Waziri wa Elimu afutwa mamlaka ya kusimamia wafanyakazi katika Wizara hiyo

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
Tume ya Utumishi wa Umma (PSC) Ijumaa ilimpokonya Waziri wa Elimu Prof George Magoha mamlaka ya kusimamia wafanyakazi katika wizara hiyo.

Kwenye taarifa iliyotumwa kwa vyombo vya habari na Mkurugenzi wa PSC Browne Kutswa, mwenyekiti wa tume hiyo Stephen Kirogo alipeleka mamlaka hayo kwa Katibu wa Wizara hiyo anayesimamia Elimu ya Msingi Dkt Belio Kipsang’.

Hii ni kufuatia kisa cha wiki iliyopita ambapo Prof Magoha alinaswa kwenye video akimfokea, kumdhalilisha na kumtusi hadharani Mkurugenzi wa Elimu wa Uasin Gishu Gitonga Mbaka katika shule ya msingi ya Langas, mjini Eldoret.

Ijumaa Bw Kirongo akasema kwenye taarifa hiyo iliyonakiliwa kwa wenyekiti wa Mabaraza ya Vyuo Vikuu na Mkuu wa Utumishi wa Umma Joseph Kinyua kwamba “masuala yote ya wafanyakazi katika Wizara ya Elimu yatasimamiwa na Dkt Kipsang’ hadi wakati usiojulikana.”

Karogo alisema kuwa hatua hiyo inatokana na mamlaka ya PSC na kujitolea kwake kuwakinga watumishi wa umma dhidi ya kukaripiwa na kudhalilishwa bila sababu maalum.

“Utekelezaji wa mamlaka ya tume uliotwikwa afisa fulani sharti undeshwe kwa njia ambayo inajenga imani, heshima na maadili ya utumishi wa umma.” Akasema Bw Kutswa.

Kufuatia kisa hicho, Prof Magoha ameapa kutoomba msamaha kwa kumkosea heshima Bw Mbaka mbele ya maafisa wadogo wake akijigamba kuwa huo ndio mtindo wake wa kufanya kazi.

“Watu hawapaswi kushangazwa na mtindo wangu wa kufanya kazi. Nilihudumu katika Baraza la Kitaifa la Mitihani (KNEC) ambako nililainisha mambo. Sasa niko hapa kuhakikisha kuwa mahitaji ya wazazi na wanafunzi yanatizwa wakati wowote ule. Ikiwa siwezi kufanya hivyo basi sio haja ya kuendelea kuhudumu katika wizara hii,” akasema siku moja baadaye alipozuru Shule ya Msingi ya Kyamutheke, Kaunti ya Machakos.
Hii ni baada ya Chama cha Walimu wa Shule za Upili na Vyuo vya Kadri (KUPPET) tawi la Uasin Gishu kumtaka ajiuzulu kwa kumtusi Bw Mbaka, mkurugenzi wa elimu mwenye tajriba ya miaka mingi. Wakenya mitandaoni pia walimtaka Profesa Magoha ajiuzulu au afutwe kazi na Rais Uhuru Kenyatta.

Mnamo siku ya tukio, Prof Magoha alionekana akimtusi Bw Mbaka, mwenye nywele nyeupe, kwa kutohakikisha kuwa usafi umedumishwa katika shule hiyo ya msingi ya Langa.

“Mazingira hapa sio safi,” akasema Waziri. Naye Bw Mbaka akajibu hivi; “Suala hili litashughulikiwa katika ripoti itakayoandaliwa na afisi yangu.”

Ndiposa Magoha akafoka: “Siongei kuhusu ripoti. Nazungumza kuhusu hali iliyoko hapa, uchafu uliotapakaa kote. Nikikuita mjinga, je, nitakuwa nimedanganya?”

Hapa ndipo Waziri huyo alimwamuru Bw Mbaka aondoke kutoka ujumbe ulioandamana naye kukagua hali ya masomo shuleni humo na utekelezaji wa mpango wa usambazaji madawati na kumsindikiza kwa tusi la: “Wewe ni mjinga kabisa.”
 
Apunguze kiburi huyu waziri na afahamu kwamba madaraka yake hayampi ruhksa ya kuwadhalilisha wadogo zake kwenye wizara ya elimu. Ajifunze kutoka kwenye kisa cha aliyekuwa Naibu Jaji Mkuu Nancy Baraza.

Ambaye alifutwa kazi baada ya kumtishia na bastola na kumchuna pua mlinzi Rebecca Kerubo na kumuambia "you should know people". Kisa tu hakuwa anataka kufanyiwa 'pekshen' kwenye lango kabla ya kuingia kwenye 'mall' ya Village Market.

Kenya's Deputy Chief Justice Suspended, Being Investigated
 
Huyu waziri huwa namkubali sana kwenye utenda kazi wake, ila kama hayo aliyoyasema ni kweli basi hicho kibano kimhusu tena bila kulegeza. Nchi hii hatupo tayari kwa madikteta na wadhalilishaji, ukiwa kiongozi unapaswa kufahamu nafasi yako lazima iakisi maadili mema.
 
Tume ya Utumishi wa Umma (PSC) Ijumaa ilimpokonya Waziri wa Elimu Prof George Magoha mamlaka ya kusimamia wafanyakazi katika wizara hiyo.

Kwenye taarifa iliyotumwa kwa vyombo vya habari na Mkurugenzi wa PSC Browne Kutswa, mwenyekiti wa tume hiyo Stephen Kirogo alipeleka mamlaka hayo kwa Katibu wa Wizara hiyo anayesimamia Elimu ya Msingi Dkt Belio Kipsang’.

Hii ni kufuatia kisa cha wiki iliyopita ambapo Prof Magoha alinaswa kwenye video akimfokea, kumdhalilisha na kumtusi hadharani Mkurugenzi wa Elimu wa Uasin Gishu Gitonga Mbaka katika shule ya msingi ya Langas, mjini Eldoret.

Ijumaa Bw Kirongo akasema kwenye taarifa hiyo iliyonakiliwa kwa wenyekiti wa Mabaraza ya Vyuo Vikuu na Mkuu wa Utumishi wa Umma Joseph Kinyua kwamba “masuala yote ya wafanyakazi katika Wizara ya Elimu yatasimamiwa na Dkt Kipsang’ hadi wakati usiojulikana.”

Karogo alisema kuwa hatua hiyo inatokana na mamlaka ya PSC na kujitolea kwake kuwakinga watumishi wa umma dhidi ya kukaripiwa na kudhalilishwa bila sababu maalum.

“Utekelezaji wa mamlaka ya tume uliotwikwa afisa fulani sharti undeshwe kwa njia ambayo inajenga imani, heshima na maadili ya utumishi wa umma.” Akasema Bw Kutswa.

Kufuatia kisa hicho, Prof Magoha ameapa kutoomba msamaha kwa kumkosea heshima Bw Mbaka mbele ya maafisa wadogo wake akijigamba kuwa huo ndio mtindo wake wa kufanya kazi.


Hii ni baada ya Chama cha Walimu wa Shule za Upili na Vyuo vya Kadri (KUPPET) tawi la Uasin Gishu kumtaka ajiuzulu kwa kumtusi Bw Mbaka, mkurugenzi wa elimu mwenye tajriba ya miaka mingi. Wakenya mitandaoni pia walimtaka Profesa Magoha ajiuzulu au afutwe kazi na Rais Uhuru Kenyatta.

Mnamo siku ya tukio, Prof Magoha alionekana akimtusi Bw Mbaka, mwenye nywele nyeupe, kwa kutohakikisha kuwa usafi umedumishwa katika shule hiyo ya msingi ya Langa.

“Mazingira hapa sio safi,” akasema Waziri. Naye Bw Mbaka akajibu hivi; “Suala hili litashughulikiwa katika ripoti itakayoandaliwa na afisi yangu.”

Ndiposa Magoha akafoka: “Siongei kuhusu ripoti. Nazungumza kuhusu hali iliyoko hapa, uchafu uliotapakaa kote. Nikikuita mjinga, je, nitakuwa nimedanganya?”

Hapa ndipo Waziri huyo alimwamuru Bw Mbaka aondoke kutoka ujumbe ulioandamana naye kukagua hali ya masomo shuleni humo na utekelezaji wa mpango wa usambazaji madawati na kumsindikiza kwa tusi la: “Wewe ni mjinga kabisa.”
Hii taarifa au huo uamuzi wa tume nao haujakaa sawa.sasa huyo bwana mkubwa si bado anakula maisha? Ilipaswa atoke kidogo kwenye mfumo ili ajifunze heshima.
 
Back
Top Bottom