Waziri wa Elimu, Prof. Ndalichako, tunaomba NACTE watoe matokeo ya Wanafunzi kwa mtindo wa NECTA. Vyuo vimegoma kutoa matokeo ya muhula 2/2020

Retired

JF-Expert Member
Jul 22, 2016
40,179
73,616
Kumekuwepo na matatizo makubwa NACTE mnapotuma matokeo ya watoto vyuoni.

Mtoto hawezi kuyaona ontime pia na wazazi. Kumekuwa au kuna uwezekano mkubwa hata wa ku- manipulate/ku-temper na ufaulu wa watoto kwa faida ya chuo/walimu etc.

Maadam chuo ndicho kinamwonesha mwanafunzi matokeo, chochote kinaweza kufanyika yakitua kwa Mkuu/Mwalimu mwenye nia OVU.

Ushahidi upo mkubwa tu.
Waziri wa Elimu tafadhali ingilia hili. Matokeo yawekwe/yatangazwe kama yanavyotangazwa matokeo ya NECTA ya forms 2,4 and 6.

NECTA kunakuwepo na uwazi wa kutosha ambapo shule haiwezi ku-temper na matokeo ya watoto.
Mpaka sasa matokeo ya Semester 2/2020 bado baadhi ya vyuo hawataki kuwaonesha wanafunzi matokeo yao.

Kunakuwa na usiri mkubwa katika kutoa matokea kwa baadhi ya vyuo, kitu ambacho kinatia mashaka na usiri huo.

Mpaka sasa/leo hii 15/11/2020 baadhi ya vyuo hawataki kutoa matokeo ya wanafunzi.
 
Kumekuwepo na matatizo makubwa NACTE mnapotuma matokeo ya watoto vyuoni. Mtoto hawezi kuyaona ontime pia na wazazi. Kumekuwa au kuna uwezekano mkubwa hata wa ku- manipulate/KU-TEMPER na passes za watoto kwa benefit ya chuo/walimu etc. As long as chuo ndicho kinamwonyesha mwanafunzi matokeo, anything can be done yakitua kwa mKuu/Mwalimu mwenye nia OVU. Ushahidi upo mkubwa tu...
Malizieni kulipa ada za watoto wenu, mpate matokeo
 
Kumekuwepo na matatizo makubwa NACTE mnapotuma matokeo ya watoto vyuoni. Mtoto hawezi kuyaona ontime pia na wazazi. Kumekuwa au kuna uwezekano mkubwa hata wa ku- manipulate/KU-TEMPER na passes za watoto kwa benefit ya chuo/walimu etc. As long as chuo ndicho kinamwonyesha mwanafunzi matokeo, anything can be done yakitua kwa mKuu/Mwalimu mwenye nia OVU. Ushahidi upo mkubwa tu...
Mkuu mbona umeshindwa kueleza kisomi?, Hakuna atakayekuelewa hapo. Ungeeleza no nyuo vya namna gani hivyo, manake mi ninavyojua vyuo vilivyochini ya NACTE vinatoa mitihani vyenyewe na kupeleka matokeo NACTE, sasa wewe unasema NACTE ndio wanatoa matokeo then vyuo vinayaficha. Fafanua ueleweke unaongelea vyuo vya namna gani?
 
Mkuu mbona umeshindwa kueleza kisomi?, Hakuna atakayekuelewa hapo. Ungeeleza no nyuo vya namna gani hivyo, manake mi ninavyojua vyuo vilivyochini ya NACTE vinatoa mitihani vyenyewe na kupeleka matokeo NACTE, sasa wewe unasema NACTE ndio wanatoa matokeo then vyuo vinayaficha. Fafanua ueleweke unaongelea vyuo vya namna gani?
1. Si vema kutaja vyuo maana uta implicate JF kwenye legal wrangle na vyuo tajwa and JF is posed to delete the thread.

2. It seems hujui how the exam system works at NACTE! tafuta mtu akuelezee....... walio kwenye system ya NACTE wanaelewa nilichoandika.

3. In a nutshell, Siyo kweli kuwa NACTE colleges wanatoa mitihani wenyewe, hizo ni CA (ambazo vile vile overseer ni NACTE), final exams ie SEMESTER EXAMS zinatolewa na NACTE. (unachanganya na Universities ambazo kila University inamaliza kila kitu yenyewe with regard to exams, ukiondoa mambo ya external examiner and paper moderation
 
Malizieni kulipa ada za watoto wenu, mpate matokeo
As long as hoja ya ada haijatajwa, basi that hoja ya ada does not arise in my post.

All in all, kwani sekondari huwa hakuna watotot ambao hawajamaliza kulipa ada? nasema watumie mtindo wa NECTA, kama kuna kulipa ada, atabanwa wakati wa kuchukua cheti kama ni finalists
 
Kumekuwepo na matatizo makubwa NACTE mnapotuma matokeo ya watoto vyuoni.

Mtoto hawezi kuyaona ontime pia na wazazi. Kumekuwa au kuna uwezekano mkubwa hata wa ku- manipulate/ku-temper na ufaulu wa watoto kwa faida ya chuo/walimu etc...
Huyo NDALICHAKO, ameteuliwa lini kuwa Waziri?
 
1. Si vema kutaja vyuo maana uta implicate JF kwenye legal wrangle na vyuo tajwa and JF is posed to delete the thread
2. It seems hujui how the exam system works at NACTE! tafuta mtu akuelezee...
Mkuu wewe ndio huelewi kabisa, au unasoma vyuo vya afya hivyo ndio vina utaratibu mitihani haitungwi na chuo. Mimi nafundisha vyuo hivyohivyo vilivyo chini ya NACTE tena Cha serikali. Hivi vyuo kila kitu kinafanywa na chuo matokea ndio hupelekwa NACTE mkuu wewe mbona unapotosha watu hivyo! Mi ni mwalimu wa hivyo vyuo ujue!
 
Mkuu wewe ndio huelewi kabisa, au unasoma vyuo vya afya hivyo ndio vina utaratibu mitihani haitungwi na chuo. Mimi nafundisha vyuo hivyohivyo vilivyo chini ya NACTE tena Cha serikali. Hivi vyuo kila kitu kinafanywa na chuo matokea ndio hupelekwa NACTE mkuu wewe mbona unapotosha watu hivyo! Mi ni mwalimu wa hivyo vyuo ujue!
Mimi naongelea vyuo vya afya! tumepishana, but all in all ebu soma bolded kipengele hiki: kina maana gani

Procedures for Assessment Conducted by NACTE and Autonomous Technical Institutions
EDITED VERSION
July 2016

3.2.2 Guidelines for Examination Setters
(a) Questions should have a positive value. They should aim at finding out what is known rather than what is not known. They should give a candidate an opportunity rather than a trap.
(b) The content of the paper should be chiefly guided by the curriculum used bearing in mind that the examination is being set for candidates in different institutions.
 
Hapo sawa, vyuo vya Afya na vile vya ualimu mitihani haitungwi na chuo, lakini vingine vyote chuo hufanya kila kitu na matokeo final ndio hupelekwa NACTE
Mkuu wewe unafundisha cha Afya au Ualimu?
Mbona hata Afya NACTE ndo wapo responsible na kutunga na kusahisha hiyo mitihani ama wewe unaongelea vipi?!
 
Mkuu wewe unafundisha cha Afya au Ualimu?
Mbona hata Afya NACTE ndo wapo responsible na kutunga na kusahisha hiyo mitihani ama wewe unaongelea vipi?!
semester exams haitungwi na chuo... usichanganye na CA
 
Hapa ukweli kuna ulazima wa hii NACTE kuchunguzwa.
Wameshindwa kabisa kukemea uozo wa uendeshaji katika vyuo.

Vyuo havina usimamizi kabisa hasa hivi vya binafsi.Mmiliki ana uwezo wa kuamka na kuamua chochote kuhusu maslahi ya mwanafunzi na mtumishi.

Mfano mwanafunzi ameambiwa atoe shilingi laki 3 kwa ajili ya mafunzo ya vitendo.Mmiliki ana uwezo wa kusema mwanafunzi aende kwao atafute sehemu ajifunze kwa gharama zake bila kusimamiwa na wakati pesa imelipwa.Ukiuliza walimu wanasema hawawezi kuja kusimamia kwa vile hawajalipwa.Unaona mambo yanapita tu na hata taarifa zikitolewa NACTE,zinabadilishwa kuwa ni majungu.

Kwa maoni yangu kuna ulazima wa kuwachunguza hawa NACTE,kuna nini kati yao na wamiliki wa vyuo!

Nimewahi kusema kuhusu vyuo kutokuwa na bodi za usimamizi.Ila hakuna anayejali.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom