#COVID19 Waziri wa Afya: Watu 408 wamebainika kuwa na Corona , 284 wakiwa katika mashine za oksijeni

Serikali ya Samia soon inakwenda kuwaweka ndani wanyonge ...hakuna beberu anayekubali kujenga banda then mifugo ikaendelea kuzulula tu

Ujinga mzigo:

IMG_20210706_203616_157.jpg
 
Huyo waziri hana tofauti yoyote na robot; tena lile la matope.

Kichwani hakuna kitu!

Sijui walisomea ujinga gani hawa watu.
 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii Dk Dorothy Gwajima amesema watu 408 wamebainika kuwa na ugonjwa wa Corona (Covid-19) nchini huku 284 wakiwa katika mashine za oksijeni.

Ni wakati sasa wa Wananchi na asasi na taasisi mbalimbali za kiserikali na zisizo za kiserikali kushirikiana na serikali katika kutekeleza na kuhamasisha maelekezo ya wataalamu wa afya juu ya hatua za kukabiliana na ugonjwa huu.

View attachment 1848604 View attachment 1848605
Huyu mama ni muongo kuliko Prof. Muhongo. Hapa nilipo Kuna watu 9 wamefariki Leo Kwa COVID-19. Hospital zimejaa wagonjwa. Mbona hakutaja waliokufa? Hiyo idadi ni kutoka mkoa au wilaya gani Tanzania?
 
Nashauri wasafiri kutoka Kilimanjaro, Arusha, Dar na Mwanza wasiruhusiwe kusambaa mikoa mingine maana katika mikoa hiyo kuna janga la juu na linalotisha la Corona.
Kumbe mna takwimu, mbona mlikuwa mnatuficha?
 
Chanjo si zimeshafika, waanze kuchanja basi. Hizi mambo za kupeana taarifa nusu nusu hivi ili tupate taharuki sio sawa kabisa.

Taarifa haielezi ni mikoa ipi ina hao wagonjwa, namna gani hawa viongozi.
 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Dorothy Gwajima amesema hadi kufikia Julai 8, 2021 jumla watu 408 walibainika kuwa na ugonjwa wa corona huku 284 wakitumia mitungi ya oksijeni...
Huyu Waziri wa Afya, ni vizuri kama na yeye angepimwa ili kujiridhisha kama na yeye atakuwa hana tatizo la afya ya akili. Vituko alivyokuwa anafanya wakati wa marehemu, havikuwa vinaashiria afya njema ya akili.

Marehemu aliwahi kutamka kuwa alimteua Mpina kuwa Waziri kwa sababu Mpina ni kichaa mwenzie kama yeye. Yawezekana kuna vichaa wengine wengi wenzie aliowateua kwa sababu ya mfanano wa matatizo yao ya afya ya akili.
 
Huyu mama ni PhD Kwa kusomea au ni Dr wa binadamu? Data alizo zitoa Leo ni maajabu ya data
 
Mmoja kakata leo mida hii huku nashuhudia akiwa na mtungi wa oxygen ni covid case.ni hatari.
 
Nani Katengeneza korona?
Kwa lengo gani
Nini hatima yake
Baada ya chanjo hizo nini kinafuata badae
 
Back
Top Bottom