Waziri wa Katiba na Sheria Mwigulu Nchemba awajibu TLS kuhusu Rais Samia Suluhu kuteua Baraza jipya la Mawaziri

Ulichokiandika nadhani sio, wewe kama uko kwenye msiba inakuwaje unaanza kujibizana kwenye mitandao, andika mambo ya msingi msiba usiwe kisingizio, kama unachosema kina mashiko kwanini ameapishwa Rais si tungesubiri JPM azikwe? aacha visingizio Katiba iko hai
 
Tuandikie ibara tafadhali. Mambo yanakwenda kwa sheria, nipo tayari kukuunga mkono kama utaandika kama mtoa Thread, kapanga na kuonyesha katiba inasemaje?

Mi si mpenzi wa mtoaji threada lakini kwa udadafuaji alioufanya nampa 5.
Kwamba Rais ni taasisi unataka upewe ibara?
 
Nimesoma andiko la TLS, kwa heshima zote kwa chombo chetu hiki kilichopewa mamlaka kisheria, Nimeshtuka sana, I wish to say,

Kwanza KATIBA HAIJAVUNJWA KWA MHE RAIS SAMIA SULUHU kuapa, na wala hakuna Mkanganyiko wowote wa Kikatiba, kwa yeye kutoteua PM na Baraza jipya. Mmekaa wote kweli mkaona hivyo.

Kwa mujibu wa Katiba Ibara ya 42(5) kuna watu wa aina mbili wanaweza kuwa Rais. Moja, Rais Mteule ambaye anatokana na Ibara ya 42(1). Mbili, Mtu anayeshika kiti cha Rais ambaye anatokana na ibara ya 37(5) na 50(2)(d) ambaye ni Makamu wa Rais. Kwa Mazingira haya, Makamu wa Rais, baada ya kifo cha Rais, anakuwa Kaimu Rais baadae ndio ameapa na kuwa RAIS wa Nchi. Rais Mteule anapatikana kutokana na uchaguzi. Hivyo basi ibara ya 57(2)(f) ya Katiba haitumiki katika mazingira haya. Kwa mjibu wa Sheria, Mhe Rais alitakiwa kutoa taarifa hii kwenye Baraza la Mawaziri baada ya kuapa na alifanya hivyo, maana yake Baraza lipo.

Hata hivyo kwa tamaduni za Kiafrika, kitanzania na Misingi ya UTU, SIONI KAMA NI JAMBO JEMA SANA KUANZA KUJADILI MGAWANYO WA MADARAKA TUNGALI HATA HATUJAMZIKA ALIYEKUWA KIONGOZI WETU. HUU SIO MSIBA MDOGO, JAMBO HILI ZITO LIKO MIKONONI MWA RAIS WETU MAMA SAMIA SULUHU, HALAFU SISI TUANZE KUMPATIA MAMBO YA MARA TEUA PM, MARA VUNJA BARAZA, KATIBA INAELEKEZA RAIS KUAPA NA NAMNA YA KUMPATA MAKAMU WA RAIS.

KWA MJIBU WA KATIBA RAIS ANARUHUSIWA KUVUNJA BARAZA MUDA WOWOTE NA KUPANGA ATAKAVYO HATA SIO KWA MAZINGIRA KUAPA KWAKE,

KWANINI HATUIONI HEKIMA YAKE YA KUSHUGHULIKIA MSIBA KUMSITIRI KWANZA ALIYEKUWA KIONGOZI WETU? TUNAANZA NA MAZISHI AU MIRATHI?

Pia soma > TLS: Kwa Mujibu wa Katiba, sasa Tanzania haina baraza la Mawaziri, Rais Samia atakiwa kuteua Waziri Mkuu ndani ya siku 14
Kweli aliye mwita Mwigulu hajakosea. Phd holder hajawaelewa TLS. Au hakusoma bandiko lote? Au ni wale wale mawaziri viherehere wa mtandaoni?
Mbona bandiko la Tls liko wazi kabisa? Kweli hii nchi ina vihiyo wengi. Ina kuwaje mtu ana Phd anashindwa kuelewa bandiko la kurasa moja? Au ni zile phd za mtaani?
Ni aibu mtu kama huyu kupewa madaraka. Au amesha panic kwamba Mh. Mama Samia akivunja baraza hata mchukua? Maana najua viherehere kama huyu labda alikuwa akimdharau Mama Samia sasa hana pa kushika.
Mwigulu kuwa mpole, Mama ni mtu mwema, haweki kinyongo. Sana sana kita kutesa wewe mwenyewe. Dharau ulizo muonyesha yeye wala hazikumbuki.
 
Kuna watu wanapima upepo nadhani sidhani kama wana nia Njema na Ta if a hilii.
 
Dah! Mwigulu kama anajua tupo kwenye msiba mzito ametoa wapi nguvu ya kuandika haya? Hapa ninachokiona ni namna ya kujipigia debe ili asiachwe kwenye baraza lijalo. Hakuna chochote cha msingi alichokiongea.

TLS wametoa mwanga kuhusu issue nzima ya kikatiba kuhusu hali iliyopo, sasa hapa Mwigulu hata haieleweki anaongea nini.
Mwigimulu si mwanasheria
 
Nimesoma andiko la TLS, kwa heshima zote kwa chombo chetu hiki kilichopewa mamlaka kisheria, Nimeshtuka sana, I wish to say,

Kwanza KATIBA HAIJAVUNJWA KWA MHE RAIS SAMIA SULUHU kuapa, na wala hakuna Mkanganyiko wowote wa Kikatiba, kwa yeye kutoteua PM na Baraza jipya. Mmekaa wote kweli mkaona hivyo.

Kwa mujibu wa Katiba Ibara ya 42(5) kuna watu wa aina mbili wanaweza kuwa Rais. Moja, Rais Mteule ambaye anatokana na Ibara ya 42(1). Mbili, Mtu anayeshika kiti cha Rais ambaye anatokana na ibara ya 37(5) na 50(2)(d) ambaye ni Makamu wa Rais. Kwa Mazingira haya, Makamu wa Rais, baada ya kifo cha Rais, anakuwa Kaimu Rais baadae ndio ameapa na kuwa RAIS wa Nchi. Rais Mteule anapatikana kutokana na uchaguzi. Hivyo basi ibara ya 57(2)(f) ya Katiba haitumiki katika mazingira haya. Kwa mjibu wa Sheria, Mhe Rais alitakiwa kutoa taarifa hii kwenye Baraza la Mawaziri baada ya kuapa na alifanya hivyo, maana yake Baraza lipo.

Hata hivyo kwa tamaduni za Kiafrika, kitanzania na Misingi ya UTU, SIONI KAMA NI JAMBO JEMA SANA KUANZA KUJADILI MGAWANYO WA MADARAKA TUNGALI HATA HATUJAMZIKA ALIYEKUWA KIONGOZI WETU. HUU SIO MSIBA MDOGO, JAMBO HILI ZITO LIKO MIKONONI MWA RAIS WETU MAMA SAMIA SULUHU, HALAFU SISI TUANZE KUMPATIA MAMBO YA MARA TEUA PM, MARA VUNJA BARAZA, KATIBA INAELEKEZA RAIS KUAPA NA NAMNA YA KUMPATA MAKAMU WA RAIS.

KWA MJIBU WA KATIBA RAIS ANARUHUSIWA KUVUNJA BARAZA MUDA WOWOTE NA KUPANGA ATAKAVYO HATA SIO KWA MAZINGIRA KUAPA KWAKE,

KWANINI HATUIONI HEKIMA YAKE YA KUSHUGHULIKIA MSIBA KUMSITIRI KWANZA ALIYEKUWA KIONGOZI WETU? TUNAANZA NA MAZISHI AU MIRATHI? 😭😭😭😭

Pia soma > TLS: Kwa Mujibu wa Katiba, sasa Tanzania haina baraza la Mawaziri, Rais Samia atakiwa kuteua Waziri Mkuu ndani ya siku 14
Nchi haiendeshwi kwa taratibu za kimila. TLS wao wamehadharisha tu muwe makini msikurupuke.
Si mara moja uongozi uliopita umekuwa ukikiuka katiba au anataka iwe mazoea? Mliwahi kuteuwa wabunge wa kiume wengi zaidi ya wanawake. Wanaharakati na wapinzani waliwashitukia na kuteka katiba ifuatwe. Posi alitolewa ubunge na kupewa ubalozi ili kukuwa soo.
Wameteuliwa mawaziri wawili bila kuwapo kwa waziri mkuu kinyume cha katiba. Kwa kuwa hakuna aliyewashitua katiba ilikanyagwa.
Mara ngapi wabunge wasio na chama wamekuwa wakishiriki Bunge kinyume cha katiba? Au unafikiri tunafurahi?
Leo TLS imewahadharisha unang'aka. Tuache kudharauliana.
 
Kwa heshima, Mwongozo huu wa Mh. Rais wa TLS na Baraza lake la Uongozi, kwa maoni yangu, haupo sahihi, au umejipotosha wenyewe kuhusiana na tafsiri sahihi ya matakwa ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (JMT).
Mwongozo una dosari ya dhahiri ya namna ya kutafsiri Katiba, lakini pia haujazingatia uwazi/ubayana wa nini Ibara husika za Katiba zili/zinanuia, au Katiba ilidhamiria.

Kwanza, kanuni ya harmonisation, kama kanuni ya kisheria ya msaada wa kutafsiri sheria au Katiba hutumika katika mazingira ambapo Ibara kadhaa za sheria au Katiba husika zinaonesha mkanganyiko bayana, au dosari, au jitihada za kutumia tafsiri ya moja kwa moja inasababisha mkanganyiko. Haitumiki katika mazingira ambapo Ibara za Katiba zipo wazi na bayana. Kwahiyo, kwa maoni yangu, Mwongozo ulipaswa kuanza kwa kuonesha mkanganyiko au dosari za tafsiri za Ibara husika. Mimi sioni ugumu katika tafsiri ya nini Ibara husika za Katiba zinadhamiria.

Pili, kanuni ya awali na pengine kuu katika kutafsiri Katiba ni "purposive approach" na sio "harmonisation". Hii inasaidia kuielezea zaidi hoja yangu ya kwanza. Mathalan, msomaji wa Katiba ya JMT ya 1977, kama ilivyorekebishwa mpaka sasa, akiisoma kwa kutumia purposive approach atayaona masuala yafuatayo bayana na yapo wazi:

Moja, kutakuwa na Rais wa JMT (Ibara ya 33),

Pili, kutakuwa na Serikali ya JMT, na mamlaka ya Serikali hiyo yatakuwa mikononi mwa Rais wa JMT (Ibara ya 34, pia Ibara ya 35),

Tatu, kutakuwa na Makamu wa Rais wa JMT... ambaye atakuwa Msaidizi Mkuu wa Rais (Ibara ya 47),

Nne, kutakuwa na Waziri Mkuu na Baraza la Mawaziri (Ibara ya 51, Ibara ya 54).

Kimtiririko, ni dhahiri kuwa Ibara nilizozitaja hapo juu, na nyingine ambazo sijazitaja, zipo katika SURA YA PILI ya Katiba... yenye kichwa, "Serikali ya JMT"... Sehemu ya Kwanza ni Ibara zinanazomhusu Rais... Sehemu ya Pili ni zile zinazomhusu Makamu wa Rais... na Sehemu ya Tatu ni zile zinazomhusu Waziri Mkuu na Baraza la Mawaziri...

Mpaka hapo hakuna ugumu wowote wa tafsiri au mkanganyiko, au ugumu. Purpose iko wazi pia... ni kuandika masharti yanayoihusu Serikali ya JMT na masuala yanayoihusu.

Tano, Rais na Makamu wa Rais wanapatikanaje? Ibara za 38, 39, 40, 41, 42 na 47, 48, 49 na 50 zinahusika. Ibara hizi zikisomwa purposively katika mtiririko huo, ni dhahiri kuwa Rais na Makamu wa Rais watachaguliwa kwa pamoja katika uchaguzi mmoja/ule ule... na wakishatangazwa kuwa hivyo, watashika nafasi zao kama masharti ya Katiba yanavyosema au taka.

Lakini, kuna kitu kimoja cha msingi sana cha kuzingatia katika masharti ya Katiba hii, kwamba, SIO KILA WAKATI KITI CHA RAIS KITAKAPO KUWA WAZI, kwasababu kadhaa zilizoainishwa na Katiba, kama vile KIFO CHA RAIS au MAKAMU WA RAIS, basi utaitishwa uchaguzi wa Rais, au Makamu wa Rais (Ibara ya 38 (2) ).

Sita, sasa, baada ya kuona hilo, ndipo Ibara ya 37, Ibara ndogo ya 5 itabisha hodi, hususan katika mazingira tuliyonayo sasa... yaani,
"Endapo kiti cha Rais kitakuwa wazi kutokana na Rais kufariki dunia..., basi Makamu wa Rais ataapishwa na atakuwa Rais kwa muda uliobaki katika kipindi cha miaka mitano na kwa masharti yaliyoelezwa katika ibara ya 40, kisha baada ya kushauriana na chama cha siasa anachotoka Rais atapendekeza jina la mtu atakayekuwa Makamu wa Rais na uteuzi huo utathibitishwa na Bunge kwa kura zisizopungua asilimia hamsini ya Wabunge wote."

Ibara hii iko wazi na bayana, kwamba Makamu wa Rais ataapishwa kuwa Rais... kisha atashauriana na chama chake kuteua mtu atakaye kuwa Makamu wa Rais...
Hakuna Ibara inayosema au hata kuashiria kuwa Waziri Mkuu atakoma kuwa Waziri Mkuu, na au Baraza la Mawaziri litavunjwa... kumbuka, Ibara ya 54 inawataja wajumbe wa Baraza la Mawaziri kuwa ni Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Rais wa Zanzibar na Mawaziri wote... Rais atahudhuria vikao vyake, na ndiye atakayeongoza vikao vyake.

Mpaka hapo, ni rahisi kubaini kuwa purposively Katiba hii haikudhamiria kuleta "mkwamo" au "ugumu" wa muendelezo wa shughuli za Serikali pale ambapo Rais atafariki... Katiba hii kama chombo kinachoishi na jamii yake, kilidhamiria kuwa ikitokea Rais akafariki, basi Makamu wake ataapishwa kuwa Rais kuendeleza Serikali ile ile... au kama yeye atakavyoona inafaa kwa mamlaka aliyopewa kwa mujibu wa Katiba. Hili nitalielezea zaidi hapa chini.

Saba, katika hali ya kawaida ni wakati gani Waziri Mkuu atateuliwa? Swali hili ni la msingi sana, na ndipo Mwongozo unapopotoka na kutaka kuleta mkanganyiko usiokuwa wa lazima au manufaa kwa nchi yetu.

Ibara ya 51 ipo wazi, kwamba, kutakuwa na Waziri Mkuu atakaye teuliwa na Rais; na kwamba, "Mapema iwezekanavyo, na kwa vyovyote vile ndani ya siku kumi na nne, baada ya kushika madaraka yake, Rais atamteua Mbunge wa kuchaguliwa kutoka katika jimbo la uchaguzi..." kuwa Waziri Mkuu ambaye atathibishwa na Bunge (Ibara ya 51 (2) ).
Swali hapa ni, Je, mara tu baada ya Makamu wa Rais kuapishwa kuwa Rais kufuatia kifo cha Rais, kwa mujibu wa Ibara ya 37, Ibara ndogo ya 5, atatakiwa kuteua Waziri Mkuu mwingine? Kwa maoni yangu ni HAPANA. HAPANA KUBWA. Kwanza, kwasababu, kama nilivyokwishasema awali, Katiba hii haijadhamiria kuleta mkwamo au kusimama kwa shughuli za Serikali kufuatia kifo cha Rais. Katiba imedhamiria mwendelezo wa maisha ya Serikali na nchi kwa ujumla. Pili, hakuna Ibara yoyote au hata sheria inayotamka bayana kuwa pindi Rais akifariki, basi Waziri Mkuu atakoma kuwa Waziri Mkuu, na Baraza la Mawaziri litavunjwa... HAKUNA. Aidha, Ibara ya 51, Ibara ndogo ya 3 haisemi kuwa Waziri Mkuu atakoma kuwa Waziri Mkuu kufuatia "kifo cha Rais". Kuegemea fasili (e) ya Ibara hiyo kuwa, "atakapoacha kushika kiti cha Waziri Mkuu kwa mujibu wa masharti mengineyo ya Katiba hii." ni kupotoka, kwasababu hakuna "masharti" au matakwa yaliyo bayana ndani ya Katiba ya eti kuwa, Rais akifariki, basi Waziri Mkuu atakoma kuwa Waziri Mkuu. Na kwa vyovyote vile, Katiba ya nchi ni lazima idhamirie utulivu na muendelezo wa shughuli za Serikali, na sio kuzisimamisha, au kuleta mkwamo au ugumu. Labda Mh. Rais wa TLS na Baraza lake warejeree upya hoja yao katika Mwongozo walioutoa kwa umma na waoneshe bayana sharti hilo ndani ya Katiba, la kwamba endapo Rais akifariki, basi Waziri Mkuu atakoma kuwa Waziri Mkuu.

Kwa maoni yangu, kwa mujibu wa Katiba ya JMT, kuna namna tatu za ujumla ambapo Waziri Mkuu anateuliwa... moja, ni mara tu baada ya uchaguzi mkuu na Rais kutangazwa na kushika madaraka yake, pili, ni pale Waziri Mkuu husika atakoma kuwa Waziri Mkuu kwa mujibu wa masharti yaliyoelezwa bayana na Katiba (kujiuzulu, kufariki, Rais akimuondoa, au atapigiwa kura ya kutokuwa na imani na Bunge), na tatu, Rais atakapomteua Mbunge mwingine kuwa Waziri Mkuu.

Nane, lakini ikumbukwe kuwa, katika masharti ya mamlaka ya Rais... bila kujali kuwa ni yule aliyechaguliwa moja kwa moja na wananchi, au yule aliyekuwa Makamu wa Rais na kisha kuapishwa kuwa Rais, kufuatia kifo cha Rais, Rais anayo mamlaka ya kuteua na kutengua uteuzi wa Mawaziri wote, ikiwemo Waziri Mkuu, wakati wowote atakapoona inafaa (Ibara ya 36, 51 na 55). Pengine sasa, ni kwa kutumia mamlaka yake katika Ibara hizi, Rais huyu wa sasa anaweza kufanya teuzi au kutengua teuzi mbali mbali kwa namna hiyo... na siyo eti, kwasababu ameshika madaraka yake kufuatia kifo cha Rais aliyemtangulia, yeye akiwa Makamu wa Rais... Ikumbukwe pia kuwa, kwa dhamiri ya Katiba ya JMT, Rais na Makamu wa Rais, kiutendaji ni ofisi moja ya Urais... Makamu wa Rais akichaguliwa pamoja na Rais, na yeye akiwa Msaidizi wa Rais.

Ni kwa mantiki hiyo, kwa maoni yangu, Mwongozo huu haupo sahihi, na umepotoka. Lakini kwa vile, kwa mujibu wa Sheria inayoanzisha TLS (Kifungu cha 4), TLS inao wajibu wa kuisaidia Serikali katika masuala yanayohusu Sheria, basi ingefaa Mh. Rais wa TLS na Baraza lake la Uongozi wakashauriana na Mh. Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuhusiana na tafsiri sahihi ya suala hili, na au wakiona inafaa, wapeleke shauri la kikatiba Mahakama Kuu ili kupata tafsiri sahihi, kama inavyofaa; wakifanya hivyo na Mimi nitaomba kuingia katika shauri hilo nikiwa na maoni tofauti.
Katiba ni chombo kitukuka, kilicho hai, kinachoiongoza nchi hai, na kwa namna yoyote ile, hakipaswi kutafsiriwa ili kuleta mkanganyiko, mkwamo au ugumu wa uendeshaji wa nchi husika. Wakati wote, awali ya yote, ni purposive approach ndiyo hutumika kuisoma na kuitafsiri Katiba; na pale kweli panapokuwa na mkanganyiko, basi kanuni za misaada ya kutafsiri, kama vile harmonisation hutumika. Katika mazingira yetu ya sasa, hakuna ugumu huo, kwani Katiba iko wazi na bayana. Na ndiyo maana jana, tarehe 19 Machi, 2021, Mh. Rais, Samia Suluhu Hassan alikuwa sahihi kuendesha kikao cha Baraza la Mawaziri. Kikatiba, kinachomkabili sasa, ni yeye kushauriana na chama chake juu ya uteuzi wa jina la mtu anaempendekeza kuwa Makamu wa Rais, ambaye atapigiwa kura na Bunge kuthibitishwa. Na tunafahamu, chama chake tayari kimetangaza kuitisha kikao cha Kamati Kuu yao; na Mh. Spika kwa upande wake, ameshaliitisha Bunge mara moja. Utaona hapo, hicho nilichokuwa nakirudia hapo juu kuhusu mwendelezo wa maisha ya Serikali na nchi.
Godwin Simba Ngwilimi, Wakili (Na. 948)
+255 756 871 669
godwinsimba1@gmail.com
Uchambuzi huu wa Katiba ndio unatoa tafsiri sahihi ya ukomo wa Waziri Mkuu na Baraza la Mawaziri kutokana na kifo cha Rais wa nchi aliyekuwa madarakani.

Wenye hoja/mtazamo tofauti, kwenye mjadala huu, wana lengo ovu la kupandikisha chuki katika jamii.
 
Hata hivyo kwa tamaduni za Kiafrika, kitanzania na Misingi ya UTU, SIONI KAMA NI JAMBO JEMA SANA KUANZA KUJADILI MGAWANYO WA MADARAKA TUNGALI HATA HATUJAMZIKA ALIYEKUWA KIONGOZI WETU.

KWANINI HATUIONI HEKIMA YAKE YA KUSHUGHULIKIA MSIBA KUMSITIRI KWANZA ALIYEKUWA KIONGOZI WETU? TUNAANZA NA MAZISHI AU MIRATHI?
[/URL][/SIZE]

Amesahau kuwa aliteuliwa kabla ya maziko ya marehemu Agustino Mahiga.
 
Nimesoma andiko la TLS, kwa heshima zote kwa chombo chetu hiki kilichopewa mamlaka kisheria, Nimeshtuka sana, I wish to say,

Kwanza KATIBA HAIJAVUNJWA KWA MHE RAIS SAMIA SULUHU kuapa, na wala hakuna Mkanganyiko wowote wa Kikatiba, kwa yeye kutoteua PM na Baraza jipya. Mmekaa wote kweli mkaona hivyo.

Kwa mujibu wa Katiba Ibara ya 42(5) kuna watu wa aina mbili wanaweza kuwa Rais. Moja, Rais Mteule ambaye anatokana na Ibara ya 42(1). Mbili, Mtu anayeshika kiti cha Rais ambaye anatokana na ibara ya 37(5) na 50(2)(d) ambaye ni Makamu wa Rais. Kwa Mazingira haya, Makamu wa Rais, baada ya kifo cha Rais, anakuwa Kaimu Rais baadae ndio ameapa na kuwa RAIS wa Nchi. Rais Mteule anapatikana kutokana na uchaguzi. Hivyo basi ibara ya 57(2)(f) ya Katiba haitumiki katika mazingira haya. Kwa mjibu wa Sheria, Mhe Rais alitakiwa kutoa taarifa hii kwenye Baraza la Mawaziri baada ya kuapa na alifanya hivyo, maana yake Baraza lipo.

Hata hivyo kwa tamaduni za Kiafrika, kitanzania na Misingi ya UTU, SIONI KAMA NI JAMBO JEMA SANA KUANZA KUJADILI MGAWANYO WA MADARAKA TUNGALI HATA HATUJAMZIKA ALIYEKUWA KIONGOZI WETU. HUU SIO MSIBA MDOGO, JAMBO HILI ZITO LIKO MIKONONI MWA RAIS WETU MAMA SAMIA SULUHU, HALAFU SISI TUANZE KUMPATIA MAMBO YA MARA TEUA PM, MARA VUNJA BARAZA, KATIBA INAELEKEZA RAIS KUAPA NA NAMNA YA KUMPATA MAKAMU WA RAIS.

KWA MJIBU WA KATIBA RAIS ANARUHUSIWA KUVUNJA BARAZA MUDA WOWOTE NA KUPANGA ATAKAVYO HATA SIO KWA MAZINGIRA KUAPA KWAKE,

KWANINI HATUIONI HEKIMA YAKE YA KUSHUGHULIKIA MSIBA KUMSITIRI KWANZA ALIYEKUWA KIONGOZI WETU? TUNAANZA NA MAZISHI AU MIRATHI? 😭😭😭😭

Pia soma > TLS: Kwa Mujibu wa Katiba, sasa Tanzania haina baraza la Mawaziri, Rais Samia atakiwa kuteua Waziri Mkuu ndani ya siku 14
TLS walitoa hoja zao kwa vigezo vya kikatiba na kisheria.

Mwigulu ame manipulate vifungu vya katiba kwa faida ya kisiasa kwake yeye binafsi kwani hana uhakika wa kurejeshwa mama akivunja baraza..... which she will do, much to the chagrin of Mwigulu & co!

Mwacheni mama afanye kazi. Kumbuka naye atakuwa anafanya kazi yake kipindi hiki with one eye on the 2025 presidential contest. So, najua yule mama yupo smart - smart enough kuweza kutumia state apparatus at her disposal katika kuhakikisha potential presidential contestants wengine kama Mwigulu wanakuwa weakened as much as possible in the public eye.... moja ya strategy kufanikisha hili inaweza kutokuwapa kina Mwigulu nafasi za uteuzi ambazo definetely zinaweza kuwapa umaarufu.

Kwako comrade Mwigulu Nchemba
 
Nimesoma mwongozo uliotolewa na chama cha wanasheria Tanzania bara( Tanganyika Law Society)* ambao umesainiwa na Rais wa chama hicho Dr Rugemeleza Nshala

Mwongozo huo unajibu swali lifuatalo

Je, Katiba inalazimisha au inamtaka Rais aunde na aapishe Baraza la Mawaziri pindi atakapotwaa madaraka baada ya Rais kufariki dunia?

Ukisoma katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania, ya mwaka 1977 kwenye ibara ya 37( 5) imeeleza kuwa, endapo kiti cha Rais kitakuwa wazi kutokana na Rais aliyeko madarakani kupoteza sifa za kuwa Rais ikiwemo kufariki dunia, basi makamu wa Rais ataapishwa na kuwa Rais mpya wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Je, baada ya makamu wa Rais kuapishwa na kuwa Rais mpya wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, baraza la mawaziri linakuwa limevunjwa?

Jibu la hilo swali ni HAPANA, baada ya makamu wa Rais kuapishwa na kuwa Rais, baraza la mawaziri la awali, bado linaendelea kama kawaida, kwa maana ya waziri mkuu, mawaziri na wajumbe wengine wanaendelea na nyadhifa zao kama kawaida.

Kwa nini?

Kwa sababu, ukisoma katiba ya jamhuri wa muungano wa Tanzania, ya mwaka 1977, kwenye ibara 42(5), inaeleza aina ya watu wanaoweza kuapishwa na kuwa Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania

Ibara hiyo ya 42(5), inasema " Kila Rais mteule na na kila mtu atakayeshikilia kiti cha Rais, kabla ya kushika madaraka yake, ataapa mbele ya jaji mkuu wa jamhuri ya muungano "

Kwa hiyo hapo kwenye hiyo ibara ya 42(5), inaeleza kuna aina 2 za watu wanaoweza kuapishwa na kuwa Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania

1. Rais mteule, ambaye huyu amefafanuliwa vizuri kwenye ibara 42(1) ya katiba ya jamhuri wa muungano wa Tanzania, ya mwaka 1977 pamoja na marekebisho yake

2. KIla mtu atakayeshika madaraka ya Rais,ambaye huyu amefafanuliwa kwenye ibara ya 37(3) ya katiba ya jamhuri wa muungano wa Tanzania, ya mwaka 1977, ambao ni wafuatao kwa kufuata mtiririko kutoka juu.

a) Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

b) Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

c) Jaji Mkuu wa mahakama kuu ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania

Kwa hiyo sasa ni Rais mteule tu, ambaye ameshinda uchaguzi mkuu wa Rais na kutangazwa mshindi na tume ya taifa ya uchaguzi( NEC), ndiye akiapishwa kushika madaraka yake, waziri mkuu, mawaziri, Naibu mawaziri na mwanasheria mkuu wa serikali wote wanakoma kuendelea na nyadhifa zao, na hiyo imeelezwa kwenye ibara ya 51(3)(a) na ibara ya 57(2)(f) ya katiba ya jamhuri wa muungano wa Tanzania ya mwaka 1977

Lakini makamu wa Rais au Spika wa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania au Jaji mkuu wa mahakama kuu ya jamhuri wa muungano wa Tanzania, endapo watatokea kuapishwa na kuwa Rais kwa sababu yeyote ile iliyotokana na Rais aliyeko madarakani kupoteza sifa za kuwa Rais, basi waziri mkuu, mawaziri , manaibu waziri na mwanasheria mkuu wa serikali, wote wanaendelea na nyadhifa zao kama kawaida

Hivyo basi, Rais aliyeko madarakani anapofariki dunia, hiyo haimfanyi makamu wake wa Rais kuwa Rais mteule,bali makamu wa Rais ataapishwa kuwa Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania,kutokea kwenye nafasi yake ya makamu wa Rais

Mheshimiwa Rais mama Samia Hassan Suluhu, kabla ya kula kiapo chake jana, hakuwa Rais mteule, bali alikuwa ni makamu wa Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania, ndio maana hata baada ya kula kiapo, baraza la mawaziri liliendelea kuwepo na mara tu baada ya kiapo, alienda kuongoza kikao cha baraza la mawaziri kwa mara ya kwanza kama Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania

Japo sasa, baada ya kushika madaraka ya Rais, mheshimiwa Rais mama Samia Hassan Suluhu, anaweza kufanya mabadiliko ya baraza lake la mawaziri kwa kadri atakavyoona yeye inafaa na kwa muda atakao amua yeye

Ngamanya Kitangalala Mwaswala
0756 669494
 
Back
Top Bottom