Waziri wa Mambo ya Ndani, George Simbachawene amewaonya viongozi wa dini na jumuiya za kijamii

Mocumentary

JF-Expert Member
Jul 31, 2017
768
1,959
HABARI: Waziri wa Mambo ya Ndani, George Simbachawene amewaonya viongozi wa dini na jumuiya za kijamii, kuepuka kutoa
matamko ya kisiasa yenye lengo la kuhamisha na kuelekeza waumini kumchagua mgombea au chama fulani "watakaoshindwa kuzingatia masharti, wizara haitasita kuifuta."

IMG_20201021_181955.jpg
 
Hana lolote huyu analinda ajira za watot wake...wapo wengi kwenye mashirika ya uma mmoja yupo PSSSF anaitwa Jeniffer hataree
 
Nyakati zinabadilika! Kila mtu afanye sehemu yake.

Sisi tunachotaka ni mabadiliko tu!
 
Mpaka Sasa Hivi Aibu Tupu
Katibu Mkuu Wa Wizara Ndiyo Mwenye Nguvu
Siyo Huyu Mgombea Simbachawene
 
Firstly, CCM is an idiot political party , people are tired to hears nonsense from those
 
Shehe wetu mzee Ponda shikilia hapohapo baba usiachie - piga spana hao dhulumati, pigaaa!

Nabii na mtume Mwingira - piga spana mtumishi!

Bishop Mpemba - nakuaminia sana mtumishi wa Mungu, wewe hurembi unapigaga kwenye bull!
 
HABARI: Waziri wa Mambo ya Ndani, George Simbachawene amewaonya viongozi wa dini na jumuiya za kijamii, kuepuka kutoa
matamko ya kisiasa yenye lengo la kuhamisha na kuelekeza waumini kumchagua mgombea au chama fulani "watakaoshindwa kuzingatia masharti, wizara haitasita kuifuta."View attachment 1607542
Mmeona BAKWATA imekosa mvuto mmeibuka na matamko ya kinoko? Alhad Musa alipokuwa anaswali swala Mseto mbona hakuongea kitu? BAKWATA Mtwara wametoa tamko hadharani wanamuunga mkono Jiwe hatukusikia lolote. Ponda kawapondaponda wanaleta fyokofyoko!!
 
Ponda na Bagonza wavue kanzu na kishabagalishia wavae magwanda ya Chadema tujue moja,wasituchanganye sisi waumini.
 
Mmeona BAKWATA imekosa mvuto mmeibuka na matamko ya kinoko? Alhad Musa alipokuwa anaswali swala Mseto mbona hakuongea kitu? BAKWATA Mtwara wametoa tamko hadharani wanamuunga mkono Jiwe hatukusikia lolote. Ponda kawapondaponda wanaleta fyokofyoko!!

Tatizo la awamu hii ni "double standard". Shehe au Askofu anayemfananisha binadamu na Mwenyezi Mungu hakemewi kisa anampamba mgawa vyeo na utukufu wa duniani.

Kama kweli baada ya maisha haya ya duniani kuna moto utakaowaunguza watenda dhambi, basi viongozi wengi wa awamu hii watakuwa mkaa!!!
 
Ponda na Bagonza wavue kanzu na kishabagalishia wavae magwanda ya Chadema tujue moja,wasituchanganye sisi waumini.
Na Mufti wenu Jana alikuwa Korogwe kwenye jukwaa la MaCCM,akaomba ajengewe Barabala,

Au macho yako yanaona upande mmoja tu?
 
HABARI: Waziri wa Mambo ya Ndani, George Simbachawene amewaonya viongozi wa dini na jumuiya za kijamii, kuepuka kutoa
matamko ya kisiasa yenye lengo la kuhamisha na kuelekeza waumini kumchagua mgombea au chama fulani "watakaoshindwa kuzingatia masharti, wizara haitasita kuifuta."View attachment 1607542
Nadharia ya kusema viongozi wa dini hawapaswi kuwa na itikadi za kisiasa mbele ya waumini wao, kwa sasa haipo tena hapa Tanzania. Hicho kitu kilishafutika. Ni nadharia ya uongo na unafiki mkubwa. Hakuna kiongozi wa dini mwenye haki ya kumnyoshea kidole mwenzie katika hilo.

Kiongozi wa kidini anaweza kukaa kimya, kuungana mkono au kukosoa, vyote hivyo vina maana kisiasa.
 
Na Mufti wenu Jana alikuwa Korogwe kwenye jukwaa la MaCCM,akaomba ajengewe Barabala,

Au macho yako yanaona upande mmoja tu?
Umeisikia Dua aliyoiomba Muft akiwa juu ya jujwaa Korogwe?
je'Muft alimuombea kura JPM ama mgombea yeyote wa CCM?
 
Back
Top Bottom