Waziri wa Ajira wa Uingereza ajiuzulu kwa kutokukubaliana na mpango wa Brexit

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,500
9,279
Waziri Mkuu wa Uingereza, Boris Johnson amemteua Therese Coffey kujaza pengo ambalo limeachwa wazi na waziri wa ajira na pensheni Amber Rudd ambaye amejiuzulu kwa kutokubaliana na namna ambavyo Johnson anaendesha mchakato wa Uingereza kujitoa katika Umoja wa Ulaya-Brexit.

Kujiuzulu kwa Rudd kumekuwa pigo kwa Johnson anayekabiliwa na ukosoaji mkali kufuatia hatua zake kama vile kuahirisha bunge, kuwafukuza wabunge kutoka kwenye chama chake na kuitisha uchaguzi wa mapema.

Johnson ameapa kuiondoa Uingereza katika Umoja wa Ulaya ifikapo Oktoba 31, iwe kwa makubaliano au bila ya makubaliano.

Coffey ambaye ni waziri wa mazingira na mbunge wa Suffolk mashariki mwa England alipinga Uingereza kujitenga na Umoja wa Ulaya wakati wa kura ya maoni
 
Limetokea wapi mzee
Ukanda wa ziwa Tangangyika majira ya saa 9 usiku kuelekea saa 10. Limedumu kwa dakika 2-4. Lina ukubwa wa magnitude 5.5: Ukitizama tovuti inayohusiana na earthquake Duniani " Earthquake today" imeelezwa hii.

Na raia wanaoishi huo ukanda wa ziwa Tanganyika kama Mapanda, Katavi n.k wamethibitisha hili. Kwa kujiridhisha zaidi unaweza kupiga simu kwa raia wanaishi maeneo hayo(kama wapo unaofahamiana nao).

Kuhusu madhara yaliyosabbishwa na hili tetemeko la ardhi sifahamu kiukweli. Ajabu vyombo vingi vya habari nchini mwetu viko kimya. Sijui taarifa zao wanakusanyaje.
 
Huyu Borris Johnson asipokuwa makini anayeweza kuwa ndie Waziri mkuu atakaye hudumu kwa kipindi kifupi zaidi
 
Back
Top Bottom