Waziri wa Mifugo na Uvuvi uje Mwanza uone kasi mpya ya uvuvi haramu

Ndebile

JF-Expert Member
Sep 14, 2011
7,237
9,871
Nipo hapa Igombe wilaya ya Ilemela jijini Mwanza kwa mwenyeji wangu ambapo nimekaa siku tatu sasa. Nimeshuhudia uvuvi haramu wa kutumia kokolo kwa kasi ya kutisha, yaani juhudi zote zilizokuwa zimefanyika kutokomeza hii hali na hali ya upatikanaji wa samaki kuwa wa kulidhisha sasa zimepotea.

Maeneo vinala wa uvuvi huu ni fukwe za Mhonze, Kayenze Ndogo hadi na maeneo yote jirani. Huitaji kuwa mtaalam sana ili kuona hali hii, pikipiki maarufu kama bodaboda zinaanza kupakia samaki magunia kwa magunia kuanzia saa kumi alfajiri kuelekea mjini kati hadi saa mbili asubuhi jambo ambalo linatufanya tujiulize kama hao watu hawaonwi na maafisa mali asili au ndio kufa kufaana.

Hapa sio lazima Rais akemee, Waziri na watu wako njoo muone kwa macho yenu huu uharibifu wa mali asili ya Watanzania.

Nipo njiani kulekea kwangu N'gwashilalage, Kwimba- MWANZA.
 
Samaki wanavuliwa wakingali wachanga cheza na Kokolo weye..ila watachwa walimpigia Kula.
 
Samaki wanavuliwa wakingali wachanga cheza na Kokolo weye..ila watachwa walimpigia Kula.
Naona wamechanga karata zao vizuri, kipindi hiki hwawezi kuguswa kawasababu sanduku la kura lipo karibu!
 
Naona wamechanga karata zao vizuri, kipindi hiki hwawezi kuguswa kawasababu sanduku la kura lipo karibu!
Tena mimi nawashauri watumie vizuri huu upenyo kama kulikausha hilo ziwa samaki wote fursa ni sasa.wakishiba Samaki wazaane kwa wingi ili kwamba wapiga kura wawe wengi siku za Usoni ili watutawale milele.
 
Acha ukuda ukienda katika miji ya watu jifunze kukaa kimya sehemu nyingine watakukeketa tena. Yaani uone kokolo halfu boda zinabeba samaki wachanga.
Unafikiri samaki wote wakikua hilo ziwa litatosha acha watu wapate kitoweo.
Nipo hapa Igombe wilaya ya Ilemela jijini Mwanza kwa mwenyeji wangu ambapo nimekaa siku tatu sasa. Nimeshuhudia uvuvi haramu wa kutumia kokolo kwa kasi ya kutisha, yaani juhudi zote zilizokuwa zimefanyika kutokomeza hii hali na hali ya upatikanaji wa samaki kuwa wa kulidhisha sasa zimepotea.

Maeneo vinala wa uvuvi huu ni fukwe za Mhonze, Kayenze Ndogo hadi na maeneo yote jirani. Huitaji kuwa mtaalam sana ili kuona hali hii, pikipiki maarufu kama bodaboda zinaanza kupakia samaki magunia kwa magunia kuanzia saa kumi alfajiri kuelekea mjini kati hadi saa mbili asubuhi jambo ambalo linatufanya tujiulize kama hao watu hawaonwi na maafisa mali asili au ndio kufa kufaana.

Hapa sio lazima Rais akemee, Waziri na watu wako njoo muone kwa macho yenu huu uharibifu wa mali asili ya Watanzania.

Nipo njiani kulekea kwangu N'gwashilalage, Kwimba- MWANZA.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom