Waziri wa Ulinzi aongoza maadhimisho miaka 95 ya Jeshi la watu wa China

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,808
11,973
LE2A6923_Easy-Resize.com.jpg

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Stergomena Lawrence Tax (Mb) ameongoza maadhimisho ya miaka ya 95 ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China (Chinese People’s Liberation Army) tangu kuanzishwa kwake mwaka 1927, maadhimisho haya yamefanyika kwenye Ubalozi wa China hapa Nchini.

Akiongea wakati wa hafla ya kuadhimisha kuanziswa kwa Jeshi hilo, Waziri kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ameipongeza Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China na Maafisa pamoja na Askari wote wa Jeshi la Ukombozi la Watu wa China kwa kuadhimisha siku hiyo muhimu yenye kumbukumbu tele na nzuri zinazoakisi mafanikio mbalimbali tangu kuanzishwa kwake.

Aidha, katika hotuba yake, Waziri aliwasilisha pia, Salaam za Pongezi kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Samia Suluhu Hassan pamoja na Watanzania kwa ujumla.

Capture_Easy-Resize.com (1).jpg

Dkt. Stergomena amebainisha kuwa tangu kuanzishwa kwa Jeshi hili, limekuwa ni kiungo muhimu katika kuwaunganisha watu wa Taifa la China na kuwafanya kuwa wamoja hadi hapo mwaka 1949, ambapo mwasisi wa Taifa hilo la China, Hayati Mao Tse Tung alipotangaza kuundwa kwa Jamhuri ya Watu wa China.

Waziri ameongeza kwa kusema kuwa kwa miaka 95 iliyopita, Jeshi hili limeweza kutoa mchango mkubwa katika kulinda utaifa, usalama, masilahi ya Taifa, kulinda na kudumisha amani na usalama duniani. Kupitia Jeshi la Ukombozi la watu wa China tumeweza kushuhudia mabadiliko makubwa ya kiteknolojia, siasa za kidunia pamoja na kiuchumi.

Jeshi la Ukombozi la Watu wa China linapodhimisha Miaka 95 ya kuanzishwa kwake ifikapo tarehe 01 Agosti, 2022 tunapongeza Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China pamoja na Jeshi la Ukombozi la Watu wa China kwa mafanikio yake kitaifa, kikanda na kimataifa Serikali ya Tanzania inathamini mchango na ushirikiano baina ya Tanzania na China katika ngazi ya kimataifa katika kulinda maslahi baina yetu.

Chini ya Uongozi imara wa Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Serikali ya Tanzania itaendelea kudumisha mahusiano ya kihistoria na Serikali Jamhuri ya Watu wa China.

Mheshimiwa Tax amesema pia, kuwa Tanzania itaendelea kukumbuka misaada iliyotolewa na China kupitia Ujenzi wa Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA), Ujenzi w Chuo cha Ulinzi cha Taifa (NDC), Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi- Monduli (TMA) pamoja na taasisi nyingine za kitaaluma.

Maadhimisho hayo yamehudhuriwa pia, na Balozi wa China hapa nchini Bi. Chen Mingjian, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini, Jenerali Jacob John Mkunda, Viongozi wa Chama na Serikali, Wakuu wa Kamandi na Waambata Jeshi wanaowakilisha majeshi yao hapa nchini.
 
Wachina wameiangamiza Sri lanka kwa kuchukua Bandari na sasa Zambia inaangamia tukae nao distance.
 
maadhimisho ya miaka ya 95 ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China (Chinese People’s Liberation Army) tangu kuanzishwa kwake mwaka 1927,

The People's Liberation Army, the PLA, marks its 95th anniversary this year. But what exactly is the PLA? Here's the backstory.

Source : CGTN
 
Making a New China : Strengthening the People's Military


Creating a #military strong enough to guarantee the security, independence and territorial integrity of the country has long been a vital component of the dream of Chinese national rejuvenation. It's precisely for this reason that the Communist Party of #China has devoted so much attention to ensuring that the Chinese army is a force to be reckoned with. Thus, it has equipped it with the best cutting-edge technology and made sure that it is well trained in all aspects to use it properly.
Source : CGTN
 
Stergomena Tax.

Mwangalie vizuri huyu mama. She certainly is going somewhere.

Hawa ndio akina Angela Merkel; akina Margreth Thatcher wetu.
 
Wachina wameiangamiza Sri lanka kwa kuchukua Bandari na sasa Zambia inaangamia tukae nao distance.
Ni shida sana kuiga kazi anayoweza kuifanya kasuku, huku ukiwa umejaaliwa akili nzuri kabisa ya kuchambua mambo na kuyaelewa mwenyewe.

Samahani sana mkuu 'Imhotep' kuhusu ukweli huu.

Hebu jaribu tena. Angalia upande wa Sri Lanka, au Zambia, au kwingineko, kama kuna ukweli huo; kwa nini tusianze kwa kutazama hao waliojihusisha katika mipango hiyo katika nchi hizo?
 
Back
Top Bottom