Mchochezi
JF-Expert Member
- Feb 29, 2012
- 10,364
- 6,511
Miaka 60 baada ya uhuruHello JF
Hii habari imenichekesha sana
----
Waziri wa Maji, Jumaa_Aweso ameeleza kupitia alipokuwa katika ziara ya kukagua miradi ya maji Vijijini moja ya kituko alichokutana nacho kwenye kijiji kimoja alipomuuliza mkandarasi sababu ya maji kutokuwepo kwenye kijiji hicho licha ya kujengwa tank kubwa la maji.
"Unakwenda Vijijini unakuta 'tank' kubwa lakini hakuna maji, unauliza kwa mkandarasi kwanini hakuna maji anakwambia Mh. Naomba nikunong'oneze namwambia hapana! Waeleze wananchi kwanini maji hakuna anasema hajawahi kuona wananchi wachawi kama Vijijini anasema mabomba Usiku yanapaa kama ndege, namuuliza rubani wake yupo wapi? Kwahiyo wahandisi wa namna ile hawawezi kufanya kazi na wizara"