Waziri wa madini, Angellah Kairuki asaini kanuni za sheria mpya ya madini

Boniphace Kichonge

JF-Expert Member
Jul 31, 2017
1,606
1,956
Waziri wa Madini Angellah Kairuki amesaini Kanuni za Sheria Mpya ya Madini ambapo Wakala wa Jiolojia Nchini (GST) amepewa nguvu ya kisheria ya kuingia katika ardhi yoyote kufanya utafiti wa kina wa madini.

Mwaka jana Bunge lilipitisha Sheria mbili za madini ambazo zinalenga kuleta mabadiliko makubwa katika Sekta ya Madini.

Hata hivyo kanuni za sheria hizo zilikuwa bado hazijasainiwa na Waziri wa Madini hadi Januari mwaka huu jambo ambalo lilimkera Rais John Magufuli na kutoa agizo zikamilike ndani siku tano.

Akizungumza leo Januari 28 Naibu Waziri wa Madini Dotto Biteko amesema kuwa kanuni hizo zimesainiwa Januari 9 mwaka huu ikiwa ni siku moja baada ya Rais John Magufuli kuagiza kukamilishwa kwa mchakato wa kanuni hizo ndani ya siku tano.Biteko alikuwa akizungumza mbele ya Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini ambayo ilitembelea ofisi za GST mjini Dodoma.

“Kuna watu wanasema sheria hii mpya itafukuza wawekezaji na hakuna wawekezaji wapya watakaokuja lakini nataka kuwaambia kuwa kuna wageni wengi wanakuja kutaka kuwekeza katika migodi mikubwa,” amesema.

Amesema wastani katika kila wiki wamekuwa wakipokea wawekezaji kati ya 10 na 20 ambao wanaonyesha nia ya kuwekeza nchini katika sekta hiyo kwa hiyo sheria sio kikwazo kwao.

Alisema kujitokeza kwa wingi kwa wawekezaji kunatokana na sheria hiyo kuweka uwazi katika taratibu na kanuni za kuwekeza.

Biteko amesema lengo la wizara yake ni kuongeza uchangiaji wa sekta ya madini katika pato la taifa kutoka asilimia 4.8 ya mwaka jana hadi kufikia asilimia 10 kama Mpango wa Maendeleo wa miaka mitano unavyosema.

Chanzo: MCL
 
Muache amecheza mchezo mchafu sana jamaa yake alipaishwa mashariki ya china huku jamaa anatumbua hadi kiumbe dooo.


Usitamani mwanamke mwaunaume asiyekuwa mke wako hata biblia imeandika


Swissme
 
Ikitokea kasema sikutaki Tena Na kumdampu walahi mamasamiha ataitisha uchaguzi baada ya siku90
 
Kila wiki wanapokea wawekezaji kati ya 10 - 20. Mbona huku mtaani hao wawekezaji hatuwaoni jamani au huko kwenu vipi?
 
Waziri wa Madini Angellah Kairuki amesaini Kanuni za Sheria Mpya ya Madini ambapo Wakala wa Jiolojia Nchini (GST) amepewa nguvu ya kisheria ya kuingia katika ardhi yoyote kufanya utafiti wa kina wa madini.Mwaka jana Bunge lilipitisha Sheria mbili za madini ambazo zinalenga kuleta mabadiliko makubwa katika Sekta ya Madini.
Hata hivyo kanuni za sheria hizo zilikuwa bado hazijasainiwa na Waziri wa Madini hadi Januari mwaka huu jambo ambalo lilimkera Rais John Magufuli na kutoa agizo zikamilike ndani siku tano.
Akizungumza leo Januari 28 Naibu Waziri wa Madini Dotto Biteko amesema kuwa kanuni hizo zimesainiwa Januari 9 mwaka huu ikiwa ni siku moja baada ya Rais John Magufuli kuagiza kukamilishwa kwa mchakato wa kanuni hizo ndani ya siku tano.Biteko alikuwa akizungumza mbele ya Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini ambayo ilitembelea ofisi za GST mjini Dodoma.
“Kuna watu wanasema sheria hii mpya itafukuza wawekezaji na hakuna wawekezaji wapya watakaokuja lakini nataka kuwaambia kuwa kuna wageni wengi wanakuja kutaka kuwekeza katika migodi mikubwa,” amesema.
Amesema wastani katika kila wiki wamekuwa wakipokea wawekezaji kati ya 10 na 20 ambao wanaonyesha nia ya kuwekeza nchini katika sekta hiyo kwa hiyo sheria sio kikwazo kwao.Alisema kujitokeza kwa wingi kwa wawekezaji kunatokana na sheria hiyo kuweka uwazi katika taratibu na kanuni za kuwekeza.
Biteko amesema lengo la wizara yake ni kuongeza uchangiaji wa sekta ya madini katika pato la taifa kutoka asilimia 4.8 ya mwaka jana hadi kufikia asilimia 10 kama Mpango wa Maendeleo wa miaka mitano unavyosema.
Chanzo: MCL


Hapa siwezi ku comment
 
10 to 20 investors wa madini kila wiki?

Hapa kuna walakini, nina shaka sana kama idadi hiyo inafika.. kwa wiki? Hii it looks like kiki.. Biteko watch out.. kiki ni mbaya sana
 
Muache amecheza mchezo mchafu sana jamaa yake alipaishwa mashariki ya china huku jamaa anatumbua hadi kiumbe dooo.


Usitamani mwanamke mwaunaume asiyekuwa mke wako hata biblia imeandika


Swissme

hello! Nani mwenzangu. Hahahaha
 
10 to 20 investors wa madini kila wiki?

Hapa kuna walakini, nina shaka sana kama idadi hiyo inafika.. kwa wiki? Hii it looks like kiki.. Biteko watch out.. kiki ni mbaya sana
Haujawazoea wanasiasa ? Waulize maana halisi ya hao "wawekezaji" unaweza kukuta hata anayenunua pete ya uchumba yenye mchanganyiko wa dhahabu na takataka zingine naye anajumuishwa humo kwenye kundi la wawekezaji
 
Bora wamalize mambo Yao hayo maana wanaofanya export ya madini kupeleka nje wamezuiwa.....kutokana na hali hyo sisi wengine tunashindwa kufanya biashara kwa ufanisi watu wanashindwa kuuza mizigo Yao

Ova
 
NI lini wataanza kutowa vibali kwa wana safarisha madini nje ya nchi(precious&semi precious)stones......ni muda tangu wamesimamisha leseni za export.....
Wanunuzi wengi hawanunui mizigo mpaka wenye hatma ya issue hii.....na mnunuzi asiponunua Hata broker atashindwa kwenda Kununua madini toka kwa wachimbaji,na wacbimbaji wasipo fatwa ili nao wauze mawe Yao ina maana kila mtu hapo hafanyi kazi na haingizi kipato.....
Tumeskia target yenu mnataka kila Aina jiwe lisitoke nchini kwenda nje bila kufanyiwa cutting.....uamuzi Huo ni mzuri sawa lkn Siyo wa kukurupuka,huwezi ukataka viwanda vya kukata mawe vije/vianzishwe mara moja
Lazima kuwe na mipango inayoandaliwa huwezi ukata tanzania iwe kama jaipur,india kwa haraka
Kwa hiyo kwa hali hii watu kazi haziendi na vipato hatuingiziii
Nimeandika Hapa kama mdau wa biashara hii

Ova
 
Wanaonesha nia tu, je baada ya kupitia sheria na kuangalia mazingira ya uwekezaji Tz ni wangapi wamewekeza?
 
Muache amecheza mchezo mchafu sana jamaa yake alipaishwa mashariki ya china huku jamaa anatumbua hadi kiumbe dooo.


Usitamani mwanamke mwaunaume asiyekuwa mke wako hata biblia imeandika


Swissme
Kwa kweli! Hivi inapatikana picha gani sisis kama Taifa! The number one citizen halafu ndio anafanya hivyo. Where the hell are all the morals in this world?
 
Back
Top Bottom