Jamani mimi binafsi kuna wizi ninafanyiwa na kampuni za simu za mkononi ambalo nimeona nikilileta JF litawafikia wahusika. Hili tatizo wenzangu mtasema kama na nyie linawapata. Ni hivi kati line ya VODA mara unatumiwa kuwa umekatwa sh: 300 kwa ajili ya wimbo wa swagga wakati hujawahi kuomba nyimbo hizo au kubonyeza nyota kama wanavyoelekeza kama unahitaji nyimbo. Mimi naweka credit kwenye simu ili niwasiliane sasa inapokatwa kwa ajili ya nyimbo ni wizi kwani zijaziomba. Ukiwafuta VODA wanaiondoa halafu wanakuambia ni system yenyewe ndio inakuunganisha, sasa huu wizi hadi lini?
Katika line ya TIGO wanakuambia umetozwa sh: 300 kwa huduma ya TIGO beatz, kwa ajili ya mwito wako wa akupigiae wakati hujaomba kwani bila nyimbo hizo naweza kuwasiliana kama kawaida, kama nataka nyimbo nitanunua CD zake au kuzirekodi nyimbo ninazoziitaji na kwa kukatwa credit niliyoiweka ili niwasiliane.
Jamani mimi naomba msaada wenu maana nimechoka kuibiwa hadi naogopa kuweka fedha kwenye simu maana nikeweka ninataka kuwasiliana imekatwa kwa nyimbo au huduma ambayo sijaiomba. Nawasilisha, asanteni kwa kunisikiliza.
Katika line ya TIGO wanakuambia umetozwa sh: 300 kwa huduma ya TIGO beatz, kwa ajili ya mwito wako wa akupigiae wakati hujaomba kwani bila nyimbo hizo naweza kuwasiliana kama kawaida, kama nataka nyimbo nitanunua CD zake au kuzirekodi nyimbo ninazoziitaji na kwa kukatwa credit niliyoiweka ili niwasiliane.
Jamani mimi naomba msaada wenu maana nimechoka kuibiwa hadi naogopa kuweka fedha kwenye simu maana nikeweka ninataka kuwasiliana imekatwa kwa nyimbo au huduma ambayo sijaiomba. Nawasilisha, asanteni kwa kunisikiliza.