Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Matajiri kuishi kama mashetani nani akiitoa hii kauli!? na unaielewaje!? BAHATI MBAYA HAKUSEMA KWAMBA WEZI WATAISHI KAMA MASHETANI BALI MATAJIRI...Rais anayajua haya?
uko sahihi asilimia 100 mimi nimekutana na wawekezaji wanajua wakija na Mitaji wakienda Tanzania Investment centre wamemaliza kila kitu to their shock wanakutana na mamlaka zingine zinapiga yowe funga sijui kibali chetu huna nk na wanachotaka afunge tu hawataki majadilianoKiwanda au biashara kufungwa kwasababu ambazo zinajadilika maana yake, mamlaka inayosimamia imeshindwa kazi.
Waziri Ndugulile pia atoe tamko hilo. Taasisi yoyote iliyo chini ya Wizara yake ikiwamo TCRA isifunge biashara za watu kwa sababuyoyote ile.Hongera Mh. Waziri ulikuwa msimamo wako thabiti tangu awali. Mara nyingi maafisa waandamizi wanatumia mianya kufunga biashara kusaka rushwa.
Mh. Biteko pata somo pia,toa nambari ipo shida wachimbaji wadogo,mialo,VAT leaching plant maafisa wako kufunga kwa vijisababu vidogo usafi mazingira, lebo usalama,uzio.... lengo wapatane rushwa kubwa.
Wanatumia seal za wizara kama silaha,bila hata muda kutoa notisi wala orodha makosa kwa wanaowakuta ,afisa ataacha nambari ya simu umfuate ofisini km kadhaa makao makuu wilaya.
Wanakera, mfanyabiashara kapanga wanakuja na rangi kuchafua ukuta.maandishi makubwaaa
Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
Ila U-turn uliyopiga kwenye uzi huu nina mashaka kama ni wewe kweli au kuna jambo limetokea..!!! Maana sijakuzoea kuandika uhalisia bali mara nyingi upenzi wa chamaKichekesho unakuta ameandika huna leseni funga !!!! si waonane na mhusika tu waongee kuwa baada ya miezi miwili tutapita tena uwe umeshatafuta leseni wanampa na tarehe ya kuja na kumtia moyo kuwa hatutapita kukuliza tena hata ukiona tunakuja usifunge usidhani tunakuja kwako.Tunakupa miezi miwili utaratibu wa keseni ni huu hata ikibidi watembee na fomu kabisa wampe wamwelekeze kujaza na viambatanishi vinavyotakiwa .Kama anavyo vyote ajaze hapo hapo wampe na control number alipe hapo hapo kama anazo kwa mobile money au akaunti kama akimaliza vyote kujaza waondoke na fomu zake wamwambie tutakuletea leseni hapahapa dukani endelea na biashara yako Hiyo ndio friendly approach inatakiwa
Lakini jitu linakwambia funga huna leseni hata ukiliambia nipe fomu basi ya kuomba leseni nijaze sasa hivi halina hata fomu limekaa kigaidi gaidi tu na mirangi ya kuandika funga na mikufuli!!! huna TIN ohh huna kibali ohhh hujalipa kodi ohhh leseni huna nk funga!!!!
Mtu leseni hana advice him or her give him or her time without asking him or her to close business
Kwani yalipokuwa hayafungwi, hakukuwa na hizo sheria unazozitaja!? Binafsi naona ni mkumbo tu wa zamu hii... kila mmoja anaimba sauti aliyopangiwa kuimba... kama ya kwanza, Haha... ya pili sawa, ya tatu twende, ya nne, ndiyo yenyewe... DAUTI SAFI SAUTI KUBWA... Philip's, ndiyo yenyewe....!!!!!Matamko ya majukwaani, kwenye televisheni na redio hayatasaidia!! Hao wanaofunga wanafanya hivo kwa sababu SHERIA zinawarusu na ndio waliopewa MAMLAKA hayo!!
Bila kubadilishwa kwa sheria na mamlaka mambo haya yataendelea kutokea!!
Tubadilishe sheria na taratibu zetu za miaka ya 70 ili kuendana na hali ya sasa!! Mahitaji ndio husababisha kuletwa masuluhisho!! Je mahitaji ya sasa yanaendana na sheria na taratibu zilizopo????!!!
Tatizo la mawaziri na watendaji wa serikali huwa mnabadilika kama kinyonga. Huyu Mwambe school mate wangu alikuwa aliharibu sana pale TIC na alikuwa ana misimamo mibovu na anajua alivyokuwa akiumiza wawekezaji, leo anatuambia kuwa watu wasiumizwe. Jamani basi muwe na msimamo moja. Kwanini mnabadilika kama vinyonga?Kwenye taarifa ya habari ITV leo ya saa mbili nimemsikia Waziri wa Biashara na Viwanda, Godfey Mwambe amepiga marufuku taasisi zilizo chini ya wizara yake kufunga biashara za watu kwa kisingizio chochote ahimiza majadiliano badala ya funga funga. Amesema asisikie. Huo ni uhujumu uchumi
TRA na Taasisi zingine za umma mnaotembea na Makufuli na wino wa kuandika maduka na viwanda vya funga funga na mi X kibao mumesikia alichosema Mwambe?
Au huko kwenu kazi yenu kufunga biashara za watu?
====
WAZIRI wa Viwanda na Biashara Mhe. Geoffrey Mwambe (Mb) amekutana na kufanya kikao na Menejimenti, wakuu wa idara, Vitengo na wakuu wa taasisi zilizochini ya Wizara hiyo kwa lengo la kuweka mikakati ya pamoja na kujadili utekelezaji wa bajeti hiyo katika kufikia malengo yaliyowekwa na kila taasisi kueleza malengo yake na vipaumbele vyake.
Akifungua kikao hicho cha siku mbili Waziri Mhe. Geoffrey Mwambe (Mb) amezitaka kila taasisi kuhakikisha zinafanya kazi kwa weredi na ubunifu mkubwa na katika bajeti yake kila taasisi ilenge katika miradi ya maendeleo na ipewa kipaumbele katika mipango ya utekelezaji wa bajeti yake.
“Nataka kila taasisi ihakikishe katika bajeti yake inalenga miradi ya maendeleo itakayosaidia kukua kwa taasisi, pia kila taasisi ipunguze kwa kiasi kikubwa matumizi yasiyo ya lazima tunataka bajeti ilete tija” amesema Mhe. Mwambe.
Aidha amezitaka taasisi katika bajeti yake zilenge vipaumbele vichache ambavyo vitatekelezeka na sio kuweka vipaumbele vingi na bajeti ikawa haitoshi na fedha kutawanywa katika sehemu mbalimbali na mwisho wa siku hakuna matokeo katika utekelezaji wake.
Amezitaka taasisi kufanya kazi kiubunifu ambapo amebainisha kuwa Tanzania ni nchi ambayo imejaliwa kuwa na fursa nyingi lakini bado hazijaleta tija kwa jamii na kuwa ni wajibu wa taasisi kuwa wabunifu nini kifanyike fulsa hizi ziwafikie walengwa hasa katika teknolojia.
“Ukiangalia katika kilimo hasa vijijini miaka nenda rudi tunatumia majembe ya mkono hiyo tija itapatikana sangapi na taasisi za utafiti zipo tu, kabla ya kuondoka katika hiki kiti nataka nizindue jembe lililobuniwa na CAMARTEC linaloleta mapinduzi” amesema.
Ameongeza kuwa “Hatuna kiwanda cha kutengeneza nguo lakini malighafi zipo na kila siku yanasafirishwa marobota mengi na mwisho wa siku tunauziwa nguo, wakati uwezo tunao wa kuwa na viwanda hapa nchini nataka hili lifanyiwe kazi haraka sababu nguvu kazi tunayo” amesema.
Ameitaka Mamlaka ya maendeleo ya biashara nchini TANTRADE kuja na mikakati ya kuhakikisha wanaweka mazingira mazuri ya biashara hasa kwa wajasiliamali katika halmashauri zote ili kuwaendeleza wafanyabiashara hao kukua kutoka hapo walipo na kuwa na biashara kubwa.
Pia ameitaka TANTRADE kuwa na mikataba ya mazao ya kibiashara kama korosho badala ya kusubiri minada ambayo sio uhakika huku akitaka kuja na teknolojia inayofaa ili kuhakikisha korosho zote zinabanguliwa na sio kuuza korosho ghafi kuongeza thamani ya zao hilo.
Aidha amekitaka chuo cha elimu ya biashara CBE kubadili mtazamo wake na kuanza kutoa elimu itakayomuwezesha mwanafunzi anapomaliza chuo kwenda kuanzisha biashara na sio mtazamo wake wa sasa wa kuzalisha wasimamizi wa biashara huku akitaka kishirikiane na vyuo vingine katika kuboresha kada hiyo.
Kwa upande mwingine ameitaka tume ya ushindani kufanyakazi kwa ubunifu na si kufanyakazi kwa mazoea ili kuhakikisha inafanyakazi na wawekezaji vizuri na sio kuwa kero kwa wawekezaji hapa nchini na hasa katika kushughulikia mapungufu ya wawekezaji hapa nchini.
“Tume ya ushindani msiwasumbue wenye viwanda kuna njia nyingi badala ya kufunga biashara yake na huyo mwenye kiwanda kuona namna ya kumaliza mapungufu hayo sio kumfungia kiwanda chake” amesema.
Naibu wa Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Exaud Kigahe (Mb) amewataka watumishi katika wizara hiyo kufanya kazi kwa nidhamu na uadilifu mkubwa na kila kiongozi katika nafasi yake ajitathmini katika utendaji wake wa kazi kama anafaa kuwa katika nafasi aliyopo.
Aidha amekemea vitendo vya uchepushaji wa fedha za miradi ambapo taasisi nyingi zimekuwa zikitumia fedha kutekeleza miradi ambayo haikukusudiwa tangu awali huku akizitaka taasisi zinazotekeleza miradi inayofanana kushirikiana na sio kila taasisi inatekeleza kivyake wakati mradi ni mmoja.
Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara Prof. Riziki Shemdoe amesema kikao hicho ni cha siku mbili kwa ajili ya kujadili vipaumbele vya kila taasisi na bajeti yake namna ya kutekeleza ili kuleta tija katika malengo ya kuanzisha taasisi hizo zilizochini ya Wizara ya Viwanda na biashara.
Uko sahihi hawaendi kirafiki wanaenda kipolisiTatizo sielewi kama ni ushamba au kitu utamaduni, maana watumishi wa serikali wa idara zote, wanapoenda kukagua au kutembelea shughuli yoyote ya mtu, hawaendi kama walezi wa raia, wanaenda kama vile polisi wanavamia nyumba ya jambazi. Wanapenda kuonyesha mamlaka na nguvu waliyonayo kwa muhusika.
Tuacheni tu tumeshazoea kuumia, muda ukifika atakuja kiongozi anayejali watu wake tutarudi kwenye hali ya kawaida. Tumemwachia Mungu, Wafanyabiashara tunaishi kama wahalifu tukitarajia ipo siku haya yatakwisha. Utawala huu siyo Taxpayer friendly, kwa hiyo acha tuzugezuge muda upite.Uko sahihi hawaendi kirafiki wanaenda kipolisi