Waziri wa JK ampinga Karamangi...

Bill

JF-Expert Member
Oct 5, 2007
8,235
8,432
Waziri wa JK ampinga Karamagi

2007-10-23 15:55:27
Na Emmanuel Lengwa, Jijini


Wakati Wizara ya Nishati na Madini inayoongwa na Waziri Nazir Karamagi ikidaiwa kutoa uamuzi kuwa mgodi wa Epanko ulioko wilayani Ulanga Morogoro umilikiwe na kampuni moja ya uwekezaji, Waziri mwenzie wa Serikali ya sasa, amepinga uamuzi huo.

Aliyepinga maamuzi yanayodaiwa kutolewa na Wizara ya Bw. Karamagi, ni Bi. Celina Kombani ambaye ni Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa.

Akizungumza na Alasiri kwa njia ya simu leo asubuhi, Bi. Kombani ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Ulanga Mashariki kuliko na mgodi huo wa Epanko, amesema kama kuna uamuzi wa kuipa uhalali wa umiliki kampuni binafsi na kuwaacha wachimbaji wadogo, yeye kamwe haungi mkono jambo hilo.

Akasema Bi. Kombani kuwa msimamo wake, kama mbunge wa wapiga kura wake hao, ni kwamba sheria za nchi zitumike ipasavyo katika kutoa uamuzi kuhusu eneo hilo ambalo limekuwa na mgogoro kwa muda mrefu.

`Msimamo wangu kama Mbunge wa eneo hilo, ni kwamba sheria itumike kumaliza mgogoro huo ? na mwishoni mwa yote, wananchi lazima wapewe haki yao,` akasema Bi. Kombani.

Akifafanua zaidi, Waziri Kombani akasema kuwa yeye yupo upande wa Serikali lakini, wakati huohuo, hawezi kuunga mkono maamuzi yanayowaumiza wapiga kura wake kwa sababu anapaswa kuwajibika kwao.

`Mimi nipo Serikalini na pia nipo kwa wananchi ambao ndio wapiga kura wangu? siwezi kupendelea upande wowote. Ninachoweza kusema ni kwamba hapo inabidi sheria itumike,` akasema.

Akifafanua zaidi, Bi. Kombani amesema wachimbaji wadogo walikuwapo katika eneo hilo tangu zamani na hivyo, anaamini kuwa sheria zikifuatwa vyema, mgodi huo utaangukia mikononi mwao.

Hata hivyo, wakati Bi. Kombani akitoa msimamo huo, inadaiwa kuwa Wizara ya Nishati na Madini imetoa umauzi wa kuumilikisha mgodi huo kwa kampuni moja ya uwekezaji.

Inaelezwa zaidi kuwa, kutokana na uamuzi huo wa Wizara ya Nishati na Madini, wananachi wa eneo hilo wamejikuta wakiwa kwenye mapambano ya mara kwa mara na walinzi wa kampuni husika.

Hatahivyo, imeelezwa zaidi kuwa juzi, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Meja Mstaafu Said Kalembo, alilazimika kuufunga mgodi huo kutokana na hali ya eneo hilo kuashiria vurugu na uvunjifu wa amani.

Meja Jenerali Kalembo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi ya Mkoa huo, alisema mgodi huo utaendelea kufungwa hadi hapo Wizara ya Nishati na Madini itakapotoa ufafanuzi zaidi juu ya mgogoro uliopo
 
Upinzani kila mahali. Vyema Kombani lazima ukweli usemwe hata kama unauma. Well done kuwapigania wapiga kura wako.
 
Sasa nadhani mkuki umekuwa kwa Nguruwe na leo umemgusa mwanadamu wa Ulanga .Sasa akina Mkono mbona hawa kumuunga mkono Chacha Wangwe ?
 
Asante mama Celina Kombani, ni Miongoni mwa viongozi makini kwenye serikali ya JK.. mama amejitahidi sana kuwanyanyua watani wangu wapogoro... na shule yake ya Selina Kombani iko kamili, shida wapogoro wengi hawapendi elimu....walimu wanatosha na vitabu.. cha muhimu asijisahau wananchi keta keta huko mwaya wanakuomba japo bara bara .....big up Kumpinga Karamagi hadharani....Dr Ngasongwa upo?
 
haya kayasema yeye au kasemewa au spinning yeye hajui ni vipi kukutana na waziri husika kulizungumza, jee vikao vya mawaziri hamna?

mie nnahofia ni udaku tu
 
Muwekezaji mzawa BW. Hendry Nyiti Mbona magazeti wanaogopa kutaja mmiliki wa mgodi huo na jina la kampuni.

jina la kampuni ni INTERSTATE MINING CO. LTD
Mmiliki ni swaiba wa Lowassa mfanyabiashara mahafuru wa madini aina ya tanzanite Bw.Hendry Nyiti.
 
Muwekezaji mzawa BW. Hendry Nyiti Mbona magazeti wanaogopa kutaja mmiliki wa mgodi huo na jina la kampuni.

jina la kampuni ni INTERSTATE MINING CO. LTD
Mmiliki ni swaiba wa Lowassa mfanyabiashara mahafuru wa madini aina ya tanzanite Bw.Hendry Nyiti.


Hasara

Hii habari ilipotoka kwamba Karamagi kafanya madudu mengine kampuni iliyotajwa sio Interstate...wewe una info nyingine zinazoihusisha Interstate na huu mgodi wa Ulanga?
 
huyo bibi ni mnafiki kama alivyo jk na baraza lote la wezi.c .kombani kama hukubaliani na maamuzi ya wenzako njia ni nyeupe ni kuachia ngazi ili uwatetee vema wapigakura yako na kujijengea heshima kwa watanzania wote.ccm hakuna sheria kama unafikiri hiyo ndio kweli basi subiri uone kilichimtoa kanga manyoya.
 
haya kayasema yeye au kasemewa au spinning yeye hajui ni vipi kukutana na waziri husika kulizungumza, jee vikao vya mawaziri hamna?

mie nnahofia ni udaku tu

Nina uhakika wanapigwa mkwara kama ule ambao EL anawapiga wabunge wa CCM.
 
;) Naomba niulize, huyu Nyiti, siye ambaye rubani wa ATC alikataa kurusha ndege mpaka ashuke? NIlisoma kwenye gazeti moja hivi majuzi.
 
haya kayasema yeye au kasemewa au spinning yeye hajui ni vipi kukutana na waziri husika kulizungumza, jee vikao vya mawaziri hamna?

mie nnahofia ni udaku tu

Tena majuzi tu kulikuwa na kikao cha siri cha baraza la mawaziri, kwa nini asisemee huko?

Hebu tupate habari zaidi kwa undani maana hii Karamagi, sasa kila kiongozi anatafuta sifa za bure!
 
At the end of the day kila mtu atabeba msalaba wake mwenyewe.
 
Tena majuzi tu kulikuwa na kikao cha siri cha baraza la mawaziri, kwa nini asisemee huko?

Hebu tupate habari zaidi kwa undani maana hii Karamagi, sasa kila kiongozi anatafuta sifa za bure!

Inawezekana kwenye hicho kikao cha siri cha baraza la mawaziri alizidiwa nguvu. Tatizo ni kwamba ukishakuwa waziri na ukazidiwa kwenye kikao cha baraza hata uende wapi hakuna atakayekusikiliza. Serikali yetu inakumbatia ulaji na haijali maslahi ya wananchi. Kombani alichofanya ni kuonyesha wapiga kura wake kwamba hakubaliani na swala hilo. Lakini approach nzuri ilikuwa ni yeye kuachia ngazi ili aweze kutumikia vyema wapiga kura wake. Ukishakuwa waziri na wakati huo huo mbunge wa kuchaguliwa, unakosa uhuru wa kutekeleza majukumu yako kama muwakilishi wa wananchi. Niliwahi kuongelea swala la mtu kuwa Mkuu wa Mkoa na Mbunge kwa wakati mmoja, leo naona tumeona kwa mfano halisi. Hata kama Kombani angemfuata waziri husika na kuongea nae kiutu uzima, unadhani kama kuna wakubwa wameishashikishwa kitu kidogo ndiyo atamsikiliza? Akikosa Ubunge 2010 hiyo ni juu yake.

Lakini sasa naona huyo mama amekalia kuti kavu, maana akiachia ngazi anaweza kupigwa chini 2010 kwenye uteuzi wa kugombea Ubunge. Akiendelea kuwa serikalini na kushindwa kuwatetea wapiga kura wake inawezekana wakampiga chini 2010!
 
Angeenda kumshitaki kwa Waziri Mkuu, baadaye kwa Makamu wa Rais, na Rais mwenyewe,

Otherwise tujihadhari sana na hawa viongozi wanaojaribu kudandia mgongo wa Karamagi, na list ya mafisadi, maana ndio hawa hawa waliolilia kuwa lazima tuongozwe na vijana safari hii!
 
Angeenda kumshitaki kwa Waziri Mkuu, baadaye kwa Makamu wa Rais, na Rais mwenyewe,

Otherwise tujihadhari sana na hawa viongozi wanaojaribu kudandia mgongo wa Karamagi, na list ya mafisadi, maana ndio hawa hawa waliolilia kuwa lazima tuongozwe na vijana safari hii!

Waziri mkuu si ndio tunasikia yeye na Karamagi ni damu damu.
 
Kwa mtizamo mwepesi,ni rahisi kuhisi kwamba huyo mama amekurupuka.Lakini,wa mtizamo wa kina zaidi,alichofanya mama huyo ni dalili ya namna serikali hii ya JK ilivyokosa mwelekeo to an extent that collective responsibility inakuwa ni ya kinadharia zaidi kwenye cabinet/ndani ya vikao vya chama while practically impossible pale waziri/mbunge anapokabiliana na wapigakura wake.

Let's face it,hivi mwakilishi gani mwenye akili timamu,na ambaye amekulia katika eneo analowakilisha (implying kwamba kuna ndugu zake wa damu watakaoathirika na maamuzi flani),anaweza kudiriki kutoa consent ya kipande cha ardhi ya nduguze ikabidhiwe kwa "mwekezaji" ambaye sanasana atakachochangia ni kunenepa kwa akaunti ya Karamagi ilhali wenye ardhi wakipokonywa haki yao?

CCM na taasisi zake za utawala (serikali,bunge,etc) wamejitengenezea mfumo ambao unahalalisha pongezi na kuunga mkono tu,na sio kukemea,kukosoa au kupinga yale yanayoelekea kuathiri wananchi.Ni dude ambalo halitaki kukosolewa,na wenyenafasi pekee ya kukosoa ni wale who have got nothing to lose (eg Butiku,Mwinyi,Bilali,etc.Naamini kuna wengi walio serikalini,bungeni au kwenye chama ambao hawaridhishwi na baadhi ya mambo flani lakini wanatambua bayana nini kitawakuta pindi wakiweka misimamo yao katika vikao husika.However,hao ni wanafiki kama CCM yao kwani kama kweli wana uchungu na nchi yao au wale wanaowawakilisha basi hawataogopa kukemewa au kunyang'anywa madaraka.Hili ndio tatizo la siasa kugeuka ajira,viongozi wanakuwa waoga kupoteza political posts kwa vile ndio eneo pekee la kupeleka mikono yao vinywani.
 
Ndio maana mimi binafsi naona Mawaziri wasiwe wabunge maana wabunge ni wawakilishi wa wananchi serikalini na mawaziri ni wawakilishi wa serikali kwa wananchi. Huyu mama anapata shida sana na ndio maana anasema kwa kuzunguka sana. Ni kweli hili jambo linamuuma na anataka kutetea wananchi at the same time anasema mimi nipo pia upande wa serikali.


Hii nasema hivyo maana mbunge wangu wa Moshi Vijijini Dr. Siril Chami watu walimchagua lakini kwa sababu ya kuwa yeye ni Naibu waziri huwezi kumsikia akiiuiza swali lolote linalohusu masilahi ya wananchi. Ni vigumu kutumikia mabwana wawili kwa wakati mmoja.

http://www.nationmaster.com/graph/eco_gdp_percap-economy-gdp-nominal-per-capita
 
manaibu hawaingiii? hii ni ya kweli wajameni na kama kweli mie nilikuwa sijui nnaomba mnipatie ushahidi ili nijue pa kushika.

basi hata iwe hivyo huyo bosi wake hawezi kushauriana nae nakumfikishia shauri hilo kikaoni?

kwa nini asioneshe kukerwa kwake on the sport tena kwa kumuandikia rais aliemteua kuwa yeye haridhiki na hilo, akipuuzwa aaamue kujiuzulu na kwenda maelezo kueleza kwa uwazi?

au ndio nitoke vipi?
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom