Waziri wa Biashara Selemani Jafo aunda kamati kwa ajili ya kuchunguza utitiri wa wafanyabiashara wa kigeni Kariakoo

Mindyou

JF-Expert Member
Sep 2, 2024
2,093
5,567
Waziri wa Viwanda na Biashara, Selemani Jafo, ameunda kamati ya watu 15 inayoongozwa na Edda Tandi Lwoga wa Chuo cha Elimu ya Biashara-CBE ili kuchunguza biashara za rejareja zinazofanywa na wageni kinyume cha sheria, hasa katika soko la Kariakoo. Kamati hiyo itafanya kazi kwa siku 30 ili kubaini uhalali wa vibali vya biashara za wageni na athari zake kwa wafanyabiashara wazawa.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukutana na uongozi wa wafanyabiashara wa Kariakoo, Februari 2, 2025 Jijini Dar es Salaam Dkt. Jafo amesema kamati hiyo itachunguza sekta zilizoathirika, mfumo wa utoaji vibali kwa wageni, na mbinu zinazotumiwa kufanya biashara kinyume cha sheria na kupendekeza hatua za kudhibiti hali hiyo na kusaidia wafanyabiashara wa Kitanzania kushindana kibiashara.

Soma Pia: Rais Samia aagiza Waziri wa Biashara kudhibiti Wageni kufanya biashara za Machinga, ahoji vijana wetu watafanya kazi gani?

Dkt.Jafo ameeleza kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amesikia malalamiko ya wafanyabiashara wa Kariakoo kuhusu wageni wanaofanya biashara za rejareja badala ya kuwekeza ambapo hali hiyo inaathiri uchumi wa Watanzania hususan vijana.

Dkt.Jafo pia amesema tatizo hili pia lipo kwenye sekta nyingine kama madini, hivyo ripoti ya kamati hiyo itapendekeza suluhisho la kudumu.



 
Hakuna kitu hapo alishanunulika hawawezi kabisa.. Watampoza na kitu kidogo sana! Maana wameshamsoma udhaifu wake
 
Uchunguzi gani tena wakati wanaoneka na biashara za uchuuzi wakifanya mpk kuchoma mahindi!!
Kamata weka ndani wajieleze, kama hawana cha kueleweka rudisha kwao!

Hv zile za usiku hawafanyi za kusimama road 😁😁
 
HiI tume hazijawahi kuwa na mrejesho inayoeleweka,hapa tumeskia tume imeundwa ila kuskia mrejesho ni majaliwa.
 
Tatizo siyo wageni kufanya biashara ila ni wafanyabiashara wazawa kutaka kuendelea ku exploit watu with unreasonable and inferior quality products.
Watanzania waliopo China nao wafukuzwe eg Silent Ocean
 
--JAFFO KARIAKOO ILITAKA TAMKO TU--
--Ni marufuku kufanya biashara ndogo ndogo kwa wageni - -
 
Waziri wa Biashara na Viwanda, Selemani Jafo, amezindua kamati ya kuchunguza biashara za wageni nchini Tanzania.

Hatua hii ni muhimu sana, hasa katika muktadha wa ongezeko la wageni kutoka nchi mbalimbali, kama Wachina, Warundi, Waganda, na Wacongo, wanaofanya biashara katika maeneo kama Kariakoo.

Swali kubwa ni: je, wageni hawa wana vibali sahihi vya kufanya biashara nchini?

Hali ya Vibali vya Biashara

Kwanza, ni wajibu wa serikali kuhakikisha kwamba wageni wanaofanya biashara nchini wanafuata sheria na kanuni zinazotakiwa.

Je, kuna mfumo mzuri wa ukaguzi wa vibali vya biashara kwa wageni? Wakati mwingine, wageni hawa wanaweza kuonekana kama wanafanya biashara kwa njia isiyo halali, na hivyo kuleta changamoto kwa wafanyabiashara wa ndani.

Serikali inapaswa kuchukua hatua madhubuti kuhakikisha kwamba kila mfanyabiashara, iwe ni mzawa au mgeni, anafuata sheria za nchi.

Usalama wa Wafanyabiashara

Pili, ni muhimu kuangalia ni nani anayewalinda hawa wageni. Katika mazingira ambapo wageni wanapata fursa nyingi za biashara, ni lazima tujiulize: je, wanapata ulinzi kutoka kwa vyombo vya usalama, au wanafanya biashara zao bila kujali sheria?

Soma Pia: Rais Samia aagiza Waziri wa Biashara kudhibiti Wageni kufanya biashara za Machinga, ahoji vijana wetu watafanya kazi gani?

Hili ni jambo la kuzingatia, kwani linaweza kusababisha upinzani kati ya wafanyabiashara wa ndani na wageni ambao wanaweza kuwa na faida zisizokuwa za haki.

Umuhimu wa Sheria

Pia, kuna swali la umuhimu wa sheria zinazowazuia wageni kufanya biashara bila vibali.

Je, kuna sheria ambazo zinawapa mamlaka maafisa wa serikali kuwakamata na kuwafungulia mashtaka wageni ambao hawana vibali?

Ni muhimu kwa serikali kuwa na sheria madhubuti zinazoweza kutekelezwa ili kuhakikisha kwamba biashara nchini inafanywa kwa njia ya haki na uwazi.
Ikiwa sheria hizi hazitekelezwi, kuna uwezekano mkubwa wa kuibuka kwa biashara haramu na udanganyifu.

Mchakato wa Malipo

Zaidi ya hayo, kuna masuala ya kifedha yanayohusiana na biashara za wageni. Kwa nini wageni hawa wanapaswa kulipa fedha kwa ajili ya kufanya biashara wakati serikali ina uwezo wa kutoa amri ya kukamata wale wanaofanya biashara bila vibali? Hili linatoa picha ya udhaifu katika mfumo wa usimamizi wa biashara na inaweza kuonekana kama njia ya kuwaruhusu wageni kuendelea na biashara zao bila kufuata sheria. Serikali inapaswa kuzingatia jinsi inavyosimamia mchakato huu ili kuhakikisha uwazi na usawa.

Hitimisho

Kwa kumalizia, hatua ya Jafo kuunda kamati ya kuchunguza biashara za wageni ni muhimu, lakini ni muhimu pia kuhakikisha kwamba kamati hii inafanya kazi yake kwa ufanisi na bila rushwa.

Ni lazima kuwe na mfumo mzuri wa ukaguzi wa vibali, usalama wa wafanyabiashara, na sheria zinazodhibiti biashara za wageni.

Serikali inapaswa kuimarisha sheria zinazohusiana na biashara za wageni ili kuzuia udanganyifu na kuhakikisha kwamba wafanyabiashara wa ndani wanapata fursa sawa.

Katika muktadha huu, ni wajibu wa kila mmoja kutafakari jinsi ambavyo wageni wanavyoweza kuchangia katika uchumi wa taifa, lakini bila kuathiri haki za wafanyabiashara wa ndani.

Hivyo, ni muhimu kwa serikali kuchukua hatua madhubuti na kuleta uwazi katika biashara za wageni ili kuhakikisha kuwa kila mtu anafanya biashara kwa njia ya haki na sawa.
 
Mkutano Mkuu wa CCM,ndio uliamua au ni UVCCM wameamua?

Hawa vijana ajira Yao ni uchawa, na hawana kazi ni sawa na wazururaji na sijui wanaishi wapi na wanakula wapi.

Kila siku ni kuomba wachangiwe safari zao
 

Attachments

  • IMG-20250203-WA0001.jpg
    IMG-20250203-WA0001.jpg
    113.8 KB · Views: 2
Back
Top Bottom