DIDAS TUMAINI
JF-Expert Member
- Nov 11, 2014
- 229
- 582
WATEULIWA WANA MENGI MOYONI.
Aliyekuwa WAZIRI wa Habari katika utawala wa Dikteta Mobutu, Mh. Sakombi Inongo siku moja alipewa saa chache abuni kitu ambacho kitamtukuza Rais wake na kumfanya watoto wanaokua kumuona ni MUNGU. Baada ya kutulia ofisini kwake,alikuja na ubunifu wa kipande cha video ambacho kinaonyesha picha ya Rais Mobutu akichomoza katika mawingu. Watoto katika Taifa la Congo waliishi wakijua Rais Mobutu ni MUNGU. Kipande kile cha video kilichezwa kabla ya kurushwa kipindi chochote kwenye luninga.
Waziri huyo ndiyo alihakikisha wasanii wa muziki na makundi mengine wanatunga nyimbo za kumsifia na kumtukuza Rais Dikteta Mobutu muda wote.
......................................................
Cha kumsikitisha WAZIRI huyo ni kwamba Rais wake huyo alikuja kutembea kimapenzi na mkewe. Tangu mkewe anatongozwa alikuwa anajua ila waziri huyo hakuwahi kufumbua mdomo kukalipia au kukemea jambo hilo kwa hofu ya kupoteza maisha yake. Katika mahojiano maalumu waziri huyo anakili wazi kuwa Rais Mobutu alikuwa akipenda sana kuchukua wake wa wateule wake.
.......................................................
Aliyekuwa WAZIRI wa Habari katika utawala wa Dikteta Mobutu, Mh. Sakombi Inongo siku moja alipewa saa chache abuni kitu ambacho kitamtukuza Rais wake na kumfanya watoto wanaokua kumuona ni MUNGU. Baada ya kutulia ofisini kwake,alikuja na ubunifu wa kipande cha video ambacho kinaonyesha picha ya Rais Mobutu akichomoza katika mawingu. Watoto katika Taifa la Congo waliishi wakijua Rais Mobutu ni MUNGU. Kipande kile cha video kilichezwa kabla ya kurushwa kipindi chochote kwenye luninga.
Waziri huyo ndiyo alihakikisha wasanii wa muziki na makundi mengine wanatunga nyimbo za kumsifia na kumtukuza Rais Dikteta Mobutu muda wote.
......................................................
Cha kumsikitisha WAZIRI huyo ni kwamba Rais wake huyo alikuja kutembea kimapenzi na mkewe. Tangu mkewe anatongozwa alikuwa anajua ila waziri huyo hakuwahi kufumbua mdomo kukalipia au kukemea jambo hilo kwa hofu ya kupoteza maisha yake. Katika mahojiano maalumu waziri huyo anakili wazi kuwa Rais Mobutu alikuwa akipenda sana kuchukua wake wa wateule wake.
.......................................................