kuwasilisha hesabu kwa mmiliki ambapo msimamizi atatakiwa kupata 20% ya hesabu yote na mmiliki kupata 80% in a weekly/monthly basis.

Hili wazo linaweza kufanyika kwenye bodaboda/bajaj na vyombo vingine vya usafiri pia.

Sijajua bado kama hapa Tanzania kuna kampuni inafanya hii biashara naomba mnijuze kama ipo na terms zao zikoje watu wajikomboe na ajira zipatikane.
 
Daah bonge la wazo mkuu, kwa hapa nilivyoelewa Hii biashara utaisajili kama kampuni sio, then Wamiliki wa vyombo watakuwa wanakuja kwako wataingia ubia na wewe kama ni mkataba etc. Marejesho ya bosi kama ni kwa mkataba au kila siku utakua unapeleka wewe. Jukumu lako sasa kuvisimamia kutafuta madereva and the so like.

Nice business idea
 
Hapo awali kulikuwa na Co-Cabs lakini kwa sasa kuna Uber, Bolt nk. Hizi zote hutoa huduma hiyo
 
Hapo awali kulikuwa na Co-Cabs lakini kwa sasa kuna Uber, Bolt nk. Hizi zote hutoa huduma hiyo

Wewe hujaelewa...hizo uber na bolt bado wamiliki wanadeal direct na madereva..

Idea ya mtoa mada ni kuondoa hii kitu, yeye anakuwa anapata tu % yake..usimamiz wa kila kitu unabaki kwa kampuni husika.
 
Ah safi sana. Hapo inaondoa stress za mmiliki wa chombo. Niliona matatus nyingi zimeandikwa sacco nilivokua nairobi ila sikuelewa wanamaanisha nini. Je gharama za service zitagharamiwa na sacco ama na mmiliki?
 
Ah safi sana. Hapo inaondoa stress za mmiliki wa chombo. Niliona matatus nyingi zimeandikwa sacco nilivokua nairobi ila sikuelewa wanamaanisha nini.
Je gharama za service zitagharamiwa na sacco ama na mmiliki?
Hiyo itategemea maelewano na makubaliano mtakayoingia.
Hili wazo ni zuri sana.
 
Ipo hyo Kuna jamaa anafanya ila kwa mkataba ndani ya miaka kadhaa gari inakuwa yake.
 
Ah safi sana. Hapo inaondoa stress za mmiliki wa chombo. Niliona matatus nyingi zimeandikwa sacco nilivokua nairobi ila sikuelewa wanamaanisha nini. Je gharama za service zitagharamiwa na sacco ama na mmiliki?
Kwenye bodaboda kama si mkataba service ni ya BOSS so hapa kampuni itakuwa imepewa mkataba na mwenye chombo
A) Kampuni itahusika kufanya Service baada ya muda bodaboda itakuwa na kampuni
B) Kama Boss kampa bodaboda mkataba service atafanya bodaboda na baadae itakuwa yake So kampuni itapata % ya usimamizi tu.

Hii kitu itakuwa Applicable kampuni ikiwa na pesa kwenye Account kwa lolote litalotokea.
 
Wazo zuri sana ila hiyo kampuni ya kusimamia inabidi wafanye kazi ya ziada na tech ihusike pakubwa kudeal na madereva na kazi kweli kweli, kuanzia kutoleta hesabu hadi wizi wa vipuri na mafuta kazi watakua nayo. Ila bonge la IDEA
 
Wakenya wametuzidi sana sie Tanzania, nimeshaanza kuamini hata hii biashara ya Real Estate ilianziaga Kenya kabla ya sisi.
 
Kikwazo kikubwa kinachoathiri biashara ya Daladala leo ni njia na usimamizi wa haya magari. Hii inajumuisha wasimamizi yaani TRA & trafiki, Bima etc.

Biashara ya Daladala imekuwa moja ya uwekezaji hatari zaidi hadi sasa kutokana na wamiliki kushindwa kushika mambo yote,tena ukizingatia wengi wamechukua mikopo na wana shughuli zingine mbali na usimamizi wa daladala.

Nimeona biashara hii kwenye nchi jirani ambapo wanaziita SACCO sijui uhusiano wake na Saccos lakini huwa wanasimamia magari ya watu..Kampuni hii inahusika na usimamizi kamili wa magari na kusimamia ufuatiliaji na tarehe na mileage ya service ya kawaida(oil, mafuta, tairi etc).

Kwa mtu mwenye muda,uwezo anaweza kubeba wazo hili na kulifanyia kazi.

Mtu huyu atakuwa na authority ya kuajiri madereva/deywaka, kupokea hesabu ya siku,pamoja na kuwasilisha hesabu kwa mmiliki ambapo msimamizi atatakiwa kupata 20% ya hesabu yote na mmiliki kupata 80% in a weekly/monthly basis.

Hili wazo linaweza kufanyika kwenye bodaboda/bajaj na vyombo vingine vya usafiri pia.

Sijajua bado kama hapa Tanzania kuna kampuni inafanya hii biashara naomba mnijuze kama ipo na terms zao zikoje watu wajikomboe na ajira zipatikane.
Haya ndiyo mawazo tulitegemea kuyasoma jukwaani ili watu wa advance kimaisha siyo mtu anazungumzia ati "kula tunda"
 
Back
Top Bottom