Waziri wa Afya, Dkt Dorothy Gwajima uje useme na wana-MOI ujue yanayowasibu kiasi cha kushusha morali ya kazi

mtakachake

New Member
Apr 16, 2021
1
0
Pamoja na yote naomba nikupe pole ya ujenzi wa Taifa.

Pili nipende kukupa hongera kwa kuaminiwa tena kuongoza Wizara hii nyeti ya Afya ambapo sisi ndio tunashikilia roho za binadamu baada ya Mungu hususani majeruhi wa barabarani waliokithiri kila kukicha.

Lakini licha ya yote kuna maeneo mengi hujayafikia bado au kuyagusa nina uhakika kuwa umewahi fika Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI) na umeongea na uongozi mara kadhaa na kudanganywa mengi juu ya hii taasisi.

Kiukweli huwajui wafanyakazi wake wana hali gani, wana madukuduku gani mioyoni mwao. Milango yako iko mbali kuweza kufunguliwa tungeweza kukueleza hali halisi sisi wafanyakazi basi tunaomba uje uongee na wafanyakazi ujue yanawasibu nini kiasi cha kushusha morali ya kazi Hapa MOI.

Viongozi uliowaweka hapa wakali kama pilipili kuficha madhaifu yao katika utendaji basi uje utusikilize.

Ukishindwa kuja basi tutayasema humu bila kuchoka mpaka mama yetu Mh. Samia atasikia na. tunaimani atakusaidia kusikiliza.

Ni sisi wanyonge tuliochoka kuvumilia.

Mtaka Chake.
 
Pamoja na yote naomba nikupe pole ya ujenzi wa Taifa.

Pili nipende kukupa hongera kwa kuaminiwa tena kuongoza Wizara hii nyeti ya Afya ambapo sisi ndio tunashikiria roho za binadamu baada ya Mungu hususani majeruhi wa barabarani waliokithiri kila kukicha.

Lakini licha ya yote kuna maeneo mengi hujayafikia bado au kuyagusa nina uhakika kuwa umewahi fika Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI) na umeongea na uongozi mara kadhaa na kudanganywa mengi juu ya hii taasisi.

Kiukweli huwajui wafanyakazi wake wana hali gani, wana madukuduku gani mioyoni mwao. Milango yako iko mbali kuweza kufunguliwa tungeweza kukueleza hali halisi sisi wafanyakazi basi tunaomba uje uongee na wafanyakazi ujue yanawasibu nini kiasi cha kushusha morari ya kazi Hapa MOI.

Viongozi uliowaweka hapa wakali kama pilipili kuficha madhaifu yao katika utendaji basi uje utusikilize.

Ukishindwa kuja basi tutayasema humu bila kuchoka mpaka mama yetu Mh. Samia atasikia na. tunaimani atakusaidia kusikiliza.

Ni sisi wanyonge tuliochoka kuvumilia.

Mtaka Chake.
MOI madaktari mnauza vifaa kwa wagonjwa, majina tunayo, ni suala la muda tu, sitaki kuwasikia kabisa, watu wanakufa hapo kwa uzembe wenu.
 
MOI madaktari mnauza vifaa kwa wagonjwa, majina tunayo, ni suala la muda tu, sitaki kuwasikia kabisa, watu wanakufa hapo kwa uzembe wenu.
najiuliza ,nchi za wenzetu yanatokea hayo?
tukubaliane tu.....mishahara na maslahi ya wafanyakazi wa afya ni duni sana.....
 
Back
Top Bottom