ubarinolutu
JF-Expert Member
- Oct 22, 2012
- 1,964
- 3,894
Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ametengua uteuzi wa viongozi 23 wa Wakala wa Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira (Ruwasa) akiwemo Mkurugenzi wa Huduma za Ufundi za mamlaka hiyo, Deusdedith Magoma. Aidha, Aweso ameiagiza Bodi ya wakurugenzi ya Ruwasa kutengua uteuzi wa meneja wa anayeshughulikia masuala ya ujenzi aliyepo makao makuu, meneja wa Mkoa wa Geita na mameneja wa wilaya 20 nchini.
Akizungumza a waandishi wa habari, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Anthony Sanga amesema Waziri Aweso amechukua uamuzi huo kutokana na udhaifu wa utendaji wa baadhi ya viongozi walioshika nafasi zinazohusiana moja kwa moja na utekelezaji wa miradi ya maji vijijini.
MAONI YANGU
Waziri wa maji ameondoa mameneja wa maji Katika wilaya 20 na wakurugenzi 5 wa mamlaka za maji za mikoa, na amesema waletwe wengine kutoka humo humo majini, hii Ni hasara kubwa sana, wizara haijui vizuri jinsi taasisi zinavofanya kazi na changamoto zinazowakabili, kwanini hakutatua changamoto zinazowakabili, siamini Kama wakuu wote 25 Ni wabovu naona Kama Ni kukurupuka.
Sasa he wakiletwa hao watu wengine ndo changamoto zitaisha, tunakosea Sana kuingiza siasa Katika Mambo haya